Rais Samia apewe haki yake katika haya

Rais Samia apewe haki yake katika haya

Getrude Mollel

JF-Expert Member
Joined
Apr 26, 2022
Posts
308
Reaction score
424
Hakika mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Anachokifanya Rais Samia Suluhu Hassan kwa watumishi wa umma na wengine, hakiwezi kupita bila kuungwa mkono.

Rais Samia amefanya mambo makubwa sana kwa watumishi katika namna tatu.

Hivi karibuni Serikali ilitangaza ongezeko la kima cha chini cha mishahara kwa asimilia 23.3, kikokotoo cha mafao kupanda haki asilimia 33 kutoka asilimia 25 na posho ya safari kutoka Sh. 12,000 kwa mwezi hadi 250,000.

Hiyo ni kwa kiwango cha juu, lakini pia kutoka Sh. 80,000 hadi Sh. 100,000 kwa mwezi kwa watumishi wa kiwango cha chini na kusaidia kupunguza ukali wa maisha kwa watumishi nchini Tanzania.

Bila shaka, hatua alizochukua Rais Samia zinatokana na mabadiliko ya muda na mazingira hasa ukizingatia kwamba watumishi nchini Tanzania katika kipindi cha miaka sita hawajawahi kupanda ongezeko lolote katika mishahara yao.

Imani yetu kwa sasa sisi Watanzania ni kuona kwamba jambo kama hili linakwenda kutokea katika sekta binafsi pia. Ni ukweli usiopingika kwamba katika sekta binafsi ndiko kuna watu wanaolipwa mishahara mikubwa sana lakini pia ndio hukohuko wapo wanaolipwa mishahara midogo sana. Serikali tulivu ya Rais Samia, tunaamini kwamba muda hautokuwa mrefu sana hadi kusikia viwango vipya ya mishahara katika sekta binafsi.

Hatujaumbwa kuja kukosea tu, na watu tuliowapa dhamana kutongoza sio malaika, hivyo tuaamini kwamba wanakosea, na hapo tunawajibu wa kuwarekebisha. Kama tuna haki ya kuwarekebisha, basi tuwe waungwana pia kumwaga sifa pale wanapofanya vyema kulingana na matarajio yetu. Hiyo inawapa motisha wa kufanya kazi na kuujenga uzalendo zaidi mioyoni mwao.

FSdPgwPXwAACJRr.jpg
 
Maisha yako juu sana kitaa. Ndio maana vijana wanaumua kuwa panya road tu, wakamatwe wakale maharagwe yao swafi.
 
Katimiza wajibu wa sheria, kama ni pongezi hata walimu huko mashuleni bas wapongezwe kwa kufundisha
 
Hakika mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Anachokifanya Rais Samia Suluhu Hassan kwa watumishi wa umma na wengine, hakiwezi kupita bila kuungwa mkono...
Wewe kwa mwezi unatumia mafuta ya kula kiasi gani? Unasafiri mara ngapi? Unatumia sabuni kiasi gani? Vyakula gharama yake sh ngapi? Sukari kiasi gani? Unajenga? Km ndiyo unajenga gharama za nondo, cement, bati, misumari, n.k ni bei gani?

Piga nyongeza ya mshahara toa mfumuko wa bei uone km kuna la kumpa sifa. 😂 mafuta ya kula na sabuni tu vinamaliza kanyongeza kooote. Hakuna la maana hapo sifa alistahili endapo kusingekuwa na mfumko wa bei kiasi hiki.
 
Kwa hio watu wote 60m waajiriwe serikalini?
Au unatakaje boss?!
Ila kwa mbaaali nakuona una dalili za kuwa mchawi. Waache waliobahatika kuwepo serikalini wafaidi uwepo wa mama na we endelea kulima tumbaku mama atapandisha bei msimu huu.
Kwa mfumko huu wa bei watalia njaa kuliko awamu zote zilizowahi kuwepo. Mark my words si uzuri tuko nao kitaani.
 
Mleta mada unafugwa kwa shemeji yako mwajiriwa wa serikali?
Maisha yamekuwa ghali sana katika uongozi wake wewe unataka tumpongeze kwa kuongeza mshahara kwani yeye ndio wa kwanza kufanya hivyo?

Apunguze gharama za maisha tutampongeza.
Acha utoto na uchawa aisee.
 
Mleta mada unafugwa kwa shemeji yako mwajiriwa wa serikali?
Maisha yamekuwa ghali sana katika uongozi wake ww unataka tumpongeze kwa kuongeza mshahara kwani yeye ndio wa kwanza kufanya hivyo??
Apunguze gharama za maisha tutampongeza.
Acha utoto na uchawa wa kingese aisee.
Waambie urusi na Ukraine waache vita uone Kama bei haishuki
 
Sasa jpm ambaye alisahau wote
Alisahau wote lkn hakukuwa na mfumko wa bei kiasi hiki. Kwa kiasi kilichoongezeka na mfumko wa bei huu, walahi mtasema bora ya awamu za nyuma maana km ulikuwa unaingiza laki 5 ukatumia 4 na kubaki na laki 1, sa hivi ukiingiza laki 6 baada ya nyongeza utatumia laki 6 na 20 elfu ya kukopa 😂😂 we subiri tu ujionee mwenyewe. Yajayo yatafurahisha zaidi.
 
Alisahau wote lkn hakukuwa na mfumko wa bei kiasi hiki. Kwa kiasi kilichoongezeka na mfumko wa bei huu, walahi mtasema bora ya awamu za nyuma maana km ulikuwa unaingiza laki 5 ukatumia 4 na kubaki na laki 1, sa hivi ukiingiza laki 6 baada ya nyongeza utatumia laki 6 na 20 elfu ya kukopa 😂😂 we subiri tu ujionee mwenyewe. Yajayo yatafurahisha zaidi.
Hii Ni Vita ya urusi na Ukraine hupaswi kumlaumu Samia. Hata jpm angekumbwa na hii Vita Bei zingekuwa juu tu
 
Hii Ni Vita ya urusi na Ukraine hupaswi kumlaumu Samia. Hata jpm angekumbwa na hii Vita Bei zingekuwa juu tu
Tulia huko huna jipya! Vita na vorona lipi lilikuwa janga zito kwa ulimwengu? Na haka kangetufungia ndani walahi.
 
Wewe kwa mwezi unatumia mafuta ya kula kiasi gani? Unasafiri mara ngapi? Unatumia sabuni kiasi gani? Vyakula gharama yake sh ngapi? Sukari kiasi gani? Unajenga? Km ndiyo unajenga gharama za nondo, cement, bati, misumari, n.k ni bei gani? Piga nyongeza ya mshahara toa mfumuko wa bei uone km kuna la kumpa sifa. 😂 mafuta ya kula na sabuni tu vinamaliza kanyongeza kooote. Hakuna la maana hapo sifa alistahili endapo kusingekuwa na mfumko wa bei kiasi hiki.
Hizi hoja za kutumia bei za vitu kupima performance ya Leadership ya Samia ni dhaifu sana.

Mnatupa kupanda kwa nondo na simenti ili ku justfy hypothesis gani? Kwanza watanzania hawajengi kila siku, mtu akijenga mara moja imekwisha. Mnawatete watu gani hapa wanaoumia?

Kupanda kwa bei za vyakula kwangu naichikukia positively kwa vile wakulima wanapata bei nzuri ya mazao Yao.

Kupanda kwa bei za vitu ambavyo hatuna control kama bei ya petroli ni upuuzi kumlaumu Rais.
 
Hizi hoja za kutumia bei za vitu kupima performance ya Leadership ya Samia ni dhaifu sana.

Mnatupa kupanda kwa nondo na simenti ili ku justfy hypothesis gani? Kwanza watanzania hawajengi kila siku, mtu akijenga mara moja imekwisha. Mnawatete watu gani hapa wanaoumia...
Tuhakikishie faida ya ongezeko la mshahara kama vitu vimepanda bei. Amepunguza ukali wa maisha au ni dana dana tu? Mkulima nu fursa wapi wakati akipata faida ya elfu 10 haina faida kwenye matumizi ya kila siku.

Majibu kama ya mama au nchemba tu eti watanzania hawajengi kila siku, lini umekuta maduka ya vifaa vya ujenzi yamefungwa nchi nzima kuwa leo hawajengi?

Sa hivi hakuna unachoweza kusema una control nacho maana vimepanda vyote.
 
Tuhakikishie faida ya ongezeko la mshahara kama vitu vimepanda bei. Amepunguza ukali wa maisha au ni dana dana tu? Mkulima nu fursa wapi wakati akipata faida ya elfu 10 haina faida kwenye matumizi ya kila siku.

Majibu kama ya mama au nchemba tu eti watanzania hawajengi kila siku, lini umekuta maduka ya vifaa vya ujenzi yamefungwa nchi nzima kuwa leo hawajengi?

Sa hivi hakuna unachoweza kusema una control nacho maana vimepanda vyote.
Hivi shuleni ulisoma nini? Unamwaga pumba kama mfanyakazi wa zizi la mifugo!!
 
Hivi shuleni ulisoma nini? Unamwaga pumba kama mfanyakazi wa zizi la mifugo!!
Wenye fikra finyu ndo majibu yao haya hasa wakikosa maelezo ya maana ili kuficha upunguwani wao kwenye suala fulani ilimradi wakuzime! Kalia kushangilia tone la maji (nyongeza ya mshahara) kwenye bahari (mfumko wa bei).
 
Wenye fikra finyu ndo majibu yao haya hasa wakikosa maelezo ya maana ili kuficha upunguwani wao kwenye suala fulani ilimradi wakuzime! Kalia kushangilia tone la maji (nyongeza ya mshahara) kwenye bahari (mfumko wa bei).
Mbona hilo tone la maji mungu wenu wa Chato hakuliongeza kwa miaka yote 5 akiwa Ikulu?
 
Hakika mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Anachokifanya Rais Samia Suluhu Hassan kwa watumishi wa umma na wengine, hakiwezi kupita bila kuungwa mkono.

Rais Samia amefanya mambo makubwa sana kwa watumishi katika namna tatu.

Hivi karibuni Serikali ilitangaza ongezeko la kima cha chini cha mishahara kwa asimilia 23.3, kikokotoo cha mafao kupanda haki asilimia 33 kutoka asilimia 25 na posho ya safari kutoka Sh. 12,000 kwa mwezi hadi 250,000.

Hiyo ni kwa kiwango cha juu, lakini pia kutoka Sh. 80,000 hadi Sh. 100,000 kwa mwezi kwa watumishi wa kiwango cha chini na kusaidia kupunguza ukali wa maisha kwa watumishi nchini Tanzania.

Bila shaka, hatua alizochukua Rais Samia zinatokana na mabadiliko ya muda na mazingira hasa ukizingatia kwamba watumishi nchini Tanzania katika kipindi cha miaka sita hawajawahi kupanda ongezeko lolote katika mishahara yao.

Imani yetu kwa sasa sisi Watanzania ni kuona kwamba jambo kama hili linakwenda kutokea katika sekta binafsi pia. Ni ukweli usiopingika kwamba katika sekta binafsi ndiko kuna watu wanaolipwa mishahara mikubwa sana lakini pia ndio hukohuko wapo wanaolipwa mishahara midogo sana. Serikali tulivu ya Rais Samia, tunaamini kwamba muda hautokuwa mrefu sana hadi kusikia viwango vipya ya mishahara katika sekta binafsi.

Hatujaumbwa kuja kukosea tu, na watu tuliowapa dhamana kutongoza sio malaika, hivyo tuaamini kwamba wanakosea, na hapo tunawajibu wa kuwarekebisha. Kama tuna haki ya kuwarekebisha, basi tuwe waungwana pia kumwaga sifa pale wanapofanya vyema kulingana na matarajio yetu. Hiyo inawapa motisha wa kufanya kazi na kuujenga uzalendo zaidi mioyoni mwao.

View attachment 2244247

Mmeanza sifa za kijinga? Sifia wa maana uko kwenye ulaji. Sisi maisha yetu ni magumu hatuoni chochote cha kusifia.
 
Back
Top Bottom