Rais Magufuli suala la viwanda tungeachana nalo limeshatushinda

Levels baby

JF-Expert Member
Sep 26, 2019
831
768
Nimeleta bandiko hili sababu toka juzi nimekuwa na survey kwenye mkoa wa Pwani kwa ajili ya uwekezaji ambao tumeamua kama familia ya mzee Mundele tuwekeze katika nchi yetu na tuonyeshe uzalendo katika sera ya Rais wetu mzalendo Dr. John Pombe Joseph Magufuli, lakini nilichokikuta kiukwel nimekata tamaa.

1. Juzi baada ya kurudi kutoka katika mihangaiko ya kazi huko Kanda ya Ziwa mzee wangu akaniambia kafanye tulichongea (kitafuta eneo la uwekezaji yaani kiwanda kidogo).

Sasa kidume nikatua Mkuranga huku nimewaweka sawa watu wangu na baadhi ya vijana wanaojua maeneo ili tusaidiane lakini nilichokikuta kwa walionitangulia ni maigizo ya kutosha.

Yaani nakuta huko watu wamejenga majengo tena hayajaisha wameyaacha wanacheza tu nyani nikasema hawa viongozi wanaomwambia Rais tuna viwanda 400 Pwani wanamdanganya mzee wa watu.

2. Kali kuliko yote leo hapo Kibaha Zegereni viwandani ndio nimekuta vituko vya kutosha zaidi kuliko vya jana Mkuranga mpaka muda huu namuhadithia mshua anasema ni kwamba Rais anadanganywa au anadanganya.

Na mzee anasema alivyoona zile pambio akajua kuna michezo sio bure.

USHAURI:
Kwa hali tuliyoiona kiukweli Rais wangu hiyo sera tuitupie mbali hatuiwezi labda ajae lakini sisi hatuwezi tusha prove failure pakubwa sana sasa turudishe sera za mtoto wa mkulima (Pinda).

Maana huko ndio tutakuweza nguvu zote tupeleke huko kiasi kwamba mbegu zipatikane kwa urahisi, mbolea ya ruzuku kwa urahisi, tutafutie wananchi wetu masoko ya nje kwa timu maalum hili tutaliweza vizuri sio la viwanda.

Viwanda (hatuviwezi kwa sasa hatukuwa na mkakati mzuri labda aandaliwe Rais ajae nae ashaurike ili afikie malengo).

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimekuelewa kua;
(i) Ulipoenda mkuranga ulikuta maigizo na nyani wanacheza kwenye maigizo!

(ii) Ulipoenda Kibaha zegereni ulimkosa nyani kwenye maigizo ukakuta "kali kuliko zote" na unampasha mshua saiv kua igizo lilikuwepo ila nyani hakuwepo; tuelezee tujue hiyo "kali kuliko zote isiyo na nyani" ya zegereni!
 
Nimekuelewa kua;
(i) Ulipoenda mkuranga ulikuta maigizo na nyani wanacheza kwenye maigizo!

(ii) Ulipoenda Kibaha zegereni ulimkosa nyani kwenye maigizo ukakuta "kali kuliko zote" na unampasha mshua saiv kua igizo lilikuwepo ila nyani hakuwepo; tuelezee tujue hiyo "kali kuliko zote isiyo na nyani" ya zegereni!
"kali kuliko zote isiyo na nyani" kuna viwanja unaambiwa na wenyew kuwa kiwanda cha cement sijui nondo kinakuja muda si mrefu hapa

Mawaziri wa awamu ya tano mungu anawaona

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkoa wa pwani una mambo yao ya kutomalizia kile unachokianza. Nadhani ndo mkoa unaoongoza kuwa na mapagale. Unaanza kujenga nyumba huimalizi pesa zinakata mpaka unaikimbia! Kuna vizee vishirikina balaa ndo maana hauendelei licha ya kuwa karibu na fursa za Dar
 
Unatakiwa kuelewa hao wawekezaji wa mkuranga na kibaha na kwa ujumla mkoa was Pwani mwanzo wao ni upi na kwanini mwanzo wao ndio imekuwa kikwazo Chao.
 
Mpeni muda.

Mwaka wa tano huu, deni la taifa limezidi kukua, na miradi miwili mikubwa ya zaidi ya 15t yote hakuna hata mmoja umefikia nusu ya malengo. Hapo unategemea kuna uwezekano wa lolote kufanyika kwenye viwanda kwa muda wa utawala wake? Kwa sasa naona dhahiri nguvu yake itaishia kwenye hiyo miradi miwili mikubwa, lakini kwenye viwanda itabaki kuwa matamanio yake yaliyokwama.
 
Umeelewa mada lakin?

Sent using Jamii Forums mobile app
Going backwards again , au wewe hukuelewa jibu langu la kwanza, ambalo lilijibu maada iliyoletwa, jibu langu la sasa linauhusiana na suala lako na si la mleta mada, moja kazungumzia past mleta mada na wewe unazungumzia present continuous, hivyo jibu haliwezi kuwa sawa na uelewa wako hauwezi kulielewa hilo ndio maana unakuja na statement za "kitoto "
 
Tanzania hatuwezi kuwa na viwanda vya maana kama uongozi wa juu hauna mkakati na unaendekeza maneno zaidi ya utendaji.

Angalia strategy ya kukuza viwanda kwa kutoa kodi nafuu kwa wajasiliamali wanaoanza, hakuna.

Angalia mkakati wa kukuza utumiaji wa bidhaa zinazotengenezwa nchini, hatuna. Tunaagiza kutoka nje kuanzia ngui mpaka pini.

Angalia mkakati wa umeme nafuu kwenye viwanda vinavyozalisha mashine za kutumika viwandani, hatuna.

Angalia mkakati wa mikopo nafuu kwa wajasiliamali wenye mawazo mazuri ya kuanzisha viwanda vidogo na vya kati, hatuna.

Angalia mkakati wa kutumia fiscal policy na monetary policy ku influence viwanda, hatuna.

Angalia ease of doing business report uone tuna rank vipi hata regionally tu, vichekesho.

Angalia muda unaotumika kufungua biashara na urasimu uliopo, angalia hata regional rankings tu usitufananishe na Ulaya na Marekani. Ni vichekesho.

Bila ku address haya, mtasema sana rais anashauriwa vibaya na anadanganywa.

Wakati yeye mwenyewe ni sehemu ya chanzo cha tatizo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe wasema, lakini fursa kwa mtu yeyote mwenye mtaji au nia ya kuwekeza kwa kutumia njia mbali mbali kupata mtaji na kupunguza risk mfano kuunda vikundi ili muweze kupata mtaji mfano was 20m badala ya Wewe pekee yako kutoa hiyo 20m
Wa bongo wana akili nyingi sana.

Hivi, mtaji wa shs 20ml utanunua ardhi ili ujenge kiwanda, ama utafungua duka la ubuyu?

Unazifanyia nini?

Nadhani haya ni matokeo ya elimu ya nadharia na wala hakuna elimu kwa vitendo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wa bongo wana akili nyingi sana.

Hivi, mtaji wa shs 20ml utanunua ardhi ili ujenge kiwanda, ama utafungua duka la ubuyu?

Unazifanyia nini?

Nadhani haya ni matokeo ya elimu ya nadharia na wala hakuna elimu kwa vitendo

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimeongelea kwa mfano ya jinsi ya ku raise capital njia iliyo bora, lakini hapo hapo kuna viwanda vya kukamua mafuta ya kula. Je wajua bei za hizo machine na akili zako kubwa? ??
 
Going backwards again , au wewe hukuelewa jibu langu la kwanza, ambalo lilijibu maada iliyoletwa, jibu langu la sasa linauhusiana na suala lako na si la mleta mada, moja kazungumzia past mleta mada na wewe unazungumzia present continuous, hivyo jibu haliwezi kuwa sawa na uelewa wako hauwezi kulielewa hilo ndio maana unakuja na statement za "kitoto "
Magufuli endelea kututawala unavyotaka maana Tanzania kuna viazi vingi sana,,yaani hujui hata mleta mada kaongelea nin na ni nan unabishana tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom