Rais Magufuli na Libya

Rais Magufuli na Libya

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
97,076
Reaction score
136,498
Ni mara kadhaa sasa nimemsikia mtukufu rais Dkt.John Pombe Joseph Magufuli, akiwa anazungumzia suala la amani, akiitolea mfano nchi ya Libya kipindi cha Gadafi.

Kwamba mambo huko Libya yalikuwa safi tu. Vijana waliokuwa wanaoa walipewa hela, nyumba, na mengineyo.

Inawezekana kweli walikuwa wanapewa hivyo vitu lakini je, walikuwa wako huru kiasi gani?

Gadafi alikuwa dikteta. Tena dikteta mkubwa tu aliyeng'ang'ania madaraka kwa muda mrefu sana hadi walipomfurumsha.

Mtukufu rais Magufuli naye watu wengi wameshaanza kumwona kuwa ni dikteta. Hataki watu wafanye siasa kwenye maeneo yasiyo yao.

Tumeshaona na kusikia watu wakikamatwa na kufunguliwa mashitaka kwa makosa ya kumtukana/ kusema maneno mabaya dhidi yake.

Tumeona vyombo vya habari vikifungiwa kwa sababu zisizo na mashiko.

Sasa haya mambo ya yeye kuisifia Libya ya Gadafi mimi yananitatiza.

Nabaki najiuliza maswali tu. Ina maana yeye Magufuli alikuwa anamwona Gadafi kuwa ni kiongozi bora aliyeweza kutunza amani huko Libya hadi awe anaisifia sifia hivyo?

Kama Gadafi ndo mmoja wa viongozi ambao Magufuli anawaona kama mfano mzuri wa utunzaji wa amani, watu wakimwona na yeye dikteta watakuwa wanakosea kweli?

Ndo mambo ya ndege wafananao hayo au..?
 
Pamoja na mapungufu yake, maisha yalikuwa nafuu sana kipindi cha Gadafi kulilo ilivyo sasa, hilo wala si jambo la kujadiliana. Hata hao waliovamia wanapata wakati mgumu maana hawakujua hali ingekuwa kama ilivyo sasa. Better the devil you know...
 
Sasa kama mtu Role model wake ni Kagame unategemea na yeye atakuwaje?
Moja wapo ya alama ya udiketa ni matamshi ya vitisho kama haya "mtu akikuchezea niambie, haitachukua hata dakika 5"

Huyu ilashaonekana toka anagombea kwake msamiati Demokrasia haupo na haamini kama upo.
 
kesho ni jumapili tukamwombee mtukufu wetu kama alivyoagiza mana ana matatizo kishajigundua ndo mana katoa ruksa ya kumwombea wale wa dini zote tufanye hivyo kabla mambo hayajaharibika lawama zitakuwa kwetu.
 
Sasa kama mtu Role model wake ni Kagame unategemea na yeye atakuwaje?
Moja wapo ya alama ya udiketa ni matamshi ya vitisho kama haya "mtu akikuchezea niambie, haitachukua hata dakika 5"

Huyu ilashaonekana toka anagombea kwake msamiati Demokrasia haupo na haamini kama upo.



anatoa hayo maagizo hajui kuwa kule yupo chini ya shein cheo chake hakitambuliki kule hizo ndo dalili za uchawara.
 
Kuna walibya WALIPOULIZWA Kwanini wanataka Gaddafi aondoke walijibu kuwa wanapenda demokrasia zaid. Wazungu wakasema shwari. Walibya wakasaidiwa kumtoa Gaddafi madarakan, tena kwa aibu kubwa. Kilichofuata ndo kama tunavyoona. Hakuna maendeleo wala demokrasia. Hakuna Uhuru wala fursa. Yaliyobaki ni majuto. Libya imevurugwa
 
Wakati mwingine unaweza kuwa mtu wa aina fulani lakini ukakosa sifa kutokana na kile unachokitetea. Ngabu unahoja dhaifu, hoja ambayo huwa naifananisha na nyimbo za mipasho. Umekuwa mmoja kati ya wenye kuziba macho na kujitia upofu hata pale linapofanywa jambo lililosahihi. Umekuwa na hulka ya kujifanya unajua kila kitu lakini hutambui kuwa hujui. Mwana Africa yoyote asiyetambua kile alichokifanya GADAFI katika uhai wake na kile kinachoendelea baada ya kuondoka kwake Ni muongo na mtu wa kuogopwa

Unafki hausaidii katika kutafuta kilicho cha kweli. Mipasho kama hii haipaswi kuandikwa na wewe. lakini kwa kuwa umekuwa muimbaji wa taarab endelea kutawala jukwaa ipo siku utapata ufalme kama sio umalikia. TANZANIA NI YA KWETU
 
Huwa anaongelea na Iraq pia...
Somo muhimu ambalo rais wetu Magufuli anashindwa kulielewa ni: hata mtu awe anapata mahitaji yote lakini kama hana uhuru na haki basi hataridhika, na akipata mwanya au sababu hata mbaya namna gani ya kurudisha uhuru na haki yake iliyopotea yupo tayari kuitumia bila kujali atapoteza zile huduma anazopata.
 
Ni mara kadhaa sasa nimemsikia mtukufu rais Dkt.John Pombe Joseph Magufuli, akiwa anazungumzia suala la amani, akiitolea mfano nchi ya Libya kipindi cha Gadafi.

Kwamba mambo huko Libya yalikuwa safi tu. Vijana waliokuwa wanaoa walipewa hela, nyumba, na mengineyo.

Inawezekana kweli walikuwa wanapewa hivyo vitu lakini je, walikuwa wako huru kiasi gani?

Gadafi alikuwa dikteta. Tena dikteta mkubwa tu aliyeng'ang'ania madaraka kwa muda mrefu sana hadi walipomfurumsha.

Mtukufu rais Magufuli naye watu wengi wameshaanza kumwona kuwa ni dikteta. Hataki watu wafanye siasa kwenye maeneo yasiyo yao.

Tumeshaona na kusikia watu wakikamatwa na kufunguliwa mashitaka kwa makosa ya kumtukana/ kusema maneno mabaya dhidi yake.

Tumeona vyombo vya habari vikifungiwa kwa sababu zisizo na mashiko.

Sasa haya mambo ya yeye kuisifia Libya ya Gadafi mimi yananitatiza.

Nabaki najiuliza maswali tu. Ina maana yeye Magufuli alikuwa anamwona Gadafi kuwa ni kiongozi bora aliyeweza kutunza amani huko Libya hadi awe anaisifia sifia hivyo?

Kama Gadafi ndo mmoja wa viongozi ambao Magufuli anawaona kama mfano mzuri wa utunzaji wa amani, watu wakimwona na yeye dikteta watakuwa wanakosea kweli?

Ndo mambo ya ndege wafananao hayo au..?


!
!
labda model wake ni waina hii....Akina Sadam wa Iraq , akina Gadaffi wa Libya, akina Asad wa Syria.
 
Nani aliomba upuuzi uo labda waulize Mimi cha kwanza kwangu ni Uhuru,
Wa kusema
Kutembea
Kutotharirishwa
Mwambie uchara ajipange tunataka democracy

Utakula huo Uhuru?

Uhuru ndio utajenga barabara na kuhakikisha watoto wote wanaenda shule na kupata elimu bora? Uhuru ndio utaleta madawa hospitalini?

Ingekuwa hivo nchi za kiafrika zisingekuwa hapa kimaendeleo miaka zaidi ya 50 tangia zilipoanza kupata Uhuru.
 
Utakula huo Uhuru?

Uhuru ndio utajenga barabara na kuhakikisha watoto wote wanaenda shule na kupata elimu bora? Uhuru ndio utaleta madawa hospitalini?

Ingekuwa hivo nchi za kiafrika zisingekuwa hapa kimaendeleo miaka zaidi ya 50 tangia zilipoanza kupata Uhuru.
Mbona Kikwete alijenga barabara za kutosha kwani udicteta wake hata saa hii unanilisha
Mwambie aachie pesa watu tuludi baa
!
!
labda model wake ni waina hii....Akina Sadam wa Iraq , akina Gadaffi wa Libya, akina Asad wa Syria.
 
Back
Top Bottom