Rais Magufuli anasalitiwa, Nyumba ya Mkuu wa Wilaya ya Urambo na Maisha halisi ya Wanatabora

Ni nzuri sana kwa wilayani! Ni mali ya serikali itatumiwa na kuiacha hapo hapo! Tuwasaidie wananchi wetu wajenge nyumba bora za hadhi ya kati kumaliza matembe wilayani na vijijini! Uwe ni mkakati wa nchi nzima! Tukiamua tunaweza
 
(Majibu ya Mtoto wa Mkulima.....) tumelichukua kwa ujumla wake, sisi tutakaa kwenye kamati zetu tuliangalie tuone namna ambavyo tunaweza kushirikisha wadau mbali mbali katika hili ikumbukwe kuwa katika mwaka wa fedha 1994/95 zilitwengwa bilioni 85 kujenga madaraja na nyumba za walimu lakini kama mjuavyo mkandarasi hakumaliza kazi aliyopangiwa...nimuhakikishie tu mheshimiwa kuwa tunalishughulikia kwa haraka zaidi
 
Huyo unayesema anasalitiwa angalia maisha wanayoishi wanawake na watoto Kule Kagera baada ya tetemeko wakati huu mvua zikiwa zimeanza na kauli zake kisha jitafakari.
Ni walewale tuu
Kwani tetemeko limeletwa na Serikali?
 
Mbona ni nyumba ya kawaida sana kwa wilaya? Mi naona VX lake lina thamani kuliko hiyo nyumba isitoshe nyumba itatumika hata kwa mkuu mwingine atakae kuja badala ya kumlaza hotel.
Hivi hawajaiona train station ya Urambo ambayo ilijengwa miaka karibia mia iliyopita?
Hadhi ya nyumba ni kawaida tena wamechelewa ilikuwa wawe na mijengo kama ya Zuma
 
Huko ndo kwa akina professor myamani . wakiwa na makazi mazuri hawatupi kura hawa
 
Kolandoto tena, wakati habari inaihusu Urambo! Au kuna Kolandoto nyingine Urambo?
Au kama vipi tuchanganyie tu na picha za tetemeko la kule Kagera.
 
Hivi akitoka hapo atakubali kuishi bangaloo kama sisi au atahakikisha kuiba hadi ajenge kubwa kuliko hiyo?
 

Kujengewa nyumba nzuri, hakika sio tatizo sana, kwa maana ni nyumba ya umma, sio ya mtu binafsi na umma unatakiwa kujenga vitu vizuri. Na wala hakuna sababu ya kujenga nyumba mbovu eti kwa kuwatetea masikini. Ila tunachotakiwa kusema, na kupiga kelele kweli kweli ni pale mkuu wa wilaya atakapokuwa kwenye nyumba nzuri na akafanya mambo ya hovyo, akaiba, akakandamiza watu watu kwa sababu sio wa chama chake, akapokea rushwa kutokea humo. Hapo ndipo lilipo tatizo, kwani nyumba ya mkuu wa wilaya ya Urambo ina tofauti gani na nyumba za wakuu wengine wa wilaya?
 
Mkuu Pasco, kumbe unaweza. Umeandika kishwahili bila kuchanganya hata neno moja la kiingereza! Nimeipenda sana.
 

Mkuu:
Tuende kwenye uhalisia na sio nadharia ya kusadikika, (Kama hali ya uchumi wa Urambo inaruhusu) Lakini ofisi ya Mh. Mbunge ni ya kawaida kabisa kwa watu wanao fahamu maana ya ujenzi wa nyumba, aidha sina hakika na kuifahamu nyumba ya mzee Sitta.
 
Mkuu Zinj, nimesema na narudia tena kusema kuwa hiyo nyumba ni ya kawaida sana. Mkuu wa Wilaya ndio rais wa wilaya husika, nyumbani kwake kunatakiwa kuwe ndio ikulu ya mahali hapo.

Hii ndio ofisi ya Mbunge wa Urambo, sasa mlitaka nyumba ya DC iweje? .
 
nyumba mliziuza sasa hiv munatetea huu utoto wa kujenga nyumba zingine.....nafkir kwa sababu zile mlizotupa hata chumba kimoja hastahili kujengewa cz bdae mtakuja kuuziana kwa bei chee
 
watupe sababu kwann waliuza nyumba za serikali na leo wajenge tena
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…