Rais Magufuli na kitabu cha siri

TumainiEl

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
7,275
Reaction score
14,315
Ni vyema tukajua Rais hafanyi jambo lolote pasipo kuwa na muongozo au watu nyuma yake kumuongozo.

Kitabu cha siri ambacho wanao kiona ni wale tu wenye cheo cha Rais wa jamuhuri wa muungano tu ndio muongozo wa kazi zake za urais.

Wajinga wachache wasiojua kuwa Rais ana muongozo ndio wanao tupotosha.

Zipo siri nzito ambazo mimi na wewe hatuzijui na ni bora tukae kimya maana Rais hajaribu kazi ila anafanya kazi kwa mujibu wa muongozo huo.

Ipo kazi lazima ifanyike chini ya Mh Magufuli. Wengi watalia na kupiga kelele ila kaz lazima ifanyike.
 
Wewe kama Rais wa jamuhuri mstaafu ulikiona?..
 
Wewe umejuaje kama kunakitabu cha siri, that means you know the content. Speak out!
 


Kama hadi wewe umekijua hicho kitabu basi si kitabu cha siri tena
 
Kitabu cha siri ambacho habari zake tayari ziko hapa na mleta hoja unajua fika kwamba Mheshimiwa anatekeleza yaliyomo humo ndani na wakati yeye sio miongoni mwa marais wastaaf tayari inatoa sifa ya hicho kitabu kuitwa cha siri.
 
100% in the Kremlin
 
Hadithi hadithi...
Hongera imara waa.

So long ni cha siri kinafanya yasirini. Sisi tunajadili yaliofunuliwa..
 
Yule aliyepita alikuwa na kitabu cha tofauti?
 
Mwongozo wa Nchi yeyote Ni KATIBA, Hayo Mengine ya Vitabu ya Matunguri Na Ramli unavijua wewe. In short there is no such thing as a secret book! Au hicho Kitabu ndicho kilichomwambia JK awalaze Wamama chini Mhuhimbili, Aachie Makontena bila Kodi, Alambe Escrow! Ashindane kuipiku record ya Vasco Da Gama, Na Kitabu hicho hicho Kikamwambia JPM, Apige vita mambo hayo. My best you sound soooooo funny! Hizo hadaa za Juma na Roza, na Bulicheka peleka kwa stooges wa Lumumba! Good try though!
 
Mleta uzi amefananisha na kitabu cha siri cha marekani ambacho rais pekee anakuwa nacho au anakijua mwanzo mwisho hakuna mwingine! Hicho nadhani hata hapa kipo au kitakuwepo ambapo kina siri zote za nchi kama kambi za majeshi tiss mikataba mikubwa ya siri ya usalama maazimio ya siri ya usalama (muungano wa zbar)..etc...hicho nadhani asichanganye na operation za kila siku za rais hizo info na files zinatoka kwa taasisi zake usalama takukuru na hata media....nimejaribu kuona Mleta uzi alichokuwa anamaanisha!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…