middo
JF-Expert Member
- Mar 21, 2011
- 207
- 56
Watoto wa snake boy walikengeuka ni wawil tu, musa na daud. Vjana wakabaj keko ni weng na wanatoka familia tofaut sidhani kama ni haki kusema rashid kaleta janga. Keko ukabaji haujaanza jana, tangu enzi hzo za akina marehem chatu, ally kingongo tena enzi hzo ukabaj ndo ulikuwa kwnye highest point siyo sasa! Hao watt wanaiga tu wala hawajawa tishio kivile kwa keko.Hakuna asiyeufahamu umahiri wa Rashid Matumla katika ndondi , huyu ni kati ya mabondia wachache sana walioliletea Taifa hili heshima kubwa sana .
Lakini kama ilivyo ada , katika kila jema kuna upande wa pili wa mabaya , Baada ya kupata umaarufu ule , Rashidi akaamua kuzaa watoto wasio na idadi , mithili ya kufyatua matofali kwenye mashine ya umeme .
Ana watoto zaidi ya 10 , ambao ameshindwa kuwatunza na wamegeuka WAKABAJI , ( Mkazi yeyote wa keko anaweza kuthibitisha )
Ukabaji ninaoumanisha hapa ni ile tabia ya vijana vibaka na mateja maeneo ya uswahilini , kuamua kuvizia na kuwakaba na kupora mali za wananchi , hadharani na gizani , kwa maana nyingine ni kwamba Rashid Matumla ameleta kundi la wakabaji kwenye mitaa ileile aliyokuwa akisifiwa kwa ushujaa wake , jambo linaloleta aibu kwake mwenyewe na kwa wote waliomsaidia kuwa bingwa .
Wito kwa wanamichezo wa Tanzania kuweni makini sana na umaarufu wa kupita , angalieni mbele zaidi , msije dhalilika kama Rashid
Kwl snakeboy ana wtt wengi lkn kama nilivyosema vijana wale wawil ndo wana mienendo ya ajab na cyo wao walioanzisha hako kamchezo keko, so huwez sema rashid kaleta janga keko.