Rais, Tanzania si chochote katika utalii

Rais, Tanzania si chochote katika utalii

Msambichaka Mkinga

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2015
Posts
1,646
Reaction score
2,911
Watanzania ni watu wenye bahati mbaya sana maana mara nyingi wanaaminishwa kuwa wao ni bora katika kila kitu. Wengi wao, kwa ujinga tu, nao wameyabeba maneno hayo na kuyaweka katika vichwa vyao.

1.Wapo Watanzania wanaoaminishwa kuwa Tanzania ina dhahabu nyingi kuliko nchi yoyote Duniani, ambao ni uwongo, lakini wao wanaamini

2. Wapo Watanzania wanaoamini kuwa tuna gas nyingi kuliko nchi yoyote, ambao ni uwongo

3. Wapo Watanzania wanaoaminishwa kuwa Tanzania ina madini ya kila namna na ina madini mengi kuliko nchi yoyote Duniani/Afrika, ambao ni uwongo

4. Wapo Watanzania wanaoamini kuwa Tanzania ni nchi yenye amani kuliko nchi zote za Afrika, ambao ni uwongo

5. Wapo Watanzania wanoamini kuwa nchi yetu ina demokrasia, utawala wa sheria na uongozi mzuri kuliko nchi yoyote ya kiafrika, nao ni uwongo lakini wanaamini

6. Wapo Watanzania wanaoaminishwa kuwa Tanzania ni nchi nzuri sana ambayo kila mwanadamu angependa kuja na kuishi, nao ni uwongo lakini wengi wanaamini hivyo

7. Wapo Watanzania wanaoamini kuwa Tanzania ni nchi yenye vivutio vingi na mazingira mazuri ya utalii ambayo hayapo mahali pengine popote Duniani, ambao ni uwongo mkubwa.

Takwimu za mwaka 2014 kuhusu utalii wa kimataifa (International tourist arrivals) inaonesha kuwa hakuna hata nchi moja ya Afrika ambayo ilikuwa miongoni mwa nchi 10 za juu katika kutembelewa na watalii. Hii inaonesha kuwa watalii hawa wa kizungu wanapendelea zaidi kwenda kwenye mabara mengine kuliko Afrika.

In 2014, there were 1.133 billion international tourist arrivals worldwide, with a growth of 4.3% as compared to 1.087 billion in 2013.[1] The top 10 international tourism destinations in 2014 were

1. France Europe 83.7 million
2. United States North America 74.8 million
3. Spain Europe 65.0 million
4. China Asia 55.6 million
5. Italy Europe 48.6 million
6. Turkey Europe 39.8 million
7. Germany Europe 33.0 million
8. United Kingdom Europe 32.6
9. Russia Europe 29.8 million
10. Mexico North America 29.1

Katika Afrika, Tanzania haipo hata katika 10 bora

In 2014, there were over 55.7 million international tourist arrivals to Africa, the top ten African destinations were
1. Morocco 10.2 million
2. Egypt 9.6 million
3. South Africa 9.5 million
4. Tunisia 6.0 million
5. Algeria — 2.7 million
6. Mozambique — 1.8 million
7. Zimbabwe 1.8 million
8. Kenya — 1.4 million
9. Uganda — 1.2 million
10. Namibia — 1.1 million

Jambo la kusikitisha ni kwamba, nchi inayoongoza kwa kutembelewa na watalii wageni katika Afrika ambayo ni Morocco, idadi ya watalii inaowapokea ni chini ya watalii wanaotembelea nchi ya mwisho ya 10 bora ya Ulaya.

In 2014, there were over 582 million international tourist arrivals to Europe, an increase of 3.0% over 2013. In 2014, the top ten destinations were

1. France 83.7 million
2. Spain 65.0 million
3. Italy 48.6 million
4. Turkey 39.8 million
5. Germany 33.0 million
6. United Kingdom 32.6 million
7. Russia 29.8 million 28.4
8. Austria 25.2 million
9. Greece 22.0 million
10. Poland 16.0 million

Ukija kwenye mapato ya utalii, Tanzania na Afrika si lolote na si chochote. Idadi kubwa ya watalii inawianika kwa kiwango kikubwa na mapato ya utalii. Hayo maneno ya kusema kuwa unaweza kuwa na watalii wachache halafu mapato yakawa makubwa ni ndoto za alinacha zinazootwa na maprofesa wa Tanzania pekee.

International tourism receipts grew to US$1,245 billion in 2014, corresponding to an increase in real terms of 3.7% from 2013.[11] The World Tourism Organization reports the following countries as the top ten tourism earners for the year 2014, with the United States by far the top earner.
1
23px-Flag_of_the_United_States.svg.png
United States North America $177.2 billion
2
23px-Flag_of_Spain.svg.png
Spain Europe $65.2 billion
3
23px-Flag_of_the_People%27s_Republic_of_China.svg.png
China Asia $56.9 billion
4
23px-Flag_of_France.svg.png
France Europe $55.4 billion
5
23px-Flag_of_Macau.svg.png
Macau Asia $50.8 billion
6
23px-Flag_of_Italy.svg.png
Italy Europe $45.5 billion
7
23px-Flag_of_the_United_Kingdom.svg.png
United Kingdom Europe $45.3 billion
8
23px-Flag_of_Germany.svg.png
Germany Europe $43.3 billion
9
23px-Flag_of_Thailand.svg.png
Thailand Asia $38.4 billion
10
23px-Flag_of_Hong_Kong.svg.png
Hong Kong Asia $38.4 billion

Kwa mapato ya utalii wa kimataifa katika Afrika, nchi inayoongoza ni Afrika Kusini ($9.4 billion) ikifuatiwa na Misri ($7.2 billion), Morrocco ($7.1 billion) na Tunisia ($2.3 bilion). Kwa ujumla yule anayeongoza kwa mapato ya utalii katika Afrika hayupo katika 10 bora za Dunia, na ni chini ya mapato ya nchi ya mwisho ya 10 bora katika mabara mengine.

Mapato ya utalii ya Tanzania kwa mwaka 2014 yalikuwa $1.95 billion, chini kuliko mapato ya Singapore ($19.20 billion), Turkey ($37.37 billion), Qatar (10.58 billion) au Misri ($7.21 billion). Singapore, Turkey, Qatar na Misri hawana twiga wala tembo lakini wanatuzidi kwa idadi ya watalii na kimapato mara dufu.

Profesa Maghembe, Rais wetu na Watanzania, wanatakiwa kufahamu kuwa vivutio vya utalii ni zaidi ya idadi ya tembo, fisi, twiga, pundamilia na ngiri tulio nao. Utalii mkubwa ni akili, yaani unaweza kufanya nini kwa kutegemea mazingira yako ili watu wa mataifa mengine waje kushuhudia na kustarehe katika mazingira yako.

Watanzania, kwa ujinga wetu, tunaamini kuwa kwa sababu tu tuna nyumbu wengi, twiga na tembo basi watu wengi, Dunia nzima wanahangaika ili waje watazame sura ya twiga. Watalii hawana haja na sura ya pundamilia wala mbwa mwitu bali wanataka kuona mazingira ya kuvutia yaliyo tofauti na mahali pengine, na sisi tunaweza kuwatumia wanyama hao kuweza kuyafanya mazingira yetu kuwa ya kuvutia zaidi kuliko Misri ambako mapiramidi na chuo kikuu cha kwanza cha Alexandria, vimetosha kuizidi Tanzania kimapato.

Ushauri wangu kwa Rais, fukuza kazi prof. Maghembe maana amekupotosha kwa kueleza kuwa hakuna uhusiano wa mapato katika utalii na idadi ya watalii. Waziri unayetakiwa kuwa naye ni yule ambaye ataihakikishia Tanzania inapata ongezeko kubwa la watalii na siyo upungufu wa watalii. Bila ya kujali kama ongezeko la idadi ya utalii na mapato ya utalii vitategemea kupungua kwa kodi au kuondoa baadhi ya kodi, au kuongeza mbinu za kujitangaza au kuboresha miundombinu na huduma za kitalii, ukweli ni kwamba tunahitaji ongezeko la idadi ya watalii na mapato yatokanayo na utalii ambavyo vinaenda sambamba hata kama siyo kwa uwiano 1:1

Rais Magufuli hatutakuelewa kama pamoja na vyote tulivyo navyo, lakini mapato ya utalii yataendelea kuwa chini kuliko ya Afrika Kusini, Misri, Morocco, Tunisia na Kenya, huku wewe mwenyewe ukisema tuna vivutio vingi vya utalii. Tuna vivutio vya utalii visivyovutia watalii.

Mheshimiwa Rais, hotuba zako za mara kwa mara za kuelezwa nchi hii imeibiwa sana tumekwishazisikia kiasi cha kutosha, sasa tunahitaji kusikia kutoka kwako juu ya mbinu za kuongeza mapato ya utalii (siyo kodi za utalii bali mapato), mbinu za kuongeza mauzo ya mazao yetu nje ya nchi, mkakati wa kujenga uchumi wa viwanda, na namna rasilimali nyingine kama gas na madini zinavyoweza kubadilishwa kuwa mapato ya wananchi na Taifa. Mheshimiwa Rais tunataka mbinu na mikakati ya kuongeza mapato ya Watanzania.

Sisi wengine daima tutazidi kueleza pale tunapoona mbinu siyo sahihi. Tunaamini una dhamira njema lakini tuna mashaka makubwa katika mbinu.

Binadamu tuna miaka michache Duniani, hatuna muda wa kufanya majaribio bali tunatakiwa kuenenda kwa namna na mbinu zilizosahihi katika kuibadilisha nchi hii iliyo maskini kupindukia lakini iliyo na fursa nyingi zilizofunikwa. Fursa ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kitalii ni kubwa sana lakini hatuna watu wa kuweza kufungua fursa hizo ili jamii iweze kuziona kwa sababu waliopewa mamlaka ya kuzifunua kwa umma wanafanya kila mbinu ya kuzifunika ili wananchi wasizione na wala wasizifaidi.
 
Watanzania ni watu wenye bahati mbaya sana maana mara nyingi wanaaminishwa kuwa wao ni bora katika kila kitu. Wengi wao, kwa ujinga tu, nao wameyabeba maneno hayo na kuyaweka katika vichwa vyao.

1.Wapo Watanzania wanaoaminishwa kuwa Tanzania ina dhahabu nyingi kuliko nchi yoyote Duniani, ambao ni uwongo, lakini wao wanaamini

2. Wapo Watanzania wanaoamini kuwa tuna gas nyingi kuliko nchi yoyote, ambao ni uwongo

3. Wapo Watanzania wanaoaminishwa kuwa Tanzania ina madini ya kila namna na ina madini mengi kuliko nchi yoyote Duniani/Afrika, ambao ni uwongo

4. Wapo Watanzania wanaoamini kuwa Tanzania ni nchi yenye amani kuliko nchi zote za Afrika, ambao ni uwongo

5. Wapo Watanzania wanoamini kuwa nchi yetu ina demokrasia, utawala wa sheria na uongozi mzuri kuliko nchi yoyote ya kiafrika, nao ni uwongo lakini wanaamini

6. Wapo Watanzania wanaoaminishwa kuwa Tanzania ni nchi nzuri sana ambayo kila mwanadamu angependa kuja na kuishi, nao ni uwongo lakini wengi wanaamini hivyo

7. Wapo Watanzania wanaoamini kuwa Tanzania ni nchi yenye vivutio vingi na mazingira mazuri ya utalii ambayo hayapo mahali pengine popote Duniani, ambao ni uwongo mkubwa.

Takwimu za mwaka 2014 kuhusu utalii wa kimataifa (International tourist arrivals) inaonesha kuwa hakuna hata nchi moja ya Afrika ambayo ilikuwa miongoni mwa nchi 10 za juu katika kutembelewa na watalii. Hii inaonesha kuwa watalii hawa wa kizungu wanapendelea zaidi kwenda kwenye mabara mengine kuliko Afrika.

In 2014, there were 1.133 billion international tourist arrivals worldwide, with a growth of 4.3% as compared to 1.087 billion in 2013.[1] The top 10 international tourism destinations in 2014 were

1. France Europe 83.7 million
2. United States North America 74.8 million
3. Spain Europe 65.0 million
4. China Asia 55.6 million
5. Italy Europe 48.6 million
6. Turkey Europe 39.8 million
7. Germany Europe 33.0 million
8. United Kingdom Europe 32.6
9. Russia Europe 29.8 million
10. Mexico North America 29.1

Katika Afrika, Tanzania haipo hata katika 10 bora

In 2014, there were over 55.7 million international tourist arrivals to Africa, the top ten African destinations were
1. Morocco 10.2 million
2. Egypt 9.6 million
3. South Africa 9.5 million
4. Tunisia 6.0 million
5. Algeria — 2.7 million
6. Mozambique — 1.8 million
7. Zimbabwe 1.8 million
8. Kenya — 1.4 million
9. Uganda — 1.2 million
10. Namibia — 1.1 million

Jambo la kusikitisha ni kwamba, nchi inayoongoza kwa kutembelewa na watalii wageni katika Afrika ambayo ni Morocco, idadi ya watalii inaowapokea ni chini ya watalii wanaotembelea nchi ya mwisho ya 10 bora ya Ulaya.

In 2014, there were over 582 million international tourist arrivals to Europe, an increase of 3.0% over 2013. In 2014, the top ten destinations were

1. France 83.7 million
2. Spain 65.0 million
3. Italy 48.6 million
4. Turkey 39.8 million
5. Germany 33.0 million
6. United Kingdom 32.6 million
7. Russia 29.8 million 28.4
8. Austria 25.2 million
9. Greece 22.0 million
10. Poland 16.0 million

Ukija kwenye mapato ya utalii, Tanzania na Afrika si lolote na si chochote. Idadi kubwa ya watalii inawianika kwa kiwango kikubwa na mapato ya utalii. Hayo maneno ya kusema kuwa unaweza kuwa na watalii wachache halafu mapato yakawa makubwa ni ndoto za alinacha zinazootwa na maprofesa wa Tanzania pekee.

International tourism receipts grew to US$1,245 billion in 2014, corresponding to an increase in real terms of 3.7% from 2013.[11] The World Tourism Organization reports the following countries as the top ten tourism earners for the year 2014, with the United States by far the top earner.
1
23px-Flag_of_the_United_States.svg.png
United States North America $177.2 billion
2
23px-Flag_of_Spain.svg.png
Spain Europe $65.2 billion
3
23px-Flag_of_the_People%27s_Republic_of_China.svg.png
China Asia $56.9 billion
4
23px-Flag_of_France.svg.png
France Europe $55.4 billion
5
23px-Flag_of_Macau.svg.png
Macau Asia $50.8 billion
6
23px-Flag_of_Italy.svg.png
Italy Europe $45.5 billion
7
23px-Flag_of_the_United_Kingdom.svg.png
United Kingdom Europe $45.3 billion
8
23px-Flag_of_Germany.svg.png
Germany Europe $43.3 billion
9
23px-Flag_of_Thailand.svg.png
Thailand Asia $38.4 billion
10
23px-Flag_of_Hong_Kong.svg.png
Hong Kong Asia $38.4 billion

Kwa mapato ya utalii wa kimataifa katika Afrika, nchi inayoongoza ni Afrika Kusini ($9.4 billion) ikifuatiwa na Misri ($7.2 billion), Morrocco ($7.1 billion) na Tunisia ($2.3 bilion). Kwa ujumla yule anayeongoza kwa mapato ya utalii katika Afrika hayupo katika 10 bora za Dunia, na ni chini ya mapato ya nchi ya mwisho ya 10 bora katika mabara mengine.

Mapato ya utalii ya Tanzania kwa mwaka 2014 yalikuwa $1.95 billion, chini kuliko mapato ya Singapore ($19.20 billion), Turkey ($37.37 billion), Qatar (10.58 billion) au Misri ($7.21 billion). Singapore, Turkey, Qatar na Misri hawana twiga wala tembo lakini wanatuzidi kwa idadi ya watalii na kimapato mara dufu.

Profesa Maghembe, Rais wetu na Watanzania, wanatakiwa kufahamu kuwa vivutio vya utalii ni zaidi ya idadi ya tembo, fisi, twiga, pundamilia na ngiri tulio nao. Utalii mkubwa ni akili, yaani unaweza kufanya nini kwa kutegemea mazingira yako ili watu wa mataifa mengine waje kushuhudia na kustarehe katika mazingira yako.

Watanzania, kwa ujinga wetu, tunaamini kuwa kwa sababu tu tuna nyumbu wengi, twiga na tembo basi watu wengi, Dunia nzima wanahangaika ili waje watazame sura ya twiga. Watalii hawana haja na sura ya pundamilia wala mbwa mwitu bali wanataka kuona mazingira ya kuvutia yaliyo tofauti na mahali pengine, na sisi tunaweza kuwatumia wanyama hao kuweza kuyafanya mazingira yetu kuwa ya kuvutia zaidi kuliko Misri ambako mapiramidi na chuo kikuu cha kwanza cha Alexandria, vimetosha kuizidi Tanzania kimapato.

Ushauri wangu kwa Rais, fukuza kazi prof. Maghembe maana amekupotosha kwa kueleza kuwa hakuna uhusiano wa mapato katika utalii na idadi ya watalii. Waziri unayetakiwa kuwa naye ni yule ambaye ataihakikishia Tanzania inapata ongezeko kubwa la watalii na siyo upungufu wa watalii. Bila ya kujali kama ongezeko la idadi ya utalii na mapato ya utalii vitategemea kupungua kwa kodi au kuondoa baadhi ya kodi, au kuongeza mbinu za kujitangaza au kuboresha miundombinu na huduma za kitalii, ukweli ni kwamba tunahitaji ongezeko la idadi ya watalii na mapato yatokanayo na utalii ambavyo vinaenda sambamba hata kama siyo kwa uwiano 1:1

Rais Magufuli hatutakuelewa kama pamoja na vyote tulivyo navyo, lakini mapato ya utalii yataendelea kuwa chini kuliko ya Afrika Kusini, Misri, Morocco, Tunisia na Kenya, huku wewe mwenyewe ukisema tuna vivutio vingi vya utalii. Tuna vivutio vya utalii visivyovutia watalii.

Mheshimiwa Rais, hotuba zako za mara kwa mara za kuelezwa nchi hii imeibiwa sana tumekwishazisikia kiasi cha kutosha, sasa tunahitaji kusikia kutoka kwako juu ya mbinu za kuongeza mapato ya utalii (siyo kodi za utalii bali mapato), mbinu za kuongeza mauzo ya mazao yetu nje ya nchi, mkakati wa kujenga uchumi wa viwanda, na namna rasilimali nyingine kama gas na madini zinavyoweza kubadilishwa kuwa mapato ya wananchi na Taifa. Mheshimiwa Rais tunataka mbinu na mikakati ya kuongeza mapato ya Watanzania.

Sisi wengine daima tutazidi kueleza pale tunapoona mbinu siyo sahihi. Tunaamini una dhamira njema lakini tuna mashaka makubwa katika mbinu.

Binadamu tuna miaka michache Duniani, hatuna muda wa kufanya majaribio bali tunatakiwa kuenenda kwa namna na mbinu zilizosahihi katika kuibadilisha nchi hii iliyo maskini kupindukia lakini iliyo na fursa nyingi zilizofunikwa. Fursa ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kitalii ni kubwa sana lakini hatuna watu wa kuweza kufungua fursa hizo ili jamii iweze kuziona kwa sababu waliopewa mamlaka ya kuzifunua kwa umma wanafanya kila mbinu ya kuzifunika ili wananchi wasizione na wala wasizifaidi.

Tufungue macho ndugu yetu na hizo mbinu mpya,naona umejikita kulalamika na kulaumu!
 
Watanzania ni watu wenye bahati mbaya sana maana mara nyingi wanaaminishwa kuwa wao ni bora katika kila kitu. Wengi wao, kwa ujinga tu, nao wameyabeba maneno hayo na kuyaweka katika vichwa vyao.

1.Wapo Watanzania wanaoaminishwa kuwa Tanzania ina dhahabu nyingi kuliko nchi yoyote Duniani, ambao ni uwongo, lakini wao wanaamini

2. Wapo Watanzania wanaoamini kuwa tuna gas nyingi kuliko nchi yoyote, ambao ni uwongo

3. Wapo Watanzania wanaoaminishwa kuwa Tanzania ina madini ya kila namna na ina madini mengi kuliko nchi yoyote Duniani/Afrika, ambao ni uwongo

4. Wapo Watanzania wanaoamini kuwa Tanzania ni nchi yenye amani kuliko nchi zote za Afrika, ambao ni uwongo

5. Wapo Watanzania wanoamini kuwa nchi yetu ina demokrasia, utawala wa sheria na uongozi mzuri kuliko nchi yoyote ya kiafrika, nao ni uwongo lakini wanaamini

6. Wapo Watanzania wanaoaminishwa kuwa Tanzania ni nchi nzuri sana ambayo kila mwanadamu angependa kuja na kuishi, nao ni uwongo lakini wengi wanaamini hivyo

7. Wapo Watanzania wanaoamini kuwa Tanzania ni nchi yenye vivutio vingi na mazingira mazuri ya utalii ambayo hayapo mahali pengine popote Duniani, ambao ni uwongo mkubwa.

Takwimu za mwaka 2014 kuhusu utalii wa kimataifa (International tourist arrivals) inaonesha kuwa hakuna hata nchi moja ya Afrika ambayo ilikuwa miongoni mwa nchi 10 za juu katika kutembelewa na watalii. Hii inaonesha kuwa watalii hawa wa kizungu wanapendelea zaidi kwenda kwenye mabara mengine kuliko Afrika.

In 2014, there were 1.133 billion international tourist arrivals worldwide, with a growth of 4.3% as compared to 1.087 billion in 2013.[1] The top 10 international tourism destinations in 2014 were

1. France Europe 83.7 million
2. United States North America 74.8 million
3. Spain Europe 65.0 million
4. China Asia 55.6 million
5. Italy Europe 48.6 million
6. Turkey Europe 39.8 million
7. Germany Europe 33.0 million
8. United Kingdom Europe 32.6
9. Russia Europe 29.8 million
10. Mexico North America 29.1

Katika Afrika, Tanzania haipo hata katika 10 bora

In 2014, there were over 55.7 million international tourist arrivals to Africa, the top ten African destinations were
1. Morocco 10.2 million
2. Egypt 9.6 million
3. South Africa 9.5 million
4. Tunisia 6.0 million
5. Algeria — 2.7 million
6. Mozambique — 1.8 million
7. Zimbabwe 1.8 million
8. Kenya — 1.4 million
9. Uganda — 1.2 million
10. Namibia — 1.1 million

Jambo la kusikitisha ni kwamba, nchi inayoongoza kwa kutembelewa na watalii wageni katika Afrika ambayo ni Morocco, idadi ya watalii inaowapokea ni chini ya watalii wanaotembelea nchi ya mwisho ya 10 bora ya Ulaya.

In 2014, there were over 582 million international tourist arrivals to Europe, an increase of 3.0% over 2013. In 2014, the top ten destinations were

1. France 83.7 million
2. Spain 65.0 million
3. Italy 48.6 million
4. Turkey 39.8 million
5. Germany 33.0 million
6. United Kingdom 32.6 million
7. Russia 29.8 million 28.4
8. Austria 25.2 million
9. Greece 22.0 million
10. Poland 16.0 million

Ukija kwenye mapato ya utalii, Tanzania na Afrika si lolote na si chochote. Idadi kubwa ya watalii inawianika kwa kiwango kikubwa na mapato ya utalii. Hayo maneno ya kusema kuwa unaweza kuwa na watalii wachache halafu mapato yakawa makubwa ni ndoto za alinacha zinazootwa na maprofesa wa Tanzania pekee.

International tourism receipts grew to US$1,245 billion in 2014, corresponding to an increase in real terms of 3.7% from 2013.[11] The World Tourism Organization reports the following countries as the top ten tourism earners for the year 2014, with the United States by far the top earner.
1
23px-Flag_of_the_United_States.svg.png
United States North America $177.2 billion
2
23px-Flag_of_Spain.svg.png
Spain Europe $65.2 billion
3
23px-Flag_of_the_People%27s_Republic_of_China.svg.png
China Asia $56.9 billion
4
23px-Flag_of_France.svg.png
France Europe $55.4 billion
5
23px-Flag_of_Macau.svg.png
Macau Asia $50.8 billion
6
23px-Flag_of_Italy.svg.png
Italy Europe $45.5 billion
7
23px-Flag_of_the_United_Kingdom.svg.png
United Kingdom Europe $45.3 billion
8
23px-Flag_of_Germany.svg.png
Germany Europe $43.3 billion
9
23px-Flag_of_Thailand.svg.png
Thailand Asia $38.4 billion
10
23px-Flag_of_Hong_Kong.svg.png
Hong Kong Asia $38.4 billion

Kwa mapato ya utalii wa kimataifa katika Afrika, nchi inayoongoza ni Afrika Kusini ($9.4 billion) ikifuatiwa na Misri ($7.2 billion), Morrocco ($7.1 billion) na Tunisia ($2.3 bilion). Kwa ujumla yule anayeongoza kwa mapato ya utalii katika Afrika hayupo katika 10 bora za Dunia, na ni chini ya mapato ya nchi ya mwisho ya 10 bora katika mabara mengine.

Mapato ya utalii ya Tanzania kwa mwaka 2014 yalikuwa $1.95 billion, chini kuliko mapato ya Singapore ($19.20 billion), Turkey ($37.37 billion), Qatar (10.58 billion) au Misri ($7.21 billion). Singapore, Turkey, Qatar na Misri hawana twiga wala tembo lakini wanatuzidi kwa idadi ya watalii na kimapato mara dufu.

Profesa Maghembe, Rais wetu na Watanzania, wanatakiwa kufahamu kuwa vivutio vya utalii ni zaidi ya idadi ya tembo, fisi, twiga, pundamilia na ngiri tulio nao. Utalii mkubwa ni akili, yaani unaweza kufanya nini kwa kutegemea mazingira yako ili watu wa mataifa mengine waje kushuhudia na kustarehe katika mazingira yako.

Watanzania, kwa ujinga wetu, tunaamini kuwa kwa sababu tu tuna nyumbu wengi, twiga na tembo basi watu wengi, Dunia nzima wanahangaika ili waje watazame sura ya twiga. Watalii hawana haja na sura ya pundamilia wala mbwa mwitu bali wanataka kuona mazingira ya kuvutia yaliyo tofauti na mahali pengine, na sisi tunaweza kuwatumia wanyama hao kuweza kuyafanya mazingira yetu kuwa ya kuvutia zaidi kuliko Misri ambako mapiramidi na chuo kikuu cha kwanza cha Alexandria, vimetosha kuizidi Tanzania kimapato.

Ushauri wangu kwa Rais, fukuza kazi prof. Maghembe maana amekupotosha kwa kueleza kuwa hakuna uhusiano wa mapato katika utalii na idadi ya watalii. Waziri unayetakiwa kuwa naye ni yule ambaye ataihakikishia Tanzania inapata ongezeko kubwa la watalii na siyo upungufu wa watalii. Bila ya kujali kama ongezeko la idadi ya utalii na mapato ya utalii vitategemea kupungua kwa kodi au kuondoa baadhi ya kodi, au kuongeza mbinu za kujitangaza au kuboresha miundombinu na huduma za kitalii, ukweli ni kwamba tunahitaji ongezeko la idadi ya watalii na mapato yatokanayo na utalii ambavyo vinaenda sambamba hata kama siyo kwa uwiano 1:1

Rais Magufuli hatutakuelewa kama pamoja na vyote tulivyo navyo, lakini mapato ya utalii yataendelea kuwa chini kuliko ya Afrika Kusini, Misri, Morocco, Tunisia na Kenya, huku wewe mwenyewe ukisema tuna vivutio vingi vya utalii. Tuna vivutio vya utalii visivyovutia watalii.

Mheshimiwa Rais, hotuba zako za mara kwa mara za kuelezwa nchi hii imeibiwa sana tumekwishazisikia kiasi cha kutosha, sasa tunahitaji kusikia kutoka kwako juu ya mbinu za kuongeza mapato ya utalii (siyo kodi za utalii bali mapato), mbinu za kuongeza mauzo ya mazao yetu nje ya nchi, mkakati wa kujenga uchumi wa viwanda, na namna rasilimali nyingine kama gas na madini zinavyoweza kubadilishwa kuwa mapato ya wananchi na Taifa. Mheshimiwa Rais tunataka mbinu na mikakati ya kuongeza mapato ya Watanzania.

Sisi wengine daima tutazidi kueleza pale tunapoona mbinu siyo sahihi. Tunaamini una dhamira njema lakini tuna mashaka makubwa katika mbinu.

Binadamu tuna miaka michache Duniani, hatuna muda wa kufanya majaribio bali tunatakiwa kuenenda kwa namna na mbinu zilizosahihi katika kuibadilisha nchi hii iliyo maskini kupindukia lakini iliyo na fursa nyingi zilizofunikwa. Fursa ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kitalii ni kubwa sana lakini hatuna watu wa kuweza kufungua fursa hizo ili jamii iweze kuziona kwa sababu waliopewa mamlaka ya kuzifunua kwa umma wanafanya kila mbinu ya kuzifunika ili wananchi wasizione na wala wasizifaidi.
Una mawazo mazuri lakini sijaona pale unapoleta suluhisho nini kifanyike bali umelalamika tu kama ilivyokawaida ya watanzania wengi ni hodari kwa kulalamika lkn wavivu kutoa suluhisho
 
Una mawazo mazuri lakini sijaona pale unapoleta suluhisho nini kifanyike bali umelalamika tu kama ilivyokawaida ya watanzania wengi ni hodari kwa kulalamika lkn wavivu kutoa suluhisho
Cha kufanya tutumie vizuri hicho kidogo tulicho nacho na tusijione kwamba sisi ni special sana kwamba tutabembelezwa na mataifa mengine.
 
Mkuu umenena ukweli mtupu.vivutio vingi vya utalii bila maarifa ni bure.hao viongozi hasa hiki kitengo cha utalii hawajui wanachofanya.hivi wanafikiri hao watalii matajiri watamiminika kuja tz katika mazingira haya ya sasa?waanze kufikiria kuwapata kwanza hawa watalii wa kawaida ambao ni wanunuz wa vinyago.nguo zetu za kitamaduni na ambao watahitaji vyumba vingi vya mahotelini na mwishowe watanufaisha wananchi wengi.fikiria idadi ya watu wataohitajika kutoa hizo huduma na bidhaa kwa hao watalii wa kawaida. Eti waziri anawaita maskini!
 
Kaka una akili sana, sio mpenzi wa uandishi wa Watanzania wengi kwani umekaa kishabiki.

Lakini ume'analyse obejectively with data and figures na zaidi umeenda mbali kwa kutoa solution nini kifanyike.

Asante sana mkuu you have made me proud kwamba kuna watanzania wachache bado wana akili.
 
Ungekuja na solutions siyo lawama mwanzo mwisho
 
Mkuu hongera kwa analysis yako na facts kuhusu utalii na siasa za bongo...respect mkuu. Nilipopata hotuba ya Rais akiongelea watalii na mapata....nilichoona ni kuwa Rais Kilaza, Worst president ever kwenye historia ya Tanzania. Lazima hatua za madhubuti zichukuliwe ili kuboresha sector ya utalii nchini ikiwa ni pamoja na kujenga ushawishi ili watalii waweze kuja. I guess tutakuja kuwa na hali mbaya ya kiuchumi huko mbeleni....
 
Hongera sana kwa kutoa data zinazoeleweka.

Acha watu waendelee kusema watakuja tu. Tunataka mabilionea waje sisi hatuna haja na vitalii visivyo na hela? 🙁Tushapoteza ramani kitambo,, na mbaya zaidi tulipotokea hata hatukuweka alama. Sijui hili treni linaenda kusimamia wapi lilishatoka kwenye rail siku nyingi linajiendesha tu, Mungu tu atunusuru...
 
Sawa! Lakini ata tukiwa wa mwisho wapo watu watakuja kitushangaa kwanini tu wajinga wa mwisho, hao sasa ndio tunataka waje walipe VAT, ata kama wawili. Waliobaki waende kunakovutia wakakwepe kodi!!.
 
Wewe mwenyewe umeshahamasishwa kujichukia nani atakupenda,na umeshavaa upofu wa kutokutaka kuona vyako nani ataviona,tunakosoa sana hatuonyeshi njia mbadala!
 
Ila ukiwaza sana unaona kama tuna shida mahali, vivutio vyenyewe vilivyopo havijatangazwa, na havijulikani hata.

Jana amefariki Mtalii akiwa Mlima Kilimanjaro, ma- reporter waliopo nje wamedai amafariki mtalii akiwa ANAPANDA MLIMA KILIMANJARO ULIOPO KENYA😀😀😀😀

Nimecheka hadi mbavu zaniuma

Na bado tunajitapa kuwa sisi hatuhitaji vitalii visivyo na hela tunahitaji mabilionea. Vivutio vyenyewe hata kufahamika havifahamiki...Ama kweli tunahitaji maombi...🙁
 
Hongera sana Msambichaka Mkinga....hakika wewe ni great thinker.

Umeandika Mada nzito kwa uchambuzi wa Maana.. Sasa wapo wavivu wa kufikiri....watachangia kwa mihemko wa kisiasa.

Natoa wito wa Waandishi wa Habari wa ITV, Guardian, Nipashe, The Citizen, Mwananchi waandike hii Mada

Please News paper rooms
 
Una mawazo mazuri lakini sijaona pale unapoleta suluhisho nini kifanyike bali umelalamika tu kama ilivyokawaida ya watanzania wengi ni hodari kwa kulalamika lkn wavivu kutoa suluhisho

Ukifuatilia kwa umakini, utaona nimetoa mapendekezo. Pendekezo kubwa ni kwa wahusika wa sekta kutambua kuwa utalii ni biashara, hivyo zinahitajika mbinu za kuboresha mazingira ya biashara hii ili yavutie watalii. Mazingira yetu yaonekane ni tofauti na ya sehemu nyingine kwa ubora kwa kutumia kile ambacho wengine hawana. Na hapo ndipo akili na werevu unapohitajika ili kujua ni nini na kwa namna gani tunaweza kufanya. Tusiamini kwa vile tu tuna pundamilia au twiga, eti kwa sababu tu hawapo sehemu nyingine, basi kila mtu atakuja kwetu au anataka kuja Tanzania. Utalii ni starehe, ni lazima uandamane na starehe. Ni namna gani utalii wetu unaweza kuwa unique na kuandamana na starehe? Haya ni mambo ambayo watendaji wa sekta hii wanatakiwa kuyafanyia kazi. Sisi kama wadau tuliopo nje, ushauri tunaotoa ni wa jumla, na wao wanatakiwa kuingia ndani zaidi kuyafanyia kazi mawazo yetu ili yaweze kuonekana katika uhalisia.
 
Back
Top Bottom