Rais Kikwete kweli ni Jembe

Na katika ishara nyingine kuwa yeye ni jembe ni uhuru mkubwa na usio na mipaka wa kutoa maoni. Sasa hivi kila mtu anaongea kwa uwazi na uhuru tofauti na serikali zote zilizopita. Ingekuwa wakati wa Mwalimu kwa uhuru huu wakuongea hivi sasa, watu wangekuwa wameisha wekwa kizuizini
 

kweli ni historia rais aliyeingia madarakani kwa rushwa(epa)
akafadhili rushwa(richmond,dowans)
akawatetea wala rushwa(kagoda na kumrudisha Menji Mang'ula wajipange kwa wizi chaguzi zijazo)
Akiwa mwenyekiti akaachia rushwa itawale kwenye chaguzi zake(mwenye vyombo vya kulalamika bila kuchukua hatua)
kavifungia vyombo vinavyoanika uozo wake(mwanahalisi)
kuua na kujaribu kuua watetezi wa haki za binadamu wa makundi jamii(Mwangosi,Ulimboka)
kwa hayo machache kwa nini jk asiwe history hapa tz?
 
Vilevile mpaka sasa kunamiradi mbali mbali nchini inayoendele chini ya uongozi uliotukuka wa JK. Pia kumbuka tanzania imewekwa kuwa mwenyekiti wa SADC katika mambo ya siasa na ulizi. Vilevile kipindi cha JK hata JKT imerudishwa kwa nguvu ili kuwajengea vijana uzalendo.

Nchi nyingi sana Africa hata asia na ulaya zinatamani sana uongozi wa kikwete.
JK ndiye aliyeruhusu mabadiliko ya katiba.
Hivi hamuyaoni hayo yote?
 
rais jembe ni yule ambaye anayatekeleza yale ambayo ameya ahidi kwa wananchiwake but jk akili yake yote imehamia chini na kusababisha chama ikawa nyufa zisizozibika hata angefanyeje,
Anaongoza nchi kwa udini, uswaiba, ubinafsi, ufisadi uliokithiri bila kujali maslahi ya wananchi waliompatia ridhaa ya kuwa kiongozi wa nchi
wew mleta mada akili yako imehamia chini kama ya jk
 
Kuna uzi m1 unazungumzia mikataba ya madini Botwana ulivyo, kama vp mleta mada usome kwanza alafu utapata tofauti ya jembe na .......
 
mtuhumiwa wa kutengeneza ARV fake naye ni jembe pia sababu ana cheo kwenye chama kinachojali wadanganyika
 

Aminia mkuu, ujinga wa asilimia kubwa ya watz ndiyo unamfanya awe jembe
 
Tatizo kubwa la watanzania ni moja, mnaona utawala mbuvu wa Kikwete unawaathiri CDM huwa haturikiri kuhusu sisi kama wananchi tunaathirika vipi bali tunafikiri kama wapinzani wanaathirika vipi, Kikwete ni rais wa Tz na siyo CDM. Na mafanikio yeyote ni kwaajili yetu waTZ na siyo CDM.
Tunaweza fikiri zaidi ya hapa wajemane
 

Ndugu yangu, suala la Rushwa si rahisi kama CHADEMA wanavyolizungumzia. Kiongozi mpya (Katibu wa chama) wa chama cha KIKOMUNISTI CHA CHINA katika hotuiba yake amelieleza tatizo la rushwa ndani ya chama kama changamoto kubwa iliyopo kwa chama sasa hivi.

Kumbuka kama kuna nchi unapata adhabu ya kifo kwa viongozi wa juu wanapokutikana na hatia hiyo duniani, ni CHINA. Lakini tatizo bado ni pevu. Hili ni tatizo zito na wala si la kutatuliwa kwa mwaka wala miaka mitano.

La msingi ni kulikubali tatizo na kuwa na dhamira ya kulitokomeza.
 
Asungwilmwaifungaaaaaaaa,
ninamaanisha ninachokisema. Nashukuru hata Mbowe aliwahi kusema hayahaya
tena mbele ya J.K hamkumtukana. Kwakuwa nimeyasema mie basi
mwanishushia mitusi ya kila aina. Matusi yanawaponzeni daily.

Hakika JK kaifanyia makubwa nchi, japo amekuwa dhaifu kwa kuwapa uhuru wa kupitiliza wapinzani wake hususan CDM
 

unatumia akili za kuazima wewe hata kama ni kipofu waulize wenzako maendeleo yaliyofanywa
 
Kama ni Jembe kwa nini hakuwalima walioufanya mradi wa gesi kukwama kwa miaka mingi huku akiwajua kuwa waliukwamisha makusudi , hivi leo hii wamekufa ndio maana akawataja kwa mabano kwamba ana vimemo vingi vya makatibu na mawaziri kukwamisha miradi mbalimbali
 



Hapo umechinja kabisa!!!!!. Watu hawataki kukubali ukweli J.K atachukua Mo. Ibrahim na chadomo watabaki kusema aaa eee. Sijawahi ona rais makini ktk kushughulikia issues za taifa kama J.K. Viva rais kichwa Mungu yu pamoja nawe hakika.
 
JK si jembe bali kijiko au hata koleo la mafisadi kuchotea utajiri wetu. Kumuita jembe ni kumuonea na kulionea jembe. Hana ujembe kitu bali ukijiko, umrija na ukoleo wa kutumalizia mali.
 
Wanachedema bana wanamambo ya kikatuni sana.

Mtu akishawazidi hoja wakiona hawana cha kujibu wanaanza kuhesabu idadi ya Posts zake na amejiunga lini.

What has the number of posts got to do with the content ?

Jipangeni mjibu hoja hatutaki vioja
 
wanachedema bana wanamambo ya kikatuni sana.

Mtu akishawazidi hoja wakiona hawana cha kujibu wanaanza kuhesabu idadi ya posts zake na amejiunga lini.

What has the number of posts got to do with the content ?

Jipangeni mjibu hoja hatutaki vioja



umeona eeeeh
wengine miaka nenda rudi wamekua wanaifuatilia jamii forum as guests mfano mimi
na sio kama najisifia,,nina siku kadhaa tuh humu ndani tokea nijisajiri kama member lakini criticisms kibao,,sijajua wanatumia vigezo gani kumfanya maundumula awe jf senior expert member na mwingne member wa kawaida,sijui ni idadi ya posts?au wanapima iq na uelewa wa member fulani moderators ndio wanajua zaid,,ila ni vema mtu akapimwa kwa uelewa wake na busara zake
 

akina EL,CHENGE hawakupitia jkt wakawa wazalendo.Mizee yote mifisadi imepitia jkt,tunataka maisha bora hela ya kuwapa wanachuo taabu mtamudu jkt.poor STRATEGIES
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…