Rais Magufuli usilie pesa "ukizichimbia" Benki Kuu, hazitazalisha faida. Jifunze kwenye hadithi ya talanta kwenye Biblia

Jana nimemsikia JPM akilalamika kwamba uzalishaji ni mdogo hivyo hawezi kuongeza mishahara ya watumishi wake

Nakumbuka awamu ya tano ilikuja na mkwara mkubwa wa kuondoa fedha zote za serikali katika mzunguko kwa mara moja,wataalamu walionya kwamba kutatokea athari kubwa sana kiuchumi kwa kuwa kimsingi,serikali ndio mwanahisa mkuu wa uchumi wa nchi na kwa vyovyote vile akijiondoa lazima kampuni iyumbe na kisha ife

Serikali ilipoondoa fedha katika mabenki na kuzipeleka Benki Kuu,ni wazi kuwa kule zimelala tu na kuozeana,haziingizi faida kwa serikali wala katika uchumi wa mtaani,hii ni tofauti na pale zilipokuwa katika mabenki ya kibiashara ambapo zilikuwa zinakopeshwa kwa wenye viwanda na wajasiliamali ambao walizizungusha na zikaleta faida kubwa,mjasiliamali alikopa,akafungua biashara,akalipa leseni ,kodi,tozo,zote zinaenda serikalini,hapa maana yake pesa hiyo imezaa kwa serikali kupata kodi,na maana yake uzalishaji umeongezeka,watumishi wataongezewa mishahara kutokana na fedha hiyo kuzunguka

Pia serikali kama imeweka fedha hiyo katika fixed deposit,nako fedha hii ingezaa riba,kwa hiyo kotekote serikali ingekula,kuna taarifa kwamba yale mashirika yaliyolazimishwa kupeleka fedha benki kuu yameomba kibali cha kutumia fedha ya mtaji ili kulipana mishahara,wakati zamani ile faida ya fixed deposit ilitosha kulipa mishahara bila kugusa mtaji,taarifa zilizopo zinaonyesha yameruhusiwa kutumia si zaidi ya asilimia 15 ya mapato kulipana mishahara

Nakumbuka Beno Ndulu,Gavana wa Benki Kuu pamoja na Bodi ya wana uchumi sugu waliokuwa TRA walikwazana naye mpaka akaivunja Bodi

Natoa wito kwa JPM,rudisha mzunguko wa fedha ili zizaane na uzalishaji wa kiuchumi uongezeke ulipe watumishi wako,vinginevyo utapaona ofisini pachungu kwa kukosa hela

Naifananisha amri yako ya kuweka fedha Benki Kuu na ile habari ya talanta kwenye Biblia,kuna mmoja alipewa hakuizalisha bali aliifukia chini ,wenzie wawili wakazalisha na wakapongezwa,yule aliyeifukia alifokewa na kutimuliwa na bosi wake

Taratibu naona waajiri wako wananchi wanaanza kufoka na kunun'gunika,wamekupa talanta,wanaona haizai

Mwisho kabisa,serikali na wananchi has a sekta binafsi,tunajenga Nyumba moja,acha kugombea fito,toa fito zako benki kuu,lete uraiani tuendelee na ujenzi
Mbona hujaifafanua vizuri hio hotuba ulimsikia????
BENKI ILIWEZA KUJIENDESHA KWA PESA ZETU WENYEWE..
YAANI IMETOLEWA MIL600 IPELEKWE HALMASHAURI YA MKOA FLANI.
HIO PESA IKAZUILIWA NA MTU MMOJA NA AKAIWEKA BANKI KWA MIEZI 6. HAPO ATAVUTA RIBA(intres)HAJALI UCHELEWESHAJI WA MISHAHARA YA WAFANYAKAZI WA HALMASHAURI.
AKISHAVUTA RIBA YAKE BAADA YA MIEZ 6 HIO PESA ANAIREJESHA HALMASHAURI .
HAPO HATA MFANYA MAHESABU WASERIKALI HATOGUNDUA KAMA KUNA SHOTI.ISIPOKUA NI UCHELEWESHWAJI WA HIZO PESA
KWA MANTIKI HIO HIZI BANKI ZILIKUA ZIKIFANYA BIASHARA NA HELA ZA SERIKALI(ambazo ni.Pesa zetu sisi walipa kodi)
KWA AWAMU HII HAIPO.HIO DILI.
NDIO MAANA WANAJILIZA LIZA KUA WANAFILISIKA..

Mleta mada fafanua ki hivi Mkuu
 
JPM anachofanya anapunguza kwa kiasi kikubwa matumizi ya uendeshaji serikali; kuweka fedha benki kuu ni kudhibiti matumizi mabovu za fedha zilizokuwa zikifanywa. Awamu hii watanzania tutegemee kuona miradi mikubwa ya serikali ikifanyika.
 
Kila Kiongozi ana njia yake ya kufikiri. Tumuache Raisi Magufuli afanye hivyo anavyoona yafaa. Baadae tutajua ilikua njia sahihi au la. Ila mnaruhusiwa kukosoa sio kukasilika. Kama Uchumi Mgumu ulikuwepo toka tawala zilizopita na hadi sasa tunasonga nao hivyo hivyo.
 
Kuna kauli moja ya malema kuhusu mtu mjinga kutokujua jinsi anavyokwaza watu., ndio yanayoendelea
 
Hivi....ah basi...lisije likawa swali la kichokozi...ila natamani wachumi wabobezi kama Prof Lipumba waje hadharani kutuambia hali ya uchumi wa nchi yetu especially money circulation , maana sasaivi kila MTU anaongea yake...tunachanganyana tu, nini kazi ya washauri wa uchumi? Mm ni mchumi mdogo sio mbobezi...sina data kwasasa...ila kwakuwa watu wanalalama na kujiuliza maswali na kujijibu wenyewe, vema akina Prof waje na majibu stahiki.
 
Uzuri wa system ya uchumi wa mzee ni uwezekano wa serikali kuwa na uwezo mkubwa kufanya big investments kwa ajili ya taifa, ambayo itasaidia kurelease fedha kwa wananchi. Labda tutegemee projects kubwa kubwa zikiwezekanika , ikifanya yenyewe au kwa ushirika na washirika wa nje...kumbuka serikali ikiwa na uwezo kipesa ni rahisi kuimplement miradi ya maendeleo na zaidi kuvutia wabia wakubwa wa maendeleo kusapoti miradi hiyo. Unaweza kushangaa reli zikatandazwa nchi nzima...viwanja ndege nchi nzima, ndege kufika hadi malinyi kwenu....viwanda vikubwa vikajengwa hapahapa Tz, hasa vile vitumiavyo raw materials za nchini mwetu...hivyo ktk kipindi hiki, Mzee hataki kuomba omba ovyo...anatubana ili apate pesa ya kutosha imsaidie amapotekeleza miradi hiyo...wabia au wafadhili wamkute kaanza au anao uwezo wa kuanza...nakwambia watagombania tenda....baada ya mda, miaka kadhaa ndo tutaona matunda yake...
 
Wewe utakuwa mchochezi!Je wewe ni mtaalamu wa kila fani?Acha mtaalamu atufikishe tunakotakiwa kwenda na atakayekwamisha hii safari atakwama yeye.Nimesahau kanuni ya saikolojia hebu nikumbusheni,hivi kutenda na kufikiri kwa kina ni kipi inabidi kianze?
 
IMG-20171005-WA0005.jpg
Magu anajisikia faraja mijinoti kulala BOT kama hivi. Misguided!
 

Attachments

  • IMG-20171005-WA0005.jpg
    IMG-20171005-WA0005.jpg
    20.9 KB · Views: 27
Acha kazi ifanyike kwa njia zake.Awamu zote haikuwepo Tanzania ya viwanda.Basi ni dhahiri haya yooote uyaonayo ni kwaajili ya kuwa na Tanzania ya viwanda.Je wewe haupendi Tanzania ya viwanda?Najuwa haya hukuwahi kuyaona before,ni kutokana na kipindi kile haikuwapo Tanzania ya viwanda.
 
World Bank ilitahadharisha kuwa mbinu anayoitumia haijawahi kufanikiwa mahali popote Duniani. Tatizo kubwa alilo nalo ni mgumu sana kukiri kosa.

Mahusiano ya kiuchumi siyo rahisi kama anavyofikiria. Ndiyo maana unaweza kufanya kitu fulani kwa mtu fulani Dar, ukitegemea atalia lakini cha ajabu ukakuta mtu wa Chato au Muze anatoa machozi na kupiga kelele kubwa, huku yule wa Dar uliyemtegemea alie, akawa ametulia tu, hacheki wala halii.
trickle down effect, sijui kama Baba jesca anayajua haya???
 
Uzuri wa system ya uchumi wa mzee ni uwezekano wa serikali kuwa na uwezo mkubwa kufanya big investments kwa ajili ya taifa, ambayo itasaidia kurelease fedha kwa wananchi. Labda tutegemee projects kubwa kubwa zikiwezekanika , ikifanya yenyewe au kwa ushirika na washirika wa nje...kumbuka serikali ikiwa na uwezo kipesa ni rahisi kuimplement miradi ya maendeleo na zaidi kuvutia wabia wakubwa wa maendeleo kusapoti miradi hiyo. Unaweza kushangaa reli zikatandazwa nchi nzima...viwanja ndege nchi nzima, ndege kufika hadi malinyi kwenu....viwanda vikubwa vikajengwa hapahapa Tz, hasa vile vitumiavyo raw materials za nchini mwetu...hivyo ktk kipindi hiki, Mzee hataki kuomba omba ovyo...anatubana ili apate pesa ya kutosha imsaidie amapotekeleza miradi hiyo...wabia au wafadhili wamkute kaanza au anao uwezo wa kuanza...nakwambia watagombania tenda....baada ya mda, miaka kadhaa ndo tutaona matunda yake...
hizo hadithi za kufikirika ni bahati na hasibu approach, approach nzuri ni bottom up siyo top down, hayo mavitu yatakuja kuwa white elefant
 
Kuna kitu hamjakijua kuhusu huyu mtu, huyu mtu raha yake ni pale anapomuona binadamu mwenzake anapata taabu! hapo ndo roho yake inasuuzika.
 
Jana nimemsikia Rais Magufuli akilalamika kwamba uzalishaji ni mdogo hivyo hawezi kuongeza mishahara ya watumishi wake

Nakumbuka awamu ya tano ilikuja na mkwara mkubwa wa kuondoa fedha zote za serikali katika mzunguko kwa mara moja,wataalamu walionya kwamba kutatokea athari kubwa sana kiuchumi kwa kuwa kimsingi,serikali ndio mwanahisa mkuu wa uchumi wa nchi na kwa vyovyote vile akijiondoa lazima kampuni iyumbe na kisha ife.

Serikali ilipoondoa fedha katika mabenki na kuzipeleka Benki Kuu,ni wazi kuwa kule zimelala tu na kuozeana,haziingizi faida kwa serikali wala katika uchumi wa mtaani,hii ni tofauti na pale zilipokuwa katika mabenki ya kibiashara ambapo zilikuwa zinakopeshwa kwa wenye viwanda na wajasiliamali ambao walizizungusha na zikaleta faida kubwa,mjasiliamali alikopa,akafungua biashara,akalipa leseni ,kodi,tozo,zote zinaenda serikalini,hapa maana yake pesa hiyo imezaa kwa serikali kupata kodi,na maana yake uzalishaji umeongezeka,watumishi wataongezewa mishahara kutokana na fedha hiyo kuzunguka

Pia serikali kama imeweka fedha hiyo katika fixed deposit,nako fedha hii ingezaa riba,kwa hiyo kotekote serikali ingekula,kuna taarifa kwamba yale mashirika yaliyolazimishwa kupeleka fedha benki kuu yameomba kibali cha kutumia fedha ya mtaji ili kulipana mishahara,wakati zamani ile faida ya fixed deposit ilitosha kulipa mishahara bila kugusa mtaji,taarifa zilizopo zinaonyesha yameruhusiwa kutumia si zaidi ya asilimia 15 ya mapato kulipana mishahara.

Nakumbuka Beno Ndulu, Gavana wa Benki Kuu pamoja na Bodi ya wana uchumi sugu waliokuwa TRA walikwazana naye mpaka akaivunja Bodi.

Natoa wito kwa JPM,rudisha mzunguko wa fedha ili zizaane na uzalishaji wa kiuchumi uongezeke ulipe watumishi wako,vinginevyo utapaona ofisini pachungu kwa kukosa hela.

Naifananisha amri yako ya kuweka fedha Benki Kuu na ile habari ya talanta kwenye Biblia, kuna mmoja alipewa hakuizalisha bali aliifukia chini ,wenzie wawili wakazalisha na wakapongezwa,yule aliyeifukia alifokewa na kutimuliwa na bosi wake.

Taratibu naona waajiri wako wananchi wanaanza kufoka nakunun'gunika, wamekupa talanta,wanaona haizai.

Mwisho kabisa,serikali na wananchi has a sekta binafsi,tunajenga Nyumba moja,acha kugombea fito,toa fito zako benki kuu,lete uraiani tuendelee na ujenzi.

Wale waliokuwa wakila fedha ya umma walikuwa wana dharau WaTanzania, Serikali na nchi yetu. Ngoja zifungiwe kwanza ili waheshimu subira yetu iliyokuwepo. Mzee mmoja alienda Uingereza kikazi. Hotelini Mjini London aliingia mtu mmoja. Mtu Yule baada ya kusikia kuwa Mgeni ni Mtanzania alisema papo hapo: "Oh! Tanzania made me richchchch!" Yaani: " Oh! Tanzania ilinitajirisha!" Mtamkumbuka Maghufuli miaka mingi baada ya kumaliza mihula yake. Leo mtamwona tofauti sana. Amerudisha heshima ya taifa letu.
 
Wale waliokuwa wakila fedha ya umma walikuwa wana dharau WaTanzania, Serikali na nchi yetu. Ngoja zifungiwe kwanza ili waheshimu subira yetu iliyokuwepo. Mzee mmoja alienda Uingereza kikazi. Hotelini Mjini London aliingia mtu mmoja. Mtu Yule baada ya kusikia kuwa Mgeni ni Mtanzania alisema papo hapo: "Oh! Tanzania made me richchchch!" Yaani: " Oh! Tanzania ilinitajirisha!" Mtamkumbuka Maghufuli miaka mingi baada ya kuwalaza mihula yake. Leo mtamwona tofauti sana. Amerudisha heshima ya taifa letu.
Una kipindupindu cha akili?
 
magu hasikii inaonesha anakisimamia anachokiamin hata kama no kitu cha kijinga, tumwache na ujinga wake wa kutotaka kuelewa
 
Una kipindupindu cha akili?
Una kipindupindu cha akili?


Elezea basi jinsi kipindupindu hicho cha akili kilivyo. Marekebisho ya uchumi huwakumba wote waliomo katika uchumi husika. Hauchagui. Kwa taarifa yako wengi wamekimbia nchi wakilalamikia kodi na mianya ya ya ulaji kufungwa. Mitikisiko ya aina hii imetokea nchi nyingi tu hasa serikali zinapobadilika. Unapotaka kuzuia nyufa zilizowezesha kuibiwa kwa mali zetu watakaoathirika ni wengi lakini kwa muda.Uganda alipoingia Museveni hilo lilitokea lakini baada ya muda UGANDA ikatulia. Umesikia juzi tu mapato ya Tanzanite yameanza kuonekana! Hata Rwanda baada ya a kuingia Kagame Marekebisho mengi ya uchumi yalifanyika na sasa wametulia. Na sisi tutatulia. Nimetumia lugha nyepesi ili nieleweke.. Sasa kipindupindu changu kipo wapi..
 
Back
Top Bottom