Rais Magufuli aamua kutuliza joto la vita vya kibiashara kati ya Tanzania na Kenya

shige2

JF-Expert Member
Oct 11, 2016
8,106
3,967
Katika vita baridi ya KIBIASHARA kati ya nchi hizi mbili ambazo zimekuwako kwa muda sasa zimeathiri pakubwa wafanya biashara, BIASHARA KITAIFA na MAPATO ya serikali kati ya nchi hizi mbili. Tanzania na Kenya.


Hali hii imeleta malumbano ya KIDIPLOMASIA na kusababisha KULIPIZIANA VISASI Kibiashara. at the expense ya wananchi na uchumi wa nchi hizi mbili.


KENYA ilianza kwa kukataza bidhaa kadhaa toka Tanzania SISIINGIE Kenya. Kama vile UNGA wa NGANO ,
GESI ya Tanzania KUINGIZWA nchini mwao huku ikitoa VISINGIZIO vingi.

TANZANIA nayo ikaamua kulipiza KISASI na KUZUIA kuingizwa kwa
TAIRI za gari toka Kenya, ikiwa ni pamoja na
MAZIWA,
MARGARINE na bidhaa zozote zinazotokana na MAZIWA.


Wakati huo huo Kenyanao wakasema GESI isipitie NAMANGA bali ipitie Mombasa ikiwa itaruhusiwa. Na hivyo kufanya Biashara kati ya nchi hizi mbili kuwa ni GHARAMA kubwa sana na kuleta usumbufu.sana kawa pande zote mbili.


Tanzania nayo tena IKAZUIA kupitishia mahindi nchini mwetu yaliyoagizwa toka ZAMBIA kwenda Kenya maana wana upungufu mkuu wa Mahindi/Njaa wakasema HAYATAPITIA nchini Tanzania.


Na hivyo kuleta UTATA USIO na TIJA kati ya nchi hizi mbili za Afrika Mashariki.
Kwa HEKIMA ya Rais Magufuli ameamua KUUMALIZA MGOGORO huu kwa kumwandikia barua Rais Kenyatta ili watafute SULUHISHO la kumaliza mgogoro huu.yaishe na WAELEWANE.

Inavyosemekana ni kuwa Kenya wamekaa NGUMU. Rais Kenyatta kwa sasa ana STUDY the brief/ Mapendekezo ya Tanzania kabla ya KUMJIBU rais mwenzake Mh. Rais Magufuli.


Nafikiri kwa ajili ya UCHUMI wetu wa Tanzania na KENYA, wote TUNAHITAJIANA. Hivyo ni vizuri WAMALIZE mgogoro huu wa KIBIASHARA HARAKA kabla haujaenda OUT OF HAND ili
wananchi na
WAKULIMA wa ngano,
GESI yetu tuweze KUIUZA ili uchumi wetu ukuwe.
Tusibaki katika vita ndogo ndogo za kibiashara zisizosaidia nchi yeyote ile.

Kwa Rais Magufuli KUINGILIA kati jambo hili ametumia HEKIMA kubwa maana katika makubaliano huwa ni GIVE and TAKE na tatizo linamalizika kati ya nchi hizi zetu mbili ziendelee kama ilivyokuwa hapo
AWALI.
Na hiyo ndo spirit of unity/NIA ya umoja wa Afrika Mashariki.
Chanzo. The East African.
 
Katika vita baridi ya KIBIASHARA kati ya nchi hizi mbili ambazo zimekuwako kwa muda sasa zimeathiri pakubwa wafanya biashara, BIASHARA KITAIFA na MAPATO ya serikali kati ya nchi hizi mbili. Tanzania na Kenya.


Hali hii imeleta malumbano ya KIDIPLOMASIA na kusababisha KULIPIZIANA VISASI Kibiashara. at the expense ya wananchi na uchumi wa nchi hizi mbili.


KENYA ilianza kwa kukataza bidhaa kadhaa toka Tanzania SISIINGIE Kenya. Kama vile UNGA wa NGANO ,
GESI ya Tanzania KUINGIZWA nchini mwao huku ikitoa VISINGIZIO vingi.

TANZANIA nayo ikaamua kulipiza KISASI na KUZUIA kuingizwa kwa
TAIRI za gari toka Kenya, ikiwa ni pamoja na
MAZIWA,
MARGARINE na bidhaa zozote zinazotokana na MAZIWA.


Wakati huo huo Kenyanao wakasema GESI isipitie NAMANGA bali ipitie Mombasa ikiwa itaruhusiwa. Na hivyo kufanya Biashara kati ya nchi hizi mbili kuwa ni GHARAMA kubwa sana na kuleta usumbufu.sana kawa pande zote mbili.


Tanzania nayo tena IKAZUIA kupitishia mahindi nchini mwetu yaliyoagizwa toka ZAMBIA kwenda Kenya maana wana upungufu mkuu wa Mahindi/Njaa wakasema HAYATAPITIA nchini Tanzania.


Na hivyo kuleta UTATA USIO na TIJA kati ya nchi hizi mbili za Afrika Mashariki.
Kwa HEKIMA ya Rais Magufuli ameamua KUUMALIZA MGOGORO huu kwa kumwandikia barua Rais Kenyatta ili watafute SULUHISHO la kumaliza mgogoro huu.yaishe na WAELEWANE.

Inavyosemekana ni kuwa Kenya wamekaa NGUMU. Rais Kenyatta kwa sasa ana STUDY the brief/ Mapendekezo ya Tanzania kabla ya KUMJIBU rais mwenzake Mh. Rais Magufuli.


Nafikiri kwa ajili ya UCHUMI wetu wa Tanzania na KENYA, wote TUNAHITAJIANA. Hivyo ni vizuri WAMALIZE mgogoro huu wa KIBIASHARA HARAKA kabla haujaenda OUT OF HAND ili
wananchi na
WAKULIMA wa ngano,
GESI yetu tuweze KUIUZA ili uchumi wetu ukuwe.
Tusibaki katika vita ndogo ndogo za kibiashara zisizosaidia nchi yeyote ile.

Kwa Rais Magufuli KUINGILIA kati jambo hili ametumia HEKIMA kubwa maana katika makubaliano huwa ni GIVE and TAKE na tatizo linamalizika kati ya nchi hizi zetu mbili ziendelee kama ilivyokuwa hapo
AWALI.
Na hiyo ndo spirit of unity/NIA ya umoja wa Afrika Mashariki.
Chanzo. The East African.
kipi alichokisema kwa ufafanuzi zaid hebu nijuze.
 
Wakenya wanapenda sana kuliamsha dude
Wakenya ni ndugu zetu. Tofauti ndogo ndogo sisiharibu uchumi kama miaka ya 70. Tunaambiwa hata viwanda ya sabuni na mafuta ya kujipaka hatukuwa navyo.
TUNAHITAJIANA!
 
Wakenya washenzi sana walifikiri watanzania ni maboya kama zamani.. Ukileta ngebe na ss tunakungebua.. Hapa kazi tu.. Tena kwenye margarine na hayo mahindi imeleta mtikisiko mkubwa sana kwa hao vilaza.
Mkuu Wakenya si jinsi unavyowaita. Wanaweza kuwa na udhaifu wao wa kujivuna kuwa wanajua. Lakini hili la MAHINDI ni vizuri wapate CHAKULA.
 
Ni kweli kuwa tunahitajiana, lakini nijuavyo mimi, zamani Tanzania tulikuwa tunawahitaji sana Kenya kuliko wao walivyokuwa wanatuhitaji sisi. Lakini siku hizi mambo yamebadilika, Hata wao wanatuhitaji sawa na sisi. Ukweli ni kwamba hata bidhaa zao za viwandani zisipoingia hapa kwetu bado tunaweza kuendelea maana siku hizi na sisi tunatengeneza zetu.
 
Ni kweli kuwa tunahitajiana, lakini nijuavyo mimi, zamani Tanzania tulikuwa tunawahitaji sana Kenya kuliko wao walivyokuwa wanatuhitaji sisi. Lakini siku hizi mambo yamebadilika, Hata wao wanatuhitaji sawa na sisi. Ukweli ni kwamba hata bidhaa zao za viwandani zisipoingia hapa kwetu bado tunaweza kuendelea maana siku hizi na sisi tunatengeneza zetu.
Nakubaliana nawe. Hata hivyo hamna nchi INAYOJITOSHELEZA yenyewe. Hata Marekani nao WANA IMPORT toka nchi zingine. Kwa hilo bado tunahitajiana kibiashara.
 
Back
Top Bottom