Rais Magufuli: Wakulima pandisheni bei za mazao kadri mtakavyo

Kigodoro

JF-Expert Member
Apr 25, 2014
1,660
1,676
Yuko mubashara Star Tv Anahutubia. Ameongeza kuwa huu ndiyo muda wa wakulima waliotunza mazao yao kutajirika.

"Asitokee kiongozi akawapangia bei ya mazao yenu", alisisitiza rais.

"Ikibidi mbadilishe debe moja la mahindi kwa ng'ombe 3", vicheko vikasikika.

=========

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli, amewataka wakulima nchini kupandisha bei ya mazao kadri watakavyo kutokana na nguvu kubwa wanayoitumia katika uzalishaji wa mazao hayo.

Amesema hayo mara baada ya kuwepo malalamiko ya kupanda kwa bei za mazao mbalimbali hasa mahindi na mchele kutokana na upatikanaji wake kuwa mdogo.

"Wakulima pandisheni bei ya mazao kwa kiwango mnachotaka bila kuzuiliwa na mtu wala kiongozi yeyote wa serikali, mmekuwa mkipata shida nyingi kuhangaika hadi kuzalisha mazao hayo, huu ni mwaka wa neema kwa wakulima, tumieni fursa hii pandisheni bei za mazao kadri mnavyotaka,"amesema Rais Magufuli.

CHANZO: JPM: Wakulima pandisheni bei mtakavyo
 
Kwa upande mmoja yuko sahihi kabisa, ingawa niko nje ya nchi na nimebahitika kununua kajishamba huko vijijini na nikajionea mimi mwenyewe jinsi watu walivyokua wavivu.

Mfano kuna kipindi hatukulima Shamba lote lakini hakuna hata mtu aliojitokeza na kuomba alime hilo eneo lililokua wazi, licha ya kuwaambia badhi ya ndugu na majirani, mwenye uwezo ajilimie hata nusu heka, lakini nilionekana mi ni mjinga, mtu anakujibu sina uwezo wa kulima, yaani mtu mwenye nguvu zake kabisa eti hana uwezo, kazi kukaa maskani na kulalamika hali ngumu.

Niliomuajiri Shamba alishindwa hata kujilimia mboga licha ya kuwepo maji ya kisima.
Kuna kijana mmoja tu kanisikiliza na yeye sasa anafaidi matunda ya ukulima, nimejaribu kumfundisha jinsi ya kulima kila Aina ya mboga pale kwake, na sasa anapanda hadi viazi kwenye magunia, amepynguza asilimia kubwa sana ya budget ya manunuzi huko sokoni.

Ndugu Watanzania tujifunze kujituma na tuwe wabunifu pale maisha yanapokua magumu. Hakuna cha bure.
 
ingependeza zaidi kama mheshimiwa angeacha mipasho na kejeli zisizo na maana kwa wananchi yake ambao ni masikini kwa hiyo inabidi aongozwe na busara na hekima

hivi aliposema kuwa yeye ni kiongozi wa wanyonge alimaanisha wanyonge wapi? au ni kiongozi wa wanyonge wa kufikiri?
 
Hahajaaaa aisee! Hapa tumepata kweli na tumepatikana kweli ila akumbuke asijisifu ana mbio amsifu na anayemfukukuza
 
Huyo atakae kubali kupokea ng'ombe na kutoa mahindi lazima ana akili za alietoa wazo hilo, ng'ombe wanakufa kwa kukosa chakula wewe upokee ng'ombe kwa kutoa chakula?! wasukuma watakuwa na tatizo ndio maana majanga kwenye ukanda wao hayaishi., hayo mahindi basi ni bora uwape hao ng'ombe wa jirani wale ujue umenusuru mifugo kuliko kuichukua kuja kuiulia kwako.
 
Huyo atakae kubali kupokea ng'ombe na kutoa mahindi lazima ana akili za alietoa wazo hilo, ng'ombe wanakufa kwa kukosa chakula wewe upokee ng'ombe kwa kutoa chakula?! wasukuma watakuwa na tatizo ndio maana majanga kwenye ukanda wao hayaishi., hayo mahindi basi ni bora uwape hao ng'ombe wa jirani wale ujue umenusuru mifugo kuliko kuichukua kuja kuiulia kwako.
NDUGU nilikuwa naandika post kama ya kwako.....sina haja ya kuongezea chochote
 
Wanyonge,wanyonge.si wavivu.angalia por lililoko toka segera mpaka chalize,watu awalim nikasema hili por kwanini alikua kwetu kilimanjaro?
 
MTU ukikosa busara na hekima ni hatari, sasa ndio najua kwanini mfalme Suleiman aliomba hekima na si Mali.

Kwanza bwana huyu hajui kuwa kwasasa wanaofaidi si wakulima wanyonge waliompigia kura bali ni wafanya biashara matajiri walioweza kukusanya chakula na kuvihifadhi.

Je anafurahia hii hali ya kupanda bei ya chakula na watu kutaabika huku matajiri wakineemeka?
BURE kabisa
 
Back
Top Bottom