Ningekuwa Mimi lakini, Kuna vitu sensitive nisingekuwa navitolea maelezo au kufanya jitihada vieleweke kwa urahisi...
Maana kuna msemo wa washenga kuwa kama umekosea au hauko sawa na unahitaji kueleweka.... JITAHIDI KUEPEUKA KUJIELEZEA ELEZEA AU KUTENGENEZA EXPLANATION kwasababu utaharibu zaidi
Maana navyokumbuka mama yangu wa kunizaa wakati anatoa maelezo siku ya kukalia kiti alichokipata, kwa maelezo yake alidai wale watoto hawakuwa wa Taifa teule na ndio maana hakukua na haja ya kuwapa pole kwa yaliyotokea.... Paap week moja baadae, Mama yangu akaunda Kamati ya kutatua na kufuatilia mienendo ya kilichotokea paap Ikatolewa POLE kwa waliokumbwa na madhira... Natafakari vingi, ngoja nikikaa naye Jioni nitaomba niwe naandika Mimi maelezo kwenye karatasi ili kupunguza mama yangu asiendelee kujikanganya...
Hello Tanzania..
See you 🤗
Tuonane tena 2026, February.. tukipewa uzima na Afya
Wazee wangu wa Diaspora tukutane huko majuu