Katavi
Platinum Member
- Aug 31, 2009
- 41,983
- 12,702
Hahaah kwa wasanii wapi?? Wasanii wenzake...!!asante kwa kunielewesha, ila pia bado ni majanga, yule jamaa angepewa nafasi kule kwa wasanii ingemfaa zaidi, huku kwenye elimu hapamfai
Hahaah kwa wasanii wapi?? Wasanii wenzake...!!asante kwa kunielewesha, ila pia bado ni majanga, yule jamaa angepewa nafasi kule kwa wasanii ingemfaa zaidi, huku kwenye elimu hapamfai
Naona spidi yake imepungua sijui kwa nini.magufuri ni walewale tu, na nasisitiza hii nguvu ya soda aliyoanza nayo mwisho wake December this year
GPA ya division 5 inahamia Udsm
naona haya ni majanga tuu, mtu ambaye nchi ilimshinda anapewa taasisi nyeti
Kwa nafasi aliyopewa ni ya kisiasa zaidi, hana impact sana.........yeye zaidi siku ya graduation kutoa hizo degree labda na ushauri tu.tatizo jk hafai popote mkuu, yani hili janga tuuu
Kweli mkuu magufuli kana mbali jamaa asiwe mpwekeHiyo nafasi ina visafari vingi vya kwenda nje, naamini JK atakuwa amefurahi sana
Hahahahaah may be.So JK atakua chini ya dharichako
Itakuwa poa sana manake mamizinga ya nyuki tu!Sio ishu auze auze nyago kidogo.Huyu mjomba wangu apewe labda SUA yule mkuu wap pale kazeeka sana.
hivi hajarudi bungeni?Asimsahau mtoto wa mkulima.Ampe hata ujumbe wa bodi.
Mzee Mkandala ni Vice Chancellor (VC)unamaanisha kachukua nafasi ya mzee mukandara?????? this can be a disaster
Yaah...ila anahitajika mtu makini zaidi. Kwa mtazamo wangu, JK sio mtu serious hivyo sio chaguo sahihi kwa nafasi kama hii.Mkuu wa chuo hana kazi ya maana, Mkandala ni Makamu mkuu wa chuo, ndiye mtendaji wa kazi za kila siku za chuo. Ukuu wa chuo ni nafasi za kisiasa zaidi hazina cha maana labda wakati wa graduation, kama sio mgeni rasmi aliyealikwa, basi mkuu wa chuo ndiye mgawa zawadi na vyeti
Ilibadilishwa nadhani kitambo, maana alikuwa Paul Bomani (sina uhakika), Rwezaura na sasa huyu J. K.Nijuavyo mkuu wa chuo kikuu cha taifa(udsm) miaka yote anakuwaga Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania!Imekuwaje sasa?au utaratibu ulishabadilika kitambo?