Rais Samia umeandika historia kubwa

Nonsense
Mmemgeuza Mungu ni wa utani ama?
Go ask your Granny akili ikae sawa khe
Kusifu na kuabudu mtu mnakera kwa ufupi
Pesa ni za walipa kodi sio mali ya Mtawala
Kujua kwa uchumi ni juhudi za wananchi
Watawala wanagawa pesa kama njugu bila kupitishwa na Bunge
Uchumi upo shimoni upo hapa nyenyenye
Unaongea blablabla tu ...huna points . Kanywe maji kwanza upunguze jazba alafu njoo usome tena uzi
 
Huyu mama kajitahidi kwa kipindi kifupi mno, na sasa hivi biashara zimeanza kurudi kwa kasi ya 5g pita mtaani ujionee, kutoa kibali Cha ajira nyingi, kulipa wakandarasi hela zao baada ya mda mrefu, pia kuhusu Hilo la bodi ya mikopo Rais katuokoa wengi Deni lilikuwa haliishi Hilo mpaka tustaafu aisee.
Nadhani mama tumuongezee mitano mingine Mimi kanifuraisha sana
Hamna kitu kesi ya Mbowe imeondoa mazuri yake Kama yapo
 
Unaelewa maana janga?Janga ni kitu ambacho binadamu hawezi kukicontroll kwa uhakika.Sisi tunamtaka Rais wa uhakika.Hatumtaki Rais wa mchongo
Kumbe Alivyosema ni janga basi yupo sahihi kwa jinsi ulivyotafsiri hapo. Urais umemfuata ni kitu haja control.

Rais wa uhakika ndio yupi ? Mbowe au lissu ? Chama chenu tu kimewashinda mtaiweza nchi .
Wamekua wabunge wameleta maajabu gani majimboni kwao au ndio mpaka wawe marais. Hao ni wapiganiaji matumbo yao tu harakati nyingi hawana lolote.

Hivi mama samia utamfananisha na hao watu wasioeleweka ndumila kuwili . Walimtakasa lowassa waliesema ni fisadi mkubwa na hafai kuwa rais ili mradi tu wapate ulaji hahaha ila mchongo ukabuma.
Sasa Kumbe wote mnapiga michongo kelele za nini ? Wote wapiga michongo tu tofauti rangi za nguo.

Kwasasa rais ni mmoja tu samia suluhu Hassan full stop.
Tukutane 2025 Kwenye majukwaa.
 
Rais wa uhakika ndio yupi ? Mbowe au lissu ? Chama chenu tu kimewashinda mtaiweza nchi .
Wamekua wabunge wameleta maajabu gani majimboni kwao au ndio mpaka wawe marais. Hao ni wapiganiaji matumbo yao tu harakati nyingi hawana lolote.

Hivi mama samia utamfananisha na hao watu wasioeleweka ndumila kuwili . Walimtakasa lowassa waliesema ni fisadi mkubwa na hafai kuwa rais ili mradi tu wapate ulaji hahaha ila mchongo ukabuma.
Sasa Kumbe wote mnapiga michongo kelele za nini ? Wote wapiga michongo tu tofauti rangi za nguo.

Kwasasa rais ni samia suluhu Hassan full stop.
Nashukuru kuwa umeelewa maana ya janga na kuwa Chief Hangaya ni Kibaka aliepora chaguzi ambae hana kibali cha wananchi.Hakubaliki Duniani wala mbinguni.
 
Hana lolote , alikua wapi siku zote. Mbona hakufurukuta kwa jiwe. Kwahiyo mama kuwapa uhuru wa kuongea imekua makosa.

Wanajaribu kumtikisa na kumchokoza mama ili wakishushiwa kitu kizito wapate lingine la kupigia debe .
Mama asikubali kutolewa kwenye reli, aendelee ku focus kwenye mipango na maendeleo ya nchi.

Halafu mwingira huwa hawapendi kabisa waislamu sijui kwanini ? Namjua vizuri Sana. Haya yote kusema ikulu Kuna shetani ni kwasababu rais ni muislamu. Hata kipindi cha kikwete alikua anamponda Sana madhabahuni. Na kuupondea uislamu. Kwahiyo kwa hili hata sijashangaa.
unachekesha, huyo maza hausi kishatoka kitambo kwenye reli, yupo mtaloni akiweweseka pasina kujua chakufanya, inshort nchi ishamshinda kitambo.
 
Moja ya jukumu la msingi kabisa la makamu wa Rais ni kujiandaa kuwa Rais kwa sababu Rais siyo Mungu na anaweza kufa muda wowote ule.

Samia hakujiandaa kuwa Rais kwa sababu hakujua majukumu yake kama makamu wa Rais.

Mtu ambae hakujua majukumu yake kama makamu wa Rais hawezi kujua majukumu yake kama Rais kwa hiyo hafai kuwa Rais.
Hakujiandaa kuwa rais = Hakutarajia kuwa rais / Hakupanga kuwa rais.
Sababu ni jambo halijawahi kutokea au hakuwahi kuwazia.
Tofautisha na siwezi kuwa rais. / Siwezi majukumu ya urais.
Upo ?
 
Nashukuru kuwa umeelewa maana ya janga na kuwa Chief Hangaya ni Kibaka aliepora chaguzi ambae hana kibali cha wananchi.Hakubaliki Duniani wala mbinguni.
Hahahaha ...ona Sasa nishakupoteza unaanza kupanick Kama kawaida yenu . Kumbe huna hoja ila basi tu chuki binafsi na husda zinawatesa.
 
unachekesha, huyo maza hausi kishatoka kitambo kwenye reli, yupo mtaloni akiweweseka pasina kujua chakufanya, inshort nchi ishamshinda kitambo.
Hebu sema in details ueleweke. Kwenye jambo gani na kuhusu nini ? Mipasho na chuki haitawasadia.

Tumsapoti , tumshauri, tumuombee mama, bahati Nzuri ni msikivu na ana jitihada.
 
Mwaka 2021 ni mwaka wa kipekee sana katika historia ya JMT, nchi yetu ilipita katika mtihani mgumu ambao utakumbukwa vizazi na vizazi vijavyo. Kuondokewa na Rais aliyepo madarakani lilikuwa pigo kubwa.

Watanzania tunazo sababu nyingi za kumshukuru Mungu kwa kutuvusha salama na zaidi kwa kujaaliwa kiongozi mwingine mwenye uzalendo, uwezo, na karama isiyo na kifani katika uongozi wa kisiasa ambaye ni Rais Samia Suluhu Hassan.

Baadhi ya mambo yaliyofanywa katika kipindi kifupi sana na Rais Samia;

1. Kuimarisha Uchumi- Ukuaji wa pato la taifa katika robo ya pili mwaka 2021, uchumi uliongezeka kufikia 4.3%, ukilinganisha na 4% mwaka jana. Mfumuko wa bei umeweza kudhibitiwa huku akiba ya fedha za kigeni ikiongezeka zaidi.

2. Kuchochea Biashara- Maboresho ya sheria na miongozo mbalimbali yamefanyika na hivyo kuvutia wawekezaji kutoka katika kila pembe ya Dunia huku uuzaji wa bidhaa (Export) ukiongezeka mara dufu.

3. Kukuza Utalii na kuitangaza nchi yetu - Katika hili Mhe. Rais ameweka rekodi ya aina yake hususani katika program maalum ya "ROYAL TOUR " ambayo inasubiriwa kwa hamu kubwa na wadau wa utalii Duniani kote.

4. Kuendeleza miradi ya kimkakati- Mhe. Rais katika hili ameonyesha umahiri na uwezo mkubwa ambapo mpaka sasa miradi yote inaendelea kama ilivyopangwa huku miradi kama SGR ya Mwanza - Isaka ikitengewa zaidi ya Trilioni 1 kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati.

5. Kuimarisha Sekta ya Kilimo na Ufugaji- Rais Samia ametatua changamoto nyingi za wakulima na kufungua masoko ndani na nje ya nchi ili kuhakikisha wakulima wanafaidika na shughuli zao. Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko, zilipatiwa zaidi ya Bilioni 129 kununua mazao ya wakulima.

6. Kukuza Diplomasia- Rais Samia ameirudisha nafasi ya Tanzania katika mawanda ya diplomasia za kikanda na kimataifa ikiwemo kushirikiana na mataifa mengine kukabiliana na janga la Corona kwa njia za pamoja, uamuzi huu umekuwa wenye manufaa makubwa.

7. Kuboresha huduma za jamii- Rais Samia amefanya makubwa kuhakikisha huduma za Afya, maji, elimu, umeme na miundombinu zinaboreshwa kila uchao. Hivi sasa tunatarajia hapo mwakani kila mwanafunzi aliye faulu darasa la saba aanze shule moja kwa moja.

8. Kuboresha sekta ya madini- Katika sekta hii Mh.Rais amewezesha utoaji wa leseni takribani 7968, huku viwanda vya uchakataji madini vikiendelea kujengwa na sekta hii ikichangia pato la Taifa kwa takribani 7.7%. Juhudi hizi ni kubwa.

9. Kuhakikisha Amani na Usalama- Kama Amiri Jeshi Mkuu, Rais Samia ameweza kusimamia vema amani na usalama wa nchi yetu licha ya hali tete kwa baadhi ya nchi jirani, umakini na uongozi wake thabiti ndio sababu ya mafanikio haya.

10. *Ajira na fursa kwa watumishi- Rais Samia ametoa vibali vingi vya ajira serikalini, ametoa fedha za malimbikizo ya madeni kwa watumishi, vibali vya kupandisha madaraja kwa wenye sifa na zaidi ameondoa tozo (VRF) 6%kwa watumishi ambao ni wanufaika wa fedha za Bodi ya mikopo (HESLB).

Tukiwa mwishoni mwa mwaka, nitoe rai yangu kwa viongozi wote wa dini na watanzania wote kwa ujumla kumuombea heri Rais wetu, kujiombea heri sisi wenyewe na nchi yetu kwa ujumla ili tuendelee kufurahia ustawi wa nchi yetu.
Umesahau kuweka namba yako ya simu kwa mawaziliano ya uteuzi wako kuwa DC.
 
Safi sana Dadake umeongea pwointi ujue

Umesahau wastaafu wanalipwa fedha zao walizokopwa na serikali, bila yeye sijui wangepata miaka gani ?

Lakini Mambo yote hayo hawayaoni , wamekazana na kesi ya mbowe tu ndio wanaona cha maana sana Mtu yuko mahakamani Kama ni haki yake atapewa tu bahati Nzuri mama Ni mtu wa haki.

Watu wame-base kwenye maudhi madogo madogo Kama vitu kupanda bei n.k Mimi naamini mambo yata settle tu Kila kitu kitakua poa . Cha Muhimu hapa tuangalie Nia ya dhati ya rais ikoje.
Duh kumbe na wastaafu wameanza kulipwa hela zao aisee, Mungu atupe nini Sasa, hao wanaohangaika na kesi na kumchafua hamnazo wako na masilahi Yao binafsi Rais anajitahidi sana imagine sikuhizi kukamatwa kamatwa hovyo kisa uchochezi kimeisha na bado watu hawana shukrani wao ni kulalamika tu ka wachawi, kipindi kikwete alipokuwa fair aliporuhusu democrasia itamalaki walimushambulia kuwa dhaifu wakawa wanasema wanataka Rais dictator akaja Magufuli akawanyoosha kila kiumbe kuanzia ccm Hadi upinzani na Raia.
In short watanzania hatujui tunataka nini na haya malalamiko na kutokuwa na shukrani na kulalamika hufanya viongozi wawe wakatili
 
Hakujiandaa kuwa rais = Hakutarajia kuwa rais / Hakupanga kuwa rais.
Sababu ni jambo halijawahi kutokea au hakuwahi kuwazia.
Tofautisha na siwezi kuwa rais. / Siwezi majukumu ya urais.
Upo ?
Hakujiandaa kuwa Rais siyo sawasawa na kutokutarajia kuwa Rais.Hakujiandaa kuwa Rais maana yake ni kwamba lile jukumu lake la msingi la kujitayarisha kuwa Rais alipokuwa makamu wa Rais hakulitekeleza.

Na jukumu hilo ni kujifunza kuwa Rais.Hakujiandaa kuwa Rais maana yake ni kwamba hakujifunza kuwa Rais

Kujiandaa/Kujitayarisha kuwa Rais ina maana pana na muhimu kwa makamu wa Rais.Hii inajumuisha kuijua katiba ya nchi,kujua diplomasia yetu ya kimataifa,kujua misingi ya uchumi wetu,kujua misingi ya demokradia yetu,kujua majukumu yote yanayamuhusu Rais,kujua mipaka ya nchi yetu na kadhalika na kadhalika.

Kwa Samia kutokujiandaa kuwa Rais maana yake ni kwamba hakujifunza yote hayo na kwa hiyo hafai kuwa Rais wetu.
 
Back
Top Bottom