Kinyungu
JF-Expert Member
- Apr 6, 2008
- 17,369
- 33,012
Baada ya kuanzisha rasmi ofisi za kibalozi hatimaye rais wa Sudan kusin Bw. Salva Kiir amefanya ziara rasmi nchini Israel ambapo amekutana na viongozi wa Israel akiwemo Rais Shimon Perez, Waziri Mkuu Binyamin Netanyahu, Waziri wa Ulinzi Ehud Barak na Waziri wa mambo ya nje Avigdor Lieberman.
Katika ziara hiyo inayoangaliwa na kufuatiliwa kwa karibu na mataifa ya kiarabu hususan yale ya Sudan na Egypt rais Kiir ameelezwa kufurahishwa kwake kwa kutembelea nchi hiyo ambapo amesema imekuwa furaha kubwa kwake kutembea kwenye nchi hiyo ya ahadi. Katika ziara hiyo rais Kiir alitembelea makumbusho ya mauji ya halaiki ya Yad Vashem akiwa ameambatana na Mbunge wa chama cha Likud Bw. Danny Danon.
Katika ziara hiyo Waziri Mkuu Netanyahu ametoa ahadi ya kusaidia kuijenga nchi hiyo husani kwa kusaidia kilimo, miundo mbinu na mawasiliano.
South Sudan president to meet wit... JPost - Diplomacy & Politics
Katika ziara hiyo Waziri Mkuu Netanyahu ametoa ahadi ya kusaidia kuijenga nchi hiyo husani kwa kusaidia kilimo, miundo mbinu na mawasiliano.
South Sudan president to meet wit... JPost - Diplomacy & Politics