Rais Kikwete: Nabii asiyekubalika nyumbani kwake?

Amemweka Babu Seya na wanae nyuma ya pazia kwa miaka yao yote duniani so kawafanya wafunge ndoa na Gereza

Kuna watu wengine JF wanakuwaga ni pointless kabisa hebu tupe link ya Babu seya na JK. Babu seya amekuwa akiharibu watoto wa watu wewe unaliona hilo sawa??? na JK yuko kwake kule Ferry alitokaje kuja kuhukumu kesi ya babu seya. Jamani tuwe home of great thinkers and not otherwise.
 
Ni mtazamo wangu na wewe unaruhusiwa kuwa na mtazamo wako. Anyway tuje katika hoja zako, hoja ya kwanza ulisema kuwa freedom of speech is a natural right yangu mie na wewe sasa nikuulize swali mlalahoi ni rais gani aliyekuwa anaruhusu mie na wewe tukawa tunaisulubu na kuisimanga serikali kwa uhuru. Mkapa alikuwa akitumia majasusi, Mwinyi makomredi, Nyerere system sasa je hiyo freedom ilikuwapo mbona unazungumzia vitu ambavyo ni non-sense kabisa. Ni nani hapa jamvini aseme alidiriki kuitamkia wazi serikali imeoza wakati wa mwinyi, nyerere na mkapa let alone kumkosoa rais kama hujaenda kujisaidia ndoo keko!!!!.

Inaonekana wewe ni mgeni kwenye mambo haya ya forums. Wakati wa mkapa kulikuwa na kitu inaitwa Bsctimes (kama sikosei) ambako watu walikuwa wakitoa nondo kama hawana akili nzuri. Walimkoma nyani giladi na wala hawakuwahi kwenda keko wala kokote kule.

Tuje katika swala muswada bunge limepitisha muswada wa utawala bora ambao unatenganisha biashara na utawala. Lakini muswada huo ni serikali ndio iliyoundaaa na kurasijisha bungeni sasa nikuulize kuna miswada mingapi serikali imeikalia kujifanya bado inaishughulikia kwanini wauruhusu kama sio mtazamo wa rais kupendelea uongozi utenganishwe na shughuli za mtu binafsi. To me I think that is irrelevant unaposema hauna faida. Mkapa aliruhusu ndio matokeo yake Kiwira Coal mine, Meremeta Gold Mine etc. Sasa huoni kama hili jambo lina manufaa kwa jamii.

Swala la kupitisha mswada ni tofauti na utendaji. Utekelezaji wa hili swala bado uko mbali sana na hali halisi.

Kuhusu CCM mie siwafagilii na nakubaliana na mtazamo wako kwani hata mie sikubaliani nao kabisa but ngoja nikuulize ndani ya CCM nani anafaa kuwa kiongozi wa nchi sasa hivi tukimtoa JK nani Lowassa?, Abdallah Kigoda, hakuna hata mmoja msafi humo ndani hadi Sitta mwenyewe anayejiita kiongozi wa kupambana na ufisadi tukitaka tutamfunulia madudu yake aliyoyafanya wakati akiwa Tanzania Investment Centre na pia wakati akiwa NDC sasa kwakweli sijaona kiongozi msafi CCM hata kidogo.

Yaani kwa vile hakuna mwingine unayemwona wewe kuwa anafaa basi Kikwete aendelee kuwa kiongozi. Wana ccm wote Tanzania hakuna yeyote mwingine zaidi ya Kikwete anayefaaa?

Kuhusu infrastructure economics sidhani hata katika nchi zilizoendelea projects zote zinaenda kwa wakati mmoja. Bali zinaenda kwa awamu kutegemeana na umuhimu wake. Unadhani soko la wakulima wa tanzania liko wapi mzee? Wakulima wako wakijengewa barabara halafu jijini dar, arusha barabara zikawa mbovu haya mazao yatafika???? Zungumza jambo ukiwa na akili timamu na sio umelewa kuendelezwa kwa miji ya kibiashara na muhimu kwani ndio soko kuu la mazao na hasa kwa tanzania ukichukulia wakulima wetu kuuza mazao nje ni ndoto. Usidhani kutawala nchi ni kama kuongoza kajumba kako!!!!

So far alichofanya Kikwete ni kipi?

Kikwete hajashindwa miaka mitano bali ameiingia na kukuta madudu yaliyofanywa na mwenzie aliyemtangulia ambayo yakamuharibia muelekeo wa utekelezaji wa sera zake. Likewise kaa mkijua kuwa hali ya uchumi wa kidunia pia imeterereka kutokana na kuanguka kwa sekta ya fedha. Zote hizi ukizichanganya unakuta ni bahati mbaya uongozi wake umekutana na masaibu hayo na sio majaribio kama unavyotaka kuileta kwani hali hiyo tuliipata wakati wa 1979-1982 tukilishwa unga wa njano na sukari guru.

Kikwete ana madudu yake mengi tu (soma post ya Kibanga hapo juu) na wala sio kwamba kakuta madudu yaliyofanywa na wengine

Kuhusu kuchaguliwa tena mie ukitaka msimamo wangu ni kwamba aje mgombea binafsi asimame kwa reputation yake kwani sijaona CCM wala wapinzani kama kuna mtu anafaa kuingoza hii nchi. Kwasababu mosi rais nayemtaka nataka awe mwadilifu, mchapakazi ya pili na tatu awe na akili na busara. Sasa katika sifa ya uadilifu sijaona anayenifaa mie na hivyo basi ni bora aendelee aliyepo anaweza kujirekebisha au aje mgombea binafsi kwani msimamo wangu ni independent voter

Hizo sifa zote ulizotaja hapo, Kikwete hana. What about makamo wa raisi Sheini?
 
Una ushahidi wa hizi tuhuma ?.,wanaojua ukweli wa hili sakata ni kina Babu Seya wenyewe na hao wahanga wa hilo tukio.,tuachane na hizi unfounded allegations.,hapa simtetei JK lakini naogopa sana kumtuhumu kwa kitu ambacho hakijawa proved..,anyway tukiachilia hilo nadhani mazuri yake ni machache kuliko mabaya.

Mazuri yenyewe bado hayajatajwa ... yanasubiriwa
 
Inaonekana wewe ni mgeni kwenye mambo haya ya forums. Wakati wa mkapa kulikuwa na kitu inaitwa Bsctimes (kama sikosei) ambako watu walikuwa wakitoa nondo kama hawana akili nzuri. Walimkoma nyani giladi na wala hawakuwahi kwenda keko wala kokote kule.



Swala la kupitisha mswada ni tofauti na utendaji. Utekelezaji wa hili swala bado uko mbali sana na hali halisi.



Yaani kwa vile hakuna mwingine unayemwona wewe kuwa anafaa basi Kikwete aendelee kuwa kiongozi. Wana ccm wote Tanzania hakuna yeyote mwingine zaidi ya Kikwete anayefaaa?



So far alichofanya Kikwete ni kipi?



Kikwete ana madudu yake mengi tu (soma post ya Kibanga hapo juu) na wala sio kwamba kakuta madudu yaliyofanywa na wengine



Hizo sifa zote ulizotaja hapo, Kikwete hana. What about makamo wa raisi Sheini?

Kaka mie ndio nilikuwa mgeni wa Jamiiforum but kama umesahau wakati mkapa jamiiforum (ambayo wakati huo ikiitwa jamboforum) iliiandamwa ikawa shut down ndio transparency hiyo!!!!

Mie nasema ndani ya CCM hakuna mwenye sifa nilizozitaja hapo juu. Shein ni simba aliyekaa kimya kama angelikuwa mwadilifu angelijuuzulu wakati wa mkapa ambapo madudu yalikuwa yakiendelea. Kaja wakati wa Kikwete salamu ndio hizo hizo je ndio kiongozi mwadilifu huyo au mwoga!!!! asiharibu kitumbua chake. Hakuna mwenyesifa mkubwa kwangu mie kama independent voter
 
Kaka mie ndio nilikuwa mgeni wa Jamiiforum but kama umesahau wakati mkapa jamiiforum (ambayo wakati huo ikiitwa jamboforum) iliiandamwa ikawa shut down ndio transparency hiyo!!!!

Unazidi kuchemsha bado ... jamii forums iliandamwa na kufungwa (shut down) wakati wa Kikwete na sio wakati wa Mkapa.

Mie nasema ndani ya CCM hakuna mwenye sifa nilizozitaja hapo juu. Shein ni simba aliyekaa kimya kama angelikuwa mwadilifu angelijuuzulu wakati wa mkapa ambapo madudu yalikuwa yakiendelea. Kaja wakati wa Kikwete salamu ndio hizo hizo je ndio kiongozi mwadilifu huyo au mwoga!!!! asiharibu kitumbua chake. Hakuna mwenyesifa mkubwa kwangu mie kama independent voter

Kwa hiyo uko wazi kusema kuwa hautapigia kura ccm kwa vile hakuna msafi na mwenye sifa ulizozitaja hapo juu?
 
Unazidi kuchemsha bado ... jamii forums iliandamwa na kufungwa (shut down) wakati wa Kikwete na sio wakati wa Mkapa.



Kwa hiyo uko wazi kusema kuwa hautapigia kura ccm kwa vile hakuna msafi na mwenye sifa ulizozitaja hapo juu?

Hebu tuambie jambo forum ilienda wapi???? na nadhani nilishasema tangu thread ya mwanzo kuwa hakuna msafi CCM labda apewe tu huyo JK which mie sitapiga kura kwake bora iwe kura mfu pengine atajirekebisha
 
Hebu tuambie jambo forum ilienda wapi????

Jamboforums ilibadilishwa jina kuwa jamii forums sometimes kati ya 2007 na 2008 (sina hakika zaidi katika hili) baada ya kutokea mgongano kati ya waanzilishi wa forums kuhusu umiliki wa jina jamboforums.

Mgogoro unaouongelea kati ya jamboforums (jamiiforums) na serikali, umetokea wakati wa serikali ya Kikwete na sio Mkapa. Mimi nimeijua hii forum mwaka 2006. Sina hakika kama ilikuwepo mwaka 2005 au kabla ya hapo. Kina Julius (au wale members tuliokuwa nao toka enzi za Bsctimes) wanaweza kudhibitisha hili.

nadhani nilishasema tangu thread ya mwanzo kuwa hakuna msafi CCM labda apewe tu huyo JK which mie sitapiga kura kwake bora iwe kura mfu pengine atajirekebisha

Kama Kikwete sio msafi kama walivyo wengine uliowataja hapo juu, kwanini waona kuwa bora Kikwete na sio wao?

Ufisadi wa Kikwete una tofauti gani na ufisadi wa Lowasa au Sitta?
 
Jamboforums ilibadilishwa jina kuwa jamii forums sometimes kati ya 2007 na 2008 (sina hakika zaidi katika hili) baada ya kutokea mgongano kati ya waanzilishi wa forums kuhusu umiliki wa jina jamboforums.

Mgogoro unaouongelea kati ya jamboforums (jamiiforums) na serikali, umetokea wakati wa serikali ya Kikwete na sio Mkapa. Mimi nimeijua hii forum mwaka 2006. Sina hakika kama ilikuwepo mwaka 2005 au kabla ya hapo. Kina Julius (au wale members tuliokuwa nao toka enzi za Bsctimes) wanaweza kudhibitisha hili.



Kama Kikwete sio msafi kama walivyo wengine uliowataja hapo juu, kwanini waona kuwa bora Kikwete na sio wao?

Ufisadi wa Kikwete una tofauti gani na ufisadi wa Lowasa au Sitta?

Kikwete naweza kukuhakishia si fisadi hao wengine ni mafisadi haswa haswa. Ila tatizo la kikwete ni mtu ambaye si mfatiliaji wa jambo na anapenda sana sifa kitu kinachomponza. Hawa wengine wanajifanya wafatiliaji kumbe wanafatilia kwa maslahi yao binafsi nadhani tofauti umeziona hapo ndio maana nasema afadhali Kikwete
 
Kikwete naweza kukuhakishia si fisadi hao wengine ni mafisadi haswa haswa. Ila tatizo la kikwete ni mtu ambaye si mfatiliaji wa jambo na anapenda sana sifa kitu kinachomponza. Hawa wengine wanajifanya wafatiliaji kumbe wanafatilia kwa maslahi yao binafsi nadhani tofauti umeziona hapo ndio maana nasema afadhali Kikwete

Mhh,

Yaani unaweza kunihakikishia kabisa kuwa Kikwete si fisadi. Kwanza unaanza kwa kusema kuwa ccm wote mafisadi na kisha unabadilika njiani na kusema kuwa Kikwete ni msafi na sio fisadi.

Hebu jibu haya yaliyoandikwa na Kibanga ampiga mkoloni


Kiukweli mimi namkumbuka haya ya kwenye list of shame na naamini hadi vizazi vijavyo vitamkumbuka:-

Rais Jakaya Kikwete amekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia Desemba 2005. Kabla ya kuwa Rais, Mheshimiwa Kikwete alikuwa Waziri wa Mambo Nje na Uhusiano wa Kimataifa kuanzia 1995 hadi 2005, Waziri wa Fedha 1994 hadi 1995 na Waziri wa Maji, Nishati na Madini kuanzia mwaka 1990 hadi 1994.
Kama Waziri wa Maji, Nishati na Madini, Mheshimiwa Kikwete alishiriki moja kwa moja katika kusaini mikataba mibovu ya madini na makampuni ya madini ya kimataifa ambayo kwayo taifa limeendelea kupoteza utajiri mkubwa na kuinyima Serikali uwezo wa kifedha wa kuhudumia wananchi. Kwa mfano, mnamo tarehe 10 Aprili 1990, Major Jakaya Mrisho Kikwete aliingia mkataba wa madini ya kampuni ya SAMAX Limited ambapo kampuni hiyo ilipewa leseni ya kuchimba dhahabu katika eneo la Lusu, Wilayani Nzega Mkoa wa Tabora. Matokeo ya mkataba huo, maelfu wa wachimbaji wadogo wadogo wa dhahabu waliokuwa eneo hilo waliondolewa kwa nguvu na vikosi vya FFU na bila ya kulipwa fidia yoyote. Hadi leo wananchi hao hawajalipwa fidia yoyote licha ya miaka zaidi ya kumi ya kufuatilia haki zao. Baada ya kutwaa utajiri wa dhahabu wa eneo hilo , SAMAX Limited iliuza eneo hilo kwa kampuni ya Ashanti Goldfields ya Ghana kwa dola za Marekani milioni 253. Ashanti Goldfields nao wakauza eneo kwa kampuni ya Resolute Limited ya Australia kwa kiasi kisichojulikana cha fedha za kigeni. Resolute Limited ndio waliojenga na wanamiliki Mgodi wa Dhahabu wa Golden Pride ulioko eneo la Lusu, Nzega hadi sasa na ambao ulifunguliwa mwezi Novemba 1998.

Mnamo tarehe 5 Agosti 1994 Luteni Kanali Jakaya Mrisho Kikwete aliingia tena mkataba na kampuni ya madini Kahama Mining Corporation Ltd., kampuni tanzu ya kampuni ya Sutton Resources ya Canada . Ijapokuwa mkataba huu unaonyesha wazi kwamba ulikuwa unahusu eneo la Butobela Wilaya ya Geita Mkoani Mwanza, mwezi Agosti mwaka 1996 Kahama Mining Corporation wakisaidiwa na vikosi vya FFU walivamia eneo la Bulyanhulu, Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga na kuwaondosha kwa nguvu watu takriban laki nne waliokuwa wakiishi na kuchimba dhahabu katika eneo hilo. Baada ya kutwaa eneo hilo kwa nguvu za kijeshi, Sutton Resources iliiuza Kahama Mining Corporation na Bulyanhulu kwa Kampuni ya Dhahabu ya Barrick Gold Corporation ya Toronto , Canada kwa dola za Marekani milioni 280. Leo hii Bulyanhulu ni moja ya migodi tajiri kwa dhahabu katika Bara la Afrika.


Akiwa kama Raisi Pia namkumbuka kwa kushindwa kuchukua hatua katika mambo yafuatayo ambayo yanalitia aibu taifa:-


•Kashfa ya Loliondo – ambapo urithi wa watoto wetu uliuzwa na umeendelea kuuzwa
kwa wageni.
•Kashfa ya IPTL -
•Kashfa ya Commodity Import Support
•Kashfa ya Mgodi wa Kiwira
•Kashfa ya Akaunti ya EPA
•Kashfa ya Meremeta Ltd, Mwananchi Gold, Deep Green Finance, na Tangold
•Kashfa ya Rada
•Kashfa ya Ununuzi wa Airbus
•Kashfa ya Ununuzi wa Gulfstream 500 (ndege ya Rais)
•Kashfa ya Richmond
•Kashfa ya Dowans
•Kashfa ya magari, silaha na helikopta za JWTZ
•Kashfa ya silaha haramu
•Kashfa za madawa ya kulevya
•Kashfa ya uuzwaji wa maeneo wazi
•Kashfa ya misamaha ya kodi ya Alex Stewart
•Kashfa ya Ujenzi wa Minara miwiliya Benki Kuu
•Kashfa ya uuzaji wa maeneo ya ufukwe Dar

 
Steve dii nimekuona hapo juu, tafadhali sana nisaidie kumkumbusha ndugu mdondoaji kuwa waendeshaji wa jamiiforums (jamboforums) walitupwa ndani wakati wa uongozi wa Kikwete na sio Mkapa
 
Ni mtazamo wangu na wewe unaruhusiwa kuwa na mtazamo wako. Anyway tuje katika hoja zako, hoja ya kwanza ulisema kuwa freedom of speech is a natural right yangu mie na wewe sasa nikuulize swali mlalahoi ni rais gani aliyekuwa anaruhusu mie na wewe tukawa tunaisulubu na kuisimanga serikali kwa uhuru. Mkapa alikuwa akitumia majasusi, Mwinyi makomredi, Nyerere system sasa je hiyo freedom ilikuwapo mbona unazungumzia vitu ambavyo ni non-sense kabisa. Ni nani hapa jamvini aseme alidiriki kuitamkia wazi serikali imeoza wakati wa mwinyi, nyerere na mkapa let alone kumkosoa rais kama hujaenda kujisaidia ndoo keko!!!!.
Kwani Mwanahalisi lilifungiwa katika utawala upi?Kulikoni je?Na Kubenea alimwagiwa tindikali wakati wa utawala wa Nyerere?Na hao majasusi wanaokesha JF kila kukicha ni waajiriwa wa Kamuzu Banda?Ni uhayawani kufikiria kwamba JK ametupa uhuru wa kuongea wakati haki hiyo iko wazi na bayana kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano.Yani haki yako ya Katiba unaihusisha na matakwa ya mtu?Kweli safari ya kumkomboa Mtanzania bado ni ndefu sana kwa mawazo kama haya!
Tuje katika swala muswada bunge limepitisha muswada wa utawala bora ambao unatenganisha biashara na utawala. Lakini muswada huo ni serikali ndio iliyoundaaa na kurasijisha bungeni sasa nikuulize kuna miswada mingapi serikali imeikalia kujifanya bado inaishughulikia kwanini wauruhusu kama sio mtazamo wa rais kupendelea uongozi utenganishwe na shughuli za mtu binafsi. To me I think that is irrelevant unaposema hauna faida. Mkapa aliruhusu ndio matokeo yake Kiwira Coal mine, Meremeta Gold Mine etc. Sasa huoni kama hili jambo lina manufaa kwa jamii.
Na hatma ya Meremeta ni ipi hadi leo?Pinda (mteuliwa wa Kikwete) alisemaje Bungeni alipoulizwa kuhusu Meremeta?

Halafu napokuona wa ajabu ni namna unavyoweza kuonyesha bayana kuwa JK ana uwezo wa kufanya mazuri lakini unajikanganya kwa kushindwa kutueleza nini kinamkwaza kufanya mazuri kama kuwachukulia hatua mafisadi wa Kagoda,Richmond,Kiwira,IPTL,rada,nk.

Tumia busara usiendeshwe na simulizi kwani simulizi zimekuwepo tangia enzi hizo.Kwanza,nimeshakujibu kuwa huo muswada wa kutenganisha biashara na siasa ni kiini macho kwa vile CCM yenyewe inaendeshwa na wafanyabiashara wa fedha chafu.Unatarajia nini kama mwenyekiti wa kamati yake ya maadili ni jambazi wa rada Chenge?

Kwa upande wa kisheria,uamuzi huo unaweza kupingwa mahakamani kuwa unawanyima wafanyabiashara waadilifu fursa ya kushiriki katika demokrasia.Kwa taarifa yako,tatizo sio wafanyabishara kujihusisha na siasa hususan katika mfumo wa uchumi wa soko.Tatizo ni wafanyabisahara wa aina ya Rostam Aziz,Lowassa,Karamagi na mafisadi kama hao.Kwani kama Rostam anaweza kuandikisha utitiri wa makampuni kwa kutumia majina mbalimbali,atashindwaje kusema anaacha biashara na kubaki mwanasiasa asilimia 100% huku makampuni anayomiliki kwa majina mbalimbali yakiendeleza ufisadi?

Pia uanapswa kuelewa kuwa tatizo sio sera,miswada au sheria bali usimamizi na utekelezaji wake.Kwani wakati tunaingizwa mkenge wa Richmond kulikuwa hakuna sheria inayosimamia manunuzi?Je wakati tunaingia mkenge wa IPTL hakukuwa na sheria za kuhakikisha kuwa mkataba huo haugeuki kuwa loba ya mbao?

Ni kipi kinakupa matumaini kuwa sheria ya kutenganisha siasa na biashara itatekelezeka ilhali hseria nyingine zinazoweza kuzuia ufisadi zimeendelea kubaki vitabuni tu?

Na muulize huyo rafiki yako JK kwanini yeye mwenyewe hafuati sheria kwa kututangazia mali zake ili tujue kama naye si mfanyabisahara?Kwanini asimuige Pinda?

Kuhusu CCM mie siwafagilii na nakubaliana na mtazamo wako kwani hata mie sikubaliani nao kabisa but ngoja nikuulize ndani ya CCM nani anafaa kuwa kiongozi wa nchi sasa hivi tukimtoa JK nani Lowassa?, Abdallah Kigoda, hakuna hata mmoja msafi humo ndani hadi Sitta mwenyewe anayejiita kiongozi wa kupambana na ufisadi tukitaka tutamfunulia madudu yake aliyoyafanya wakati akiwa Tanzania Investment Centre na pia wakati akiwa NDC sasa kwakweli sijaona kiongozi msafi CCM hata kidogo.

Kwahiyo kwa vile ndani ya CCM hakuna aliye bora basi tuendelee na Kikwete?Hivi unafahamu kuwa membership ya CCM ni takriban asilimia 10 tu ya population ya Tanzania?Yani unachosema ni kwamba laiti ungekuwa na mke malaya ungeendelea nae hivyohivyo kwa vile tu kwa mtizamo wako huko nje hakuna wanawake walio bora zaidi?Haya ndio yanayowaua watu kwa ukimwi.

Kumbuka kuwa uongozi wa TAIFA LETU sio divine right ya CCM pekee.Kumsifia Kikwete kuwa ni bora kwa vile tu wenzake huko CCM ni wachafu,au hakuna aliye bora zaidi yake,ni ufinyu wa mawazo.

I would say kuna watu kama Dr Slaa ambao at least wametuonyesha nini maana ya kiongozi kuwa na uchungu na nchi.

Kuhusu infrastructure economics sidhani hata katika nchi zilizoendelea projects zote zinaenda kwa wakati mmoja. Bali zinaenda kwa awamu kutegemeana na umuhimu wake. Unadhani soko la wakulima wa tanzania liko wapi mzee? Wakulima wako wakijengewa barabara halafu jijini dar, arusha barabara zikawa mbovu haya mazao yatafika???? Zungumza jambo ukiwa na akili timamu na sio umelewa kuendelezwa kwa miji ya kibiashara na muhimu kwani ndio soko kuu la mazao na hasa kwa tanzania ukichukulia wakulima wetu kuuza mazao nje ni ndoto. Usidhani kutawala nchi ni kama kuongoza kajumba kako!!!!

Na kwa akili yako iliyo timamu ukishakuwa na barabara nzuri hapo Dar wakati wakulima huko mahenge wanasumbuana na kivuko feki unatarajia hayo mazao yanafikaje bandarini Dar?Eti infrastructural economics!Yaani barabara za lami mijini zimekusahaulisha kabisa adha ya watanzania wenzako wanayipata huko reli ya kati na Tazara?Vipi kuhusu ATC?

Ni ulevi wa kifikra kuangalia upande mmoja wa "maendeleo" na kupuuza upande mwingine.Tegemeo la uchumi wa Tanzania ni katika kilimo,na kama unafuatilia mijadala ya bunge vizuri utakumbuka kwanini bajeti ya WIzara ya Miundombinu iliwekewa ngumu katika kikao cha bajeti kilichopita.Fuatilia hilo kisha ufanye review ya hoja yako dhaifu.

Of course,kutawala nchi sio sawa na kuongoza nyumba ndio maana hatutaki kiongozi dhaifu ang'anganie kuongoza wakati ameshindwa hata kumudu nidhamu ya baraza lake "dogo" la mawaziri waziofika 60.Kama hawezi kuwamudu hao "wachache" alowateua ataweza kumudu kuwatumikia watanzania zaidi ya milioni 40?

Kikwete hajashindwa miaka mitano bali ameiingia na kukuta madudu yaliyofanywa na mwenzie aliyemtangulia ambayo yakamuharibia muelekeo wa utekelezaji wa sera zake. Likewise kaa mkijua kuwa hali ya uchumi wa kidunia pia imeterereka kutokana na kuanguka kwa sekta ya fedha. Zote hizi ukizichanganya unakuta ni bahati mbaya uongozi wake umekutana na masaibu hayo na sio majaribio kama unavyotaka kuileta kwani hali hiyo tuliipata wakati wa 1979-1982 tukilishwa unga wa njano na sukari guru.

Unavyoongea kuwa ameingia na kukuta madudu inasomeka kana kwamba ALILAZIMISHWA KUINGIA MADARAKANI.Dont tell me kuwa hakujua madudu yalokuwepo before hajaingia madarakani because HE WAS PART YA MADUDU ALIYOYAKUTA ALIPOINGIA MADARAKANI.Kwa kumbukumbu zako,JK alianza kushika madaraka ya kitaifa lini?Mwaka 2006?Alikuwa anafahamu fika uzito wa jukumu analolipokea na akatuahidi kutupatia ufumbuzi.

Halafu baadhi ya kauli zako ni kama za KUJIPENDEKEZA.Mbona sijamsikia JK mwenyewe akisema kuwa CHANZO CHA MATATIZO YALIYOPO NI WATANGULIZI WAKE?
 
Mazuri yenyewe bado hayajatajwa ... yanasubiriwa

Hana Mazuri kama yapo waseme na si kusema tu waje na ushahidi!

Mwenye mada hii alikuwa anazungumzia kuwa Raisi anakubalika nje kuliko ndani, na yote inatokana na kusifiwa na wazungu.

Hivi tumesahau ya Mkapa walivyokuwa wana msifia? Kikowapi sasa hivi aibuuu anatamani ata kuhama nchi!

Mfano waingereza wealikuwa wanamsifia kumbe watu wana mradi wao wa Radar wanataka kutuhumiza wamechukua hela ambazo zilibidi ziende kwenye elimu ya msingi wao wakaenda kununua Radar (HakiElimu waliongea sana haya mambo kuwa 10,000 kwa kila mwanafunzi wa msingi azijafika kumbe wajanja wameenda kununulia Radar)
 
Kikwete naweza kukuhakishia si fisadi hao wengine ni mafisadi haswa haswa. Ila tatizo la kikwete ni mtu ambaye si mfatiliaji wa jambo na anapenda sana sifa kitu kinachomponza. Hawa wengine wanajifanya wafatiliaji kumbe wanafatilia kwa maslahi yao binafsi nadhani tofauti umeziona hapo ndio maana nasema afadhali Kikwete

Kaka sio uvivu wa kufuatilia ni magusudi jamaa anapewa 10% unafikiri Lowasa alikuwa anakula peke yake? au hujuhi habari ya Chenge, Idriss, na mwingine wanasema awamtaji(SFO) walivyogawana za rada?

Hivi kweli Balali alikula peke yake bila Mkapa?

sasa kaa ukijua sio uzembe ni makusudi kwa sababu jioni hesabu inaingia au jamaa wanamdai za uchaguzi kwahiyo anawachunia warudishe chao( Rostam & Lowasa)
 
Yes, Mh. Kikwete ame-cement kwa upana mahusiano ya kimataifa kati ya Tanzania na nchi mbalimbali duniani. Pia ameonesha ukomavu wa Tanzania kwenye ulinzi wa sovereignty za nchi nyingine kama vile kule Comoros na upelekaji wa majeshi yetu pande mbalimbali zenye migongano under UN.

Ukiachilia hayo ya kimataifa, pamoja na kasoro chache zilizotokea, i.e. kufungia magazeti na kukamata baadhi ya wenye vyombo vya habari, Mh. Rais Kikwete amekuwa mstari wa mbele kuendeleza uhuru wa vyombo vya habari. Nadhani wengi mtakubali kwamba ni mengi ambayo yanaandikika hivi sasa kwenye frontpages ambayo yasingeweza kugusa walau tu middle pages ndani ya magazeti miaka 6 iliyopita. Kwa haya machache namsifu Mh. Kikwete.


Hayo mambo ya PhD mimi naona ni ulimbukeni tu wa kuoneshana fadhila.
Commoro wapi best, kumkimbiza mgambo ndo unamsifia? Kwanza wale jamaa walikuwa kama sungusungu wa Mh. Mrema! Mwabie aende Somalia au Afghanistan akapambane na wanaume wa kazi!
 
Amewatunuku vyeo ndugu na marafiki zake hata pale ambapo hawakuwa na uwezo na matokeo yake wamevurunda na kumuaibisha ; mifano michache ni pale Board of External Trade na ATCL kwa wale wanaotaka kuthibibitishiwa!!
 
Amewatunuku vyeo ndugu na marafiki zake hata pale ambapo hawakuwa na uwezo na matokeo yake wamevurunda na kumuaibisha ; mifano michache ni pale Board of External Trade na ATCL kwa wale wanaotaka kuthibibitishiwa!!

Kaka aihitaji ushahidi kwani Shukuru Kawambwa amjuhi? mtu anahama wizara kama watu wanavyopanda vidato leo form one, mwaka form two,....
 
Ulitaka akulipie ada za shule wanao? ukiwa mchoyo usiwe mroho pia! agh

Shule za msingi na sekondari zimejengwa chini usimamizi na utawala wake

Vyuo vya elimu na vyuo vikuu vimejengwa chini ya usimamizi na utawala wake

Barabara za mikoa, Maji mikoa na DSM zimejengwa chini ya usimamizi wake

Mafisadi wamepelekwa mahakamani chini ya usimamizi na utawala wake

Uhuru wa vyombo vvya habari, uwazi katika shuighuli za serikali (ndio maana malalamiko mengi kwakuwa mmepewa habari enzio hizo ilikuwa sirikali)

Peace, Foreign Direct Invesment increase, employment ..list goes on and on!
Rafiki yangu, hayo niliyowekea red yana ukweli. Unajua ni lini mpanga wa MMEM na MMES zilianza? Yeye amefanya lipi zaidi ya kutimiza tu aliyofanya mwenzake? Kwenye hili la shule naliogopa, kwa sababu mwenzake Mkapa aliongeza shule nyingi za msingi pasipo kuathiri ubora. Yeye ameachiwa kusimamia tu hizi shule za secondary ambazo mwenzake alishakuwa na mpango kabambe ndo katutokea na ziro zaidi ya 60000. Aibu kuwapotezea muda watoto zaidi ya 60000 kwa zaidi ya miaka minne. Umeongelea kuhusu barabara, maji and the like. barabara zipi, maji yapi, hizo project zote sializianzisha Mkapa? Hili suala la kusimamia hata wewe tu unaweza kusimamia. Tunachotaka ni innovation and creativity ambazo zimeibuka wakati wake ambazo yumkini zinaviashiria vizuri kwa uchumi na ustawi wa jumla wa nchi yetu.
Napenda nimpongeze sana kuhusu chuo kikuu cha Dodoma. Katika hicho sina upinzani naye, kafanya kazi nzuri yenye maslahi makubwa kwa taifa.
 
Kwani Mwanahalisi lilifungiwa katika utawala upi?Kulikoni je?Na Kubenea alimwagiwa tindikali wakati wa utawala wa Nyerere?Na hao majasusi wanaokesha JF kila kukicha ni waajiriwa wa Kamuzu Banda?Ni uhayawani kufikiria kwamba JK ametupa uhuru wa kuongea wakati haki hiyo iko wazi na bayana kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano.Yani haki yako ya Katiba unaihusisha na matakwa ya mtu?Kweli safari ya kumkomboa Mtanzania bado ni ndefu sana kwa mawazo kama haya!
Na hatma ya Meremeta ni ipi hadi leo?Pinda (mteuliwa wa Kikwete) alisemaje Bungeni alipoulizwa kuhusu Meremeta?

Halafu napokuona wa ajabu ni namna unavyoweza kuonyesha bayana kuwa JK ana uwezo wa kufanya mazuri lakini unajikanganya kwa kushindwa kutueleza nini kinamkwaza kufanya mazuri kama kuwachukulia hatua mafisadi wa Kagoda,Richmond,Kiwira,IPTL,rada,nk.

Tumia busara usiendeshwe na simulizi kwani simulizi zimekuwepo tangia enzi hizo.Kwanza,nimeshakujibu kuwa huo muswada wa kutenganisha biashara na siasa ni kiini macho kwa vile CCM yenyewe inaendeshwa na wafanyabiashara wa fedha chafu.Unatarajia nini kama mwenyekiti wa kamati yake ya maadili ni jambazi wa rada Chenge?

Kwa upande wa kisheria,uamuzi huo unaweza kupingwa mahakamani kuwa unawanyima wafanyabiashara waadilifu fursa ya kushiriki katika demokrasia.Kwa taarifa yako,tatizo sio wafanyabishara kujihusisha na siasa hususan katika mfumo wa uchumi wa soko.Tatizo ni wafanyabisahara wa aina ya Rostam Aziz,Lowassa,Karamagi na mafisadi kama hao.Kwani kama Rostam anaweza kuandikisha utitiri wa makampuni kwa kutumia majina mbalimbali,atashindwaje kusema anaacha biashara na kubaki mwanasiasa asilimia 100% huku makampuni anayomiliki kwa majina mbalimbali yakiendeleza ufisadi?

Pia uanapswa kuelewa kuwa tatizo sio sera,miswada au sheria bali usimamizi na utekelezaji wake.Kwani wakati tunaingizwa mkenge wa Richmond kulikuwa hakuna sheria inayosimamia manunuzi?Je wakati tunaingia mkenge wa IPTL hakukuwa na sheria za kuhakikisha kuwa mkataba huo haugeuki kuwa loba ya mbao?

Ni kipi kinakupa matumaini kuwa sheria ya kutenganisha siasa na biashara itatekelezeka ilhali hseria nyingine zinazoweza kuzuia ufisadi zimeendelea kubaki vitabuni tu?

Na muulize huyo rafiki yako JK kwanini yeye mwenyewe hafuati sheria kwa kututangazia mali zake ili tujue kama naye si mfanyabisahara?Kwanini asimuige Pinda?



Kwahiyo kwa vile ndani ya CCM hakuna aliye bora basi tuendelee na Kikwete?Hivi unafahamu kuwa membership ya CCM ni takriban asilimia 10 tu ya population ya Tanzania?Yani unachosema ni kwamba laiti ungekuwa na mke malaya ungeendelea nae hivyohivyo kwa vile tu kwa mtizamo wako huko nje hakuna wanawake walio bora zaidi?Haya ndio yanayowaua watu kwa ukimwi.

Kumbuka kuwa uongozi wa TAIFA LETU sio divine right ya CCM pekee.Kumsifia Kikwete kuwa ni bora kwa vile tu wenzake huko CCM ni wachafu,au hakuna aliye bora zaidi yake,ni ufinyu wa mawazo.

I would say kuna watu kama Dr Slaa ambao at least wametuonyesha nini maana ya kiongozi kuwa na uchungu na nchi.



Na kwa akili yako iliyo timamu ukishakuwa na barabara nzuri hapo Dar wakati wakulima huko mahenge wanasumbuana na kivuko feki unatarajia hayo mazao yanafikaje bandarini Dar?Eti infrastructural economics!Yaani barabara za lami mijini zimekusahaulisha kabisa adha ya watanzania wenzako wanayipata huko reli ya kati na Tazara?Vipi kuhusu ATC?

Ni ulevi wa kifikra kuangalia upande mmoja wa "maendeleo" na kupuuza upande mwingine.Tegemeo la uchumi wa Tanzania ni katika kilimo,na kama unafuatilia mijadala ya bunge vizuri utakumbuka kwanini bajeti ya WIzara ya Miundombinu iliwekewa ngumu katika kikao cha bajeti kilichopita.Fuatilia hilo kisha ufanye review ya hoja yako dhaifu.

Of course,kutawala nchi sio sawa na kuongoza nyumba ndio maana hatutaki kiongozi dhaifu ang'anganie kuongoza wakati ameshindwa hata kumudu nidhamu ya baraza lake "dogo" la mawaziri waziofika 60.Kama hawezi kuwamudu hao "wachache" alowateua ataweza kumudu kuwatumikia watanzania zaidi ya milioni 40?



Unavyoongea kuwa ameingia na kukuta madudu inasomeka kana kwamba ALILAZIMISHWA KUINGIA MADARAKANI.Dont tell me kuwa hakujua madudu yalokuwepo before hajaingia madarakani because HE WAS PART YA MADUDU ALIYOYAKUTA ALIPOINGIA MADARAKANI.Kwa kumbukumbu zako,JK alianza kushika madaraka ya kitaifa lini?Mwaka 2006?Alikuwa anafahamu fika uzito wa jukumu analolipokea na akatuahidi kutupatia ufumbuzi.

Halafu baadhi ya kauli zako ni kama za KUJIPENDEKEZA.Mbona sijamsikia JK mwenyewe akisema kuwa CHANZO CHA MATATIZO YALIYOPO NI WATANGULIZI WAKE?

I like this dialogue. Mlalahoi, nadhani sasa unakea kuwa mlalahai. keep it up
 
Mlalahoi nimekupa thanks watu wanakuja na cheap politics eti JK ameleta freedom of speech eti utawala bora sijui upi wa kutowapeleka wezi wa EPA mahakamani utawala bora wa kuingia mikataba mibovu utawala bora wakuuza Migodi yetu kwa bei chee wa kuuza fukwe zetu wa kuuza Kigamboni

mmekazania freedom of speech mnasahau nchi ina uzwa jamani acheni utani wakati mwingine tuwe serious wakati wa Mkapa tulikuwa wa tano kwa umasikini duniani sasa ni wa pili toka mwisho bado tunang'ang'ania eti freedom of speech imekua wakati tunalipa mamilion kila siku kwa mikataba fake kama ya IPTL big up Mlalahoi
 
Back
Top Bottom