Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,172
- 7,429
Rais Magufuli anataka viwanda ambavyo vilikuwa vya serikali vikabinafsishwa na kisha vimekufa , vitaifishwe na vifufuliwe jambo ambalo bila shaka lina nia njema.
Aidha, pamoja na nia hiyo njema, ni vyema wanaohusika kwenye zoezi hilo kujiuliza yafuatayo ili jambo hilo jema liweze kufanikiwa.
1. Ni lazima wajiulize ni sababu zipi zilifanya viwanda hivyo vibinafsishwe, na kwa nini walipewa hao waliopewa.
2. Inafaa wafanye utafiti kama sababu zilizotumika kuvibinafsisha bado zipo ama laaa!
3. Wanatakiwa wafanye utafiti pia kujua kuwa ni sababu zipi zilizopelekea waliomilikishwa viwanda hivyo kushindwa kuviendesha hata vikafa na kuwa magofu na kujiuliza kama sababu hizo hazipo tena kwa sasa na kama zipo, ni kwa namna gani zitashughulikiwa ili sasa viwanda hivyo viweze kusimama.
4. Inafaa kutafakari pia kuwa baada ya kutaifisha viwanda hivyo, serikali ndio itakayo viendesha au watapewa wawekezaji wengine, na kama itaendesha serikali, ni vyema kufanya utafiti wa namna ambavyo serikali inaweza kuviendesha kwa ufanisi, na kama ni wawekezaji, ni vizuri kujiridhisha kama kuna wawekezaji wako interested kuwekeza kwenye maeneo husika na ni kwa vipi wao wanaweza kuwa na uwekezaji endelevu tofauti na wawekezaji wa hapo awali.
Mwisho, niwatakie kila la heri wote watakaosaidia kufufua viwanda vilivyokufa wakiongozwa na Mh. Rais.
usitembee juu ya ardhi kwa majivuno
Aidha, pamoja na nia hiyo njema, ni vyema wanaohusika kwenye zoezi hilo kujiuliza yafuatayo ili jambo hilo jema liweze kufanikiwa.
1. Ni lazima wajiulize ni sababu zipi zilifanya viwanda hivyo vibinafsishwe, na kwa nini walipewa hao waliopewa.
2. Inafaa wafanye utafiti kama sababu zilizotumika kuvibinafsisha bado zipo ama laaa!
3. Wanatakiwa wafanye utafiti pia kujua kuwa ni sababu zipi zilizopelekea waliomilikishwa viwanda hivyo kushindwa kuviendesha hata vikafa na kuwa magofu na kujiuliza kama sababu hizo hazipo tena kwa sasa na kama zipo, ni kwa namna gani zitashughulikiwa ili sasa viwanda hivyo viweze kusimama.
4. Inafaa kutafakari pia kuwa baada ya kutaifisha viwanda hivyo, serikali ndio itakayo viendesha au watapewa wawekezaji wengine, na kama itaendesha serikali, ni vyema kufanya utafiti wa namna ambavyo serikali inaweza kuviendesha kwa ufanisi, na kama ni wawekezaji, ni vizuri kujiridhisha kama kuna wawekezaji wako interested kuwekeza kwenye maeneo husika na ni kwa vipi wao wanaweza kuwa na uwekezaji endelevu tofauti na wawekezaji wa hapo awali.
Mwisho, niwatakie kila la heri wote watakaosaidia kufufua viwanda vilivyokufa wakiongozwa na Mh. Rais.
usitembee juu ya ardhi kwa majivuno