Rais Magufuli aambiwe kuwa ndege, madaraja, reli za umeme sio vipaumbele vyetu

Hiyo reli ingejengwa kwenɗa kilimanjaro pongezi zingkuwa nyingi kiasi kuwa server ya jamii forums inge collapse kwa uwingi wa commeɗs za watu wenye Iɗ elfu moja tofauti kila mmoja nawangempingEza mɓowe,mɓatia,goɗbles lema,mrema na halima mɗee kwa kufanikisha hilo!!!!!
Hawa jamaa wamejaa sana mitandaoni ( si unajua wako madukani ndo kazi zao wanachat tu ) - wanateteana na kutukana mitandaoni balaa
 
Niyasemayo nikwakuwa katiba ya Tanzania inanipa mamlaka of free expression.

Kutumia mabilioni kununua Ndege,pia bilions zimetengwa kununua Boeing kule America sio kipaumbele kwa taifa kwa sasa.

Kujenga flyover ndani ya Daresalaam Na kutumia bilions sio kipaumbele chetu. kwanini masoko Na ofisi kuu zisihamishwe katika ya jiji Na kuwekwa pembezoni.

kujenga reli ya umeme Tanzania ni kutojua vipaumbele vya watanzania. si kwamba haifai Bali time yetu bado.

vipaumbele vya watanzania.

1)Kilimo.

Fedha zote zilizo nunulia ndege zingewekezwa kwenye kilimo, kwa kuwekeza kwenye benki Za wakulima,kuwekeza kilimo cha umwagiliaji,serikali kutumia taasisi kama jeshi,vyuo vya kilimo kufanya tafiti Za udongo Na mbegu,wadudu. pia kuwekeza kwenye pembejeo Za kilimo kama matrekta ya kulimia,kuvuna nk.

kilimo kimedharauliwa sana.

2)Elimu.

Serikali ilitakiwa iboreshe elimu hasa Veta,ijenge vyuo kila wilaya tupate wataalamu WA Kati Na Kati kwa ajili ya viwanda vidogo. pia iwekeze kwa vyuo vya kilimo tupate maafisa ugani WA kutosha.

pia elimu kwa vitendo kuanzia sekondari mpaka vyuo vikuu iboreshwe. nimesoma science udsm kwakweli lab ya chuo kikuu ni aibu, watu wanadesa tu km taifa litadharau quality ya elimu tutazani tunawasomi lakini incompetent.

3)Afya.

Serikali ilipaswa iwekeze kwenye afya. fikiria hata wewe, WAZAZI wanala chini,dawa hakuna,vifaa tiba vichache,gharama kubwa kwa magonjwa serious, kweli tujenge reli ya umeme?

4)Tuwekeze kwenye madini Na gesi asilia.

Uchumi wetu unakuwa boosted Na madini. je kama kule merererani kungejengwa viwanda vya Vito Na madini yale kuongezewa thamani.

pili kuwekeza ni pamoja Na kureview mikataba kwa kuiweka wazi hasa bungeni ikapitiwa upya.

tatu ni kuwekeza kwenye nishati ya umeme kupitia gesi asilia. umeme ndio determinant WA kila kitu Na ndio engine ya uchumi wowote. sasa unanunua sh500 unauza 200,halafu unahubiri Tanzania ya viwanda, are we serious.


nimetaja vipaumbele vichache Kati vingi ambavyo serikali ilipaswa ianze navyo kuinua mateso Na umaskini WA watu wetu.

assadsyria3

vipaumbele vya inch hii vimo kwenye ilani ya uchaguzi ambayo wanainch waliikubali na kuichagua, hii ni ilani ya ccm.

hivyo vipaumbele vyako subiri uchaguzi mwingine 2020 ukawashauri waviweke kwenye ilani ya ccm au ukawa uwachague.
 
mkuu Mimi sio chadema wala sio CCM ,mim sina chama, nimetumia Uhuru wangu kutoa maoni,is my right.

sasa kununua Boeing wakati kilimo kinasuasua,magonjwa yanaua watu wetu,wengine wanalala chin does it make sense to u?

hatusemi visifanyike but not right now coz bado sie maskini tuangalie urefu WA kambi yetu.

sio kuwa ukiwa CCM unapoteza rational thinking. hembu jaribu kutulia badala ya kuwa jingalao utakuwa tena sio jinga lao
Jinga lao wewe, ushaambiwa anatekeleza ilani ya ccm iliyokubaliwa na WA tz bado huelewi, haya basi 2020 mchague huyo Lowasa wako afanye Hayo unayotaka
 
Niyasemayo nikwakuwa katiba ya Tanzania inanipa mamlaka of free expression.

Kutumia mabilioni kununua Ndege,pia bilions zimetengwa kununua Boeing kule America sio kipaumbele kwa taifa kwa sasa.

Kujenga flyover ndani ya Daresalaam Na kutumia bilions sio kipaumbele chetu. kwanini masoko Na ofisi kuu zisihamishwe katika ya jiji Na kuwekwa pembezoni.

kujenga reli ya umeme Tanzania ni kutojua vipaumbele vya watanzania. si kwamba haifai Bali time yetu bado.

vipaumbele vya watanzania.

1)Kilimo.

Fedha zote zilizo nunulia ndege zingewekezwa kwenye kilimo, kwa kuwekeza kwenye benki Za wakulima,kuwekeza kilimo cha umwagiliaji,serikali kutumia taasisi kama jeshi,vyuo vya kilimo kufanya tafiti Za udongo Na mbegu,wadudu. pia kuwekeza kwenye pembejeo Za kilimo kama matrekta ya kulimia,kuvuna nk.

kilimo kimedharauliwa sana.

2)Elimu.

Serikali ilitakiwa iboreshe elimu hasa Veta,ijenge vyuo kila wilaya tupate wataalamu WA Kati Na Kati kwa ajili ya viwanda vidogo. pia iwekeze kwa vyuo vya kilimo tupate maafisa ugani WA kutosha.

pia elimu kwa vitendo kuanzia sekondari mpaka vyuo vikuu iboreshwe. nimesoma science udsm kwakweli lab ya chuo kikuu ni aibu, watu wanadesa tu km taifa litadharau quality ya elimu tutazani tunawasomi lakini incompetent.

3)Afya.

Serikali ilipaswa iwekeze kwenye afya. fikiria hata wewe, WAZAZI wanala chini,dawa hakuna,vifaa tiba vichache,gharama kubwa kwa magonjwa serious, kweli tujenge reli ya umeme?

4)Tuwekeze kwenye madini Na gesi asilia.

Uchumi wetu unakuwa boosted Na madini. je kama kule merererani kungejengwa viwanda vya Vito Na madini yale kuongezewa thamani.

pili kuwekeza ni pamoja Na kureview mikataba kwa kuiweka wazi hasa bungeni ikapitiwa upya.

tatu ni kuwekeza kwenye nishati ya umeme kupitia gesi asilia. umeme ndio determinant WA kila kitu Na ndio engine ya uchumi wowote. sasa unanunua sh500 unauza 200,halafu unahubiri Tanzania ya viwanda, are we serious.


nimetaja vipaumbele vichache Kati vingi ambavyo serikali ilipaswa ianze navyo kuinua mateso Na umaskini WA watu wetu.

assadsyria3
Your leaving in old stage age,how do you expect to generate revolving capital of potential investment without infrastructure?
 
Ndio maana nasema na nitaendelea kusema na sitachoka ili kila mwenye akili anielewe.

"People with great minds can not be comfortable in this country and actually have nothing to celebrate so far."

Mleta mada you are not comfortable kwasabubu unaona kama Taifa tunapotea.

Tunaunga mkono ujenzi wa miundombinu ila kosa kubwa ni kutoa kipaumbele kwenye sekta hiyo moja tu huku sekta zingine zinazopaswa kwenda sambamba na sekta ya ujenzi na mawasiliano zikidorora.

Ukigundua kasoro hii na nyinyinezo you can never be comfortable.
 
Wewe ni sawa na wanaomwambia baba yako kuwa kipaumbele chao si kuwekeza,bali ni kula.Faida inayoletwa na usafiri wa anga nenda Airport ukaulize.Ethiopia wanaendesha uchumi wao kwa asilimia kubwa kwa kutumia usafiri wa anga.Unasema tuwekeze kwenye kilimo,nenda Kigoma uone miradi ya umwagiliaji kama inatumika ipasavyo.Wananchi Kasulu mwaka 2014 walikataa mradi wa umwagiliaji mpaka wafadhili wakaondoka na fedha zao takriban billion 1.Usafiri wa reli hujapima faida yake.Hivi mizigo ya Uganda,Rwanda,Burundi na DRC ikipita kwetu tutapata faida kiasi gani?.Fedha itakayopatikana hatuwezi kuwekeza kwenye kilimo?.Wananchi mpaka juzi walikuwa wanapelekewa pembejeo za ruzuku,lakini badala yake walikuwa wanapewa elfu 5 na wafanyabiashara na pembejeo zinabaki na wafanyabiashara.
 
Hii awamu kasi Ya GoT haiendani na Private sector awamu iliyopita kasi Ya private sector haikuendana na GoT ......the pple at the ends hawaumii sana huyu wa kat kat the hoi polloi anakuwa hoi kweli
 
Kwa akili hizi ndio maana hata baada ya miaka 20 CDM hawana hata ramani ya ofisi wanayotaka kujenga. Bila miundombinu bora huwezi ona faida ya kilimo, zahanati na shule hazitafikika. Mwambie Mbowe hatudanganyiki...

..binafsi naunga mkono ujenzi wa reli mpya sgr.

..lakini ingependeza kama serikali ya ccm ingetueleza kwanini hatufaidiki na reli ya tazara.

..waTz tunapenda sana vitu vipya. Kwa mfano sasa hivi tunafurahia mradi wa bomba la mafuta toka Uganda. Lakini tayari tunalo bomba la mafuta la Tz to Zambia. Je linatuingizia mapato kiasi gani? Je tunalitumia kwa ufanisi?
 
Wenzetu walianza na kilimo mengine yakafuata.China walianza na green revolution ,uingereza agrarian revolution ....na kwingine pote walihakikisha kilimo kipo vizuri ili kitoe Mali ghafi na chakula cha kutosha.sisi tunakimbizana na reli ya Umeme wakati zile za kale tumeshindwa na hata Umeme wenyewe hautoshelezi kwa mahitaji ya taa(mwanga)!!!!
 
Tumengia na sera ya viwanda,lakini naona gia imebadilishiwa angani sasa ni infrastructure.
Mabarabara yaliyokula fedha na kuongeza deni la Taifa tungevuta subira ya pay back tuweke nguvu kwenye kilimo na viwanda vidogo vya kutosheleza mahitaji yetu muhimu.
Maana hata tooth pick tunaagiza china.
Nyerere alikuwa anaandaa wananchi kwa sloghamu ya " kupanga ni kuchagua". Aliwaandaa wananchi sasa tunafunga mkanda ili tufanikishe jambo fulani na wananchi wanaandaliwa kisakolojia.
Kwa sasa hakuna hili jambo tunakutana na matukio kwenye vyombo vya habari.
Hata tukifuata mfano mdogo jinsi projects zinavyofanya Kazi tungepitia hatua zote.
Tungemaliza swala la umeme vijiji vyote na kuhamia kilimo na ufugaji.
Mambo ya afya,maji na elimu hivyo huwezi sema
Kipaumbele,haya ni mahitaji ya lazima na huwezi kwepa.
Wanaanchi wajulishwe na kuandaliwa kuhusu mioango ya maandeleo na wakubali. Ownership,maana mwananchi ukimwambia ndege,treni ya umeme anakushangaa maana huko vijijini anashindwa kuleta mazao wilayani njia mbovu,hamna madaraja.
 
Back
Top Bottom