Rais Magufuli azindua barabara ya KIA hadi mji wa Mererani, Awataka JWTZ kujenga Ukuta kuzunguka Machimbo ya Tanzanite

Rais Magufuli azindua barabara ya KIA hadi mji wa Mererani, Awataka JWTZ kujenga Ukuta kuzunguka Machimbo ya Tanzanite

Kwamba utapata chakula kwa bei nzuri kama barabara ni mbovu?hivyo vitu vya kutengenezea malazi mfano nyumba vitafika sehem husika bila barabara?Hiyo elimu ktk kuhakikisha usimamizi mzur je maafisa watafika eneo husika na kwa wakati bila barabara?unaitoaje barabara ktk maendeleo?

Unatukana wananchi wewe ukuleta tetemeko huto wajengea nyumba, wakikulilia njaa unawatukana wakalime wakati wao hutegemea mvua!

Barabara isafirishe mazao yapi kama wakulima wadogo hawazalishi? Maafisa wakasimamie mtaala uchwara ambao watoto wana soma KKK (kusoma, kuhesabu na kuandika) kwa miaka mitatu!

Barabara ni huwezesha maendeleo walakini sio chazo cha maendeleo! Tradeoff ya kupuuzia madawa na wazalishaji wadogo wadogo kama wakulima kutasababisha kesho ukose hata kodi za kujenga barabara!
 
Hebu tuwe serious

Tunataka kujenga ukuta wenye urefu wa kilomita 81 na upana wa kilomita 81? Hii ndio mbinu ya kitaalamu kudhibiti biashara ya madini?
 
Huko un kuna siku walijadili matatizo ya jimboni kwako au ni kujipendekeza tu kwa wazungu? Wazungu hawana shida ya maendeleo kwenye nchi zao ndio mana wanna muda mchafu wa kwenda kujadiliana namna ya kuongezea vikwazo Pyongyang.
Na kutuibia sisi huku,ndo mada kuu ya wazungu
 
Nachukizwa na kauli hizi za kibaguzi na wakati huohuo anasema maendeleo hayana vyama.

Kwanini anapenda kusema kitu flani kimejengwa na ccm badala ya kodi za wananchi wote wenye vyama na wasio na vyama ikiwemo hata wasio raia wa nchi hii?

Anasema maendeleo hayana vyama mbona anatanguliza sana uccm kwa kila kitu? Huu si ubaguzi wa wazi?

Tushike lipi kama kila kitu kimejengwa na ccm basi vyama vingine visitozwe kodi ijulikane moja kuwa ni wanaccm sio wananchi wote?
Bombadier mbili zililetwa na CCM....moja imezuiwa na TUNDU LISSU (Chadema)
 
Kweli hili taifa limeoza..viongozi wenzie wote wako UN kujadili mambo ya maana lenyewe liko Sijui Simanjiro...yaani these 5 yrs is a waste to this nation
Acha kuwa na akili finyu, hivi ulishamuona Queen Elizabeth huko un au ni uzezeta tu? Lini huko un walishapitisha bajeti kutatua kero za maji jimboni kwako?
 
Inasikitisha kuwa na kizazi cha namna hii, kizazi kilichojaa kulalamika, majungu na fitina zisizo na maana kwa serikali.

Watanzania lazima tukubali kwamba katika hii inchi hakutokuja kutokea marais wawiki wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hivyo tukipata rais awe wa chama chochote ni vizuri kumuunga mkono kama anaonesha ana nia nzuri na nchi yetu,
Hivi vyama vya siasa walivyotuletea wazungu visituchanganye akili hadi ikafikia hatua tukasahau maendeleo ya nchi sababu hivi vyama vitapita lakini nchi haiwezi kupita na vizazi vyetu badae vitakuja kuishi katika hii nchi.
Hivyo hakuna sababu ya kuvuruga uongozi wa nchi kwa vigezo vya demokrasia aliyoleta mzungu ili atutawale kirahisi.

Kwa hiyo tusipende kujitoa ufahamu vimaneno visivyokuwa na tija kwa rais bila sababu ya msingi ila ni uchu wa madaraka tu.
Rais anaweza akatokea hata katika chama chako ila kibinadamu hawezi kukamilika hivyo katika hali kama hiyo ni jambo la kheri kuangalia masirahi mapana ya nchi kuliko masirahi madogo ya chama chako
 


Habari waungwana,
Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli ameshatua uwanja wa ndege wa Kilimanjaro na kupokelewa na mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Mama Anna Elisha Mngwira. Muda mchache ujao anatarajiwa kuzindua barabara ya KIA mpaka Mererani.

Fuatana nami kujua yanayojiri..
====

Magufuli: Adui yetu mkubwa ni maendeleo sio vyama, ninawashukuru sana kwa kura, nina uhakika hata Malya alinipa, nawashukuru sana wizara ya ujenzi na uchukuzi, TANROADS, wakandarasi na consultants ambao wamefanikiwa kumaliza hii barabara hii ya KM 26 kwa gharama ya bilioni 32.5 na fedha zote zimetokana na kodi za watanzania, nawapongeza sana watanzania wanaolipa kodi.

Barabara ambazo tumeamua kutengeneza zipo yingi, tumeanza na Km 26 lakini haiwezi kuishia hapa kabla haijafika makao makuu ya wilaya na Mkoa.

Nawapongeza sana kwa kumchagua Milya, amelelewa na CCM. Nchi hii ni tajiri na historia inazungumza wazi, tukapewa madini ambayo hayapo pengine kokote duniani, tujiulize haya madini yanatusaidia? Mungu ametupa madini lakini tunapata shida ndio maana nimefika hapa ila mtu analilia shida, Tanzanite tunayo lakini tunaitumiaje? Tulimkosea nini Mungu? Hilo ndio somo langu la leo.

Tanzania matatizo yetu sio vyama, matatizo yetu ni kwanini tunaibiwa? Wangepewa nchi nyingine, hapa pangekuwa kama Ulaya. Ripoi ya Tanzanite iliyoundwa na Spika, Tanzania haiwanufaishi hata wananchi wa hapa, pia haiwanufaishi watanazania. Tanzania inapata asilimia tano, ndio maana nasema nasema tuna changamoto.

Katika uongozi wangu nimeamua kuongoza hii vita, naomba tusimame pamoja kushinda hii vita. Tanzanite ina eneo la kilometa za mraba 81.99, kuna block zimegawanywa. Tanzanite zinaibiwa sana, ni shamba la bibi, nafikiri mabibi waliokufa miaka mingi sana.

Kuna wawekezaji ambao wana asilimia 50 lakini mali zinasombwa. Nimeamua lile eneo ili tuzuie wizi, block A mpaka D, naagiza JWTZ waanze kulijenga ukuta eneo lote, kazi ifanyike haraka. Wakimaliza wake fence na kamera, kutakuwa na mlango mmoja. Hata kama utameza Tanzanite itaonekana.

Serikali ipate pesa yake na mchimbaji apate pesa yake, tunataka soko la Tanzanite liwe hapa Simanjiro na wala sio Arusha. Wanunuzi wote waje kununua hapa Simanjiro, barabara ni lami.

Nimeona tuanze na hii hatua, nina hakika watu wa Tanzanite one na wengine watakaa na kutengeza mkataba wenye faida kwa serikali. Ni lazima tujipange vizuri, hili suala naona sasa linafika mwisho wake.

Biashara haijazuiliwa lakini tunaitoa kwenye biashara ya magendo kuwa biashara halali. Ukishapata mali yako ndani ya uzio, peleka kwenye duka lolote na wateja watakufata hapo hapo. Biashara hii unaondoka umeficha na unapeleka anakulalia kwa sababu anajua huwezi kuipeleka popote.

Benki kuu pia watengeze mkakati wa kushiriki katika kununua zawadi. Tuna madini kila maali lakini majamaa wamekuwa wakisomba tu, tunaendelea kubaki maskini.

Nafahamu katika hatua mlizoanza kuchukua, kuna wengine wamekimbia na hamtawaona kwa sababu ya waliochokuwa wanafanya.

Malya sio adui yetu, adui yetu ni yule anae tuibia. Barabara imejengwa na CCM lakini watapita watanzania wote, tunagombania nini? Wanasema kitunze kidumu, naomba mtunze hii barabara. Kuhusu suala la maji naomba mniachie, kuna mradi mkubwa wa bilioni 45 kwenda makao makuu ya wilaya, eneo hili ambalo halina vyanzo vya maji naomba mniachie.




ni kweli mzee wewe piga kazi achana na hao wanaopiga kelele kila kukicha , hakuna vita isiyokuwa na wasaliti hao wapo tu kwa maslahi yao binafsi ila sisi ni vizuri kutazama dira yetu ya hapa kazi tu
 
Kuna baadhi ya watanzania ni kama akili zimeoza, Rais JPM kaongea mambo ya msingi ikiwemo ujenzi wa ukuta pale mererani ila, wenyewe wamekazana na vijembe na maneno ya shombo kwa Rais.
Watu wanashindwa kujadili ni namna gani kutakuwa na fursa baada ya ujenzi wa ule ukuta pale mererani na ni kwa namna serikali itaongeza mapato pale ila mijitu imejaa majungu na fitina kwa Rais kama michawi.

Nafikiri adui mkubwa wa maendeleo hii inchi ni wananchi wenyewe kutojitambua. Mana haiwezekani Rais JPM kaongea mambo ya msingi watu wanaanza kupotosha na kukashifu kama wametumwa na shetani kuvuruga nchi.

Hivi mimi niwaulize wote wanaomkashifu Rais JPM tatizo lao hasa minini?
Adui yetu anajulikana kuanzia kupata uhuru hadi leo.
Yuko peupeeee
 
Ni kweli kwakuwa wakwepa kodi si wako chagadema tunawaona? Hadi Mahakama imethibitisha hilo na Mwenyekiti wetu amepigwa faini.

Pia si tunaona wasio CCM wakiwatetea mafisadi?. Kwasasa CCM ndio chama kinachohimiza kulipa kodi.
 
Barabara imejengwa kwa kodi za wanatanzania wanaolipa kodi true barabara zimejengwa na wana CCM False hapo Mzee alikuwa anapiga siasa tu ya Kazi yake lakini anajua ni uongo!!
Hyo kodi ya kujengea nani aliikusanya na kuiweka ktk miradi ya barabara, tatzo sie ndivyo tulivyo hatutabadilika
 
Acha kuwa na akili finyu kama za funza, hivi ulishamuona Queen Elizabeth huko un au ni uzezeta tu? Lini huko un walishapitisha bajeti kutatua kero za maji jimboni kwako?
Anagalia ulivyo uharo..malkia sio kiongozi wa serikali huko UK..ndio maana Teresa May yuko UN..mambo kama hujui kaa jikoni wasaidia dada zako kumenya mbaazi pimbi wewe
 
Daahh!!

Inasikitisha sana, hasara hii haijawahi kutokea.

Tunakoelekea Mungu ndie anajua peke yake
Kivipi haijatokea kwani Mahiga hatoshi kumwakilisha? Hivi mnadhani hawa watu wanasumbuka na marais wa Afrika?
 
Acha kuwa na akili finyu kama za funza, hivi ulishamuona Queen Elizabeth huko un au ni uzezeta tu? Lini huko un walishapitisha bajeti kutatua kero za maji jimboni kwako?
Yaani sijui hata umeishia darasala ngapi..hujui hata majukumu ya UN..miaka 50 ya uhuru unajiona fahari kuongelea matatizo ya maji..
 
Back
Top Bottom