Rais Magufuli: Tetemeko halijaletwa na Serikali, watu wafanye kazi

Dah! inasikitisha sana,yaani kweli hivi kuna mtu mwenye uwezo wa hali na mali ataacha kushughulikia nyumba yake au mali zake eti anasubiri msaada kutoka serikalini?

Mbona watu wanakosa mioyo ya utu na huruma kiasi hicho jamani?mnajisahau na kuanza kuwasimanga raia waliopatwa na majanga ya asili raia ambao mliwaomba kura zao ili mpate kuwaongoza na kuahidi kuwawekea mazingira mazuri ya kimaisha?

Halafu viongozi wanapaswa watambue linapotokea janga kama hili sio swala la kuombwa kusaidia raia wako bali ni suala lililo katika wigo na wito wa kazi yako,unapaswa uguswe na kujitoa katika suala hili moja kwa moja bila hata kukumbushwa au kukurupushwa inabidi ulitambue hili kuanzia siku ya kwanza unapoanza kazi za umma na sio kujichimbia na kuibuka na kauli za kufikirisha.
 
Too low-escrow escrow escrow! Ni mafisadi gani wanashughulikiwa Kama waliohusika na skendali ya escrow wanatanua mitaani?
Kuna ambao wameshashungulikiwa na kuna baadhi bado kama Escrow. Kumbuka serikali hii haina hata mwaka tangia imeingia madarakani lakini imeweza kuwaondoa viongozi wengi waliokuwa wanasababisha kutokea na kuenea.

Tumpe muda ingawa sasa hivi kuna resistance kubwa kutoka kwa mafisadi na waliokuwa wananufaika na ufisadi, Kuhakikisha Magufuli hafanikiwi kwenye vita ya ufisadi!
 
Kwa kweli sina milioni saba ya kulipa... Ila Mkuu ana maneno mazito! Anasema waathirika wasikae tu huko wanangoja hela za serikali kwa sbb wanasikia zimechangwa,waanze kujisaidia kwanza wao na serikali itawasaidia pale waliposhindwa.

Mkuu anasema mtu ukuta umedondoka, anataka asubiri serikali ndio imtengenezee! Watu wajue tetemeko ni janga la asili halijaletwa na CCM. Waanze kwa kujenga wenyewe kuta zilizodondoka sio wasubiri serikali, sababu maisha yanendelea na watu wanatakiwa wafanye kazi kwa kujenga nyumba zao na sio kila kitu serikali itafanya.

Na wale wanasiasa wanaotaka kutumia janga hili kujinufaisha kisiasa mkuu anasema waache mara moja.

Na kasema wote wanaotumia janga hili kukusanya misaada kwa njia ya kitapeli, basi wakamatwe mara moja.

Kwanza napenda nikupongeze Mkuu kwa kujitahidi kutuletea hii habari. Hata hivyo naomba tu niseme kuwa kuna baadhi ya maneno (mekundu hapo juu) umeyaongeza wewe, Mheshimiwa Rais hakuyatamka.

Pili, niliamua kuyasikiliza maneno yote ya Mheshimiwa Rais, baada ya kusikiliza kwa makini Zaidi ya mara moja nimejiridhisha kuwa Mheshimiwa Rais ametamka kama ifuatavyo:

"Hii ni mipango ya Mungu, tetemeko haliletwi na Serikali, wala tetemeko haliletwi na CCM. Ni jukumu la sasa hivi sisi kama nchi ni kuhakikisha tunawasaidia wenzetu ambao wamepata matatizo haya. Tusilitumie tetemeko hili kwa njia zingine sijui za kujiimarisha kisiasa, mtu unakwenda unazungukia weee nyumba zilizozunguka, unatoka unatamka huko. Watu wa Kagera wanahitaji msaada, siyo maneno.

Matapeli wapo na wamejipanga kweli; tunachangia Kagera, tunafanya nini, kumbe anachangia tumbo lake. Hili ni lazima tuliangalie na nitoe wito kwa vyombo vya dola, muwafuatilie hawa ambao wamekuwa wanasingizia wanachangia Kagera na nini, wakati wanajichangia wao, washikwe na ikiwezekana wapelekwe kwenye vyombo vya sheria ili wakajibu hizo hoja za kitapeli na wizi wa kuwaibia watu maskini ambao wana shida za kiukwelikweli.

Wananchi waambiwe ukweli, hili tetemeko halikuletwa na Serikali; wote tunasikitika, wote tunalia na ndiyo maana hata sisi Serikali tunajipanga katika kusaidia, tutaendelea kuwasaidia lakini na wao pia wajisaidie. Wasikae wakasubiri tu kwamba ukuta wangu umebomoka hapa hata kuparudishia hataki, anasubiri nasubiri kuna hela za Serikali zinakuja. Tetemeko limetokea, siyo mwisho wa maisha, waanze kujipanga kwa kufanya kazi.
"

Ni ushauri wangu kuwa tuwe makini tunapoandika mada ili kuepuka kuongeza chumvi au kuhafifisha ujumbe uliotolewa.
 
Kwanza napenda nikupongeze Mkuu kwa kujitahidi kutuletea hii habari. Hata hivyo naomba tu niseme kuwa kuna baadhi ya maneno (mekundu hapo juu) umeyaongeza wewe, Mheshimiwa Rais hakuyatamka.

Pili, niliamua kuisikiliza maneno yote ya Mheshimiwa Rais, baada ya kusikiliza kwa makini Zaidi ya mara moja nimejiridhisha kuwa Mheshimiwa Rais ametamka kama ifuatavyo:

"Hii ni mipango ya Mungu, tetemeko haliletwi na Serikali, wala tetemeko haliletwi na CCM. Ni jukumu la sasa hivi sisi kama nchi ni kuhakikisha tunawasaidia wenzetu ambao wamepata matatizo haya. Tusilitumie tetemeko hili kwa njia zingine sijui za kujiimarisha kisiasa, mtu unakwenda unazungukia weee nyumba zilizozunguka, unatoka unatamka huko. Watu wa Kagera wanahitaji msaada, siyo maneno.

Matapeli wapo na wamejipanga kweli; tunachangia Kagera, tunafanya nini, kumbe anachangia tumbo lake. Hili ni lazima tuliangalie na nitoe wito kwa vyombo vya dola, muwafuatilie hawa ambao wamekuwa wanasingizia wanachangia Kagera na nini, wakati wanajichangia wao, washikwe na ikiwezekana wapelekwe kwenye vyombo vya sheria ili wakajibu hizo hoja za kitapeli na wizi wa kuwaibia watu maskini ambao wana shida za kiukwelikweli.

Wananchi waambiwe ukweli, hili tetemeko halikuletwa na Serikali; wote tunasikitika, wote tunalia na ndiyo maana hata sisi Serikali tunajipanga katika kusaidia, tutaendelea kuwasaidia lakini na wao pia wajisaidie. Wasikae wakasubiri tu kwamba ukuta wangu umebomoka hapa hata kuparudishia hataki, anasubiri nasubiri kuna hela za Serikali zinakuja. Tetemeko limetokea, siyo mwisho wa maisha, waanze kujipanga kwa kufanya kazi.
"

Ni ushauri wangu kuwa tuwe makini tunapoandika mada ili kuepuka kuongeza chumvi au kuhafifisha ujumbe uliotolewa.
Nashukuru mkuu kama imeisikiliza kiasi cha kuandika neno kwa neno!!Lkn je umeishia kusikiliza hii hotuba ya ITV tu?Au ulipata nafasi ya kusikiliza pia AZAM TWO?Umeona hotuba nzima au ni hii ya vipande vipande?

Umehitimisha vizuri sana,tunapoandika mada,tujitahidi kuacha kuongeza chumvi au kuandika kile ambacho hatujakisikia kwa mapana na marefu.

Halafu mkuu,unapokea report ya Tetemeko siku saba baada ya tukio?Hapo ndio uanze kutoa msaada!!Maana siku zote hizo kuna watu wamelala nje wao na watoto wao.Standard Operating Procedures za Disaster Management hazisemi hivyo.Hili linalofanyika leo,lilipaswa kufanyika ktk hatua za mwanzo kabisa.

Kuna Zero Hour,Past Zero Hour,Day One,Day Two na kuendelea...Sasa jambo lilipaswa kufanywa kwenye Zero Hour linafanyika kwenye Day Two,na jambo la kwenye Past Zero Hour linafanyika kwenye Day Seven...Bado unatetea?Hapa tuweke mahaba ya siasa pembeni mkuu
 
Kwaiyo tunaofiwa wote ndugu zetu tuitegemee serikali kutusaidia misaada? Rais kawaambia unwell ili wasibweteke sana

Bado kidogo siku rais akitoa hotuba juu ya umuhimu wa kuvuta hewa na kwamba usipovuta hewa utakufa tutasikia pongezi kibao kwake kwa kutuambia "ukweli mtupu"!
 
unashangaa? wapo wanasiasa tena wakubwa wanataka ionekane kama serikali na ccm ndio wameleta tetemeko bukoba. baada ya tetemeko wamefika bukoba kama mshale hadi after shocks zimewakuta bukoba. kufika tu wakaanza kumlaumu rais kwamba hajafika bukoba na kulaumu serikali.
Kwa hiyo unataka kusema kuwa hicho ndicho kilichomfanya asiende!!?
 
Kuna usahihi katika kauli ya Rais hasa kwa wale wanaoutumia haya Majanga kama njia ya kubweteka, maana majanga yameshatokea na maisha yatendelea na serikali haitaweza kusaidia kila mtu , mfano wale wanaotaka wajengewe Nyumba na serikali.

hata hivyo kuna ambao hawataweza kufanya shughuli zao za kila siku mpaka mambo yawe shwari.
Rais ametoa ukweli wenye uchungu! Ni kweli c wote wenye uwezo wa kununua hata bati 2 ila wale wenye UWEZO waonyeshe njia ya kusaidiwa! Siamini kuwa umejenga boma afu serikali ikashindwa kukuchangia bati za kuezekea!! Naomba nisieleweke vibaya ila tu serikali inatakiwa kupeleka hiyo misaada haraka sana kabla mvua hazijaanza kunyesha!
 
Nimekuwa nikisia kila wakati "Tamko la HATUTAKI SIASA. au tusifanye siasa katika jambo X. Nimewah kumuuliza Dr. Mmoja wa Falsafa aliyesoma na kufundisha siasa. Siasa ni nini? Alinipa nukuu za kutosha na mwishowe hakuweza kuhitimisha siasa ni nini.

Kila mtu amekuwa akitafsiri kwa maana inayokidhi matakwa yake. Ni rahisi kumwambia mwingine asifanye siasa. Lakin tukiulizana ni wapi mipaka ya siasa. Tunaweza fafanua? Na ni wapi hakuna siasa katika maisha haya? Naanza pata shida kuwa naweza kuwa mwanasiasa maarufu nikakuta kuna wakati nakatazwa kutembea kwa miguu maana itakuwa siasa. Nakatazwa nisihudhurie misiba maana iitakuwa siasa. Nakatazwa nisihudhurie kwenye matamasha au michezo sababu itakuwa nafanya siasa.

Naomba mnisaidia siasa ni nini na mipaka yake ni ipi?
 
Makoye Matale
Rais kafika BK kujiinea mwenyewe wapiga kura wake wanavyo teseka na wengine kufiwa zaidi ya kaya 15?

Kumtetea kwako hakuna maana yyt
Mkuu hapo ndipo unapo_miss target; kilicho mbele yetu hapa jamvini ni maneno aliyoyatoa ambayo yameleta ukakasi mwingi miongoni mwetu.

Hoja ya kutoenda huko ni mjadala mpya ambao unahitaji kujadiliwa.

Mkuu naomba uzingatie kuwa simtetei Mheshimiwa Rais, nimewasilisha kile alichokisema kwa kuzingatia hiyo clip iliyopo hapa jamvini ili ninyi wakuu mtoe 'hukumu' zenu kwa kuzingatia maneno yake mwenyewe na siyo maneno ya kuwekewa kinywani na mtoa mada.
 
Siasa ni taratibu za maisha ya kila siku ya binadamu zinazoratibiwa na sheria na kanuni mbalimbali. Kusema hutaki siasa ni kusema hutaki watu waishi kwa mujibu wa sheria ila tamko la mtu ni ubatili na kulewa madaraka
 
Back
Top Bottom