Rais Magufuli hajawahi kataza mtu kutembelewa na wageni

MwanaPekee

JF-Expert Member
Jul 18, 2014
382
385
Mwaka 2015 hasa katika kuelekea katika uchaguzi mkuu, tuliona Mh. Edward Lowassa akitembelewa na wageni katika makundi mbalimbali. Tuliona makundi ya vijana waliojiita “Wazalendo”, makundi ya Viongozi wa dini, Makundi ya wafugaji na wakulima, na makundi mengineyo.

Ni makundi yaliyodai kuwa yanakwenda kwake kwa lengo la kumsalimia mpendwa wao huyo, lakini pia kumshawishi kuchukua fomu za kugombea katika nafasi ya Urais wa JMT kupitia CCM. Ni makundi yaliyotushangaza wengi kwa namna ambavyo yalikuwa yakipishana mlangoni, na kuitawala kalenda ya mheshimiwa Eddo kwa kiasi kikubwa.

Yaliibuka madai kutoka kwa watu mbalimbali kwamba makundi hayo yaliandaliwa na kugharamiwa na “mtembelewaji”, lakini wengine tulikataa na kusema hayo makundi yaliashiria upendo mkubwa wa Watanzania kwa Mzee wetu huyo. Lakini cha kushngaza tangu aangushwe katika uchaguzi ule wa Mwaka 2015, hao wageni hawaendi tena kwake kwa lengo la kwanza ambalo ni kumsalimia. Ni kama amekuwa adui yao sasa, maana urafiki wao haupo kwa kiasi kile tulichoshuhudia kipindi hicho. Hali hii inatufanya sasa tuamini kwamba huo mchezo aliucheza Mzee mwenywewe ili kuweza ku-win mawazo ya watu wengi kwamba anapendwa sana, ambapo kwa kiasi chake alifanikiwa; maana alipata kura nyingi though hazikutosha. Mh. Rais Magufuli hajakataza watu kutembelewa na wageni nyumbani kwao, hivyo makundi yale bado yana nafasi ya kwenda kumsalimia mpendwa wao kama upendo walionao kwake ulikuwa ni real.

Otherwise tunasubiri kwa shauku kubwa movie nyingine hapo 2020, ambayo wengi wanadai kwamba Eddo anaiandaa kimya kimya kwa sasa na ambayo ni tamu zaidi ile movie ya Mafuriko ya 2015.
 
We hewa kweli, kila siku mnawakamata kuwa wameandamana bila kibali au huwa mnamaanisha nini? achieni mikutano ya hadhara muone kama mtukufu anapendwa au Edo.
 
We hewa kweli, kila siku mnawakamata kuwa wameandamana bila kibali au huwa mnamaanisha nini? achieni mikutano ya hadhara muone kama mtukufu anapendwa au Edo.

Kwani kumtembelea mtu nyumbani unahitaji mkutano wa hadhara ndugu yangu? Watu wakiingia kwenye gari na kwenda straight nyumbani kwake nani atawakamata? We umeniita mie hewa lakini sijui wewe nikuitaje kwa mawazo yako hayo
 
Achieni bunge liwe live na mikutano ya kisiasa iwe huru ndio muone kama Magufuli anakubalika ama la.

Wageni kumtembelea mtu na Bunge Live wapi na wapi? Post hii wala haijazungumzia mikutano ya kisiasa, bali ni kumtembelea tu mpendwa wao
 
Mwaka 2015 hasa katika kuelekea katika uchaguzi mkuu, tuliona Mh. Edward Lowassa akitembelewa na wageni katika makundi mbalimbali. Tuliona makundi ya vijana waliojiita “Wazalendo”, makundi ya Viongozi wa dini, Makundi ya wafugaji na wakulima, na makundi mengineyo.

Ni makundi yaliyodai kuwa yanakwenda kwake kwa lengo la kumsalimia mpendwa wao huyo, lakini pia kumshawishi kuchukua fomu za kugombea katika nafasi ya Urais wa JMT kupitia CCM. Ni makundi yaliyotushangaza wengi kwa namna ambavyo yalikuwa yakipishana mlangoni, na kuitawala kalenda ya mheshimiwa Eddo kwa kiasi kikubwa.

Yaliibuka madai kutoka kwa watu mbalimbali kwamba makundi hayo yaliandaliwa na kugharamiwa na “mtembelewaji”, lakini wengine tulikataa na kusema hayo makundi yaliashiria upendo mkubwa wa Watanzania kwa Mzee wetu huyo. Lakini cha kushngaza tangu aangushwe katika uchaguzi ule wa Mwaka 2015, hao wageni hawaendi tena kwake kwa lengo la kwanza ambalo ni kumsalimia. Ni kama amekuwa adui yao sasa, maana urafiki wao haupo kwa kiasi kile tulichoshuhudia kipindi hicho. Hali hii inatufanya sasa tuamini kwamba huo mchezo aliucheza Mzee mwenywewe ili kuweza ku-win mawazo ya watu wengi kwamba anapendwa sana, ambapo kwa kiasi chake alifanikiwa; maana alipata kura nyingi though hazikutosha. Mh. Rais Magufuli hajakataza watu kutembelewa na wageni nyumbani kwao, hivyo makundi yale bado yana nafasi ya kwenda kumsalimia mpendwa wao kama upendo walionao kwake ulikuwa ni real.

Otherwise tunasubiri kwa shauku kubwa movie nyingine hapo 2020, ambayo wengi wanadai kwamba Eddo anaiandaa kimya kimya kwa sasa na ambayo ni tamu zaidi ile movie ya Mafuriko ya 2015.

Mamvi hakupendwa kwa dhati kabisa kiasi kile, usicheze na nguvu ya noti ndugu yangu; nguvu hiyo iliwafanya hata viongozi wa dini wakaingia mtegoni. Fedha kitu kingine, haijawahi kumuacha mtu salama.
 
Mamvi hakupendwa kwa dhati kabisa kiasi kile, usicheze na nguvu ya noti ndugu yangu; nguvu hiyo iliwafanya hata viongozi wa dini wakaingia mtegoni. Fedha kitu kingine, haijawahi kumuacha mtu salama.

Kwa kweli fedha noma sana
 
Mwaka 2015 hasa katika kuelekea katika uchaguzi mkuu, tuliona Mh. Edward Lowassa akitembelewa na wageni katika makundi mbalimbali. Tuliona makundi ya vijana waliojiita “Wazalendo”, makundi ya Viongozi wa dini, Makundi ya wafugaji na wakulima, na makundi mengineyo.

Ni makundi yaliyodai kuwa yanakwenda kwake kwa lengo la kumsalimia mpendwa wao huyo, lakini pia kumshawishi kuchukua fomu za kugombea katika nafasi ya Urais wa JMT kupitia CCM. Ni makundi yaliyotushangaza wengi kwa namna ambavyo yalikuwa yakipishana mlangoni, na kuitawala kalenda ya mheshimiwa Eddo kwa kiasi kikubwa.

Yaliibuka madai kutoka kwa watu mbalimbali kwamba makundi hayo yaliandaliwa na kugharamiwa na “mtembelewaji”, lakini wengine tulikataa na kusema hayo makundi yaliashiria upendo mkubwa wa Watanzania kwa Mzee wetu huyo. Lakini cha kushngaza tangu aangushwe katika uchaguzi ule wa Mwaka 2015, hao wageni hawaendi tena kwake kwa lengo la kwanza ambalo ni kumsalimia. Ni kama amekuwa adui yao sasa, maana urafiki wao haupo kwa kiasi kile tulichoshuhudia kipindi hicho. Hali hii inatufanya sasa tuamini kwamba huo mchezo aliucheza Mzee mwenywewe ili kuweza ku-win mawazo ya watu wengi kwamba anapendwa sana, ambapo kwa kiasi chake alifanikiwa; maana alipata kura nyingi though hazikutosha. Mh. Rais Magufuli hajakataza watu kutembelewa na wageni nyumbani kwao, hivyo makundi yale bado yana nafasi ya kwenda kumsalimia mpendwa wao kama upendo walionao kwake ulikuwa ni real.

Otherwise tunasubiri kwa shauku kubwa movie nyingine hapo 2020, ambayo wengi wanadai kwamba Eddo anaiandaa kimya kimya kwa sasa na ambayo ni tamu zaidi ile movie ya Mafuriko ya 2015.
Wewe mwenyewe umesema walikuwa wanaenda kumshawishi kugombea urais,kwa hiyo sasa hivi waende kumshawishi agombee nini? Subili uchaguzi mwingine ndio useme.
Huyo mwingine Sasa hivi amekataza kutembelea wagonjwa na mahabusu!
 
Mamvi hakupendwa kwa dhati kabisa kiasi kile, usicheze na nguvu ya noti ndugu yangu; nguvu hiyo iliwafanya hata viongozi wa dini wakaingia mtegoni. Fedha kitu kingine, haijawahi kumuacha mtu salama.
Hats huyu ni nguvu ya dola
 
Kwani kumtembelea mtu nyumbani unahitaji mkutano wa hadhara ndugu yangu? Watu wakiingia kwenye gari na kwenda straight nyumbani kwake nani atawakamata? We umeniita mie hewa lakini sijui wewe nikuitaje kwa mawazo yako hayo
Nani kakuambia Lowasa hatembelewi na wageni?
 
Walienda kumtolea MTU damu ikawa shida,,

Walienda nyumbani kwa Mamvi? Mbona zamani watu walikuwa wanamfuata nyumbani kwake? Kubalini tu kwamba ilikuwa ni nguvu ya mpunga ndiyo iliwavuta wageni, kwa sasa hatoi mpunga huo
 
Wewe mwenyewe umesema walikuwa wanaenda kumshawishi kugombea urais,kwa hiyo sasa hivi waende kumshawishi agombee nini? Subili uchaguzi mwingine ndio useme.
Huyo mwingine Sasa hivi amekataza kutembelea wagonjwa na mahabusu!

Unasoma kwa kurukaruka? Angalia sababu nyingine waliyotoa ambayo nimeiandika hapo
 
Mshenzi huyu, alikakataa watu wasiende kumtembelea Lema gerezani kwamba ni wasaliti, sembuse mzee Eddo?
Hataki kuona hata wanaccm wale ambao hawana chuki wala kutanguliza itikadi ya chama hasa kwenye majanga waende wakamuone Lissu akiwa kitandani, sembuse Eddo?
Tuambie ni kwa nini hakuna mwanaccm yeyote tukiacha Lazaro ambaye sasa keshatimka alikwenda kumtembelea Lissu kwa kujitokeza hadharani?
Halafu mzee Eddo siyo mtu wa mauzo au mtu wa media kwamba basi akitembelewa hata na wakwe sharti iwe habari!
 
Back
Top Bottom