Rais Magufuli, tunapaswa kuanza kutengeneza zana zetu za kijeshi kuanzia sasa kama Taifa

wwww

JF-Expert Member
Mar 20, 2012
350
252
Mgogoro wa Korea Kasikazini na Marekani umetengeneza uzi huu na kuona kuwa kuna umuhimu wa makusudi kabisa wa kuanza kutengeneza zana zetu za kijeshi mapema sana. Ukisoma historia nchi nyingi ambazo tulikuwa nazo kwenye uchumi wa daraja la tatu kama China, Korea, Philipino na nyingine nyingi zimepiga hatua sana za kimaendeleo achilia mbali silaha za kijeshi.

Hatua iliyofikiwa na Korea ya Kasikazini ya kuwekeza kwenye silaha za kujilinda kunaifanya leo ifikie hatua ya kuitishia hata nchi kama Marekani ambayo imeanza kutengeneza silaha zake miongo mingi iliyopita. Hii ni hatua nzuri na mimi binafsi naipongeza sana Serikali ya Korea ya Kasikazini. Ili nchi iwe salama lazima ijilinde dhidi ya adui yeyote yule haijalishi ni mkubwa au mdogo kiasi gani na ni wajibu wa Serikali yoyote kuhakikisha usalama wa watu wake unalindwa kwa nguvu yoyote ile.

Nchi yetu Tanzania ni kubwa sana kieneo na kuna mataifa mengi yanaitamani kuiona ikiwa imemeguka vipande vipande ili kuipunguza nguvu yake. Hivyo ili tuwe na uhakika wa kuilinda mipaka yetu kisawasawa lazima tuwe na silaha za kutosha, kisasa na ambazo adui yetu atapata kigugumizi kutuvamia huku akijua tuna uwezo mkubwa kidhana za kivita.

Tanzania ukimlinganisha na binadamu ni mtu mzima, tuachane na mawazo ya kujiona kama bado ni nchi changa, tumekua sasa tunatakiwa tuanze sasa kujiwekea mazingira mazuri ya kujilinda kama nchi.

Mhe. Rais tuanze kidogo kidogo angalau kwa silaha ndogo kama Pisto, SMG na silaha nyingine za kawaida kabla ya kufikia kwenye silaha za Nyuklia. Tunapaswa kufika huko sasa na sio kesho. Tuanze leo kutengenza. JWTZ linaweza kufanya hivyo kupitia kikosi chake cha NYUMBU au kikosi chochote kile kama ambavyo tunatengenza risasi kwenye kikosi cha Mizinga kule Morogoro. Mhe. Rais tumechelewa sana kuanza, katika umri huu tulitakiwa tuwe tayari tunatengeneza vifaru.

Mhe. Rais nakuomba sana usiwasikilize askari pale Makao Makuu ya JWTZ (NGOME) kuhusu hili watakupotosha kwa sababu wao wanataka tuendelee kununua silaha nje ili wapate commission (10%) zao kwenye bei za silaha zinazonunuliwa nje. Fanya maamuzi leo usingoje kesho, hapo utakuwa umejiwekea historia kubwa sana katika nchi hii na kuiondolea Serikali mzigo mkubwa sana wa kununua silaha nje ya nchi kama tunavyofanya sasa.

Najua kuna Watanzania wataona kama sio kipaumbele lakini hakuna kipaumbele zaidi ya ulinzi katika maisha ya mwanadamu yoyote hapa duniani.

Mhe. Rais nakutakia kila la kheri katika uamuzi huu mgumu utakaokuwa na vikwazo mbele yako, SIMAMA IMARA KATIKA HILI.

Naomba kutoa hoja!!!!!!!!!!!!!!
 
Jeshi limejaa wahuni hilo ndio lifanye hayo...
Cha msingi nchi iwekeze kwa watu wenye Ideas na maono.
Watundu na wabunifu ambao kuvumbua kitu sio tatizo.
Itengwe bajeti ya kupelekwa kwenye research na experiments kadha wa kadha za kikeemia, biologia na physics.
 
Una point za msingi kuhusu viwanda vya silaha lakini kwa Tanzania bado na sidhani kama mataifa yanayotengeneza silaha yatakupa license yao ili uanze kutengeneza silaha.

Labda kama una silaha ambayo utakuwa umeigundua wewe mtanzania lakini bado kuna mamlaka za uhakiki kabla ya production kuanza

Rais lazima awasikilize makamanda wa Ngome kwasababu ndiyo waliopewa dhamana ya usalama na kupanga uwezo wa kijeshi ktk nchi kwa nyanja tofauti
 
Tanzania ipi inayoweza kufanya hivyo mkuu?

Nchi za wenzetu viongozi wanatanguliza maslahi ya nchi mbele. Ila Tz tunatanguliza maslahi ya tumbo.

Sasa issue ndogo kama ya kusupply camera kwenye vituo vya polisi imetushinda,tumeishia kula hela.

Tanzania labda silaha za jadi.
 
Mgogoro wa Korea Kasikazini na Marekani umetengeneza uzi huu na kuona kuwa kuna umuhimu wa makusudi kabisa wa kuanza kutengeneza zana zetu za kijeshi mapema sana. Ukisoma historia nchi nyingi ambazo tulikuwa nazo kwenye uchumi wa daraja la tatu kama China, Korea, Philipino na nyingine nyingi zimepiga hatua sana za kimaendeleo achilia mbali silaha za kijeshi.

Hatua iliyofikiwa na Korea ya Kasikazini ya kuwekeza kwenye silaha za kujilinda kunaifanya leo ifikie hatua ya kuitishia hata nchi kama Marekani ambayo imeanza kutengeneza silaha zake miongo mingi iliyopita. Hii ni hatua nzuri na mimi binafsi naipongeza sana Serikali ya Korea ya Kasikazini. Ili nchi iwe salama lazima ijilinde dhidi ya adui yeyote yule haijalishi ni mkubwa au mdogo kiasi gani na ni wajibu wa Serikali yoyote kuhakikisha usalama wa watu wake unalindwa kwa nguvu yoyote ile.

Nchi yetu Tanzania ni kubwa sana kieneo na kuna mataifa mengi yanaitamani kuiona ikiwa imemeguka vipande vipande ili kuipunguza nguvu yake. Hivyo ili tuwe na uhakika wa kuilinda mipaka yetu kisawasawa lazima tuwe na silaha za kutosha, kisasa na ambazo adui yetu atapata kigugumizi kutuvamia huku akijua tuna uwezo mkubwa kidhana za kivita.

Tanzania ukimlinganisha na binadamu ni mtu mzima, tuachane na mawazo ya kujiona kama bado ni nchi changa, tumekua sasa tunatakiwa tuanze sasa kujiwekea mazingira mazuri ya kujilinda kama nchi.

Mhe. Rais tuanze kidogo kidogo angalau kwa silaha ndogo kama Pisto, SMG na silaha nyingine za kawaida kabla ya kufikia kwenye silaha za Nyuklia. Tunapaswa kufika huko sasa na sio kesho. Tuanze leo kutengenza. JWTZ linaweza kufanya hivyo kupitia kikosi chake cha NYUMBU au kikosi chochote kile kama ambavyo tunatengenza risasi kwenye kikosi cha Mizinga kule Morogoro. Mhe. Rais tumechelewa sana kuanza, katika umri huu tulitakiwa tuwe tayari tunatengeneza vifaru.

Mhe. Rais nakuomba sana usiwasikilize askari pale Makao Makuu ya JWTZ (NGOME) kuhusu hili watakupotosha kwa sababu wao wanataka tuendelee kununua silaha nje ili wapate commission (10%) zao kwenye bei za silaha zinazonunuliwa nje. Fanya maamuzi leo usingoje kesho, hapo utakuwa umejiwekea historia kubwa sana katika nchi hii na kuiondolea Serikali mzigo mkubwa sana wa kununua silaha nje ya nchi kama tunavyofanya sasa.

Najua kuna Watanzania wataona kama sio kipaumbele lakini hakuna kipaumbele zaidi ya ulinzi katika maisha ya mwanadamu yoyote hapa duniani.

Mhe. Rais nakutakia kila la kheri katika uamuzi huu mgumu utakaokuwa na vikwazo mbele yako, SIMAMA IMARA KATIKA HILI.

Naomba kutoa hoja!!!!!!!!!!!!!!
Wananchi wa Korea Kaskazini wana faida gani ya maana kwa kutengejeza silaha badala ya kujenga uchumi imara?
 
Jeshi limejaa wahuni hilo ndio lifanye hayo...
Cha msingi nchi iwekeze kwa watu wenye Ideas na maono.
Watundu na wabunifu ambao kuvumbua kitu sio tatizo.
Itengwe bajeti ya kupelekwa kwenye research na experiments kadha wa kadha za kikeemia, biologia na physics.
Wanaotengeneza silaha za Korea ni wachina sio wakorea wenyewe.Mchina ndio mtawala wa Korea kwa kila kitu
 
Juzi kati hapa magereza walipewa cheque iliyozua manung'uniko Bungeni wasaidie kupunguza tatizo la madawati. Mkuu wa Mkoa kutwa kucha haishi matangazo kwenye media wananchi wachangie madawati. Halafu unazungumzia nyambizi! Utekelezaji wa bajeti ya mwaka unaoisha umeusikia lakini?
 
sasa mkuu sidhani kama kutengeneza Pistol na SMG ambazo tayari zimeshatengenezwa na wenda gharama na ubora wa kununua ni chini ya kutengeneza mwenyewe.
Mapinduzi makubwa ni kufanya Tanzania ya Technolojia, Mapinduzi ya kitechnolojia yaanzie Jeshini. Hata kama wengi hawana nia, au maarifa ya kutosha mfano watafutwe watu, wapelekwe nje waje wasaidie. Katika nchi yenye amani nadhani watu wetu wanamuda mwingi wa kudesign,Coding, Kujaribu vitu vingi vya kiteknolojia.
Wananafasi pia kuwa mstari wa mbele katika mapinduzi ya kiteknolojia na kilimo.
Mambo mengi duniani yalianzishwa na ubunifu wa wanajeshi. Kipindi cha amani ndio Kipindi cha Jeshi letu kuwa mstari wa mbele katika Shughuli za kimaendeleo na kitaalamu. Tunafanya vizuri hadi sasa ila tnatakiwa kufanya vizuri zaidi, hii nchi imechelewa sana. Na silaha kubwa waliyonayo wanajeshi ambayo mtaani haipo sana ni NIDHAMU. Ukiwa na nidhamu hakn kiachoshindikana.
huwa naamini jeshi letu ni bora kabisa na chochote wakiamua kinafanikiwa...
 
Hivi ni mfano wa vitu vilivyobuniwa Jeshini na Vina faida sana kwa Raia.
1:RADA - ilibuniwa jeshini, lakni leo inasaidia hali ya hewa na Civil Aviation.
2:TWO WAYS RADIO - Jeshi lilibuni lkn leo Viwandani,Migodini,Watafiti,Usafirishaji, maengineers wanatumia kuwasiliana
3:Internet - hapa hakuna haja ya kuelezea.
4:Super glue
Digital Cameras, Nuclear energy kwa ajili ya umeme, GPS, Antibiotics,Vyakula vya kopo, Ambulance services, MIcrowave oven, Nyepe za kunyolea ndevu, Pedi za wakina mama, na mengine mengi...
Hata sisi tukijipanga kwa uwezo wtu huu mdogo tunaweza kusaidia jamii mengi.
 
Hivi ni mfano wa vitu vilivyobuniwa Jeshini na Vina faida sana kwa Raia.
1:RADA - ilibuniwa jeshini, lakni leo inasaidia hali ya hewa na Civil Aviation.
2:TWO WAYS RADIO - Jeshi lilibuni lkn leo Viwandani,Migodini,Watafiti,Usafirishaji, maengineers wanatumia kuwasiliana
3:Internet - hapa hakuna haja ya kuelezea.
4:Super glue
Digital Cameras, Nuclear energy kwa ajili ya umeme, GPS, Antibiotics,Vyakula vya kopo, Ambulance services, MIcrowave oven, Nyepe za kunyolea ndevu, Pedi za wakina mama, na mengine mengi...
Hata sisi tukijipanga kwa uwezo wtu huu mdogo tunaweza kusaidia jamii mengi.
Jeshi la wapi unaloongelea?
 
Watu wajinga sana! Watu hawana maji safi ya kunywa nyinyi mnaongelea silaha.
 
sasa mkuu sidhani kama kutengeneza Pistol na SMG ambazo tayari zimeshatengenezwa na wenda gharama na ubora wa kununua ni chini ya kutengeneza mwenyewe.
Mapinduzi makubwa ni kufanya Tanzania ya Technolojia, Mapinduzi ya kitechnolojia yaanzie Jeshini. Hata kama wengi hawana nia, au maarifa ya kutosha mfano watafutwe watu, wapelekwe nje waje wasaidie. Katika nchi yenye amani nadhani watu wetu wanamuda mwingi wa kudesign,Coding, Kujaribu vitu vingi vya kiteknolojia.
Wananafasi pia kuwa mstari wa mbele katika mapinduzi ya kiteknolojia na kilimo.
Mambo mengi duniani yalianzishwa na ubunifu wa wanajeshi. Kipindi cha amani ndio Kipindi cha Jeshi letu kuwa mstari wa mbele katika Shughuli za kimaendeleo na kitaalamu. Tunafanya vizuri hadi sasa ila tnatakiwa kufanya vizuri zaidi, hii nchi imechelewa sana. Na silaha kubwa waliyonayo wanajeshi ambayo mtaani haipo sana ni NIDHAMU. Ukiwa na nidhamu hakn kiachoshindikana.
huwa naamini jeshi letu ni bora kabisa na chochote wakiamua kinafanikiwa...
Jeshi ni kipaji kwa watu fulani kama ilivyo siasa au uchoraji. Kukiwa na watu wanaowaza na kufikiria vita tu ndo kunakuwepo na ubunifu wa zana. Kule China unakuta mtu hajafika hata chuo lakini anaweza kuunda kifaa cha mawasiliano kwa sababu akili yake iko kwenye ubunifu huo.
 
sasa mkuu sidhani kama kutengeneza Pistol na SMG ambazo tayari zimeshatengenezwa na wenda gharama na ubora wa kununua ni chini ya kutengeneza mwenyewe.
Mapinduzi makubwa ni kufanya Tanzania ya Technolojia, Mapinduzi ya kitechnolojia yaanzie Jeshini. Hata kama wengi hawana nia, au maarifa ya kutosha mfano watafutwe watu, wapelekwe nje waje wasaidie. Katika nchi yenye amani nadhani watu wetu wanamuda mwingi wa kudesign,Coding, Kujaribu vitu vingi vya kiteknolojia.
Wananafasi pia kuwa mstari wa mbele katika mapinduzi ya kiteknolojia na kilimo.
Mambo mengi duniani yalianzishwa na ubunifu wa wanajeshi. Kipindi cha amani ndio Kipindi cha Jeshi letu kuwa mstari wa mbele katika Shughuli za kimaendeleo na kitaalamu. Tunafanya vizuri hadi sasa ila tnatakiwa kufanya vizuri zaidi, hii nchi imechelewa sana. Na silaha kubwa waliyonayo wanajeshi ambayo mtaani haipo sana ni NIDHAMU. Ukiwa na nidhamu hakn kiachoshindikana.
huwa naamini jeshi letu ni bora kabisa na chochote wakiamua kinafanikiwa...
Wewe na mtoa Uzi nyote nawaunga mkono, tuanze sasa. hoja zenu ni za kizalendo. hivi kiwanda cha magari nyumbu kibaha kimeishia wapi?
 
Wanaotengeneza silaha sio wanajeshi tu. Kuna kampuni za watu wenye weledi wa kisomo zaidi ndio huanzisha viwanda vya silaha na kuuzia majeshi ya nchi mbalimbali. Huwezi tumia aina ya vijana waliopo pale jkt au jwtz ambao ufundi ni ule wa kuunga vyuma tu. Ufundi wa silaha ni eneo la Wataalam waliobobea katika fani mbalimbali.
 
Kwanza mentality ya viongozi wetu lazima ibadilike.... wawekeze kwenye elimu kwanza .. na science kwa ujumla.
Uchumi wa nchi nao unatakiwa uwe imara maana mambo kama hayo yanahitaji pesa nyingi.
 
Back
Top Bottom