Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Mgombea Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi CCM Samia Suluhu Hassan amewataka wananchi wa Mtama Mkoani Lindi kujiandaa na ujio wa Bima ya afya kwa wote, ambayo amesema ndani ya siku mia moja za uongozi wake ikiwa atapewa ridhaa na watanzania, zoezi hilo la bima litaanza kwa majaribio ili kupima ufanisi wake.
Rais Samia amebainisha hayo leo Septemba 24, 2025 wakati akizungumza kwenye Uwanja wa Mtama, Wilayani Mtama Mkoani Mtama kwenye Mkutano wake wa kampeni, akiwataka wananchi kuhifadhi sehemu ya fedha watakayoipata wakati wa mavuno ya korosho ili kuweza kugharamia Bima hizo za afya zitakazosimamiwa na serikali ijayo ikiwa wananchi watakichagua Chama Cha Mapinduzi.
Rais Samia amebainisha hayo leo Septemba 24, 2025 wakati akizungumza kwenye Uwanja wa Mtama, Wilayani Mtama Mkoani Mtama kwenye Mkutano wake wa kampeni, akiwataka wananchi kuhifadhi sehemu ya fedha watakayoipata wakati wa mavuno ya korosho ili kuweza kugharamia Bima hizo za afya zitakazosimamiwa na serikali ijayo ikiwa wananchi watakichagua Chama Cha Mapinduzi.