Rais Mteule wa Zanzibar Dkt.Shein kuapishwa kesho

dubu

JF-Expert Member
Oct 18, 2011
3,502
3,483
Dr.shein.jpg

Rais Mteule wa Zanzibar Dkt.Ali Mohamed Shein anatarajiwa kuapishwa alhamisi asubuhi ambapo Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe.Othman Makungu atamuapisha katika sherehe zitakazofanyika uwanja wa Amani.

Kwa mujibu wa Makamu wa pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi ambaye pia ni mwenyekiti wa kamati ya sherehe ya kitaifa amesema maandalizi yanaendelea vizuri ambapo ametembelea uwanja wa Amani na kushuhudia harakati za sherehe hizo ambazo zitashirikisha vikosi vya ulinzi na usalama huku Balozi akiwataka Wazanzibar kujitokeza kwa wingi kushuhudia kuapishwa kwa Dkt.Shein.

Balozi Seif Ali Iddi akizungumzia uchaguzi mkuu uliomalizika juzi amesema Serikali imeridhika na jinsi uchaguzi huo ulivyosimamiwa,kwa vile ulikuwa wa amani na amewataka wananchi kuacha fikra na mazungumzo yasiyo na tija na sasa kushughulika na kazi za maendeleo kwa vile uchaguzi umekwisha na Rais ameshapatikana pamoja na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi.

Dkt.Shein ambaye ni Rais Mteule wa awamu ya saba anaapishwa kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi baada ya kushinda uchaguzi wamarudio wa jumapili kwa ushindi wa asilimia 91.4 na kuwaacha wapinzani wake kwa kiwango kikubwa.

Chanzo: ITV
 
Kwa wapenda demokrasia ya kweli, suala la Zanzibar na mchakato wake mzima wa uchaguzi, na matokeo yake, kiujumla ni pasua kichwa.

Sijawapatia picha wafuasi wa Cuf ni maumivu kiasi gani wanayapitia. Mungu awajalie ustahimilivu ktk kipindi hiki kigumu cha mpito.Kama kweli ilikua ni haki yao basi ipo siku bila shaka wataipata.
 
so wee ni mchawi or dada poa flani ivi??
Chochote kikujiacho akilini mwako ndio hicho
maana sipendi kuendelea kumjibu
mtu
Alie zaliwa kwa bahati mbaya
Anaishi kwa makusudi

Sent from my HUAWEI Y520-U22 using JamiiForums mobile app
 
Nimesikia Rais wetu mtetezi wa wanyonge atafunga safari kuelekea visiwani Zanzibar kushudia Dr.Ali Mohammed Shein akiapishwa kuwa Rais wa Zanzibar.
Mwenye taarifa zaidi atupe mchapo kamili isije kuwa ni tetesi tu.
 
Nimesikia rais wetu mtetezi wa wanyonge atafunga safari kuelekea visiwani kushudia shein akiapishwa kuwa rais wa zanzibar.
Mwenye taarifa zaidi atupe mchapo kamili isije kuwa ni tetesi tu.
Hii siyo tetesi mkuu, ni hali halisi. Lazima amir jeshi mkuu awepo kuangalia usalama kwa mtu yeyote atayeleta fyoko fyoko.
 
Katika vitu ambavyo sivielewi mpaka sasa ni pale CUF wanapoitafuta haki kwa amani wakati wakiona CCM wanamwapisha mteule wao.
Wakati huo huo nchi hizo mnazotegemea kuwasaidia zinaishia kutoa matamko na mwisho wa siku watakubaliana na serikali iliyopo madarakani.
Kuzira kwa maalim seif kumewapotezea na hata wawakilishi wa CUF ndani ya baraza!ina maanisha CCM wamepewa rasmi uwezo wa kutunga sheria zote bila kupata ushindani.Mnategemea hizo sheria zitakazotungwa huko barazani zitawaacha salama wana CUF!
N:B ngoja tuangalie gwaride la utii kutoka uwanja wa Amani Zanzibar
 
Katika vitu ambavyo sivielewi mpaka sasa ni pale CUF wanapoitafuta haki kwa amani wakati wakiona CCM wanamwapisha mteule wao.
Wakati huo huo nchi hizo mnazotegemea kuwasaidia zinaishia kutoa matamko na mwisho wa siku watakubaliana na serikali iliyopo madarakani.
Kuzira kwa maalim seif kumewapotezea na hata wawakilishi wa CUF ndani ya baraza!ina maanisha CCM wamepewa rasmi uwezo wa kutunga sheria zote bila kupata ushindani.Mnategemea hizo sheria zitakazotungwa huko barazani zitawaacha salama wana CUF!
N:B ngoja tuangalie gwaride la utii kutoka uwanja wa Amani Zanzibar


vipi mabalozi na walezi wetu wamekubali kuja???
 
Kwani lile agizo la watumishi wa serikali kutotoka nje ya nchi ameshalitengua?
 
Uwanja umejaa kulinganisha na upi au nini!!

Mafisi mwachage ungese.....
 
Back
Top Bottom