Rais Magufuli anaendesha nchi kwa misingi ya upendeleo wa kifamilia, kikabila na kikanda!

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,252
113,647
Hayo ni maneno aliyoyatamka Tundu Lissu juzi kwenye mkutano wake na waandishi wa habari.

Mimi bado kabisa sijashawishika kuwa rais Magufuli anaendesha nchi kwa hiyo misingi.

Nakubaliana kwa kiasi kikubwa na wengine wanaosema au kuona kuwa tokea rais huyu aingie madarakani kumekuwepo unyanyaswaji wa wanasiasa wa vyama vya upinzani.

Nakubaliana na wanaoona kuwa kumekuwepo na jitihada za kuminya uhuru wa vyombo vya habari.

Nakubaliana na wanaoona kuwa kwenye baadhi ya mambo, iwe kwa matendo au kauli zake, huyu rais kaonyesha tabia za kidikteta. Hili nimeshawahi kuliandika humu kwenye moja ya mada zangu za kumpinga huyu rais.

Nakubaliana kabisa na wanaohoji ujengwaji wa kiwanja cha ndege huko Chato ambako ndiko nyumbani kwa rais. Sioni sababu yoyote ile iliyo ya msingi kutumia mahela mengi kujenga kiwanja cha ndege huko. Ni heri hizo hela wangezitumia hata kununua madawati ya shule na kuziboresha shule na hospitali za huko na kwingineko. Lakini li kiwanja la ndege? Hapana kwa kweli.

Kwa kifupi ni kwamba, kuna mambo mengi tu ninayoyapinga kumhusu huyu rais. Vilevile, yapo mengi au kadhaa ninayokubaliana naye. Hii ni hali ya kawaida sana hususan kama mtu uko huru kifikra na si mtu wa kuburuzwa buruzwa tu kama zuzu.

Inapokuja kwenye hili suala la yeye kuendesha nchi kwa misingi ya kifamilia, kikabila, na kikanda, hapo bado kabisa sijashawishika na sikubaliani na wote wanaodai hivyo.



Tuangalie suala la kifamilia:

Kuna huyo Dotto James ambaye ni katibu mkuu kwenye wizara ya fedha na mipango. Pia, Lissu kamtaka mdogo wa huyo Dotto ambaye ndo naibu wa Dotto.

Hawa, inasemwa kuwa ni watoto wa dada wa Magufuli. Sina hakika kama ni dada kweli [yaani wa mama mmoja baba mmoja au mama/baba mbalimbali]. Magufuli ana dada?

Suala la kikabila na kikanda:

Hapa aliwataja Medard[spelling?] Kalemani ambaye ni naibu waziri wa wizara ya nishati na madini na ambaye pia aliwahi kuwa mwanasheria wa wizara hiyo hiyo. Huyu naye sijui ana undugu na Magufuli....[sasa hivi Magufuli baada ya kuwa rais atapata ndugu wengi sana].

Mkuu wa majeshi Jenerali Venance Mabeyo - anatokea kanda ya ziwa [ni Msukuma huyu]

Mkuu wa polisi, Kamanda Sirro - anatokea kanda ya ziwa [silijui kabila lake].

Mwanasheria mkuu, George Masaju - anatokea kanda ya ziwa [huyu naye hata silijui kabila lake na aliteuliwa kwanza kuwa mwanasheria mkuu na rais mstaafu Kikwete na kabakishwa na rais Magufuli].

Hivi Frederick Werema naye alikuwa anatokea kanda gani huyu? Hiyo hiyo ya ziwa?

Mwendesha mashtaka - Biswalo Mganga - naye anatokoea kanda ya ziwa [sijui hata yeye ni kabila gani ila naye najua aliteuliwa kuwa mkurugenzi na rais mstaafu Kikwete na mpaka sasa rais Magufuli kambakisha].

Kaimu Jaji Mkuu - Ibrahimu Hamisi Juma - naye anatokea kanda ya ziwa [sijui yeye ni kabila gani].

Hivyo ndo 'vizibiti' alivyovitaja huyo 'wakili msomi' katika kuonyesha kuwa rais anaendesha nchi kwa hiyo misingi.

Now let's get down to the nitty-gritty so we can separate the wheat from the chaff.


1] Serikali ya Tanzania ina watumishi wangapi?

2] Wangapi kati ya hao watumishi ni Wasukuma na/au wanatokea kanda ya ziwa?

3] Tokea Magufuli awe rais keshateua Wasukuma na/au watu wa kanda ya ziwa wangapi ukilinganisha na idadi ya makabila na/au watu wa kanda zingine?

4] Kulinganisha na marais wa awamu zilizopita, rais Magufuli kateua Wasukuma na/au watu wa kanda ya ziwa wangapi?

5] Rais Magufuli ananufaikaje na kuteua watu wa familia, kabila lake [Magu kwanza wala si Msukuma..], na ukanda atokao?

6] Hao Wasukuma walioteuliwa na Magufuli na hao wengine watokeao kanda ya ziwa ni wangapi kati ya hawana sifa za kushika hizo nyadhifa walizonazo? Jenerali Mabeyo hana sifa za kuwa mkuu wa majeshi? Kamanda Sirro hana sifa za kuwa mkuu wa polisi? Biswalo Mganga hana sifa za kuwa mkurugenzi wa mashitaka? George Masaju hana sifa za kuwa mwanasheria mkuu? Hawa wawili wa mwisho waliteuliwa na rais Kikwete, btw.

7] Mnaoshadadia hiyo hoja ya ukabila na ukanda, ili msilalamike, mlitaka wawepo Wasukuma na watu wa kanda ya ziwa wangapi kwenye serikali ya Magufuli?

Katika hoja zote dhidi ya urais wa Magufuli hii ya ukabila, ukanda, na kwa kiasi fulani Ukatoliki ndo hoja dhaifu kuliko zote.

Mpaka hapo mtapokuja na takwimu madhubuti zinazothibitisha hayo mnayoyadai ndo labda mtapoeleweka.

Zaidi ya hapo hizo kelele ni sawa na tapatapa za mfa maji tu. Mfa maji atang'ang'ania chochote kile kilicho mbele yake kwa matumaini ya kwamba labda kinaweza kumwokoa asife maji.

Jumatano njema.
 
Wakuu,
Nimemsikiliza Mh Tundu Lissu jana, mbunge na mwanasheria wa chadema, akilalamika kuwa teuzi za mtukufu Rais ni za kikanda.

Mheshimiwa Lissu alidai kwa kueleza teuzi nyeti za serikali kuwa ni za kibaguzi na hazileti picha ya kitaifa.

Lissu aliwataja watu wafuatao kuwa wanatoka kanda ya ziwa.
1. Mwanasheria mkuu
2. Mkuu wa JWTZ
3.IGP
4.Mkuu wa usalama wa taifa
5.Katibu wa fedha na naibu wake
6. Katibu mkuu

Lakiki Lissu hakuangalia nafasi nyingine nyingi ambazo Rais ameteua watu ambao sio kanda ya ziwa, mfano
1. Baraza la mawaziri,
2. Wakuu wa mikoa wanatoka kila kanda
3. Waziri mkuu
4. wakuu wa wilaya

Bado hoja ya Lissu inahitaji kujadiliwa ili kuweza kubaini ukweli wa jambo hili vinginenvyo etaleta sinto faham nyingi sana kiasi cha watu kushangaa mbona Rais hazindui miradi katika mikoa ya kaskazini.

Hatuwezi kuacha hili jambo kuelea, nilazima Lissu ajibiwe kwa ushahidi aondoe hii dhana potofu.

General Mangi
 
Kimsingi Lissu anahoja na ameziweka.bayana.Hata hilo baraza la mawaziri liangalie kwa ukaribu zaidi.

Naibu Gavana wawili mmoja Mtutsi mwingine msukuma,Katibu Mkuu wa wizara ya fedha musukuma mtoto wa Dada.

Lissu ametoa ushahidi wake ni kiasi cha kufanya utafiti kama.hao wateuliwa ni ndugu wa damu na Mukullu??

Ukweli una kitu kimoja huonekana ukiwa umechelewa.

Mnyeti DC Arumeru mtoto wa Dada,Shemeji Mkurugenzi hapo Pwani .
 
Toka ameingia madarakani.. Mambo ya msingi ambayo yalikua yakifanyia katika maeneo yanayokubalika na wapinzani amekataa kabisaa kuyaendeleza


Mfano.. Vikao vya east Africa iliyokua ikifanyika Mara zote Arusha saiv hakuna... Kuapishwa kwa wanajeshi Monduli ambapo haikuwai kufanyika nje ya hapo tangu kuanzishwa kwa Jeshi... Saiv hakuna tena..

Ni lini ameshawahi kuzindua miradi ya maendeleo Arusha zaid ya kuzindua ujenzi wa barabara ya moshi iliyokua chini ya mipango ya jk....


Rais kajaa chuki na visasi... Toka amechaguliwa lini kazindua miradi mbeya mjini.. Kwann anakua hvyoo...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu,
Nimemsikiliza Mh Tundu Lissu jana, mbunge na mwanasheria wa chadema, akilalamika kuwa teuzi za mtukufu Rais ni za kikanda.

Mheshimiwa Lissu alidai kwa kueleza teuzi nyeti za serikali kuwa ni za kibaguzi na hazileti picha ya kitaifa.

Lissu aliwataja watu wafuatao kuwa wanatoka kanda ya ziwa.
1. Mwanasheria mkuu
2. Mkuu wa JWTZ
3.IGP
4.Mkuu wa usalama wa taifa
5.Katibu wa fedha na naibu wake
6. Katibu mkuu

Lakiki Lissu hakuangalia nafasi nyingine nyingi ambazo Rais ameteua watu ambao sio kanda ya ziwa, mfano
1. Baraza la mawaziri,
2. Wakuu wa mikoa wanatoka kila kanda
3. Waziri mkuu
4. wakuu wa wilaya

Bado hoja ya Lissu inahitaji kujadiliwa ili kuweza kubaini ukweli wa jambo hili vinginenvyo etaleta sinto faham nyingi sana kiasi cha watu kushangaa mbona Rais hazindui miradi katika mikoa ya kaskazini.

Hatuwezi kuacha hili jambo kuelea, nilazima Lissu ajibiwe kwa ushahidi aondoe hii dhana potofu.

General Mangi
Huyo Lissu hana lolote zaidi ya kutafuta support ya Wachaga ambao wanalalamika kuachwa kwenye teuzi ambazo kwao ni fursa ya ulaji.
 
Habari maelezo wameleta poda ya serikali ili kupaka nondo za Lissu wameshindwa kufua dafu. Kimsingi baada ya Lissu kupigilia misumari na nondo za maana jana watu wameanza kufunguka akili na kuanza kuuhisi, kuuona na kuuthibitisha ukanda, ukabila na udikteta wa Magufuli.
 
Toka ameingia madarakani.. Mambo ya msingi ambayo yalikua yakifanyia katika maeneo yanayokubalika na wapinzani amekataa kabisaa kuyaendeleza


Mfano.. Vikao vya east Africa iliyokua ikifanyika Mara zote Arusha saiv hakuna... Kuapishwa kwa wanajeshi Monduli ambapo haikuwai kufanyika nje ya hapo tangu kuanzishwa kwa Jeshi... Saiv hakuna tena..

Ni lini ameshawahi kuzindua miradi ya maendeleo Arusha zaid ya kuzindua ujenzi wa barabara ya moshi iliyokua chini ya mipango ya jk....


Rais kajaa chuki na visasi... Toka amechaguliwa lini kazindua miradi mbeya mjini.. Kwann anakua hvyoo...

Sent using Jamii Forums mobile app

Jamani Mh.Raisi anazidiwa na mambo kwahiyo kama hakuja kuzindua miradi atakuja kuomba kura na mazoezi lukuki zaidi ya pushups
 
Hahahahaaa...nadhani Lissu atazimia kabisa siku Jaji Mkuu atapotangazwa, aanze kujiandaa kisaikolojia asompenda anakuja.
 
Wakuu,
Nimemsikiliza Mh Tundu Lissu jana, mbunge na mwanasheria wa chadema, akilalamika kuwa teuzi za mtukufu Rais ni za kikanda.

Mheshimiwa Lissu alidai kwa kueleza teuzi nyeti za serikali kuwa ni za kibaguzi na hazileti picha ya kitaifa.

Lissu aliwataja watu wafuatao kuwa wanatoka kanda ya ziwa.
1. Mwanasheria mkuu
2. Mkuu wa JWTZ
3.IGP
4.Mkuu wa usalama wa taifa
5.Katibu wa fedha na naibu wake
6. Katibu mkuu

Lakiki Lissu hakuangalia nafasi nyingine nyingi ambazo Rais ameteua watu ambao sio kanda ya ziwa, mfano
1. Baraza la mawaziri,
2. Wakuu wa mikoa wanatoka kila kanda
3. Waziri mkuu
4. wakuu wa wilaya

Bado hoja ya Lissu inahitaji kujadiliwa ili kuweza kubaini ukweli wa jambo hili vinginenvyo etaleta sinto faham nyingi sana kiasi cha watu kushangaa mbona Rais hazindui miradi katika mikoa ya kaskazini.

Hatuwezi kuacha hili jambo kuelea, nilazima Lissu ajibiwe kwa ushahidi aondoe hii dhana potofu.

General Mangi
Mtanyooka tu mlizoa kila kitu kanda ya kaskazini kwa sasa lazima mpumzike kidogo na wengine wafaidi matunda ya nchi hii. Ukiangalia hoja za Lissu ni za kipuuzi tu. Mwanasheria Mkuu hakuteuliwa na JPM ukija kwa CDF aliyepo sasa hivi alikuwa ndio next to CDF Mwamunyange ambaye aliteuliwa na utawala uliopita. Kitu cha kuziuliza sasa TZ tumeanza kuchaguana kwa kufuata ukanda?? Au ni merit ya mtu? Kwani hao waliochaguliwa hawafai kushika nafasi hizo kwa sababu wanatoka kanda ya ziwa?? Nafikiri Lissu sasa ameshindwa siasa anataka kutupeleka pa baya!!
 
Toka ameingia madarakani.. Mambo ya msingi ambayo yalikua yakifanyia katika maeneo yanayokubalika na wapinzani amekataa kabisaa kuyaendeleza


Mfano.. Vikao vya east Africa iliyokua ikifanyika Mara zote Arusha saiv hakuna... Kuapishwa kwa wanajeshi Monduli ambapo haikuwai kufanyika nje ya hapo tangu kuanzishwa kwa Jeshi... Saiv hakuna tena..

Ni lini ameshawahi kuzindua miradi ya maendeleo Arusha zaid ya kuzindua ujenzi wa barabara ya moshi iliyokua chini ya mipango ya jk....


Rais kajaa chuki na visasi... Toka amechaguliwa lini kazindua miradi mbeya mjini.. Kwann anakua hvyoo...

Sent using Jamii Forums mobile app
......ZAIDI YA KUZINDUA.....
Wakuu,
Nimemsikiliza Mh Tundu Lissu jana, mbunge na mwanasheria wa chadema, akilalamika kuwa teuzi za mtukufu Rais ni za kikanda.

Mheshimiwa Lissu alidai kwa kueleza teuzi nyeti za serikali kuwa ni za kibaguzi na hazileti picha ya kitaifa.

Lissu aliwataja watu wafuatao kuwa wanatoka kanda ya ziwa.
1. Mwanasheria mkuu
2. Mkuu wa JWTZ
3.IGP
4.Mkuu wa usalama wa taifa
5.Katibu wa fedha na naibu wake
6. Katibu mkuu

Lakiki Lissu hakuangalia nafasi nyingine nyingi ambazo Rais ameteua watu ambao sio kanda ya ziwa, mfano
1. Baraza la mawaziri,
2. Wakuu wa mikoa wanatoka kila kanda
3. Waziri mkuu
4. wakuu wa wilaya

Bado hoja ya Lissu inahitaji kujadiliwa ili kuweza kubaini ukweli wa jambo hili vinginenvyo etaleta sinto faham nyingi sana kiasi cha watu kushangaa mbona Rais hazindui miradi katika mikoa ya kaskazini.

Hatuwezi kuacha hili jambo kuelea, nilazima Lissu ajibiwe kwa ushahidi aondoe hii dhana potofu.

General Mangi


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hiyo ina maana bombadia zimenunuliwa kwa siri ya mtu na mpwa?
Bila sheria za manunuzi kuzingatiwa? Hata leo wakitudanganya kuwa kila moja wamenunua kwa Tsh milioni moja na nusu hakuna wa kubisha maana hazina ya nchi kwa sasa ni siri ya wanandugu hawa.
 
Back
Top Bottom