Mpaka Sasa Kuna vyama viwili vya walimu vilivyosajiliwa na vinafanya kazi kwa mujibu wa sheria na kwa kufuata katiba zao Kila kimoja. Vyama hivyo ni CWT na CHAKUHAWATA.
Mimi siyo mwumini wa mojawapo ya hivyo vyama Ila ni mpenda haki, napoona Kuna upande unakandamizwa ni wajibu kusema na kukemea kwa nguvu zote.
Ukisoma hiyo barua iliyosainiwa na RAS wa Arusha ni wazi kabisa hakuna sehemu yoyote ametaja kifungu Cha sheria kilichokiukwa. Yaani ni kama stori fulani Fulani za mtaani zimeandikwa. Na ukiona kasaini kitu ambacho hakina kichwa Wala miguu hapo kapewa rushwa kubwa ili atumike kuwamonitor wakurugenzi wa halmashauri waliopo chini yake ili wavunje sheria na kuwanyima walimu haki.
Mwezi April mwaka huu CWT walipeleka barua kwa huyo RAS wakimwomba awasaidie ili kuzuia walimu wanaoihama CWT, Sasa ni wazi wamefika maelewano hadi amesaini hiyo barua ambayo imeandikwa na hao CWT na kusainiwa na RAS hapo ndipo kajichanganya na anapaswa kuchunguzwa na TAKUKURU kwa hizo hoja alizoandikiwa kama zipo na ana ushahidi kwanini hajachukua hatua kwa walimu anaowatuhumu.
1. Hao walimu anaowatuhumu kutumia muda mwingi kuhamasisha walimu wengine wajiunge kwenye chama ni wepi? Katika halmashauri zake makatibu wa TSC wanatembea na makitibu wa CWT kulazimisha walimu wa ajira mpya wajiunge CWT kwa kuwarubuni na chakula na kuwatishia kufutwa kazi kama watajiunga na chama kingine, hili hulikemei sababu na wewe ni mnufaika na huu uonevu.
2. Hii hoja ya vyama kutokuwa na ofisi imekuwa hoja ya CWT kwa CHAKUHAWATA wametembea nayo kwa wakurugenzi wameenda mpaka mahakamani ikakosa mashiko baada ya kujibiwa kwa mujibu wa katiba ofisi inayotambulika ni ofisi ya makao makuu ambayo IPO Kigoma na maeneo mengine ofisi ni yule kiongozi aliyeteuliwa ama kuchaguliwa kwa ajili ya kuratibu shughuli za chama sehemu husika na kukishakuwa na wanachama ndipo Wanaweza kukodi jengo kama ofisi. Sasa hapa unasema wamekosa pa kupeleka changamoto, Kuna mwanachama wa CHAKUHAWATA aliyekuja kwako ama kwenda kwa mkurugenzi akasema amekosa pa kupeleka changamoto?
3. Hao walimu waliojazana kwa mkurugenzi hawafundishi ili waondolewe kwenye chama wamechukuliwa hatua gani? Kwanini mwl aende kwa mkurugenzi kutaka aondolewe CWT huku ametoa notice ya siku 30? Akiondolewa kwa wakati ataenda huko? Hapa kemea wakurugenzi wanaosababisha walimu kupoteza muda kwenda kufuatilia majibu ya barua zao kwa wakurugenzi badala yake barua zifanyiwe kazi kwa wakati na siyo barua za kujitoa tu CWT Bali barua zote wanazomwandikia mkurugenzi zijibiwe kwa wakati.
4. Walimu wasiowaheshimu wakuu wao kwasababu ya tofauti zozote za kimtizamo au kiutendaji zilikuwepo tangu zamani na zipo na zitaendelea kuwepo Wala siyo kwa ajili ya uwepo wa CHAKUHAWATA shida CWT wanawazuia wakuu wa shule kujitoa CWT wakiwatishia watatolewa kwenye nafasi zao.
5. CHAKUHAWATA ni chama Cha walimu na siyo chama Cha siasa na wanachama wake wapo waliopo kwenye vyama vya siasa, Kuna makada wengi tu, Kuna mashabiki wa Simba na YANGA huwezi kuwakuta hata siku moja wanajadili mambo ya siasa maana lengo siyo hilo. Labda uwakute kwenye utani wa Simba na YANGA na siyo siasa hivyo hizo hoja zote ni dhaifu zenye lengo la kuwasaidia CWT ili walimu wasihame huko. RAS acha kutumika, tenda haki.
5. Nikupe taarifa kuwa kwenye katiba ya CHAKUHAWATA hakuna ngazi ya Mkoa. Kuna uongozi ngazi za Wilaya ambao walichaguliwa na majina ya viongozi wa Wilaya ambazo chama kipo yapo kwa msajili wa vyama.
Walimu wameibiwa sana mishahara Yao, kumbuka kauli ya hayati Rais Magufuli pamoja na mambo ya wizi na ubadhilifu wa Mali ndani ya CWT hakuna mwalimu mwenye hamu na hicho chama hivyo kujaribu kukitetea na kujaribu kuzuia walimu kuhama CWT kwa kutumia madaraka uliyo nayo ya muda, unataka kuleta sintofahamu katika Mkoa wa Arusha ambao utaathiri elimu ya watoto.
Mimi siyo mwumini wa mojawapo ya hivyo vyama Ila ni mpenda haki, napoona Kuna upande unakandamizwa ni wajibu kusema na kukemea kwa nguvu zote.
Ukisoma hiyo barua iliyosainiwa na RAS wa Arusha ni wazi kabisa hakuna sehemu yoyote ametaja kifungu Cha sheria kilichokiukwa. Yaani ni kama stori fulani Fulani za mtaani zimeandikwa. Na ukiona kasaini kitu ambacho hakina kichwa Wala miguu hapo kapewa rushwa kubwa ili atumike kuwamonitor wakurugenzi wa halmashauri waliopo chini yake ili wavunje sheria na kuwanyima walimu haki.
Mwezi April mwaka huu CWT walipeleka barua kwa huyo RAS wakimwomba awasaidie ili kuzuia walimu wanaoihama CWT, Sasa ni wazi wamefika maelewano hadi amesaini hiyo barua ambayo imeandikwa na hao CWT na kusainiwa na RAS hapo ndipo kajichanganya na anapaswa kuchunguzwa na TAKUKURU kwa hizo hoja alizoandikiwa kama zipo na ana ushahidi kwanini hajachukua hatua kwa walimu anaowatuhumu.
1. Hao walimu anaowatuhumu kutumia muda mwingi kuhamasisha walimu wengine wajiunge kwenye chama ni wepi? Katika halmashauri zake makatibu wa TSC wanatembea na makitibu wa CWT kulazimisha walimu wa ajira mpya wajiunge CWT kwa kuwarubuni na chakula na kuwatishia kufutwa kazi kama watajiunga na chama kingine, hili hulikemei sababu na wewe ni mnufaika na huu uonevu.
2. Hii hoja ya vyama kutokuwa na ofisi imekuwa hoja ya CWT kwa CHAKUHAWATA wametembea nayo kwa wakurugenzi wameenda mpaka mahakamani ikakosa mashiko baada ya kujibiwa kwa mujibu wa katiba ofisi inayotambulika ni ofisi ya makao makuu ambayo IPO Kigoma na maeneo mengine ofisi ni yule kiongozi aliyeteuliwa ama kuchaguliwa kwa ajili ya kuratibu shughuli za chama sehemu husika na kukishakuwa na wanachama ndipo Wanaweza kukodi jengo kama ofisi. Sasa hapa unasema wamekosa pa kupeleka changamoto, Kuna mwanachama wa CHAKUHAWATA aliyekuja kwako ama kwenda kwa mkurugenzi akasema amekosa pa kupeleka changamoto?
3. Hao walimu waliojazana kwa mkurugenzi hawafundishi ili waondolewe kwenye chama wamechukuliwa hatua gani? Kwanini mwl aende kwa mkurugenzi kutaka aondolewe CWT huku ametoa notice ya siku 30? Akiondolewa kwa wakati ataenda huko? Hapa kemea wakurugenzi wanaosababisha walimu kupoteza muda kwenda kufuatilia majibu ya barua zao kwa wakurugenzi badala yake barua zifanyiwe kazi kwa wakati na siyo barua za kujitoa tu CWT Bali barua zote wanazomwandikia mkurugenzi zijibiwe kwa wakati.
4. Walimu wasiowaheshimu wakuu wao kwasababu ya tofauti zozote za kimtizamo au kiutendaji zilikuwepo tangu zamani na zipo na zitaendelea kuwepo Wala siyo kwa ajili ya uwepo wa CHAKUHAWATA shida CWT wanawazuia wakuu wa shule kujitoa CWT wakiwatishia watatolewa kwenye nafasi zao.
5. CHAKUHAWATA ni chama Cha walimu na siyo chama Cha siasa na wanachama wake wapo waliopo kwenye vyama vya siasa, Kuna makada wengi tu, Kuna mashabiki wa Simba na YANGA huwezi kuwakuta hata siku moja wanajadili mambo ya siasa maana lengo siyo hilo. Labda uwakute kwenye utani wa Simba na YANGA na siyo siasa hivyo hizo hoja zote ni dhaifu zenye lengo la kuwasaidia CWT ili walimu wasihame huko. RAS acha kutumika, tenda haki.
5. Nikupe taarifa kuwa kwenye katiba ya CHAKUHAWATA hakuna ngazi ya Mkoa. Kuna uongozi ngazi za Wilaya ambao walichaguliwa na majina ya viongozi wa Wilaya ambazo chama kipo yapo kwa msajili wa vyama.
Walimu wameibiwa sana mishahara Yao, kumbuka kauli ya hayati Rais Magufuli pamoja na mambo ya wizi na ubadhilifu wa Mali ndani ya CWT hakuna mwalimu mwenye hamu na hicho chama hivyo kujaribu kukitetea na kujaribu kuzuia walimu kuhama CWT kwa kutumia madaraka uliyo nayo ya muda, unataka kuleta sintofahamu katika Mkoa wa Arusha ambao utaathiri elimu ya watoto.