Rais Samia awaapisha Viongozi wateule leo Februari 15, 2023

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan akiwaapisha Viongozi wateule leo tarehe 15 Februari, 2023 Ikulu jijini Dares Salaam.

Viongozi walioapishwa ni pamoja na:

- Mohamed Omary Mchengerwa aliyekuwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo aliyehamishiwa Wizara ya Maliasili na Utalii, huku Balozi Dkt. Pindi Chana aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii akihamia Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo

- Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbas Said, amekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii. Dkt. Hassan Abbas aliyechukua nafasi ya Prof. Eliamani M. Sedoyeka.

- Mwingine ni Said Othman Yakub aliyeapishwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo akichukua nafasi ya Dkt. Hassan Abbas



PHILIP MPANGO, MAKAMU WA RAIS

Kocha yoyote yule huwa anatazama timu yake inavyocheza. Na baada ya pale, anafikiria ili nipate ushindi basi nitabadilisha namba hii iende defense au iende ikafunge magoli. Tunakupongeza Mheshimiwa Rais.

Niwapongeze na ninyi mlioaminiwa. Bahati nzuri Mh. Mchengerwa, Mh. Pindi Chana, mmekuwepo mnajua maadili ya kiserikali. Natumai jambo mtakalolifanya ni kukaa pamoja nakuona namna gani mnabadilishana hizo namba.

Katim ya wizara ambazo zimekuwa na mawaziri wengi ni pamoja na Wizara ya Maliasili na Utalii. Ambayo ni sekta muhimu sana kwa maendeleo ya taifa letu. Ni sekta ambayo mchango wake katika fedha za kigeni, katika ajira ni kubwa sana. Kwahiyo umepewa dhamana ya kuhakikisha sekta hii inaendelea kukua na kuchangia zaidi katika maendeleo ya nchi yetu.

Lakini vilevile sekta hiyo bahati mbaya sana ina vishawishi vingi. Nina uhakika Dkt. Pindi Chana atakudokeza mengi aliyoona katika kipindi chake. Nadhani mjiepushe na vishawishi hivyo – kama ni kwenye vital una mengineyo.

Lakini katika upande wa sekta ya utamaduni, kwenye takwimu ndiyo sekta ambayo inakuwa hivi sasa kuliko sekta nyingine zote. Na ndiyo sekta ambayo inaajiri vijana wengi – tegemeo la taifa letu kesho. Kwahiyo, ukaitendee haki. Mh. Pindi Chana, uende ukaitendee haki. Vijana wetu wanaitegemea sana hiyo sekta.
 
Kila siku kuteua kuapisha. Upinzani haya ndio mnatakiwa kuyazingatia. Hizi teuzi za mjomba shangazi has to stop.
Afrika aliyetuloga aje ategue.
 
Napenda jinsi mama alivyowajibu spika na wabunge wake kuhusu wao kuendelea kujadili mambo ya jadi, na kwa wale ambao hamjafika Bujumbura muanze safari tuu...

Kafanya Mabadiriko madogo ili KAZI IENDELEE 😂😂😂
 
Utamaduni na sanaa ndo wizara tegemeo la kutoa ajira kwa wingi kwa vijana 😅vijana changamkieni fursa white collar job tuachieni sisi wateule😅
 
Napenda jinsi mama alivyowajibu spika na wabunge wake kuhusu wao kuendelea kujadili mambo ya jadi, na kwa wale ambao hamjafika Bujumbura muanze safari tuu...

Kafanya Mabadiriko madogo ili KAZI IENDELEE 😂😂😂
Hahah hata kama wakazisomee phdii,siyo kusubiri za kupewa kimaamuna.na mwigu ni mzee wa ndagu hawezi ondolewa hapo,mganga wake fundi 🙏
 
Makamu wa Rais Dr Mpango anesema Wizara ya Maliasili na Utalii ina vishawishi vingi vya Rushwa hivyo Waziri mpya mh Mchengerwa ajiandae vema kupambana na changamoto hiyo

Aidha amemtaka Pindi Chana kuendeleza pale alipoishia Mchengerwa Kwenye Michezo na Utamaduni

Source Star tv
 
Hizi zama za rushwa kuruhusiwa, watu kula kwa urefu wa kamba zao.

Hayo yanasemwa tu hadharani hivyo lakini ukweli ni kwamba rushwa imetamaladadi.
 

Ukute hata hakushirikishwa kwenye uamuzi wa kumpeleka huko Maliasili.
 
Makamu wa Rais Dr Mpango anesema Wizara ya Maliasili na Utalii ina vishawishi vingi vya Rushwa hivyo Waziri mpya mh Mchengerwa ajiandae vema kupambana na changamoto hiyo

Aidha amemtaka Pindi Chana kuendeleza pale alipoishia Mchengerwa Kwenye Michezo na Utamaduni

Source Star tv
Atamsikiliza Mkwe au Mpango!
 
Inaonekana huyu Dr.pindi chana alilamba asali mpaka akapaliwa sasa mchengerwa na wewe ule taratibu ukizidisha ukapaliwa watakuhamisha hapo.
 
Makamu wa Rais Dr Mpango anesema Wizara ya Maliasili na Utalii ina vishawishi vingi vya Rushwa hivyo Waziri mpya mh Mchengerwa ajiandae vema kupambana na changamoto hiyo

Aidha amemtaka Pindi Chana kuendeleza pale alipoishia Mchengerwa Kwenye Michezo na Utamaduni

Source Star tv

Tatizo la ajali za Tanzania ni barabara kuwa ndogo,halafu magari ni mengi.Kinachotakiwa kifanyike ni kupanua barabara zote kuu,Dar to Tunduma, Dar to Mwanza, Dar to Arusha, Dar to Mtwara.Hizo njia kuu zikishatanuliwa, tutakuwa tumeokoa vifo vya ajali kwa asilimia 90

Madereva wengi hawazingatii Sheria ya ku-overtake,kwenye kona,kwenye mwinuko,wanaen dekeza mzoea mbona jana nilipita
 
Back
Top Bottom