Rais Magufuli ulituahidi wana-Arumeru kututetea na kutusemea! Tafadhali sema neno uovu na dhuluma hii itakoma!

amanison

Member
Jul 31, 2015
10
3
Mh,Raisi,ulipokuwa wilayani Arumeru kuzindua mradi mkubwa wa maji, ulitamka maneno magumu na mazito kwa akili za wengi kuyaelewa! Lakini kwetu sisi tuliona pengine kilio na machozi yetu ya muda mrefu, ya zaidi ya miaka 26, ya kukandamizwa,kupigwa,kufungwa na kudhulumiwa ardhi yetu yamefika kitini mwa Mwenyezi Mungu. Naye anataka kupitia kwa mkono wako ayafute machozi yetu!!

Mh,Raisi wetu mpendwa,mbali migogoro kadhaa inayosumbua wilaya yetu, upo mmoja ambao usingelipaswa hata kidogo kuwepo.Nao Ni wa shamba la Arusha Coffee estate ex.112. lililoko katika kitongoji Cha Maksoro na Moivaro,katika Kijiji Cha Nguruma wilayani Arumeru!

Shamba hilo lenye eka 721 katika hali isiyo ya kawaida,limeshafutwa (revocade) Mara 2.mwaka 1990 na baadae 2001.sababu ya kufutwa Mara mbili Ni kukengeushwa kwa maagizo halali ya serikali kuu na kutoa shamba hilo kwa mtu mmoja badala ya kuwapa wananchi Kama ilivyokuwa imeagizwa!

Na hapa ndipo, chanzo kikuu Cha madhila mabaya na maovu makubwa mno yalipo Anza kutupata wananchi tuliokuwa tayari tumeshajenga makazi ya kudumu hapo.watesi wetu walitumia nguvu ya dola na hata vijana wa kukodi kutuhamisha,kubomoa,vipigo kesi za kumbikwa nk, ilimradi tusalimu amri. Kwa jinsi mateso na kilio Cha wanachi kilipoongezeka, hatimae serikali ya mweshimiwa Mkapa, ilionelea ifute kwa upya kwa kufuata hatua zote za kisheria(nyaraka zote tunzo), na mnamo mwaka 2001 serikali kuu ikawaagiza serikali ya wilayani ya AruMeru kugawia wananchi shamba hilo bila Jambo jingine lolote...!!(kwa maneno mengine mgogoro wa shamba hilo ulimalizwa tangu 2001)

Rais huwezi Amini,mpaka sasa haki hiyo haijatolewa!!!!!na hakuna sababu yeyote ya msingi.

Raisi wetu,katika kufuatilia haki hiyo iliyowazi, tulibahatika kufika Dodoma tukiwa na aliyekuwa mwenyekiti wa kitongoji hicho (CCM)kwa kipindi chote Cha mgogoro, na ambàye Ni makamu kamati hii,Mzee Charles Amosi, tukafanikiwa kukutana na Mh.Ashasante Nditie,kipindi hicho akiwa mwenyekiti kamati ya ardhi ya Bunge,na sasa naibu waziri. Pia mh. William Lukuvi waziri wa ardhi.kwa pamoja na kwa namna tofauti walitusaidia Sana.

Waliridhishwa na vielelezo na documents zetu zote.Mh. Lukuvi, kiukweli alihuzunishwa na madhila tulofanyiwa na akasema hakukuwa na sababu yeyote ya kwamba kwanini tusiwe tumeshagawiwa ardhi hiyo,na pia hakukuwa na sababu hata ya Rais Mkapa kufuta hati kwa Mara ya pili.kutokana na uzito wake, aliahidi atakapopata nafasi nzuri atakuja mwenyewe kutukabidhi na kuwashuhulikia waliofanya mchezo huo muovu.lakini mpaka sasa bado hatujafanikiwa!

Mh, Raii,pamoja na hayo yote, tulishawashinda Hawa watesi wetu Mara kadhaa mahakamani,pale walipotushtaki kwa kuingia kwa sehemu katika shamba hilo. Kila Mara walishindwa kwa kupeleka nyaraka za kufoji.na hivyo Mahakama kutupilia mbali mashtaka na haki kubaki kwa wananchi.! Kwa huzuni bado hutapewa haki hiyo!

Mh Rais, kilio chetu kwako, useme neno tu, kwa Hawa wateule wako hapa wilayani, mh Jerry Muro na mkurugenzi wake ambao ndo wenye dhamana hiyo kisheria, ili tupate kupona!! Maana tunawindwa usiku na mchana sisi tuliojitoa mhanga kwa ajili ya wananchi wetu, wakiwemo yatima na wajane!

Nimalizie kwa kukushukuru, na kuomba radhi kwa kutumia njia hii.hakuweza kupata namna nzuri zaidi ya kukufikia.::(tunaamini hata wasaidizi wako wakiona watakuletea mezani kwa uone maajabu yanayotendewa watu wako huku chini)
Mungu akubariki Sana!!

Ni Mimi Mchungaji Eliudi Kaaya
(0756579200)
Mwenyekiti kamati ya mgogoro huo!
kjh
 

Attachments

  • IMG_20181210_091555_3.jpg
    IMG_20181210_091555_3.jpg
    105.5 KB · Views: 26
Hii taarifa kanitoa machozi mchungaji, kwani hao watesi wenu ni kina nani na kwani wako na nguvu aina gani hizo, hamna mbunge ambae anaweza hika kwa mkuu wa mkoa, na kisa mkuu wa mkoa kutoa amri kwa mkuu wa wilaya, lakini lingine mchungaji ni hili, pengine hao watesi wenu wanajuana na wakuu wa ccm, na kaa iko hivyo hata magufuli hawezi fanya kitu, but i wish you all the best
 
Hii taarifa kanitoa machozi mchungaji, kwani hao watesi wenu ni kina nani na kwani wako na nguvu aina gani hizo, hamna mbunge ambae anaweza hika kwa mkuu wa mkoa, na kisa mkuu wa mkoa kutoa amri kwa mkuu wa wilaya, lakini lingine mchungaji ni hili, pengine hao watesi wenu wanajuana na wakuu wa ccm, na kaa iko hivyo hata magufuli hawezi fanya kitu, but i wish you all the best

..Kiukweli hili Jambo Ni vigumu kulielezea kwa maneno machache. Lakini niseme tu mbunge wa Arumeru amelipigania sana.si hili tu hata na migogoro mingine inayofananafanana na huo. Lakini hatujafanikiwa. .!
Kuhusu mweshimiwa Raisi kushindwa, hatudhani hata kidogo!
Hatuamini Kama Yuko Raisi ama kiongozi yeyote Duniani anaweza kuvumilia uovu wa aina hi unaotedwa chini yake labda Kama yeye binafsi Ana maslahi ya mojakwa moja na mradi huo.!Maraisi Wana fursa zote katika nchi.hata akiwa fisadi huwekeza mahali hagusi yatima,wajane na maskini mojakwamoja. Kwani wanajua Hawa hutetewa na Mungu peke yake.Na malipo yake huwa Ni hapa hapa Duniani, na kumalizia huko tuendako!

Raisi, wetu amejipambanua kwa kuwa kinyume na mambo kama hayo. Na hi ni mojawapo ya sifa muhimu iliyompa madaraka aliyo nayo.hivyo hatuamini Kama akipata taarifa hi atakuwa na dakika ya kusubiri zaidi!
 
..Kiukweli hili Jambo Ni vigumu kulielezea kwa maneno machache. Lakini niseme tu mbunge wa Arumeru amelipigania sana.si hili tu hata na migogoro mingine inayofananafanana na huo. Lakini hatujafanikiwa. .!
Kuhusu mweshimiwa Raisi kushindwa, hatudhani hata kidogo!
Hatuamini Kama Yuko Raisi ama kiongozi yeyote Duniani anaweza kuvumilia uovu wa aina hi unaotedwa chini yake labda Kama yeye binafsi Ana maslahi ya mojakwa moja na mradi huo.!Maraisi Wana fursa zote katika nchi.hata akiwa fisadi huwekeza mahali hagusi yatima,wajane na maskini mojakwamoja. Kwani wanajua Hawa hutetewa na Mungu peke yake.Na malipo yake huwa Ni hapa hapa Duniani, na kumalizia huko tuendako!

Raisi, wetu amejipambanua kwa kuwa kinyume na mambo kama hayo. Na hi ni mojawapo ya sifa muhimu iliyompa madaraka aliyo nayo.hivyo hatuamini Kama akipata taarifa hi atakuwa na dakika ya kusubiri zaidi!
Naoma hujanielewa vile nimeandika na kumaanisa, kweli kila rais dunia ana mamulaka hio kweli kabbisa lakini kaa umesoma vizuri hio andiko langu, nimesema pengine kuna mtu au watu maarufu humo ccm au serikalini ambao ndio wanasababisa hayo kwenu na hao watu wako na nguvu ajabu, kila naona umesahau ni hiki, katika kila raisi kuna watu nyuma yake ambao uma hawaoni na hao ndio wanatawala taifa, sasa lazima kuna hao watu hapo tz, na hao watu magufuli hata kaa yeye ni raisi HAWEZI KAMWE kweda kiyume na wao, PERIOD, usifikiria magufuli hajui hii hali yenu anaijua kabisa, lakini hawezi fanya lolote hata kaa yeye ni raisi iko watu ambao hawezi enda kiyume na mapezi yao, kubali au ukatae hii ndio ukweli, na sijui kaa kweli wewe unamufahamu magufuli acha kumupa sifa mtu ambae ameharibu taifa, watu kuyimwa uhuru wa kuongea maovu humu nchini, watu kina Mo kutekwa na serikali ndio watoe mashamba yao na hela, waandishi wa habari kupotea kina azory, kina ben saaa nane sasa nafikiri wako maiti, kaa wewe ni mchungaji ONGEA UKWELI KAA WEWE NI MCHUNGAJI WA KWELI, magufuli amekuwa gaidi takika taifa hili, mimi huongea ukweli mtupu maana mimi ni mkiristo
 
Ndugu Mchungaji. Hilo ni shamba siasa au niseme shamba darasa la siana za dunia ya 3. Unakumbuka wakati wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo wa kuunga juhudi baada ya Diwani kuunga juhudi za muungwa juhudi? Alikuja Lukuvi na Polepole yule chakubanga wakasema hilo shamba ni la Singasinga, na kwamba mkichagua CCM uchaguzi huo mdogo basi ekari 6 zitatolewa. Ina maana hao hawajui kuwa hata gazeti la serikali lilishatangaza kuwa ekari mia nane zote ni za wananchi? Hiyo barua mngewaonyesha siku ile ewalahi wananchi wangeingia.
 
Ndugu Mchungaji. Hilo ni shamba siasa au niseme shamba darasa la siana za dunia ya 3. Unakumbuka wakati wa kufunga kampeni za uchaguzi mdogo wa kuunga juhudi baada ya Diwani kuunga juhudi za muungwa juhudi? Alikuja Lukuvi na Polepole yule chakubanga wakasema hilo shamba ni la Singasinga, na kwamba mkichagua CCM uchaguzi huo mdogo basi ekari 6 zitatolewa. Ina maana hao hawajui kuwa hata gazeti la serikali lilishatangaza kuwa ekari mia nane zote ni za wananchi? Hiyo barua mngewaonyesha siku ile ewalahi wananchi wangeingia.
Ni matumaini yetu ya kuwa, muda wa haki kutamalaki unawadia
 
Back
Top Bottom