Rais Samia, naomba ajira

Hii kazi haiombwi kama kuomba chumvi,
Una Elimu gani,umefanya nini mpaka sasa hv kwenye nyanja za usalama,hii kazi wanapewa watu waliopo kwenye kada za usalama,jeshini,polisi,kitendo Cha wewe kuiomba tu,umethibitisha kwamba hufai
 
Yaan we jamaa unavowashwa kuhusu usalama,utafkiri yaan we ndio the best candidate ambae unapaswa kuwa recruited kumbe ni mchumia tumbo ambae ni much know kutwa kushinda mtandaoni badala ya kufanya kazi
 
Hata marehemu Ruge ktk moja ya interview yake pale mjengoni alitaka sana hiko cheo, alikutamani na kusema hataki cheo chochote au uteuzu wowote serikalini labda tu kwa nafasi aliyonayo diwani sasa
 
Sijui ni nani anawadanganya ( amewadanganya ) kuwa kwa Ukanda wetu huu wa Maziwa Makuu Kenya wako vizuri sana Kiujasusi kuliko Tanzania.

Nashukuru Mungu na nashukuru pia kwa angalau kuweza Kuzitembelea nchi kadhaa za Afrika na kubahatika kukutana na Watu wa hii Kada Nyeti wa nchi hizo huku nikiwa ni Raia wa kawaida tu.

Ninachojua likija Suala zima la Ujasusi ( Espionage ) kwa hapa Afrika ( tena kwa Kujiamini kabisa 100% ) Tanzania huenda ikazidiwa tu na nchi Tatu za Egypt, South Africa na Ethiopia ila siyo zingine.

Hawa Wakenya wako unaowasifia Kutwa wao Wenyewe tokea kutokee Mashambulizi ya Kigaidi huko Kwao wamekuwa wakija Kuomba Msaada wa Watu wetu ( Watanzania kutoka Idarani ) waweze Kuwasaidia na hata Kuwafunza zaidi Watu wao ( Wakenya )

Ungeniambia ( ungekuja na Hoja ) kwamba Wakenya wameamua Kuwekeza na ' Kujikita ' zaidi katika Ujasusi pekee wa Kiuchumi kidogo ningekuelewa ila Tanzania kwa miaka mingi ' imejikita ' katika ' Ujasusi ' wa jumla ambao hata ' Kimedani ' ndiyo una faida Kubwa kama waufanyao Israel ( Wayahudi )

Namalizia kwa Kusisitiza tena kuwa kwa hapa Afrika na hata Ukanda wetu huu sijaona nchi ya Kushindana ' Kiujasusi ' na Tanzania na hakuna Taifa ' linaloogopeka ' kwa Unjagu ( Ujasusi ) Barani Afrika na hata baadhi ya nchi Kubwa ( Mataifa Makubwa ) yanaiogopa kama Tanzania.

Popote mlipo TISS Agents tembeeni Vifua mbele, tunajivunia Uimara na Utendaji wenu ulioandaliwa vyema ' Kimisingi ' Imara ya ' Kiujasusi ' tokea enzi ya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere hadi hivi Sasa. Watanzania leo tuna huu Ustawi, Amani na Uhuru kutokana na Kufanya Kwenu Kazi ya Kutulinda ' Kiusalama ' ndani na nje ya mipaka huku mkishirikiana vyema tu na Idara Nyeti za Jeshi ( CMI )

Nchi pekee kwa Ukanda huu ambayo kidogo inakuja kwa Kasi ' Kiujasusi ' japo bado ina Safari ndefu ya Kuikuta Tanzania ni Rwanda ( ila nao wana Mapungufu ya Kimsingi ambayo yanawagharimu ) na kwa Uganda ndiyo kabisa hawatutishi kwa Ukanda huu kwani Idara zao zote za ' Kiusalama ' hasa hasa zile za Polisi na Jeshini ' wamepikwa ' na bado mara kwa mara Rais Museveni anawaleta Watendaji wake hao ' Kupikwa ' huku Tanzania au ' Trainers ' wetu wanaenda huko Uganda.

Tanzania 'Kiusalama' ni habari nyingine.
 
Upo sahihi mkuu,ingawa miaka ya hivi karibuni TISS inaonyesha madhaifu kiasi fulani
 
TISS miaka ya hivi karibuni imeyumba.

Kuna maamuzi yamefanyika nchini na yamegharimu maisha ya watu hao TISS ilibidi waepushe hayo mapema.
 
TISS miaka ya hivi karibuni imeyumba.

Kuna maamuzi yamefanyika nchini na yamegharimu maisha ya watu hao TISS ilibidi waepushe hayo mapema.
Mapungufu hayo 'yanadhibitiwa' vilivyo.
 
🤣🤣
 
Yule mtu mwenye ghadhabu niliyemwona juzi nilipokuwa Ikulu sidhani kama atafurahi mtu yoyote kuitamani kazi yake.
Lakini
kama unataka kuwa mkubwa wa TISS lazima ujue kuhusu CIA,FSB,MOSSAD,MI6.
 
Tatizo hata kazi unayoiomba hujui inahusu nini inasimamiwa na sheria gani ,eti unaongelea mambo ya kuiba ,mkuu TISS ni kazi ya uzalendo na uadilifu sio ya kihuni .Hao kina makonda na sabaya nadhani ndo waliokuwa wanawadanganya vijana kuwa kazi ya tiss ni kupambana na maadui wa rais na kulinda maslahi ya nchi hata kwa kuvunja sheria .
 
Popoma uliyetukuka,umepotea sana mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…