Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,815
- 11,992
Rais Samia Suluhu Hassan akiwaapisha viongozi wateule Ikulu Chamwino, Dodoma, leo Jumamosi Mei 21, 2022
Pia soma > Uteuzi: Rais Samia afanya teuzi mbalimbali za Wenyeviti wa Bodi/Baraza la Chuo na Watendaji Wakuu wa Taasisi
----
- Zoezi la kuapisha limekamilika, baadhi ya viongozi akiwemo Spika Dkt. Tulia Akson ambaye amewapongeza viongozi wote walioteuliwa, amempongeza Rais Samia kwa mafanikio mbalimbali katika utawala wake. Pia amewahimiza viongozi walioteuliwa kuwa waadilifu na wachapakazi.
- Akiwaapisha viongozi wateule leo Mei 21, 2022, Ikulu Dodoma, Rais Samia Suluhu amewataka Makamishna kusimamia haki kwa kuwa Watanzania wote wana haki sawa lakini akagusia suala la nidhamu kutetereka katika Utumishi wa Umma.
Leo nimepata kazi kidogo ya kumuapisha Mwalimu wangu, huyu Bi. Khadija vyovyote alivyo ni Mwalimu wangu wa hesabu na kiingereza form 2 na form 3. Lakini pia kwenye hii timu nina College Mate wangu nayeye pia nimemuapisha Haule naomba usimame.
Rais Samia: Niwapongeze wale wote walioapa ni nafasi chache za Makatibu Wakuu ambao tumehisi wanaweza kwenda kuziba nafasi katika zile tulizofanya mabadiliko muda mfupi uliopita.
Rais Samia: Ndugu Kazi unakwenda mambo ya ndani, najua unafikiri kichwani kuwa mimi nimetoka zangu Benki Kuu na Uwekezaji mambo ya ndani naenda kufanya nini? Lakini nadhani utaweza. Nimefikiri mara tatu na nne nikasema kazi ataweza, kwahiyo nenda kafanye kazi mambo ya ndani na ni kuongeza CV yako.
Rais Samia: Ndugu yangu Msonde umezoea madisc yale unatuletea na vitabu vikubwa vikubwa na namba za mtihani sasa unakwenda TAMISEMI lakini nimekupa eneo lilelile ulilolizoea. Kwahiyo utakwenda kusimamia elimu ile ngazi ya TAMISEMI Msingi na ile kabla ya msingi na najua una uzoefu mkubwa ndani ya Wizara ya Elimu.
NIDHAMU YA WATUMISHI WA UMMA IMETETEREKA
Rais Samia: Makanishna niwaombe sana mkasimamie haki, Watanzania wote wanahaki sawa, juzi wamefurahi wamepanda madaraja kwa mserereko lakini hawajui wajibu wao.
Rais Samia: Watumishi wetu hawajielewi, nidhamu yao mpaka wapate vitisho, vitisho vikiondoka nidhamu hakuna, tunataka utumishi ambao watakuwa na itikadi mioyoni kwao mimi ni mtumishi wa umma ethics zangu ni hizi, nidhamu yangu mstari ni huu hapa
Rais Samia: Watumishi wa Umma wanakwenda tu, nadhani ni kwa sababu kwa muda mrefu sasa hakuna mafunzo ya kada mbalimbali katika Utumishi wa Umma, kwa hiyo mnavyoenda kujipanga, mkasimamie hilo.
Rais Samia: Kila baada ya muda tunaona wakurugenzi wana mabweni yao, walikuwa wanakuja na kuondoka kupata refresher courses kuwakumbusha wajibu wao, jambo ambalo kwa muda mrefu nadhani limekufa kwa maana hiyo watumishi wa umma wanajikuta wanapandishwa vyeo bila kupata mafunzo.
Rais Samia: Makamishna wa tume ya utumishi, najua wengi ni wenyeji mlikuwa huko na mnajua kazi zinavyofanywa, na wengine ni wapya lakini niwaombe sana mkasimame katikati, mkasimamie haki watanzania wote wanahaki sawa.
Pia soma > Uteuzi: Rais Samia afanya teuzi mbalimbali za Wenyeviti wa Bodi/Baraza la Chuo na Watendaji Wakuu wa Taasisi
----
Updates
- Rais Samia amewasili na zoezi la viongozi kuapishwa limeanza- Zoezi la kuapisha limekamilika, baadhi ya viongozi akiwemo Spika Dkt. Tulia Akson ambaye amewapongeza viongozi wote walioteuliwa, amempongeza Rais Samia kwa mafanikio mbalimbali katika utawala wake. Pia amewahimiza viongozi walioteuliwa kuwa waadilifu na wachapakazi.
HOTUBA YA RAIS SAMIA
- Akiwaapisha viongozi wateule leo Mei 21, 2022, Ikulu Dodoma, Rais Samia Suluhu amewataka Makamishna kusimamia haki kwa kuwa Watanzania wote wana haki sawa lakini akagusia suala la nidhamu kutetereka katika Utumishi wa Umma.
Leo nimepata kazi kidogo ya kumuapisha Mwalimu wangu, huyu Bi. Khadija vyovyote alivyo ni Mwalimu wangu wa hesabu na kiingereza form 2 na form 3. Lakini pia kwenye hii timu nina College Mate wangu nayeye pia nimemuapisha Haule naomba usimame.
Rais Samia: Niwapongeze wale wote walioapa ni nafasi chache za Makatibu Wakuu ambao tumehisi wanaweza kwenda kuziba nafasi katika zile tulizofanya mabadiliko muda mfupi uliopita.
Rais Samia: Ndugu Kazi unakwenda mambo ya ndani, najua unafikiri kichwani kuwa mimi nimetoka zangu Benki Kuu na Uwekezaji mambo ya ndani naenda kufanya nini? Lakini nadhani utaweza. Nimefikiri mara tatu na nne nikasema kazi ataweza, kwahiyo nenda kafanye kazi mambo ya ndani na ni kuongeza CV yako.
Rais Samia: Ndugu yangu Msonde umezoea madisc yale unatuletea na vitabu vikubwa vikubwa na namba za mtihani sasa unakwenda TAMISEMI lakini nimekupa eneo lilelile ulilolizoea. Kwahiyo utakwenda kusimamia elimu ile ngazi ya TAMISEMI Msingi na ile kabla ya msingi na najua una uzoefu mkubwa ndani ya Wizara ya Elimu.
NIDHAMU YA WATUMISHI WA UMMA IMETETEREKA
Rais Samia: Makanishna niwaombe sana mkasimamie haki, Watanzania wote wanahaki sawa, juzi wamefurahi wamepanda madaraja kwa mserereko lakini hawajui wajibu wao.
Rais Samia: Watumishi wetu hawajielewi, nidhamu yao mpaka wapate vitisho, vitisho vikiondoka nidhamu hakuna, tunataka utumishi ambao watakuwa na itikadi mioyoni kwao mimi ni mtumishi wa umma ethics zangu ni hizi, nidhamu yangu mstari ni huu hapa
Rais Samia: Watumishi wa Umma wanakwenda tu, nadhani ni kwa sababu kwa muda mrefu sasa hakuna mafunzo ya kada mbalimbali katika Utumishi wa Umma, kwa hiyo mnavyoenda kujipanga, mkasimamie hilo.
Rais Samia: Kila baada ya muda tunaona wakurugenzi wana mabweni yao, walikuwa wanakuja na kuondoka kupata refresher courses kuwakumbusha wajibu wao, jambo ambalo kwa muda mrefu nadhani limekufa kwa maana hiyo watumishi wa umma wanajikuta wanapandishwa vyeo bila kupata mafunzo.
Rais Samia: Makamishna wa tume ya utumishi, najua wengi ni wenyeji mlikuwa huko na mnajua kazi zinavyofanywa, na wengine ni wapya lakini niwaombe sana mkasimame katikati, mkasimamie haki watanzania wote wanahaki sawa.