Rais Samia Suluhu imulike NHIF

Rais Samia Suluhu imulike NHIF

"Mwanachama anapoenda kupata huduma za kiafya sehemu husika kuna huduma anazozipata hazilingani kabisa na gharama NHIF itakazolipa kwa mtoa huduma. Yaani hapa mgonjwa Mwanachama wa NHIF anaweza tibiwa kwa gharama anazoweza kuziona labda Tsh 9000. Lakini kinachopelekwa NHIF ni tofauti na hiyo gharama aliyoiona mteja".

Hii kwa sasa ni ngumu kidogo kwa sababu: kwa sasa ukitibiwa mgonjwa wa NHIF taarifa za gharama zilizotumwa NHIF kwenye mfumo zinakwenda pia moja kwa moja kwa aliyepewa huduma.

Hivyo, uliyepewa huduma, una nafasi ya kuwajulisha NHIF kuwa huduma uliyopewa si ya kiasi kilichopelekwa kwao/NHIF.
Labda kama teknolojia haijafika huko.
Huduma hii ipo kwenye hospital chache sana, nyingi bado hazijafikiwa na hii
 
Huu mfuko unatakiwa uvunjwe haraka
Alafu ukishavunjwa?.Toa ufumbuzi wanini kifanyike sio kusema uvunjwe tu.maana huo mfuko bsdo ni msaada kwa wananchi wengi kwahiyo kama kuna mapungufu ni jukumu la wadau kuyazungumza na wahusika kuyafanyia kazi.
 
Huu mfuko lengo lilikuwa nzuri lakini baadae serikali ya awamu ya mwendazake ilianza kutumia pesa hizi kama chanzo cha mapato hivyo kuharibu kabisa mfumo wa matibabu.
 
Mkuu Hapo kwenye Wanafaika una hoja ,ila tatizo lilianza pale Waswahili tulipoanza ujanja 2,ili.kuepuka hayo wewe kachikue Cheri Cha Ndoa!
Gharama take sio kubwa ...by the way ,kama mna ndoa yenye amani na utulivu na mlofunga Kimila!
Serikali ikikuambia katafute Cheti kuna shida Gani...haiathiri chochote!
Kimyume chake ,Kuna kitu ndani ya hiyo Ndoa ya Kimila unakificha[emoji2958]
Hata ya kimila wanatoa cheti,alafu unataka wakupe kadi bila cheti hivi inaingia akilini kweli?nani anauhakika umeoa bila kuwepo na document,je kama ni hawara yako nawe ukasema ni mke wangu?
 
Alafu ukishavunjwa?.Toa ufumbuzi wanini kifanyike sio kusema uvunjwe tu.maana huo mfuko bsdo ni msaada kwa wananchi wengi kwahiyo kama kuna mapungufu ni jukumu la wadau kuyazungumza na wahusika kuyafanyia kazi.
Mapungufu yamezungumzwa miaka yote lakini hakuna kinachobadilika zaidi ya upigaji, bora ku-outsource
 
Hata ya kimila wanatoa cheti,alafu unataka wakupe kadi bila cheti hivi inaingia akilini kweli?nani anauhakika umeoa bila kuwepo na document,je kama ni hawara yako nawe ukasema ni mke wangu?
Hiyo bima unapewa sio kama msaada kuna hela ambayo unakatwa ili kucover hizo gharama za matibabu mchangiaji ndio mwenye mandate ya kuamua amuweke nani huo urasimu wa kuzuia mtu asimweke anayemtaka unatokana na sababu zipi zenye mashiko mbali na kuhofia kupungua kwa kibubu chao ambacho obviously kujaa kwake kumetokana na michango ya mchangiaji.Kama ni sheria au kanuni lazima ifanyiwe amendment
 
Kitu kingine cha ajabu kwa huo mfuko ni pale unapotaka kumuweka mnufaika ambaye lazima awe mzazi au mtoto na uweke cheti cha kuzaliwa.

Kwa upande wa watoto sina tatizo shida upande wa wazazi lazima awe mzazi wako na cheti chako cha kuzaliwa kidhihirishe hivyo je kwa wale ambao walisomeshwa na ndugu wanapokosa fursa hiyo ya kupatiwa kadi watakuwa wanatendewa haki?

Maskini wa Mungu utakuta mchangiaji alishafiwa na wazazi zamani na waliomsomesha ni hao wanaokatatazwa kwa sheria za NHIF kugharamiwa matibabu na mfuko
 
Hakuna kitu kinakera,kinaumiza wachangiaji kama hiki hasa unapofika hosptali na kuambiwa gharama fulani hazilipiwi na BIMA.
Mbaya zaidi unapofika hosptali gharama ulizotumia Kwenye form ya BIMA huzioni kwa ujumla ni wizi mtupu juu ya wizi.Serikali itupie macho huku.
Ushauri form za matibabu tunazotibiwa zionyeshe malipo ya huduma mchangiaji anayopewa.Pili huduma zisiwe za kubagua bagua.pili BIMA inapotumika mchangiaji atumiwe sms kuonyesha gharama alizotumia badala ya kutishia kutuma sms ya kuonyesha kadi ya BIMA imetumika
Kwa Sasa gharama ulizotumia.... Zinatumwa.
 
  1. Unakwenda kituo cha afya/hospital unaambiwa kipimo cha typhoid kinalipiwa bima hailipi.
  2. Una malaria wanakuambia uwezo wa bima ni kulipia mseto dawa zingine hazimo, kama mgonjwa una aleji na mseto basi hizo zinazokuponya nenda kanunue
  3. Ukiwa na UTI, unachaguliwa dawa, ukiwa na dawa zinakudhuru basi hizo mbadala kanunue
  4. Ukilazwa unaambiwa baadhi ya huduma unajazia pesa bima hailipi
  5. Wanachama tunaumia sana mioyo tunapoona maafisa wa hiyo bima wanajilipa mishahara mikubwa huku huduma zikiwa hafifu, wanatembelea magari ya bei kubwa badala ya kuboresha huduma.
  6. Ushauri ni kwamba michango ya wanachama iingizwe kwenye akaunti maalumu ya matibabu na mwanachama apewe electronic card ili akifika hospital deductions zifanyike kwenye card na hivyo mgonjwa atapata dawa zinazomfaa badala ya kupangiwa dawa zisizomfaa mwisho wa siku anaingia gharama kuzinunua huku akiwa amekatwa michango yake
Kuna wakati mtu unaamua uingie tu mfukoni kutibiwa kuliko kutegemea hiyo bima.
 
Kitu kingine cha ajabu kwa huo mfuko ni pale unapotaka kumuweka mnufaika ambaye lazima awe mzazi au mtoto na uweke cheti cha kuzaliwa .Kwa upande wa watoto sina tatizo shida upande wa wazazi lazima awe mzazi wako na cheti chako cha kuzaliwa kidhihirishe hivyo je kwa wale ambao walisomeshwa na ndugu wanapokosa fursa hiyo ya kupatiwa kadi watakuwa wanatendewa haki?Maskini wa Mungu utakuta mchangiaji alishafiwa na wazazi zamani na waliomsomesha ni hao wanaokatatazwa kwa sheria za NHIF kugharamiwa matibabu na mfuko
Hapa ndio penye shida ,sijui waliwaza nini
 
NHIFTZ

Naomba kufahanu mfuko ulitumia kigezo Gani kuwaondoa ndugu wengine kama waanaufaika!

Katika jamii zetu Kuna watu walifiwa na wazaI wakatunzwa na ndugu wengine ...kama wazazi ,Sasa Kuna ubaya gani mtu huyu akimwingiza huui mlezi wake kuwa mnufaika!

Kiafrika kusomesha au kumtunza mtoto ni uwekezaji, no kama hifadhi ya Jamii isiyo Rasmi ,iqeje Mfuko usitambue hili!

Au kwa kudura ya Mnyazi Mungu Mwanachama hakubahatika kupata m/watoto Kuna ubaya Gani akawaingiza ndugu wengine...ambapo pia atajuwaa anatanua WiGo was Hifadhi ya Jamiikatika Afya Kwa familia yake?!

Naomba ufafanuzi ktk hili!
 
Nao
Naomba kufahanu mfuko ulitumia kigezo Gani kuwaondoa ndugu wengine kama waanaufaika!
Katika jamii zetu Kuna watu walifiwa na wazaI wakatunzwa na ndugu wengine ...kama wazazi ,Sasa Kuna ubaya gani mtu huyu akimwingiza huui mlezi wake kuwa mnufaika!
Kiafrika kusomesha au kumtunza mtoto ni uwekezaji, no kama hifadhi ya Jamii isiyo Rasmi ,iqeje Mfuko usitambue hili!
Au kwa kudura ya Mnyazi Mungu Mwanachama hakubahatika kupata m/watoto Kuna ubaya Gani akawaingiza ndugu wengine...ambapo pia atajuwaa anatanua WiGo was Hifadhi ya Jamiikatika Afya Kwa familia yake?!
Naomba ufafanuzi ktk hili!
NHIF Ina maana hujauona huu mchango😣
 
Hawa watu wa NHIF wana mambo ya hovyo sana unaenda hospitali nzuri inafika wakati wa dawa dr kufanya prescription analazimisha dawa flani

, Kuna siri nliipata kua kama una NHIF na unastahili dawa fulani hasa za nje ya tz Dr anakuambia tu hiyo hapa hatuna ili usilalamike kumbe ni vile miongozo ya bima inazuia maana ina “bei” !
 
  1. Unakwenda kituo cha afya/hospital unaambiwa kipimo cha typhoid kinalipiwa bima hailipi.
  2. Una malaria wanakuambia uwezo wa bima ni kulipia mseto dawa zingine hazimo, kama mgonjwa una aleji na mseto basi hizo zinazokuponya nenda kanunue
  3. Ukiwa na UTI, unachaguliwa dawa, ukiwa na dawa zinakudhuru basi hizo mbadala kanunue
  4. Ukilazwa unaambiwa baadhi ya huduma unajazia pesa bima hailipi
  5. Wanachama tunaumia sana mioyo tunapoona maafisa wa hiyo bima wanajilipa mishahara mikubwa huku huduma zikiwa hafifu, wanatembelea magari ya bei kubwa badala ya kuboresha huduma.
  6. Ushauri ni kwamba michango ya wanachama iingizwe kwenye akaunti maalumu ya matibabu na mwanachama apewe electronic card ili akifika hospital deductions zifanyike kwenye card na hivyo mgonjwa atapata dawa zinazomfaa badala ya kupangiwa dawa zisizomfaa mwisho wa siku anaingia gharama kuzinunua huku akiwa amekatwa michango yake
Umeandika kishabiki vitu vingi ulivyoandika si vya kweli
 
Hospital ya Ben Mkapa kila huduma unayopewa na gharama ipo kwenye risiti na hata msg ikija kwenye simu inakuja na jumla ya gharama ulizotumia
NHIF walazimishe Hospital iandike gharama za biadhaa ma huduma zao. Bei iandikwe Mapokezi, kwenye fomu na ukiondoka upewe risiti ya huduma na bidhaa husika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimekuwa mdau muhimu kwenye hii taasisi inayojihusisha na huduma muhimu za Afya yetu watanzania. Kuna mengi yamejificha nyuma ya pazia inayopelekea hii NHIF kuwa chaka la kupiga fedha za Serikali,nikimaanisha michango ya wanachana kuwa ni pombe ya ngomani kila mmoja anajichotea tu.

Kuna malalamiko mengi yanayojitokeza kati wa Mwanachama mchangiaji anapopata huduma,Mfuko wenyewe NHIF kama mlipaji, na watoa huruma. Huu ni utatu mchafu.

Mwanachama anapoenda kupata huduma za kiafya sehemu husika kuna huduma anazozipata hazilingani kabisa na gharama NHIF itakazolipa kwa mtoa huduma. Yaani hapa mgonjwa Mwanachama wa NHIF anaweza tibiwa kwa gharama anazoweza kuziona labda Tsh 9000. Lakini kinachopelekwa NHIF ni tofauti na hiyo gharama aliyoiona mteja.

Mtoa huduma naye akishapeleka hizo gharama zake alizozitoa kwa huyu Mwanachama wa NHIF,sizo atakazolipwa na NHIF.

Huyu anaweza kupeleka madai ya Tsh 9000 ile na akalipwa Tsh 6000 kama si 5000. Na NHIF hutoa sababu mbalimbali za hayo makato ikiwa ni pamoja na Mdai kuambia kuwa kuna dawa au vipimo kavitoa kimakosa au bila usahihi

Mtoa huduma akirudi kwenye mwongozo unaomtaka ahudumieje,anakuta yuko sahihi kabisa.

Sasa hapa ndipo tatizo linapoanzia, Mtoa huduma anajikuta anaingia kwenye ukurasa mwingine wa kujaza form tofauti na aliyoitoa kwa Mteja aliyemtibu na kujaza nyingine yenye gharama za juu ili kufidia hayo makato yasiyo na tija wayafanyayo NHIF. Wizi unaanzia hapa.

NHIF naye anapopelekewa hizo gharama zisizo sahihi kama kawaida yake atakata anavyojisikia na kurejesha kwa mtoa huduma anachoona kinamfaa.

Huko NHIF haijulikani kama wanavyompa mtoa huduma ndivyo vinavyokuwa sahihi na kwao!!!!? Hilo ni jambo la huko. Nako kwa kumulika.

Huu utatu mchafu unamuumiza zaidi huyu mchangiaji maana hii sio NSSF ambako atakuja kupigiana hesabu na mwajili apate chake sahihi.

Ushauri
NHIF ikiwezekana wajenge vituo vyao vya kutolea huduma hizi kwa wanachama wao ili kusiwe na hili la Mwanachama kupata huduma zisizoendana na uhalisia wa alichohudumiwa maana imekuwa ni tatizo kwelikweli.

Kama wanakusanya michango ya kutosha isiyo na rejesho kwa Mwanachama.,Basi wanao uwezo wa kujenga vituo na wanachama tukapata huduma sahihi kwao kuliko tunayofanyiwa huku walikotoa tenda za kutibiwa ambako ni upigaji mwanzo mwisho.

Wanaajiri Madaktari na kuwezesha kukopesha vituo vya kutolea huduma hivyo wanaweza kuyafanya haya yoote wao wenyewe NHIF. Waige kwa NSSF nk wanaojiwekezea kwenye miradi mingi kwa manufaa ya mfuko na wanachama wao.
Landcruiser ndo mpango mzima
 
Umeandika kishabiki vitu vingi ulivyoandika si vya kweli
Yawezekana wewe ni NHIF, nakushauri wewe na timu yako mwende mkakutane na watumiaji wa NHIF msikie live dukuduku zao dhidi yenu, itisheni mikutano na wadau wawaambie wanayokutana nayo huko mahospitalini, msijifungie vyumbani kuogopa mashambulizi, kama mnazo hoja mbona hamjitokezi hadharani kujibu mapigo?
 
DAAH MIE NMEKATA JUZI JUZI YA 240K , NATUMAINI WATAKUWA WAMEISHA BORESHA HIZI CHANGAMOTO ZA HAPA NA PALE.
 
Back
Top Bottom