Rais Samia na Serikali yake ameiteka mijadala kuliko habari za Yanga na Simba kufuzu Robo Fainali

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,305
9,734
Ndugu zangu watanzania,

Hii ni rekodi mpya. Ni historia ya kipekee aliyojiwekea Rais Samia na serikali yake mitaani, haijawahi kutokea kiongozi wa kisiasa kuteka mijadala mitaani kupita hata habari za michezo na burudani, kwa Sasa Rais Samia ni zaidi ya habari za michezo maana kaweza kuteka Hadi mioyo ya wanamichezo ambao ushindi ukipatikana uwanjani unaona watu wanavyotabasamu na kusema kwa bashasha na furaha kuwa huu ni ushindi na zawadi kwa ajili ya mama yetu na Rais wetu mama Samia.

Kila Kona kila mahali Ni Rais Samia juu ya uchapa kazi wake na umahiri wake katika uongozi,ukienda kwa wakulima unawakuta wanatafuna mahindi ya kuchomaa na kumzungumza Rais Samia namna alivyowasaidia katika kilimo baaada ya kutoa Ruzuku ya billion Mia moja hamsini katika mbolea na hivyo kupelekea kushuka kwa Bei ya mbolea sokoni.

Ukienda kwa akina mama magengeni unawakuta na kuwasikia namna alivyowasaidia kuwatua ndoo kichwani baada ya kuwasogezea maji karibu yao na hivyo kuwapunguzia adha ya kusafiri umbali mrefu kutafuta maji,Ndio maana wanawake wengi Sana saizi mitaani wakijifungua watoto wa kike Ni kawaida kusikia mtoto anapewa jina la Samia Kama sehemu ya kufurahishwa na uchapa kazi na namna mama Samia alivyogusa maisha Yao, na siku zote jina jema huvuma na kukaa midomoni mwa watu na kukumbukwa na wengi Sana hata ikiwa mtu husika ametangulia mbele za haki Kama anavyokumbukwa Hayati Baba wa Taifa mwalimu Nyerere au Nelson Mandela au Dr Martin Luther King junior au John F Kennedy au George Washington.

Ukienda kwa wanachuo, vijana, wanafunzi, wafanyabiashara, wajasiriamali, bodaboda,madereva bajaji kwote huko unakuta Rais Samia Ameziteka nyoyo zao kwa namna alivyowawezesha na kuwasaidia kutimiza Ndoto zao na kufanya shughuli zao kwa amani pasipo bugudha Wala kero ilimradi tu watu wazingatie Sheria, kanuni na taratibu.

Ukienda kwa watumishi wa umma wanatamani hata uchaguzi ufanyike kesho ili wampigie kura za Ndio kwa kishindo Rais Samia kutokana na namna alivyowafuta machozi na kuwapa Tabasamu Katika Mioyo yao hasa baada ya kuwapatia Nyongeza ya mshahara ya 23%, kuwapandisha madaraja na kuwalipa kulingana na madaraja Yao, kuwalipa malimbikizo ya madeni Yao, kuwaboreshea mazingira ya kazi Hali iliyowapatia morali kubwa Sana ya kuchapa kazi kwa bidii kubwa Sana na kujituma katika kuwahudumia Watanzania.

Kwa Sasa Rais Samia Ni Kama maji usipoyanywa utayaoga tu, kwa hakika Rais Samia amepewa kibali na Mwenyezi MUNGU cha kuongoza Taifa letu, Mungu kambariki na Kumjalia uwezo mkubwa Sana wa kiuongozi Rais Samia,kamjalia na kalama ya uongozi, kampa kila kitu anachopaswa kuwa nacho kiongozi wa ngazi ya juu kiuongozi Kama alivyo Rais Samia.

Rais Samia ni Kama Mti uliopandwa kandokando ya chemchemi ya maji isiyo kauka maji masika na kiangazi haukauki Wala kusinyaa majani yake ,Rais Samia hakauki Wala kukatika katika midomo ya Watanzania, watu wote wanayo amani na furaha ya uwepo wa Rais Samia, Rais Samia Anatazamwa Kama Mtumishi mwema na mnyenyekevu kwa watu, mtetezi na mfariji wa Taifa letu na kiongozi wa watu wote.

Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
 
Ndugu zangu watanzania,


0742-676627.
Mkuu Lucas, Hongera sana, hakika umenena vyema pasipo kuongeza chunvi. Ila kuna hawa Wananchi wake wa Kimara -Mbezi, waliovunjiwa nyumba zao, bado wanasubili huruma yake, japo kwa kifuta machozi. Kutokana na tathimini ya hoja zako, hapana shaka upo karibu naye; hivyo sio vibaya ukamkumbusha Mh. Rais maana ana MAJUKUMU mengi.
 
Mkuu Lucas, Hongera sana, hakika umenena vyema pasipo kuongeza chunvi. Ila kuna hawa Wananchi wake wa Kimara -Mbezi, waliovunjiwa nyumba zao, bado wanasubili huruma yake, japo kwa kifuta machozi. Kutokana na tathimini ya hoja zako, hapana shaka upo karibu naye; hivyo sio vibaya ukamkumbusha Mh. Rais maana ana MAJUKUMU mengi.
Kama walipeleka kesi mahakamani Basi hapo Ni mpaka wasubiri hukumu ya mahakama,Kulipwa fidia inategemeana eneo waliokuwa wamejenga makazi Yao Kama yalikuwa ndani ya hifadhi ya Barabara au nje ya hifadhi,Kama walikuwa nje na wakavunjiwa Basi hapo utaratibu na Sheria IPO wazi kuwa lazima walipwe fidia baada ya kufanyika kwa tathimini ya kina juu ya stahiki za kila mtu kulingana na Eneo lake na vitu vilivyopo
 
geimg-lo.jpg
 
Acha kujipendekeza kwa kiwango hicho.
Maisha mtaani magumu na hakuna raia anayemtilia maanani.
Mitaani watu wanaendelea kumpongeza Sana mh Rais kwa uchapa kazi wake na kugusa maisha Yao,wanasema Asante Rais Samia kwa kuleta Tabasamu na matumaini katika mioyo yao
 
Kama walipeleka kesi mahakamani Basi hapo Ni mpaka wasubiri hukumu ya mahakama,Kulipwa fidia inategemeana eneo waliokuwa wamejenga makazi Yao Kama yalikuwa ndani ya hifadhi ya Barabara au nje ya hifadhi,Kama walikuwa nje na wakavunjiwa Basi hapo utaratibu na Sheria IPO wazi kuwa lazima walipwe fidia baada ya kufanyika kwa tathimini ya kina juu ya stahiki za kila mtu kulingana na Eneo lake na vitu vilivyopo
Mkuu hakuna kesi mahakani na hata hizo barabara 8 hazijafika kwenye nyumba zao zilizo bomolewa.. Mkuu mkumbushe mbona unaanza kusita; WANAKUTEGEMEA na KUKUAMINI
 
Mkuu hakuna kesi mahakani na hata hizo barabara 8 hazijafika kwenye nyumba zao zilizo bomolewa.. Mkuu mkumbushe mbona unaanza kusita; WANAKUTEGEMEA na KUKUAMINI
Naamini Kama suaa Hilo wananchi hawakutendewa haki Basi Taarifa hizo lazima awe nazo Mwenyekiti ngazi ya mtaa,Diwani ngazi ya kata pamoja na mbunge ngazi ya Jimbo, ambapo mbunge anao uwezo wa kuwasilisha na kufikisha malalamiko ya wananchi wake serikalini kupitia bunge kwenda kwa Waziri wa ardhi,na hata kumuuliza mh Waziri mkuu suali la papo kwa papo siku ya alhamisi, lakini pia mh Rais anapo fanya ziara katika eneo lenu Ni jukumu lenu kumfikishia kero yenu maana Rais wetu no msikivu Sana na mwenye huruma na upendo.

Mimi sipo karibu na Rais kiutendaji Wala kiitifaki na Wala sipo katika utumishi wa umma katika secta yoyote Ile ya umma
 
Huu uharo wako harishia humu humu ndani ya Jf, ukitoka humu ndani uende ukaoge kabisa maana ukiingia na hiyo harufu kinyesi mtaani raia watakurandika bakora za kutosha.

Wewe ni wa hovyo kabisa....fedha za umma zinaporwa mchana kweupe alafu unakuja hapa jukwaani na mapambio ya ibilisi??
Hakuna anayeweza kubaki salama akigusa pesa za umma, serikali ya Rais Samia haina Subira kwa mtu yeyote atakaye chezea pesa za walipa Kodi wa Taifa letu.

Ndio sababu ya Rais Samia Kuendelea kuungwa mkono na watanzania kutokana na Imani kubwa waliyo nayo watanzania kwake juu ya dhamira yake njema na uzalendo kwa Taifa letu
 
Ndugu zangu watanzania,

Hii ni rekodi mpya. Ni historia ya kipekee aliyojiwekea Rais Samia na serikali yake mitaani, haijawahi kutokea kiongozi wa kisiasa kuteka mijadala mitaani...
Ni kweli kabisa. Mwenzangu unaishi Mtaa gani huo?
 
Kama walipeleka kesi mahakamani Basi hapo Ni mpaka wasubiri hukumu ya mahakama,Kulipwa fidia inategemeana eneo waliokuwa wamejenga makazi Yao Kama yalikuwa ndani ya hifadhi ya Barabara au nje ya hifadhi,Kama walikuwa nje na wakavunjiwa Basi hapo utaratibu na Sheria IPO wazi kuwa lazima walipwe fidia baada ya kufanyika kwa tathimini ya kina juu ya stahiki za kila mtu kulingana na Eneo lake na vitu vilivyopo
Mbona waliojenga bonde la mto msimbazi wanalipwa na walijenga kwenye hifadhi ya mto?
 
fedha za umma kuibiwa maana yake kuna mianya ya watu kuiba, kuwepo na mianya tayari ni udhaifu wa kiungozi.

Toka report ya CAG mpaka sasa hatujasikia mtu yeyote kukamatwa, kutumbuliwa wala kupelekwa mahakamani.

Nidhamu ya kiutendaji kwenye taasisi za umma imekuwa zero kabisa japo kuna muda awamu ya tano haya mambo yalianza kukaa sawa, ila kwasasa business as ussual.

Rushwa kwenye ofisi na taasisi za umma imerudi kwa kasi na hakuna pakulia wala hakuna mchukua hatua yeyote.

Tatizo la ajira mitaani bado limekuwa ugonjwa sugu, ajira zimekuwa zakujuana, ajira za vimemo na vibarua zipo palepale na tatizo la kuajiri incompetency bado linasumbua.

Miji mikubwa imeendelea kujengwa hovyohovyo bila mpangilio, miji michafu na hakuna hatua zozote zakudhibiti hilo.

Machinga kwenye majiji wamejazana bila mpango, wako kila mahala na kusababisha misongamano isiyo na tija.
 
Ninavyomfahamu Madam President, siku alifanikiwa kusoma uzi wako ataishia tu kusema kwa kumaanisha,

STUPID.
 
Luca amefika. Uzuri hana baya na mtu. Akishashiba makatapera na panya-buku, yatosha. Hana habari ya kujishughulisha na magumu wapitiayo watu wa nchi hii.
 
Luca amefika.Uzuri hana baya na mtu.Akishashiba makatapera na panya-buku,yatosha.Hana habari ya kujishughulisha na magumu wapitiayo watu wa nchi hii.
Rais Samia na serikali yake Amefanya kazi kubwa Sana ya kupambana na changamoto zinazo wakabili watanzania,ndio maana unaona Hadi akifikia hatua ya kutoa mabillioni ya Ruzuku ili kumpunguzia mzigo wa gharama mtanzania
 
Back
Top Bottom