Kwa kutumia fagio hata lingekuwa la chuma kuna watu wangekuwa salama nionavyo anatumia reki la chuma na linapapatua kikweli kweli, japo wananchi wanaitazama hii movie ya Samialism baada ya Magufulism kusimamishwa na alie mbinguni ambayo ilikuwa inaelekea katika uchumi wa juu.
Tunaona baada ya Mheshimiwa Samia kunogewa na kazi ya uteuzi sasa ameshika kasi kubadilisha na kuondoa magome yaliyopevuka katika sehemu mbalimbali za nchi hii, kisemwacho kuwa walikuwa ni mirija ya magufulism. Hatutosikia kutuhumiwa kwa watu wanaoondolewa lakini wabobezi wa mambo ya ndani huwaga wanamwaga mtama.
Tufahamu kuwa Mheshimiwa Rais Samia sio chaguo ni mrithi, kama mambo yake yatakuwa supa katika kuinyanyua Tanzania na watu wake basi anaweza kuwepo madarakani kwa miaka 14, sijui katiba ikoje, ila kama akigombea rasmi 2025 ndio itakuwa ni Rais wa Kuchaguliwa.
Wacha amalize kuseti volume ya Serikali yake tuone kipya atakachokifanya, hadi sasa bado hajatulia na utamu wa uteuzi, lini atamaliza ni kitendawili, ila akitulia na baada ya siku mia, kipimo cha ufanisi wa uongozi wake ndio, utakaowapa dira Watanzania hapo 2025.
Hili reki lipite kwenye tume ya uchaguzi.
Tunaona baada ya Mheshimiwa Samia kunogewa na kazi ya uteuzi sasa ameshika kasi kubadilisha na kuondoa magome yaliyopevuka katika sehemu mbalimbali za nchi hii, kisemwacho kuwa walikuwa ni mirija ya magufulism. Hatutosikia kutuhumiwa kwa watu wanaoondolewa lakini wabobezi wa mambo ya ndani huwaga wanamwaga mtama.
Tufahamu kuwa Mheshimiwa Rais Samia sio chaguo ni mrithi, kama mambo yake yatakuwa supa katika kuinyanyua Tanzania na watu wake basi anaweza kuwepo madarakani kwa miaka 14, sijui katiba ikoje, ila kama akigombea rasmi 2025 ndio itakuwa ni Rais wa Kuchaguliwa.
Wacha amalize kuseti volume ya Serikali yake tuone kipya atakachokifanya, hadi sasa bado hajatulia na utamu wa uteuzi, lini atamaliza ni kitendawili, ila akitulia na baada ya siku mia, kipimo cha ufanisi wa uongozi wake ndio, utakaowapa dira Watanzania hapo 2025.
Hili reki lipite kwenye tume ya uchaguzi.