Rais Magufuli aagiza kiwanda cha Buko kuanza kazi ya kubangua korosho mara moja. Waziri aita wanasayansi wa UDSM haraka

Walimu wa chuo kikuu siyo watu wa field. Hawana uzoefu wa kutengeneza mitambo. Hawa ni watu wa kufundisha principles lakini ukiwapeleka field, utashangaa. Wanaweza kuzidiwa na fundi wa darasa la saba.

Tunawaona wanapokuja kuwasimamia wanafunzi wakati wa field. Kitu kidogo ambacho mfanyakazi wa kawaida ambaye yupo kwenye field, unamwuliza mara moja, na anakupa jibu sahihi, mhadhiri wa chuo kikuu itamchukua hata mwezi kukupa jibu, na wakati mwingine anakupa jibu siyo sahihi.

Aiseee!! Bams?

"----kitu kidogo ambacho mfanyakazi wa kawaida anaweza kukifanya mara moja, kinamchukua mhadhiri inamchukua mwezi?"

Wacha bhwana!. nakubali, mhadhiri anaweza asikupe jibu la kiwandani kwako papo kwa papo, kwa sababu ya mazingira ya kiwandani kwako hana uzoefu nayo, lakini akae mwezi hata wiki?
WaTanzania tuache utani huu Bhwana.
 
Wananikumbusha pale Hitler alipokusanya wanasayansi wa Kijerumani akawaambia hakuna atakeyoondoka mpaka wamekuja na gari matata!. kweli bwana wazee wakajipinda ile kuibuka tu wakaja na volkswagen(beetle)!.Sasa hao wanasayansi wa UDSM walioitwa kazi wanayo!

Usiwasahau Korea Kaskazini. Wamejipinda ndani ya miaka kumi wakafanya kweli - makombora na mabomu kwa pamoja.
Usifanye mzaha binaadam anaponuia kufanya jambo kama kweli amedhamilia kulifanya kwa dhati.
 
Waziri wa biashara amesema ameagizwa na Rais Magufuli kuhakikisha kiwanda cha Buko kilichosimama kufanya kazi kinaanza kazi ya kubangua korosho mara moja.

Kufuatia agizo hilo waziri amewataka mafundi wabobezi na wanasayansi wenye ubunifu kutoka Udsm wafike haraka Mtwara na kuhakikisha kiwanda hicho kinaanza kazi ndani ya wiki moja.

Source ITV habari!
Halafu wakibangua nani atakuwa mlaji ?
 
Kwa nini wasipeleke technicians kutoka VETA na DIT, hao maprofessa watakuwa wanapiga tu story huko maana sidhani kama wanaweza hata kushika spanner
 
Kwa nini wasipeleke technicians kutoka VETA na DIT, hao maprofessa watakuwa wanapiga tu story huko maana sidhani kama wanaweza hata kushika spanner
And this is not a sophisticated factory. Watalaamu wasikimbilie per diem tu
 
Tatzo anawaamini sana UDSM, kuna watu wengine nao wangepewa nafasi pengine tungeona utofauti.. Watu kama SIDO, VETA, SUA, MUST, DIT n.k
No, hata hao wasingesaidia chochote kama wanataka kiwanda chakavu kifufuliwe haraka. Walitakiwa wawatafute mafundi mitambo wa kawaida. Vinginevyo itawachukua hata miezi 6 kukifufua.
 
Magufuli kachanganikiwa. Haelewi ashike kipi aache kipi. Had anatia huruma. Haya ndyo matatizo ya kumsukumizia mtu majukumu yakiyojuu ya uwezo wake. JK alikosea sana kumsukumiza. Sijui alfanya makusudi ili tumkumbuke?
 
Waziri wa biashara amesema ameagizwa na Rais Magufuli kuhakikisha kiwanda cha Buko kilichosimama kufanya kazi kinaanza kazi ya kubangua korosho mara moja.

Kufuatia agizo hilo waziri amewataka mafundi wabobezi na wanasayansi wenye ubunifu kutoka Udsm wafike haraka Mtwara na kuhakikisha kiwanda hicho kinaanza kazi ndani ya wiki moja.

Source ITV habari!
Uchumi hauendeshwi kwa amri za namna hiyo
 
Halo zamani za kale kulikuwepo na mze mmoja na mkewake aliishi ktk maisha ya shida na taabu sana ikawa inalazimika muda mwingine huwasha moto na kuanza kuchemsha mawe ili kuwadanganya watoto kuwa Kuna chakula kinapikwa ili wakiwa na tamaa hiyo watoto hupatwa na matumiani kuwa chakula kinaiva wakapitiwa na usingizi nabkulala.

Lakini ki uhalisia bado Kuna njaa na ufumbuzi bado haujapatikana
 
Mambo kama haya yalitakiwa kuwa na mandalizi ya miaka miwili, bila hivyo tumefeli na tutaendelea kufeli miaka yote. Tujiandae ndipo tuamue
 
Waziri wa biashara amesema ameagizwa na Rais Magufuli kuhakikisha kiwanda cha Buko kilichosimama kufanya kazi kinaanza kazi ya kubangua korosho mara moja.

Kufuatia agizo hilo waziri amewataka mafundi wabobezi na wanasayansi wenye ubunifu kutoka Udsm wafike haraka Mtwara na kuhakikisha kiwanda hicho kinaanza kazi ndani ya wiki moja.

Source ITV habari!
Hivi ni nani anamdanganya Mh. Rais?

Mkuu wa Mkoa wa Lindi alimuambia waziri mkuu Mh. MKM kuwa kile kiwanda hakiwezi kubangua hata kg 5 za korosho kutokana mashine zake chakavu, nunueni mitambo na sio kulazimisha kubangua tu korosho.
 
Back
Top Bottom