Rais Magufuli aambiwe ukweli

Rais Magufuli aambiwe ukweli

Duniani kote pesa za serikali hukaa Central Bank na wala si Commercial Banks ilikuwa TZ pekee ambako pesa za serikali zilikuwa zinakaa kwenye Commercial Banks ambapo hizo hizo Commercial Banks zinakwenda kuchukua mikopo BOT kwa kutumia pesa za serikali huu ulikuwa ujinga uliopitiliza ndiyo maana Kenya na India walikuwa wauzaji wa Tanzanite kuliko TZ huo nao ni ujinga uliopitiliza kiasi cha hali ya juu! Sasa amekuja mwanaume wa shoka amewanyoosha ni lazima mtalalamika tu kwa sababu nyinyi mlikuwa wanufaikaji wa mfumo huo wa kifisadi. Kwa waelewa wote wanajua Mh. Rais Magufuli anafanyakazi kubwa sana na atakuwa na wapingaji kama nyinyi lakini tunajua ataendelea kuwanyooka kwa kuwa watz walio wengi wako nyuma yake wanamuunga mkono.

Mkuu nachelea kusema ni wew pekee na baadhi ya mwenye akili finyu ndiyo wako nyuma ya jiwe, nitajie mtu mwenye utimamu wa akili na asiyelinda tumbo lake aliye nyuma kumsapoti jiwe
 
Mkuu ebu ainisha kwa mifano anuai hizo biashara ambazo zilitegemea mafisadi. Umejaribu kutumia elimu yako japo kidogo kujua effect ya serikari kuhamishia pesa zake zote BOT?
Wachumi tunaomba mtufafanulie vizuri effects za fedha yote kurudi BOT ili tuwe na uelewa mpana katika hili
 
Wananchi wa Tanzania ndio wajinga,
Magufuli na ccm yako endelea tu maana Hakuna namna.
 
Umeongea vizuri sana ila jiwe sijuwi kama litabadilika na kuwa mwamba tabaka walau maji na hewa vipate kupita. Ngoja nichepuke kidogo maana kuuamini utawala huu ni kutafuta jahanamu ya milele.
 
Tanzania yetu hii wengi ni wachezaji ambao wako nje ya uwanja. kazi yao ni kukosoa tu, hebu tujiulize hao wanaomponda Mh. waliwahi kuokoa majanga gani hapa nchini tukafahamu kwamba mbunge fulani ameshaokoa mali fulani ikiibiwa kwenda ulaya au kazi yao ni kusema tu as if wamekunywa pombe ya mnazi, nawasilisha
 
Wafuasi wa ZITTO au CHADEMA naona ukweli imewakuna juu ya uchapaji kazi wa MH, Na katika maandishi ya humu kwenye jf tunaangalia tu mantik au point hatusahishi sentensi,naona mnaonesha uwezo wenu wa kielimu mmmh!!!
 
Back
Top Bottom