Habari za Zanzibar
JF-Expert Member
- Dec 18, 2024
- 260
- 199
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, ataongoza zoezi maalum la upandaji miti litakalofanyika tarehe 27 Januari, 2026, maeneo ya Bungi Kilimo na Kizimkazi, Zanzibar, ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku yake ya kuzaliwa.
Zoezi hili lenye kaulimbiu “Uzalendo ni Kutunza Mazingira, Shiriki Kupanda Miti” linaakisi dhamira ya Mhe. Rais Dkt. Samia katika kuendeleza ajenda ya Taifa ya uhifadhi na utunzaji wa mazingira, ikiwemo upandaji miti, ulinzi wa vyanzo vya maji, kuimarisha uoto wa asili, na kuchangia kwa vitendo juhudi za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Aidha, zoezi hili ni ishara ya uwajibikaji wa pamoja na linatoa fursa kwa kila mmoja, kwa nafasi yake na mahali alipo, kushiriki katika kulinda na kuenzi mazingira kwa manufaa ya sasa na kizazi kijacho.
Mheshimiwa Rais anatoa wito kwa Watanzania kuendelea kujenga utamaduni wa kulinda na kuhifadhi mazingira kwa hiari, wakitambua kuwa ulinzi wa mazingira ni msingi wa uhai, maendeleo, na usalama wa Taifa.
HalikaDhalika, Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, inawahimiza wananchi, taasisi na wadau wa mazingira kuunga mkono dhamira ya Mhe. Rais Dkt. Samia kwa kuendeleza ajenda ya uhifadhi wa mazingira, ikiwemo kupanda angalau mti mmoja nyumbani, shuleni, kazini, au kwenye maeneo ya jamii.
Zoezi hili lenye kaulimbiu “Uzalendo ni Kutunza Mazingira, Shiriki Kupanda Miti” linaakisi dhamira ya Mhe. Rais Dkt. Samia katika kuendeleza ajenda ya Taifa ya uhifadhi na utunzaji wa mazingira, ikiwemo upandaji miti, ulinzi wa vyanzo vya maji, kuimarisha uoto wa asili, na kuchangia kwa vitendo juhudi za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.
Aidha, zoezi hili ni ishara ya uwajibikaji wa pamoja na linatoa fursa kwa kila mmoja, kwa nafasi yake na mahali alipo, kushiriki katika kulinda na kuenzi mazingira kwa manufaa ya sasa na kizazi kijacho.
Mheshimiwa Rais anatoa wito kwa Watanzania kuendelea kujenga utamaduni wa kulinda na kuhifadhi mazingira kwa hiari, wakitambua kuwa ulinzi wa mazingira ni msingi wa uhai, maendeleo, na usalama wa Taifa.
HalikaDhalika, Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu, inawahimiza wananchi, taasisi na wadau wa mazingira kuunga mkono dhamira ya Mhe. Rais Dkt. Samia kwa kuendeleza ajenda ya uhifadhi wa mazingira, ikiwemo kupanda angalau mti mmoja nyumbani, shuleni, kazini, au kwenye maeneo ya jamii.