Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,622
- 8,397
Rais Magufuli ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuwakamata wanaohusika na Dawa za Kulevya. Asema si kazi ya Makonda pekee.
Rais Magufulia amesema hakuna wa kuachwa hata akiwa mkewe Mama Janet Magufuli, na kuongeza kuwa wakamatwe bila ya kujali majina yao.
Rais Magufuli amesema anamuomba Jaji Mkuu asizicheleweshe kesi za madawa ya kulevya kwani kuna mtuhumiwa mkubwa wa Dawa za Kulevya anashikiliwa Lindi bila ya kufikishwa Mahakamani.
Najua IGP Mangu watu walikupigia simu wanakupa ushauri kuhusu Dawa za Kulevya, ungewasikiliza leo usingekuwa IGP.
Vita ya dawa za kulevya haina cha umaarufu, haijalishi ni mtoto wa nani anahusika, hata kama ni mke wangu mkamateni.
=======
Rais Magufulia amesema hakuna wa kuachwa hata akiwa mkewe Mama Janet Magufuli, na kuongeza kuwa wakamatwe bila ya kujali majina yao.
Rais Magufuli amesema anamuomba Jaji Mkuu asizicheleweshe kesi za madawa ya kulevya kwani kuna mtuhumiwa mkubwa wa Dawa za Kulevya anashikiliwa Lindi bila ya kufikishwa Mahakamani.
Najua IGP Mangu watu walikupigia simu wanakupa ushauri kuhusu Dawa za Kulevya, ungewasikiliza leo usingekuwa IGP.
Vita ya dawa za kulevya haina cha umaarufu, haijalishi ni mtoto wa nani anahusika, hata kama ni mke wangu mkamateni.
=======
Wanabodi,
Mimi ni chipukizi kwenye uchambuzi wa medani za siasa. Style ya Magufuli ya uongozi wengi hamtaki kuamini. Mheshimiwa rais ni mzalendo wa juu. Hii season Sasa tutakwenda kushuhudia jambo kubwa.
Hoja ninazo hizi hapa;
1. Kumbuka matukio yamefuatana kama hivi lilianza la siku ya sheria. Rais alionya mambo makubwa alisema hataki mambo ya kuchelewesha kesi.. Aliashiria kitu.
2. Makonda kijana mchapakazi ametoka marekani juzi, amefika akaanza moja kwa moja na hii ishu ya hii vita.
3. Kesho yake wanakuja watu wanawatetea Hawa wasanii kwamba tunakwenda eti kuua brand. Kuna waziri ame mbeep mheshimiwa rais.
4. Tukio lililofuatia ni sauti za Wakuu wa vikosi. Alianza IGP, kisha kamanda Sirro.
5. Kwa akili ya kawaida unaona kabisa hawa wasanii wanamilikiwa na wanasiasa fulani vinara wa unga.
6. Tukio lililofuatia ni rais akamteua mkuu wa majeshi mpya
7. Kisha Akasema kabisa meli ya MV Bagamoyo ya enzi ya awamu ya nne itakuwa ya jeshi kufanya doria. Ikumbukwe baharini ndio unga unapitia sana.
8. Kisha makonda akajitokeza kuwapa siku kumi. Wenye uelewa mkubwa wa saikolojia wanajua ki nacho endelea.
9. Msumari wa mwisho tutashuhudia mpaka mkuu wa nchi amesema tena kama wewe ni great thinker utagundua facial expressions aliyokuwa nayo rais.
Tazama serikali yote ilikuwepo ikulu. Hamuoni hii ishu ni kubwa imefikia?
My Take: Watanzania tumempata Rais. Tumpe ushirikiano kwa vyombo vyake. Tazama litakalotokea hivi karibuni.. Mark my word. Hakuna rais Tanzania kama Magufuli.
Msioamini kuwa hii vita sasa imeanza subirini muone. Hisia zote zinanipeleka jambo kubwa litagusa mpaka vigogo wakubwa. Msishtuke kutajiwa viongozi fulani. Hilo Kwa Sasa Tanzania linatokea.
Ma drug dealer Imekula kwenu. Muda mrefu Sasa mmetamba. Ishara zote Sasa wazi.