Rais Magufuli kuibadilisha TANESCO

Rais Magufuli kuibadilisha TANESCO

Kichwa cha habari yako badilisha kimejaa uongo.
Ubinafsishaji dunia nzima haufanyiki kwenye kila kitu.Maji ni bidhaa nyeti na adimu huwezi kuibinafsisha.Biashara ya maji ipo lakini ni ile kama ya maji ya kilimanjaro,Uhai nk ya kufunga kwenye chupa lakini huwezi binafsisha watu wamiliki mito na maziwa na waamue hayo maji wanayasambazaje.

Umeme pia ni swala nyeti huwezi kukabidhi bepari apewe bwawa la kidatu azalishe umeme asambaze nchi nzima kwa pesa yake .Siku mkimtibua anazima switch umeme unakatika nchi nzima anagoma kuwasha hadi msalimu amri kwenye matakwa yake.Kiusalama ni hatari Umeme ni eneo nyeti.Lakini kuuza majenereta ruksa au kujiwekea umeme unaotumia upepo sio maporomolko ya maji au mito mbona inaruhusiwa.Ndio maana hata IPTL wanaotumia mitambo (majenerator makubwa) kuzalisha umeme WAPO
Hoja dhaifu. Nchi nyingi kuna kampuni binafsi za uzalishaji na usambazaji wa umeme. Nchi kama Japan umeme wote unazalishwa na kasambazwa au na kampuni binafsi au kampuni binafsi zenye ubia na serikali.

Haya mambo ya kila wakati kusema kwaajili ya usalama wa nchi ndiyo yanalirudisha nyuma Taifa letu. Zamani hata ukitaka kujua JWTZ ina askari wangapi, utaambiwa hutakiwi kujua kwa sababu ya usalama wa nchi. Leo hii taarifa za majeshi ya nchi mbalimbali unazipata mpaka kwenye mitandao.

Zamani hata huduma za simu tuliaminishwa haiwezekani kutolewa na kampuni kwa sababu ya usalama wa nchi. Leo zinatolewa. Ni usalama gani wa nchi uliotokea?

Tuondokane na mawazo mgando.
 
Suala la Tanesco ku-monopoly soko la umeme ni la kijinga sana. Bila ushindani na kupewa ruzuku ni shida. Japokuwa mimi naona Serikali ingejikita vilivyo katika kuzalisha umeme lakini msambazaji awe mwingine na hata mkusanya mapato iwe ni kampuni nyingine. Si kama ilivyo Tanesco inazalisha, inasambaza na kuuza. Hapana. Tukifagawa hili eneo la usambazaji waje mult-companies wasambaze hapo ndo ushindani utakuwa mkubwa na mlaji kama wewe hapo juu unayeomba kuunganishwa miezi 4 ungeshaunganishwa maana kama huyu angekuzingua ungeenda kwa yule. Naunga mkono hoja 90%.
Kula like mkuu. Hapo ndio kwenye hoja zaidi.
Tanesco ya sasa igawanywe katika mashirika matatu.
1. Wazalishaji.(Kuzalisha na kutafuta vyanzo vipya vya umeme).
2. Supplier(kununua umeme kutoka kwa mzalishaji na msambazaji wa umeme, pia kazi yake ni kutafuta wateja,kutoa huduma ya umeme(bidhaa) na kufanya makusanyo(bill charge collection).
3. Technical support. Kazi yake ni kuunganisha wateja wapya baada ya kuwa approved na supplier, kuboresha miundo mbinu na matengenezo.

Hapa tutapata mashirika matatu timilifu na sio kana hivi sasa shirika la tanesco limekuwa kama kichaka na pango la wezi na kupigia dili. Hapa kuna mikono mikubwa ya wanyonyaji na watanzania wasio waaminifu.
 
Walishaambiwa sana hawa lakini wametia pamba maskioni. Kuna kampuni moja hivi inashughulika na installation ya grid ya umeme kwa solar panel na kusambaza hasa vijijin, lakini wanapigwa zengwe na kunyimwa access ya kufunga mitambo yao sehem zingine nchi ishauzwa na kununuliwa kwa mkopo.
 
Kichwa cha habari yako badilisha kimejaa uongo.
Ubinafsishaji dunia nzima haufanyiki kwenye kila kitu.Maji ni bidhaa nyeti na adimu huwezi kuibinafsisha.Biashara ya maji ipo lakini ni ile kama ya maji ya kilimanjaro,Uhai nk ya kufunga kwenye chupa lakini huwezi binafsisha watu wamiliki mito na maziwa na waamue hayo maji wanayasambazaje.

Umeme pia ni swala nyeti huwezi kukabidhi bepari apewe bwawa la kidatu azalishe umeme asambaze nchi nzima kwa pesa yake .Siku mkimtibua anazima switch umeme unakatika nchi nzima anagoma kuwasha hadi msalimu amri kwenye matakwa yake.Kiusalama ni hatari Umeme ni eneo nyeti.Lakini kuuza majenereta ruksa au kujiwekea umeme unaotumia upepo sio maporomolko ya maji au mito mbona inaruhusiwa.Ndio maana hata IPTL wanaotumia mitambo (majenerator makubwa) kuzalisha umeme WAPO
Sawa kabisa kila kubinafsha, utaishia kubinafsha hata polisi, keshi, usalama wa taifa. Issue hapa ni kuboresha. Toa uzi wa luboresha sio lawama na lugha za majukwaani na ajira za vijana. Jamani tubadilike
 
kwahiyo nchi nzima si itajaa mistimu na waya za umeme au wao watafanya wireless au watasimamisha minara kma ya simu?
 
Sawa kabisa kila kubinafsha, utaishia kubinafsha hata polisi, keshi, usalama wa taifa. Issue hapa ni kuboresha. Toa uzi wa luboresha sio lawama na lugha za majukwaani na ajira za vijana. Jamani tubadilike
Mkuu, hapa hatuongelei kubinafsishwa, hapa tunaongelea tanesco ipunguziwe majukumu. Hii inaendana na tanesco isiwe monopoly kwenye nishati ya umeme pekee.

Je, unafahamu haya?
1) mpaka sasa Tanesco inaogharimu nchi kiasi gani? Serikali inakopa hela world bank, ADB, European Union kuifadhili Tanesco. Swali, mpaka leo imeshatokea mwaka wowote wa fedha Tanesco ikasema imepata faida? Hapo utagundua, Tanesco ni kichaka cha watu kula pesa, sio kufanya biashara ya umeme.

2) ufisadi mkubwa nchini. Richmond, escrow, umetokea Tanesco.

3) nchi yetu bado maskini, walimu wanalia njaa, polisi wanalia njaa, madaktari wanalia njaa. Hizi pesa za kuwekeza Tanesco kwenye biashara ambayo hailipi? kwanini serikali isafanye mambo mengine ya muhimu. Na kuacha umeme uwe biashara huru kama ilivyo biashara ya mawasiliano ya simu? Hivi leo umeshaona TTCL inaumiza kichwa? Mh, Mkapa aliicha ifanye biashara kwa ushindani sio kutegemea ruzuku za serikali kila siku.

4) Ata aje raisi mkali zaidi ya Mh. Magufuri. Miaka100 ijayo, umeme bado utakuwa shida Tanzania.
Na ndugu yangu usiangalie hapa Dar es salaamu tu, uko vijijini ndo shida zaidi. Tanesco sio wabunifu, na hawawezi kuwa wabunifu kwa sababu hawana ushindani wa soko.
Utashangaa watu vijijini wana simu, lakini umeme hawana. Why, Tanesco haijaweza kutafuta soko. Kwa population ya watu mil 50. Tanesco has proved failure
 
Tusirukie vitu bila kujua athari zake kubwa kwa wateja. Hayo mataifa makubwa mengi sasa hivi yamegundua kwamba walifanya makosa makubwa sana kubinafsisha huduma muhimu za maji na umeme.

Privatisation of energy industry was a mistake, Ed Miliband suggests
Mkubwa hakuna kitu kisicho na hasara. And you know mataifa makubwa hawapendagi nchi masiki zifunguke macho. Watakupa misaada, ili kukufanya uwe tegemezi kila siku. They will even write articles kukukatisha tamaaa. Hivi, unajua kwanini walimuua Gadafi?

Obama amefanikiwa kutengeneza ajira nyingi marekani. Unajua hizo ajira almost zote zimetokana na private sector. Huyo anayeandika hizo articles is just fooling arround.

Ndugu nikupe tu taarifa, hakuna nchi duniani inaweza ikawa mfanyabiashara mzuri. Nchi nzuri kazi yake ni kukusanya kodi na kutunga sheria, ili wafanyabiashara wawe na nidhamu. Na uzuri Mh, Raisi wetu anajua hilo. Ndo maana kwenye ufunguzi wa flyover ya Tazara aliongelea miradi ya PPT. Ata china wenyewe magwiji wa communist, kwao kuna madaraja ya watu binafsi, umeme wa watu binafsi. Nenda Russia, India etc.

nchi tukitaka kufanya mambo yote kwa wakati mmoja tuta-fail. Barabara, ulinzi, elimu, madawa. Hivi vyote na bado tunafanya biashara ya umeme kupitia tanesco ambayo hatupatagi faida zaidi ya hasara tu.

Kikubwa ni mipango. Swali kubwa ni mnataka private sector wababaishaji au walio serious. Ukiwa serious utapata watu serious, ukiwa legelege utapata wawekezaji wababaishaji.

Sisi hatukuwa serious ndo maana ata madini tunaibiwa. Angalia nchi za kiarabu, je wao wanaibiwa natural resources kama sisi? All count ni mipango na sera za nchi.

Na private sector sio lazima aje mzungu au muhindi. Ndo maana Mh Raisi amempa Bakhresa ekari 10,000 bure. Mh Raisi anatambua kuwa ata wawekaziji wa ndani wanaweza kuwa serious kuliko wa nje. Marekani, china, wanawatumia matajiri wao kuwekeza, ndo maana Raisi wa marekani, china, india akitembea, huwa anatembea na wafanyabiashara wake.

Waziri Mpango yuko Marekani kwa sasa. Amekutana na viongozi wa wakubwa wa World bank. Moja ya ajenda, ni kusaidiwa kulipa deni kubwa la Tanesco. This is shame, am telling you. Kwanini Tanesco iendelee kufilisi nchi??
 
Mkuu hapo unalaumu kivuli. Hayo yote yasemee kwa mwenye kivuli. Unaonea kivuli jitahidi kuwa more investigative plse halafu baada ya mwezi utafuta huu uzi.
 
Andiko murua kabisa.Nikukumbushe jambo moja kubwa linalokwamisha nchi hii.Jambo lenyewe ni kwamba nchi yetu UHABA WA WASOMI WAADILIFU.Hili ni janga la taifa.Simaanishi wasomi wote ila walio wengi wanatia shaka uadilifu wao.Ukiangalia majipu yote aliyotumbua Rais Magufuli ni wasomi,na chanzo kikubwa ni kutokua waadilifu.Kwa hiyo mnaweza kupanga mipango mizuri lakini unapokua watekelezaji wasio na uzalendo ni kazi bure.
 
Na mwandishi wetu.

Promoting private sector will be a permanent solution kwa uchumi wa Tanzania. Kwa vizazi hivi na vijavyo.

MWANZO

Hatuwezi kulilia viwanda vilete ajira. Wakati sector kama umeme na maji, zinaweza kutuletea ajira kubwa. Kuna hoja kubwa na za msingi kuzitumia (exploit) sector hizi ziweze kutengeneza ajira nyingi na za kutosha.

Mpaka sasa Tanesco imeweza kuwafikia sio zaidi ya asilimia 20 ya watanzania wote. Kwa population ya watu milion 50 ina maana Tanesco inahudumia wateja milion 10 tu. Mbali na serikali kutumia hela nyingi kuwekeza Tanesco, sijwahi kusikia hata siku moja Tanesco imefanikiwa kujiendesha yenyewe. Umeme ni kichaka kingine kinachosababisha serikali kukopa fedha nyingi nje kuisaidia Tanesco. Inasababisha hata deni la taifa kuwa kubwa. Mbali na kashfa ambazo haziishi (dowans, Richmond, escrow).

NINI KIFANYIKE

  • Huduma ya Umeme inatakiwa iwe ya ushindani kama ilivyo kwenye masiliano. Serikali iruhusu watu binafsi wawekeze kwenye umeme. Swala la umeme kuiachia Tanesco kuwa monopoly, (ambayo kimsingi imesha prove failure kwa mda mrefu) ni kuziminya fursa nyingi za uchumi.
  • Tuangalie mapinduzi ya technology na mawasiliano yaliyoletwa na makampuni ya simu, baada ya serikali kuacha TTCL monopoly. Tigo, airtel, vodacom, halotel, zantel . Kwa ujumla wao wametoa ajira kwa vijana wangapi Tanzania? Je, leo hii tungekuwa na tigopesa au mpesa kama TTCL ingekuwa bado monopoly?
  • Kwa takwimu za mwezi uliopita Tanzania ni nchi ambayo inaongoza Duniani kwa matumizi ya pesa za simu. Takribani watu milioni 21 kila siku wanafanya money transaction kupitia mitandao ya simu. Tuje kwa Tanesco, hawa jamaa wana wateja wangapi wa kuwahudumia kwa siku? kama wateja wao kwa jumla hawazidi milioni 10?
  • Unagundua kwamba Tanesco has low capacity, and imekalia fursa nyingi za uchumi bila sababu. Tanesco iko busy mjini tu, vijijini uko hakuna kitu wala dalili za umeme.
FAIDA
  • Sector ya umeme na maji ikiachiwa kuwa huru, nina uhakika inaweza kutengeneza ajira zaidi ya watu milioni 10. Ni zaidi ya viwanda tunavyovisubiria.
  • Private sector inaleta ushindani mkubwa kwenye soko, ata bei ya bidhaa hupungua. Umeme utashuka bei tukiruhusu hili.
  • kuna vijiji hapa Tanzania kwa miaka 1000 ijayo havitapata umeme. Hata Kama Prof Muhogo akiwa anakesha mikoni kuzunguka. Lakini utashangaa hivyo vijiji mitandao ya simu imefika, vocha wanapata, na bado pesa wanatoa kwenye simu.
  • Deni la taifa litashuka. Serikali ipunguze pesa kufadhili hili shirika, na hizi pesa zipelekwe kwenye sector muhimu kama polisi, barabara, elimu. Ambayo Mh Raisi amehaidi
TUNACHOPASWA KUJUA
  • Hakuna nchi duniani imeshawahi kuwa mfanyabiashara mzuri. Nchi zilizoendelea duniani zinatumia private sector kuwekeza in their behalf. Wamefanikiwa kutawala dunia kupitia private sectors za nchi zao.
  • Inshort Public sector huwa hazina ubunifu na focus kama ilivyo private sector. Na ndo maana ata ukiongelea rushwa. Zaidi utaikuta kwenye mashirika na ofisi za serikali. why? Because nobody cares. Na hii sio Tanzania tu, duniani kote. Serikalini urasimu hauwezi kuisha ata kama Mh Raisi akiwa mkali mpaka mwisho. Kuruhusu uwekezaji huru, unapunguza kichaka cha urasimu na rushwa kwenye huduma za jamii.
  • mbali na kutoa ajira, itaisaidia serikali punguza mzigo kutoa fedha kila siku kwa biashara ambayo imeshindikana. kwa kutegemea Tanesco na Dawasco Miaka 10 ya Mh Raisi itaisha, lakini bado vijijini hakuna umeme wala Maji.
  • Tunahitaji mashirika ya umeme kutembea kila nyumba kutafuta wateja, sio kama ilivyo sasa unaandika barua ya maombi mwezi mzima, na bado rushwa juu unatoa. Transforma inaharibika, unaambiwa tunapeleka maombi makao makuu usubiri mwezi mmoja. Karne hii kweli biashara inaenda kwa style hii?
  • Tusiogope uwekezaji binafsi, na tusione private sector ni adui. Cha msingi ni kuweka mikakati ya kipamoja na kimaslahi kwa pande zote mbili. Mfano, Malaysia miundo mbinu kama umeme, treni, madaraja yamejengwa na watu binafsi. kwa kushirikiana na private sector nchi nyingi zimepiga hatua haraka. cha msingi ni kuweka mikakati mizuri ambayo kila mtu anafaidika.
conclusion
Kwa mtaji wa population ya watu milion 50, Sector ya umeme na maji, inaweza kutengenzea ajira kubwa kuliko viwanda ambavyo bado tunavifikira.

Katiba ndio issue namba moja. Kwmfn walisema watapunguza idadi ya wizara, wameongeza mikoa na wilaya! Matumizi ya Serikali ni tundu linalopoteza fedha nyingi kwa mambo yasiyo muhimu. Hata idadi ya wabunge ni kubwa kupita kiasi ambapo kazi za Bunge <budget> sasa zimemezwa na maamuzi ya Rais. Nia ya JPM ni nzuri lakini ingefaa kufuata sheria na miongozo rasmi.
 
Mkuu Ulichomjibu Mdau Ni Kweli Ama Vp
Maana Nami Nimelipia Umeme Tangu 24.06.2016 Morogoro Kingolwira Ila Daily Naambiwa Mita Hakuna Sasa Ni Chache Ana Huduma Ni First In,First Out
Maana Nina Miezi Minne Sasa!
Nasisi wakazi ws Kasanga Morogoro hatujawahi kupata umeme toka dunia iumbwe...eneo lenyewe liko karibu na mji na wala haliko vijijini. Tuliomba umeme wa REA tukaambiwa eti hapo sio vijijini...haya tuletee umeme wa mjini hapana...je TANESCO inatufaa kweli?.

Kasanga tunahitaji umeme...
 
Nasisi wakazi ws Kasanga Morogoro hatujawahi kupata umeme toka dunia iumbwe...eneo lenyewe liko karibu na mji na wala haliko vijijini. Tuliomba umeme wa REA tukaambiwa eti hapo sio vijijini...haya tuletee umeme wa mjini hapana...je TANESCO inatufaa kweli?.

Kasanga tunahitaji umeme...

Tanesco sio wafanya biashara, kukupa umeme wanaona kama wanakupa msaada. Wakati huo huo mwisho wa mwezi unalipa bill yao.
Tanesco hawawezi kumsaidia Mh Raisi kwenye swala la kuongeza ajira, na hata swala la kuleta viwanda nchini. Bila kubadilisha mfumo wa biashara ya umeme, Muheshima ata awe mkali kama pilipili. miaka 10 yake itaisha. umeme utakuwa bado fumbo.

Tanzania ni nchi ambayo uchumi wake unakua kwa kasi. Sekta inayochangia kasi hii ni sekta ya mawasiliano. Haya ni matunda ya Ndg Ben Mkapa baada ya kuacha monopolism ya TTCL na kuruhusu uwekezaji binafsi. Hili limeleta mageuzi makubwa. leo ata vijijini watu wanatumia simu. Je, bila akili ya ndugu Mkapa, leo tungekuwa wapi kwenye mawasiliano?
 
Jamani Mimi naomba ushauri nimelipia umeme miezi minne iliopita na sijapata hadi Leo ukiwauliza sababu haziishi sasa waugwana nipeni njia itakayo nisaidia Mimi kupata umeme pasipo rushwa


subiri tuuu....huwa mara nyingi hadi wapate watu wengi wanaotaka umeme katika eneo hilo ndio wanaita mradi... wanakuja kuwawekea...au ujitoe kimaso maso kama nguzo zinahitajika ununue, na luku na uwe na kifuta jasho cha anayekuja kuweka ndipo uongee nao
 
..umeme.

..reli.

..bandari.

..havitakiwi kubinafsishwa.

Nb.

..tulikosea kubinafsisha ttcl.
 
Kichwa cha habari yako badilisha kimejaa uongo.
Ubinafsishaji dunia nzima haufanyiki kwenye kila kitu.Maji ni bidhaa nyeti na adimu huwezi kuibinafsisha.Biashara ya maji ipo lakini ni ile kama ya maji ya kilimanjaro,Uhai nk ya kufunga kwenye chupa lakini huwezi binafsisha watu wamiliki mito na maziwa na waamue hayo maji wanayasambazaje.

Umeme pia ni swala nyeti huwezi kukabidhi bepari apewe bwawa la kidatu azalishe umeme asambaze nchi nzima kwa pesa yake .Siku mkimtibua anazima switch umeme unakatika nchi nzima anagoma kuwasha hadi msalimu amri kwenye matakwa yake.Kiusalama ni hatari Umeme ni eneo nyeti.Lakini kuuza majenereta ruksa au kujiwekea umeme unaotumia upepo sio maporomolko ya maji au mito mbona inaruhusiwa.Ndio maana hata IPTL wanaotumia mitambo (majenerator makubwa) kuzalisha umeme WAPO
Umenifulahisha,huo ndio ukweli.vitu ambavyo sio vizuri kubinafsisha ni maji,umeme,mawasiliano,viwanja vya ndege,bandari,sehemu hizo ukizibnafsisha nchi yako haitakua walama hata kidogo.
 
Na mwandishi wetu.

Promoting private sector will be a permanent solution kwa uchumi wa Tanzania. Kwa vizazi hivi na vijavyo.

MWANZO

Hatuwezi kulilia viwanda vilete ajira. Wakati sector kama umeme na maji, zinaweza kutuletea ajira kubwa. Kuna hoja kubwa na za msingi kuzitumia (exploit) sector hizi ziweze kutengeneza ajira nyingi na za kutosha.

Mpaka sasa Tanesco imeweza kuwafikia sio zaidi ya asilimia 20 ya watanzania wote. Kwa population ya watu milion 50 ina maana Tanesco inahudumia wateja milion 10 tu. Mbali na serikali kutumia hela nyingi kuwekeza Tanesco, sijwahi kusikia hata siku moja Tanesco imefanikiwa kujiendesha yenyewe. Umeme ni kichaka kingine kinachosababisha serikali kukopa fedha nyingi nje kuisaidia Tanesco. Inasababisha hata deni la taifa kuwa kubwa. Mbali na kashfa ambazo haziishi (dowans, Richmond, escrow).

NINI KIFANYIKE

  • Huduma ya Umeme inatakiwa iwe ya ushindani kama ilivyo kwenye masiliano. Serikali iruhusu watu binafsi wawekeze kwenye umeme. Swala la umeme kuiachia Tanesco kuwa monopoly, (ambayo kimsingi imesha prove failure kwa mda mrefu) ni kuziminya fursa nyingi za uchumi.
  • Tuangalie mapinduzi ya technology na mawasiliano yaliyoletwa na makampuni ya simu, baada ya serikali kuacha TTCL monopoly. Tigo, airtel, vodacom, halotel, zantel . Kwa ujumla wao wametoa ajira kwa vijana wangapi Tanzania? Je, leo hii tungekuwa na tigopesa au mpesa kama TTCL ingekuwa bado monopoly?
  • Kwa takwimu za mwezi uliopita Tanzania ni nchi ambayo inaongoza Duniani kwa matumizi ya pesa za simu. Takribani watu milioni 21 kila siku wanafanya money transaction kupitia mitandao ya simu. Tuje kwa Tanesco, hawa jamaa wana wateja wangapi wa kuwahudumia kwa siku? kama wateja wao kwa jumla hawazidi milioni 10?
  • Unagundua kwamba Tanesco has low capacity, and imekalia fursa nyingi za uchumi bila sababu. Tanesco iko busy mjini tu, vijijini uko hakuna kitu wala dalili za umeme.
FAIDA
  • Sector ya umeme na maji ikiachiwa kuwa huru, nina uhakika inaweza kutengeneza ajira zaidi ya watu milioni 10. Ni zaidi ya viwanda tunavyovisubiria.
  • Private sector inaleta ushindani mkubwa kwenye soko, ata bei ya bidhaa hupungua. Umeme utashuka bei tukiruhusu hili.
  • kuna vijiji hapa Tanzania kwa miaka 1000 ijayo havitapata umeme. Hata Kama Prof Muhogo akiwa anakesha mikoni kuzunguka. Lakini utashangaa hivyo vijiji mitandao ya simu imefika, vocha wanapata, na bado pesa wanatoa kwenye simu.
  • Deni la taifa litashuka. Serikali ipunguze pesa kufadhili hili shirika, na hizi pesa zipelekwe kwenye sector muhimu kama polisi, barabara, elimu. Ambayo Mh Raisi amehaidi
TUNACHOPASWA KUJUA
  • Hakuna nchi duniani imeshawahi kuwa mfanyabiashara mzuri. Nchi zilizoendelea duniani zinatumia private sector kuwekeza in their behalf. Wamefanikiwa kutawala dunia kupitia private sectors za nchi zao.
  • Inshort Public sector huwa hazina ubunifu na focus kama ilivyo private sector. Na ndo maana ata ukiongelea rushwa. Zaidi utaikuta kwenye mashirika na ofisi za serikali. why? Because nobody cares. Na hii sio Tanzania tu, duniani kote. Serikalini urasimu hauwezi kuisha ata kama Mh Raisi akiwa mkali mpaka mwisho. Kuruhusu uwekezaji huru, unapunguza kichaka cha urasimu na rushwa kwenye huduma za jamii.
  • mbali na kutoa ajira, itaisaidia serikali punguza mzigo kutoa fedha kila siku kwa biashara ambayo imeshindikana. kwa kutegemea Tanesco na Dawasco Miaka 10 ya Mh Raisi itaisha, lakini bado vijijini hakuna umeme wala Maji.
  • Tunahitaji mashirika ya umeme kutembea kila nyumba kutafuta wateja, sio kama ilivyo sasa unaandika barua ya maombi mwezi mzima, na bado rushwa juu unatoa. Transforma inaharibika, unaambiwa tunapeleka maombi makao makuu usubiri mwezi mmoja. Karne hii kweli biashara inaenda kwa style hii?
  • Tusiogope uwekezaji binafsi, na tusione private sector ni adui. Cha msingi ni kuweka mikakati ya kipamoja na kimaslahi kwa pande zote mbili. Mfano, Malaysia miundo mbinu kama umeme, treni, madaraja yamejengwa na watu binafsi. kwa kushirikiana na private sector nchi nyingi zimepiga hatua haraka. cha msingi ni kuweka mikakati mizuri ambayo kila mtu anafaidika.
conclusion
Kwa mtaji wa population ya watu milion 50, Sector ya umeme na maji, inaweza kutengenzea ajira kubwa kuliko viwanda ambavyo bado tunavifikira.
Uwekezaji wa umeme ni tofauti sana na uwekezaji wa mawasiliano. Kwenye umeme kuna miundombinu ya kuzalisha umeme, kuusafirisha na kuusambaza kwa watumiaji. Hakuna nchi duniani inayoruhusu soko la umeme kuwa la kila anayetaka kama ilivyo kwa mawasiliano. Mawasiliano ya simu miundombinu yake ni rahisi zaidi ya mara 1000 ya gharama za uwekezaji wa umeme. Miundombinu ya umeme ndio usalama wa nchi yeyote duniani.
Hata nchi zenye mashirika zaidi ya moja mengi yanamilikiwa na Serikali husika na watu binafsi wanapewa either wazalishe na kuiuzia Serikali au wanunue Serikalini wasambaze kwa wateja wao. Ila ni ngumu au hakuna anayeweza kuzalisha, kusafirisha na kusambaza kwenda kwa wateja wake binafsi. Vilevile uendeshaji wa umeme si kama uendeshaji wa mitandao ya mawasiliano. Umeme kuna kipindi utalazimika kuwasha mitambo iliyo ghari zaidi ili uwaridhishe wateja wako hasa kipindi cha matumizi yakiwa juu.
Kwa sasa hata kama watu wataeuhusiwa kuzalisha na kuuza kwa wateja wengi watashindwa! Posbility iliyopo ni kuigawa TANESCO kikanda au kukodisha baadhi ya maeneo kwa watu binafsi wayaongoze kibiashara
 
Back
Top Bottom