Chimba ujue kwa nini wale makandarasi waliondolewa kinyume na sheria, eti hawatakiwi DSM.
Waliombwa rushwa na hawakutoa, mmoja aliombwa 200m na kiongozi mkoani.
Sasa nyie mazwazwa hamjui hata kandarasi zinaeneshwaje.
Mkandarasi akikosea kazi ANAIRUDIA kulingana na mkataba.
Hao makandarasi vile vile waliingia siasa.
Wakaipata.
Sio kweli hakuna mkandarasi aliombwa rushwa akakataa kwanini asiende TAKUKURU badala yake akangoja asimamishwe baada ya kugundulika kuwa kazi zake ni substandard? Hao makandarasi tunawajua na michongo yao kwani tumeishi nao toka wanaanza hizo kazi na jinsi walivyotajirika na kujenga majumba !! Tunawajua sio kana kwamba tunawasingizia ni wapigaji lakini hamjui kuwa mnawaumiza walipa kodi kwa utapeli wenu halafu mnakwenda kutangaza ufalme bar!!
Kwanini mkandarasi makini arudie kazi yake; huo ndio ubabaishaji wenyewe tunaousema, watu wanapewa tenda za kujenga huku hawana vifaa wala utaalam!!