Binti Msichana
Senior Member
- Oct 9, 2016
- 109
- 247
Rais JPM amepiga simu moja kwa moja katika kipindi cha televisheni cha Clouds 360 kinachofanyika katika hotel ya White Sands iliyopo Dar es Salaam.
Rais akiongea kutoka Chato mapumzikoni amefurahishwa jinsi kipindi hiko kinavyoendeshwa kwa ubunifu wa hali ya juu.Amevutiwa uwepo wa wageni kutoka taasisi mbalimbali kama BIMA, NHC, ATCL, Vodacom na taasisi nyingine.
Hakusita kuonesha hisia zake jinsi viongozi was taasisi hizo walivyoelezea mikakati na mipango yao katika kuboresha Huduma kwa wananchi.Amevutiwa na shirika la BIMA lilivyojiandaa kutoa Huduma bora katika BIMA za nyumba.
Ametumia fursa hiyo kuwatakia Watanzania heri ya Mwaka Mpya 2017.
Mtangazaji wa Clouds ameahidi kipindi kijacho kitafanyika Chato, kwa utani JPM amesema yeye yupo Chato analima.
Rais akiongea kutoka Chato mapumzikoni amefurahishwa jinsi kipindi hiko kinavyoendeshwa kwa ubunifu wa hali ya juu.Amevutiwa uwepo wa wageni kutoka taasisi mbalimbali kama BIMA, NHC, ATCL, Vodacom na taasisi nyingine.
Hakusita kuonesha hisia zake jinsi viongozi was taasisi hizo walivyoelezea mikakati na mipango yao katika kuboresha Huduma kwa wananchi.Amevutiwa na shirika la BIMA lilivyojiandaa kutoa Huduma bora katika BIMA za nyumba.
Ametumia fursa hiyo kuwatakia Watanzania heri ya Mwaka Mpya 2017.
Mtangazaji wa Clouds ameahidi kipindi kijacho kitafanyika Chato, kwa utani JPM amesema yeye yupo Chato analima.