FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 92,894
- 109,227
Mheshimiwa Rais Magufuli, Asalaam Alaikum (Salama na Amani iwe juu yako).
Tunafahamu kuwa wewe ni Rais wa wanyonge na ni mpenda haki usiyependa yeyote adhulumiwe.
Sisi Waislam, mkoloni Mjerumani alitudhulumu majengo yetu mengi hapo jijini Dar Es Salaam, jina ambalo limetokana na jengo ambalo sasa linaitwa "Ikulu". Majengo hayo ni pamoja na jengo la Dar us Salaam ambalo ndilo ikulu ya sasa, hospitali inayojulikana kama "Ocean Road" pamoja majengo ambayo yalibadilishwa na kufanywa makanisa katika ufukwe wa Bahari ya Hindi ulio jijini Dar Es Salaam.
Kwa kuwa sasa unahamia rasmi Dodoma basi tunaomba haki itendeke na jengo hilo au majengo na viwanja vinavyozunguka majengo hayo yarudishwe kwa wenyewe ili haki itendeke.
Naomba ujisikilizie mwenyewe ushahidi huu hapa, nauweka chini, wa mali hizo kuwa si za wengine bali za Waislam waliodhulumiwa.
Pia tunaomba mali hizo zisikikabidhiwe Bakwata kwani wana koo za waliojenga na wenye kumiliki ardhi hizo, kabla hazijadhulumiwa, wapo hai na wakabidhiwe wao haki zao.
Natumai kilio na ombi hili la kutafuta haki zilizodhulumiwa kitakufikia nawe utatenda haki ya msingi ya kurudisha mali za waliodhulumiwa.
Ahsante.
Tunafahamu kuwa wewe ni Rais wa wanyonge na ni mpenda haki usiyependa yeyote adhulumiwe.
Sisi Waislam, mkoloni Mjerumani alitudhulumu majengo yetu mengi hapo jijini Dar Es Salaam, jina ambalo limetokana na jengo ambalo sasa linaitwa "Ikulu". Majengo hayo ni pamoja na jengo la Dar us Salaam ambalo ndilo ikulu ya sasa, hospitali inayojulikana kama "Ocean Road" pamoja majengo ambayo yalibadilishwa na kufanywa makanisa katika ufukwe wa Bahari ya Hindi ulio jijini Dar Es Salaam.
Kwa kuwa sasa unahamia rasmi Dodoma basi tunaomba haki itendeke na jengo hilo au majengo na viwanja vinavyozunguka majengo hayo yarudishwe kwa wenyewe ili haki itendeke.
Naomba ujisikilizie mwenyewe ushahidi huu hapa, nauweka chini, wa mali hizo kuwa si za wengine bali za Waislam waliodhulumiwa.
Pia tunaomba mali hizo zisikikabidhiwe Bakwata kwani wana koo za waliojenga na wenye kumiliki ardhi hizo, kabla hazijadhulumiwa, wapo hai na wakabidhiwe wao haki zao.
Natumai kilio na ombi hili la kutafuta haki zilizodhulumiwa kitakufikia nawe utatenda haki ya msingi ya kurudisha mali za waliodhulumiwa.
Ahsante.