Rais Samia aache kutuuzia Uoga

Ni vema akamtumbua Gavana wa Benki(BOT) na amteue Gavana ambaye amebobea kwenye uchumi. Kila siku shillingi ya Tanzania inashuka thamani. Thamani ya fedha ya Burundi ambayo ni nchi maskini inaizidi thamani ya shillingi ya Tanzania.
Yeye mwenyewe anapaswa kujiengua.
 
Kuna watu wanasema Zanzibar inaendelezwa kwa hii mikopo, ambapo japokuwa ina sura ya kitaifa, lakini ile asilimia wanayopewa Zanzibar inawainua sana. Na huu ni mkakati maalum, kwamba Samia achukue mikopo, na hata kama Zanzibar wanapewa 10% ya mikopo bado inawasaidia sana, bila kusahau jukumu la kulipa mikopo ni la Tanzania bara. Uliza Zanzibar kama Zanzibar nchi inachangia kiasi gani katika kulipa deni la Taifa - zero! Lakini tukichukua mkopo kuna asilimia lazima iende Zanzibar.Unaona walichofanya?
 
Wapo wazalendo wachache sana kama Traore, Faye wa Senegal. Ila ni kweli binadamu wengi ni wahuni hasa ukiwapa madaraka ya kifalme, yasiyo na mipaka, kuwafunga, kuua wapinzani wako bila kushtakiwa.

Hata upinzani ukiwapa hayo madaraka wata- behave the same way. Muhimu kuwe na katiba mpya proper checks and balance. Kama Nordic countries hasa nchi kama Switzerland. Kule wakiona uamuzi wako ni mbovu kwa maslahi ya taifa unapigiwa kura ya maoni na wananchi ukishindwa unaondolewa.
 
Shida nchi hii raia tupo kama wakimbizi
 
Mimi mwenyewe kila nikitaka kumlaumu kwa mambo yanayoendelea nakumbuka huyu uraisi aliuokota tu hakujiandaa kwa vyovyote vile acha tu amalize muda wake aondoke
Muda wake anaumaliza 2030. Huwezi kuona mengi anayoyafanya ukiwa umejifungia kwenye haya majiji makubwa, zunguka Tanzania nzima uone yanayofanyika.
 
Muda wake anaumaliza 2030. Huwezi kuona mengi anayoyafanya ukiwa umejifungia kwenye haya majiji makubwa, zunguka Tanzania nzima uone yanayofanyika.
Hatutaki anayofanya,tunaangalia trend ya household capacity,watu wengi wako kama vichaa wamevurugwa hawaoni future wanajipooza na Cuca pamoja na Kitoko
 
Kwanini Halembwe06, , tuna Tofauti gani na Raia wa Senegal, Burkina Faso?
Hatujui haki zetu za kiraia,Rais sio taasisi ya kujiamlia kila jambo mambo mengine ni ya mstakabri wa taifa zaidi,huwezi ongeza mgao wa Zanzibar kutoka 3,%hadi 10% bila kuwajuza walipa Kodi na bado wananufaika na madeni tunayokopa,tunapata nini in return, bara inashindwa kuhudumia taasisi zake na kuishia kutishia eti mashirika mzigo au kichefuchefu wakati Kuna taasisi za production direct na service direct.
 
Hii nchi tatizo kubwa Viongozi wanaotuongoza wanakua hawajajipanga alafu Dunia ya leo imebadilika sana
 
Baada ya Samia na Mkwe wake kuuharibu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Watanzania hawamuamini tena kusimamia Uchaguzi Mkuu.

NO REFORMS NO ELECTION ✌️
LINDA DEMOKRASIA 🤚
 

Elewa hivi Tanzania Rais ni kama Mungu, Mfalme, akilala na kuamuka anaweza kuamua chochote.

Hata kuuza nchi kama ananyofanya kwa ubinafshaji wake akiwatumia waarabu. Kafulila, Mwigulu, Kitila Mkumbo.

Tuwekeni mkataba tunapata nini, asilimia ngapi kwenye huu uwekezaji. Ni miaka mingapi, Return on investment.
 
Hiyo elimu, akili kujua rais ni mwajiliwa wao, kama kiongozi wa halmashauri hawana. Wanamuona kama ni Mungu.
 
Basi tufungue kesi ya kupinga haya
 
Basi tufungue kesi ya kupinga haya
Itasikilizwa na nani? Rais akimuambia hakimu sema hivi utashindana naye.

Rais ni Mungu Tanzania, mahakama zote haziwezi kumpinga rais. Akisema ufungwe hata kama ni kosa utafungwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…