Bashe amefanyia kazi zile semi za 'mtumikie kafir upate mradi wako' na 'ukienda Roma ishi kama wa Roma'....sasa yupo mezani ametulia tuli anachapa zake pork chop kwa kwenda mbere.
Aisee! Wewe kweli duuh! Noma sana. Aisee una mawazo ya kikamba kweli.
No, ulimwengu wa leo hauko hivyo. Unajua, nilitegemea vijana wa leo kama nyie sio kuwa watu tena wa kuwaza upuuzi kama huo. Enzi zetu za Mwalim Nyerere ningeweza sema uko right, lakini katika karne hii 21 na maendeleo yote haya ya teknolojia katika kitengo cha mawasiliano, nisinge tegemea kusikia kijana kama wewe ukiwa na mawazo haya.
Nyie vijana wa leo mna bahati kubwa sana ya kuishi katika bahari ya Information Technology kifupi IT. Kwa hali hiyo nilitegemea nyie kuwa watu wenye mawazo mapana sana ya maisha, kwani mnashuhudia mengi yanayo tokea ulimwenguni kupitia hiyo Technology development. Kwa hali hiyo nina uhakika kuwa katika Generation yenu nyie sio watu tena wa kuburuzwa buruzwa kama enzi zetu sisi.
Nyie ni vizazi vya watu wa kujiamini sana na watu wenye msimamo mkubwa, kwani mara nyingi mna tetea mawazo yenu kwa hali na mali kwa kutumia mifumo ya kisasa ya mawasiliano ya habari
Nasema haya kwa sababu naona hivi sasa Europe pia, jinsi gani teen agers wanavyo kuwa mashupavu katika kushikilia ideology yao ya mazingira.
Yalianza na msichana wa kiswidish mwenye umri wa miaka 16 Greta Thunberg huko Stockholm, Sweden na kusambaa Europe nzima, hasa huko Ujerumani ndiyo mambo moto moto. Wanafunzi wa shule za msingi, Secondary na hata high schools baadhi ya siku hawaendi shule wakidai upatikanaji wa ufumbuzi wa matatizo yanayo ikabali dunia kutokana na climate changes.
Naibu Waziri mpya wa Kilimo Mh. Bashe nahisi sasa yuko katika nafasi ambayo nyota yake ilikuwa ina mwongoza. Nategemea atajitahidi kuyatekeleza yale ambayo mwenyeezi Mungu amempangia kuyatekeleza kwa manufaa yetu wote.
Sisi tunacho taka ni maendeleo yetu watanzania kama ambavyo Rais wetu mpendwa ameyaanzisha na sisi wote kushuhudia.
Kuwa positive na mpe naib waziri nafasi.
Nilitegemea Rais Magufuli angeyafanya haya yote kwa mda mfumo hivi? Sidhani! Lakini kwa ujasiri wake kama binafam na mwanamme mwenye msimamo amefanikisha.
Hizi ndiyo tabia za majasiri ya wenzetu wazungu walio waletea wenzao maendeleo. Tukiendelea hivi nafikiri Tanzania tunaweza tukiwa trend setter wa mabadiliko ya maisha ya watu warusi Afrika. Ngoja tuone!! Mimi generally niko very very optimistic na haya ambayo Rais wetu Buldozer ameyaanzisha.
Namwombea uzima na afya njema ili aendelee kutuleta maendeleo chanya na hivyo ukombozi wa maisha bora na uhuru wa kiuchumi.