Rais Samia aomboleza kifo cha Mwasisi wa CHADEMA, Edwin Mtei

Rais Samia aomboleza kifo cha Mwasisi wa CHADEMA, Edwin Mtei

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mzee Edwin Isaac Mbiliewi Mtei, kilichotokea usiku wa tarehe 19 Januari, 2026, jijini Arusha.

1768902222966.png

Kupitia ujumbe wake wa rambirambi, Rais Dkt. Samia amesema kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa niaba yake binafsi, anatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na wote walioguswa na msiba huo.

Rais Samia amemkumbuka marehemu Mzee Mtei kama mmoja wa watumishi na viongozi waliotoa mchango mkubwa katika ujenzi wa Taifa, hususan katika sekta ya fedha, mipango na uchumi. Amesema Mzee Mtei aliwahi kuhudumu katika nafasi mbalimbali muhimu ikiwemo kuwa Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuanzia mwaka 1966 hadi 1974, akishiriki kuweka misingi imara ya uendeshaji wa benki hiyo na uthabiti wa mfumo wa fedha nchini.

Aidha, Rais Samia amesema marehemu ataendelea kukumbukwa katika historia ya siasa za vyama vingi nchini, kama mmoja wa waasisi wa demokrasia ya ushindani wa vyama, akitajwa kuwa miongoni mwa waanzilishi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Rais ameongeza kuwa mchango wa Mzee Mtei utaendelea kuenziwa na vizazi vya sasa na vijavyo, hususan kupitia maandiko yake binafsi (autobiography) yanayoelezea safari ya maisha yake, utumishi wa umma na mchango wake katika ujenzi wa Taifa.

Katika hitimisho la salamu zake, Rais Dkt. Samia amewaombea faraja, nguvu na amani familia, ndugu na wafiwa wote, huku akimuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.

Pia Soma: TANZIA - Mwasisi wa CHADEMA, Edwin Mtei afariki Dunia

1768890706336.png
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mzee Edwin Isaac Mbiliewi Mtei, kilichotokea usiku wa tarehe 19 Januari, 2026, jijini Arusha.


Kupitia ujumbe wake wa rambirambi, Rais Dkt. Samia amesema kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa niaba yake binafsi, anatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na wote walioguswa na msiba huo.

Rais Samia amemkumbuka marehemu Mzee Mtei kama mmoja wa watumishi na viongozi waliotoa mchango mkubwa katika ujenzi wa Taifa, hususan katika sekta ya fedha, mipango na uchumi. Amesema Mzee Mtei aliwahi kuhudumu katika nafasi mbalimbali muhimu ikiwemo kuwa Gavana wa kwanza wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuanzia mwaka 1966 hadi 1974, akishiriki kuweka misingi imara ya uendeshaji wa benki hiyo na uthabiti wa mfumo wa fedha nchini.

Aidha, Rais Samia amesema marehemu ataendelea kukumbukwa katika historia ya siasa za vyama vingi nchini, kama mmoja wa waasisi wa demokrasia ya ushindani wa vyama, akitajwa kuwa miongoni mwa waanzilishi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Rais ameongeza kuwa mchango wa Mzee Mtei utaendelea kuenziwa na vizazi vya sasa na vijavyo, hususan kupitia maandiko yake binafsi (autobiography) yanayoelezea safari ya maisha yake, utumishi wa umma na mchango wake katika ujenzi wa Taifa.

Katika hitimisho la salamu zake, Rais Dkt. Samia amewaombea faraja, nguvu na amani familia, ndugu na wafiwa wote, huku akimuomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.

Pia Soma: TANZIA - Mwasisi wa CHADEMA, Edwin Mtei afariki Dunia
Mnafiki mkubwa
 
Rais ameongeza kuwa mchango wa Mzee Mtei utaendelea kuenziwa na vizazi vya sasa na vijavyo, hususan kupitia maandiko yake binafsi (autobiography) yanayoelezea safari ya maisha yake, utumishi wa umma na mchango wake katika ujenzi wa Taifa.
.....mkumbushe Mama yako kuwa hata kule maabusu anakomtesea Lissu ni nusu ya kifo! Unafiki haujawahi kuwa na mbadala!!!
 
"akitajwa kuwa miongoni mwa waanzilishi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)"

Kauli hii ina maana hawajui kama ni mwanzilishi au siyo? CCM mbona wanapenda sana kuvunjia heshima watu na taasisi wasio serikalini?

"amemkumbuka marehemu Mzee Mtei kama mmoja wa watumishi na viongozi waliotoa mchango mkubwa katika ujenzi wa Taifa, hususan katika sekta ya fedha, mipango na uchumi."

Hii sentensi ni kama vile shughuli zake za siasa hawajaziona za muhimu hadi wanakuja kuzitaja baadae kama "by the way...."

Pia, mbona hawajatoa salamu za pole specifically kwa CHADEMA na Mwenyekiti wake wa sasa? Nadhani protocal haijazingatiwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom