Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,493
- 14,907
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amewatakia kheri ya sikukuu ya Uhuru Watanzania kupitia kurasa zake za mitandao ya Kijamii.
Rais Samia amesema 'Kheri ya Miaka 64 ya Uhuru wa nchi yetuTunamshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa hatua hii kubwa. Tunapoadhimisha siku hii muhimu, tukumbushane umuhimu wa kuendelea kulinda tunu za Taifa letu za amani, umoja na mshikamano. Tunu hizi ndizo msingi wa mafanikio ya safari yetu ambayo ni mfano wa kipekee Afrika na dunia kwa ujumla' - Rais Samia.
Rais Samia ameongeza kwa kusema 'Matunda ya Uhuru wetu yanaendelea kudhihirika katika uwezo wetu wa kuamua, kupanga na kutekeleza mipango yenye manufaa kwa wananchi na yenye kulinda maslahi ya Taifa letu. Haya ndiyo matunda ambayo waasisi wa Taifa letu waliyapigania na ambayo daima tutayalinda'
Na mwisho amesema 'Tuufurahie, tujivunie, tuulinde na tuuthamini Uhuru wetu. Mungu Ibariki Tanzania.' - Rais Samia.
Rais Samia ameongeza kwa kusema 'Matunda ya Uhuru wetu yanaendelea kudhihirika katika uwezo wetu wa kuamua, kupanga na kutekeleza mipango yenye manufaa kwa wananchi na yenye kulinda maslahi ya Taifa letu. Haya ndiyo matunda ambayo waasisi wa Taifa letu waliyapigania na ambayo daima tutayalinda'
Na mwisho amesema 'Tuufurahie, tujivunie, tuulinde na tuuthamini Uhuru wetu. Mungu Ibariki Tanzania.' - Rais Samia.