Rais Kikwete ateua Wakuu wa Wilaya, wengine waenguliwa kutoka kwenye nafasi zao

Dotto Mnzava

R I P
Mar 6, 2014
865
427
Kupitia ITV na Radio One hivi sasa wanasema Rais Jakaya Kikwete, amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya Wapya nchini na kuwaengua wengine katika nafasi zao.

Majina ya Wakuu hao wa Wilaya imetajwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

============= Updates ============
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

RAIS KIKWETE ATEUA WAKUU WA WILAYA WAPYA 27
*Atengua uteuzi wa Ma-DC 12, awabadilisha vituo 64, awabakiza 42 kwenye vituo vyao vya zamani

RAIS Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya Wakuu wa Wilaya kwa kuwateua Wakuu wapya 27, kuwahamisha vituo vya kazi 64 na wengine 42 amewabakisha kwenye vituo vyao vya kazi vya zamani.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa OWM TAMISEMI leo mchana (Jumatano, Februari 18, 2015) Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema mabadiliko hayo yamesababishwa na kuwepo kwa nafasi wazi 27 ambazo zilitokana na wakuu wa wilaya watatu kufariki dunia; kupandishwa cheo wakuu wa wilaya watano, kupangiwa majukumu mengine wakuu wa wilaya saba na kutenguliwa kwa uteuzi wa wakuu wa wilaya 12.

Hata hivyo, Waziri Mkuu alisema, Rais Kikwete amewabadilisha vituo vya kazi wakuu wa wilaya 64 na kuwabakiza kwenye vituo vyao vya zamani wakuu wa wilaya 42.

Wakuu wa Wilaya wapya 27 walioteuliwa ni Mariam Ramadhani Mtima anayeenda Ruangwa; Dk. Jasmine B. Tiisike anayeenda Mpwapwa; Pololeti Mgema (Nachingwea); Fadhili Nkurlu anayeenda Misenyi; Felix Jackson Lyaniva anayeenda Rorya na Fredrick Wilfred Mwakalebela anayeenda wilayaya Wanging'ombe.

Wengine na vituo vyao kwenye mabano ni Zainab Rajab Mbussi (Rungwe); Francis K. Mwonga (Bahi); Kanali Kimiang'ombe Samwel Nzoka (Kiteto), Husna Rajab Msangi (Handeni), Emmanuel J. Uhaula (Tandahimba); Mboni Mhita (Mufindi); Hashim S. Mgandilwa (Ngorongoro); Mariam M. Juma (Lushoto); Thea Medard Ntara (Kyela); Ahmad H. Nammohe (Mbozi); Shaban Kissu (Kondoa) na Stephen Zelothe (Musoma).

Wengine ni Pili Moshi (Kwimba); Mahmoud A. Kambona (Simanjiro); Glorius B. Luoga (Tarime); Zainab R. Telack (Sengerema); Bernard Nduta (Masasi); Zuhura Mustafa Ally (Uyui); Paulo Makonda (Kinondoni); Mwajuma Nyiruka (Misungwi) na na Maftah Ally Mohamed (Serengeti).

Wakuu wa Wilaya saba ambao uteuzi wao umetenguliwa lakini watapangiwa kazi nyingine ni Brig. Jenerali Cosmas Kayombo aliyekuwa Simanjiro; Kanali Ngemela E. Lubinga (aliyekuwa Mlele); Juma S. Madaha (aliyekuwa Ludewa); Mercy E. Silla (aliyekuwa Mkuranga); Ahmed R. Kipozi (aliyekuwa Bagamoyo); Mrisho Gambo (aliyekuwa Korogwe) na Elinas A. Pallangyo (aliyekuwa Rombo).

Waziri Mkuu pia aliwataja Wakuu wa Wilaya 12 ambao uteuzi wao umetenguliwa kutokana na sababu za umri, kiafya na kuimarisha utendaji Serikaini na wilaya zao kwenye mabano kuwa ni James K. Ole Millya (Longido); Elias Wawa Lali (Ngorongoro); Alfred Ernest Msovella (Kongwa); Danhi Beatus Makanga (Kasulu); Fatma Losindilo Kimario (Kisarawe); Elibariki E. Kingu (Igunga); Dk. Leticia Moses Warioba (Iringa); Evarista N. Kalalu (Mufindi); Abihudi M. Saideya (Momba); Martha J. Umbulla (Kiteto); Khalid J. Mandia (Babati) na Elias Goroi (Rorya).

(mwisho)

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,

S. L. P. 980,

DODOMA.

JUMATANO, FEBRUARI 18, 2015.


==================

Orodha nzima ya wakuu wa Wilaya Soma Hapa Chini
;

Wakuu wa Wilaya waliofariki dunia

NA JINA WILAYA
1. Capt.(mst)JamesC.Yamungu Serengeti
2. AnnaJ.Magoha Urambo
3 MoshiM.Chang'a Kalambo

Wakuu wa Wilaya
walio pandishwa cheo

Wakuu wa Wilaya wafuatao wamepandishwa cheo kuwa Wakuu wa Mikoa

NA JINA WILAYA MKOAALIOPANGIWA
1. JohnVianneyMongela Arusha Kagera
2. AminaJumaMasenza Ilemela Iringa
3 Dkt.IbrahimHamisMsengi Moshi Katavi
4 HalimaOmariDendego Tanga Mtwara
5 DaudiFelixNtibenda Karatu Arusha

Wakuu wa Wilaya waliopangiwa majukumu mengine

Wakuu wa Wilaya ambao uteuzi wao umetenguliwa na watapangiwa kazi nyingine ni hawa wafuatao;

NA. JINA WILAYA
1 Brig.GeneralCosmasKayombo Simanjiro
2 Col.NgemelaElsonLubinga Mlele
3 JumaSolomonMadaha Ludewa
4 MercyEmanuelSilla Mkuranga
5 AhmedRamadhanKipozi Bagamoyo
6 MrishoGambo Korogwe
7. ElinasAnaelPallangyo Rombo

Wakuu wa Wilaya Wanaotenguliwa

Wakuu wa Wilaya ambao uteuzi wao umetenguliwa kutokana na sababu za umri, kiafya na nyinginezo na vituo vyao ni kama inavyoonekana hapa chini:

NA JINA WILAYA
1. JamesKisotaOleMillya Longido
2. EliasWawaLali Ngorongoro
3. AlfredErnestMsovella Kongwa
4. DanyBeatusMakanga Kasulu
5. FatmaLosindiloKimario Kisarawe
6. ElibarikiEmanuelKingu Igunga
7. Dr.LeticiaMosesWarioba Iringa
8 EvaristaNjilokiroKalalu Mufindi
9. AbihudiMsimediSaideya Momba
10. MarthaJachiUmbula Kiteto
11 KhalidJumaMandia Babati
12 EliasiGoroiBoeBoeGoroi Rorya

Wakuu wa Wilaya wapya walioteuliwa

Wakuu wa Wilaya wapya walioteuliwa na Wilaya zao niwafuatao;
NA. JINA JINSI WILAYA
1. MariamRamadhaniMtima KE Ruangwa
2. Dkt.JasmineB.Tiisike KE Mpwapwa
3. PololetiMgema ME Nachingwea

NA. JINA JINSI WILAYA
4. FadhiliNkurlu ME Misenyi
5. FelixJacksonLyaniva ME Rorya
6. FredrickWilfredMwakalebela ME Wanging'ombe
7. ZainabRajabMbussi KE Rungwe
8. FrancisK.Mwonga ME Bahi
9. Col.Kimiang'ombeSamwel
Nzoka
ME Kiteto
10. HusnaRajabMsangi KE Handeni
11. EmmanuelJumanneUhaula ME Tandahimba
12. MboniMhita KE Mufindi
13. HashimS.Mngandilwa ME Ngorongoro
14. MariamM.Juma KE Lushoto
15. TheaMedardNtara KE Kyela
16. AhmadH.Nammohe ME Mbozi
17. ShabanKissu ME Kondoa
18. ZeloteStephen ME Musoma
19. PiliMoshi KE Kwimba
20. MahmoudA.Kambona ME Simanjiro
21. GloriusBernardLuoga ME Tarime
22. ZainabR.Telack KE Sengerema
23. BernardNduta ME Masasi
24. ZuhuraMustafaAlly KE Uyui
25. PauloMakonda ME Kinondoni

NA. JINA JINSI WILAYA
26. MwajumaNyiruka KE Misungwi
27. MaftahAllyMohamed ME Serengeti

Wakuu wa Wilaya waliobadilishwa Vituo

Wakuu wa Wilaya wafuatao wamebadilishwa vituo vya kazi kama ifuatavyo;
NA JINA JINSIAWILAYA
ATOKAYO
WILAYA
AENDAYO
1. NyerembeDeusdeditMunasa ME Arumeru Mbeya
2 JordanMungireObadiaRugimbana ME Kinondoni Morogoro
3 FatmaSalumAlly KE Chamwino Mtwara
4 LephyBenjaminiGembe ME DodomaMjini Kilombero
5 ChristopherRyobaKangoye ME Mpwapwa Arusha
6 OmarShabanKwaang' ME Kondoa Karatu
7 FrancisIsackMtinga ME Chemba Muleba
8 ElizabethChalamilaMkwasa KE Bahi Dodoma
9 AgnesEliasHokororo(Mb) KE Ruangwa Namtumbo
10 ReginaReginaldChonjo KE Nachingwea Pangani
11 HusnaMwilima KE Mbogwe Arumeru
12 GeraldJohnGuninita ME Kilolo Kasulu
13 BiZipporahLyonPangani KE Bukoba Igunga
14 Col.IssaSuleimaniNjiku ME Missenyi Mlele

NA JINA JINSIA WILAYA
16 Bw.RichardMbeho ME Biharamulo Momba
17 Bw.LembrisMarangushiKipuyo ME Muleba Rombo
18 RamadhaniAthumanManeno ME Kigoma Chemba
19 VenanceMethusalahMwamoto ME Kibondo Kaliua
20 GishuliMbegesiCharles ME Buhigwe Ikungi
21 NovatusMakunga ME Hai Moshi
21 AnatoryKisaziChoya ME Mbulu Ludewa
22 ChristineSolomoniMndeme KE Hanang' Ulanga
23 JacksonWilliamMusome ME Musoma Bukoba
24 JohnBenedictHenjewele ME Tarime Kilosa
25 Dkt.NormanAdamsonSigalla ME Mbeya Songea
26 Dr.MichaelYuniaKadeghe ME Mbozi Mbulu
27 CrispinTheobaldMeela ME Rungwe Babati
28 MagrethEsterMalenga KE Kyela Nyasa
29 SaidAliAmanzi ME Morogoro Singida
30 AntonyJohnMtaka ME Mvomero Hai
31 EliasChoroJohnTarimo ME Kilosa Biharamulo
32 FrancisCryspinMiti ME Ulanga Hanang'
33 HassanEliasMasala ME Kilombero Kibondo

NA JINA JINSIA WILAYA
34 AngelinaLubaloMabula KE Butiama Iringa
35 FaridaSalumMgomi KE Masasi Chamwino
36 WilmanKapenjamaNdile ME Mtwara Kalambo
37 PonsianDamianoNyami ME Tandahimba Bariadi
38 MariamSefuLugaila KE Misungwi Mbogwe
39 MaryTeshaOnesmo KE Ukerewe Buhigwe
40 KarenKemilembeYunus KE Sengerema Magu
41 JosephineRabbyMatiro KE Makete Shinyanga
42 JosephJosephMkirikiti ME Songea Ukerewe
43 AbdulaSuleimanLutavi ME Namtumbo Tanga
44 ErnestNg'wendaKahindi ME Nyasa Longido
45 AnnaRoseNdayishimaNyamubi KE Shinyanga Butiama
46 RosemaryKashindiKirigini
(Mb)
KE Meatu Maswa
47 AbdallahAliKihato ME Maswa Mkuranga
48 ErastoYohanaSima ME Bariadi Meatu
49 QueenMwanshingaMulozi KE Singida Urambo
50 YahyaEsmailNawanda ME Iramba Lindi
51 ManjuSalumMsambya ME Ikungi Ilemela
52 SaveliMangasaneMaketta ME Kaliua Kigoma
53 BituniAbdulrahmanMsangi KE Nzega Kongwa
54 LucyThomasMayenga KE Uyui Iramba

NA JINA JINSIA WILAYA
55 MajidHemedMwanga ME Lushoto Bagamoyo
56 MuhingoRweyemamu ME Handeni Makete
57 HafsaMahinyaMtasiwa KE Pangani Korogwe
58 Dr.NasoroAliHamidi ME Lindi Mafia
59 FestoShemuKiswaga ME Nanyumbu Mvomero
60 SaudaSalumMtondoo KE Mafia Nanyumbu
61 SelemanMzeeSeleman ME Kwimba Kilolo
62 EsterinaJulioKilasi KE Wanging'o
mbe
Muheza
63 SubiraHamisMgalu KE Muheza Kisarawe
64 JacquelineJonathanLiana KE Magu Nzega

Wakuu wa Wilaya wanaobaki katika vituo vyao vya sasa

Wakuu wa Wilaya wafuatao wanaendelea kubaki katika vituo vyao vya sasa;
NA JINA JINSIA WILAYA
1 JowikaWilsonKasunga ME Monduli
2 RaymondHieronimiMushi ME Ilala
3 SophiaEdwardMjema KE Temeke
4 Bw.AmaniKiungaduaMwenegoha ME Bukombe
5 Bw.IbrahimWankangaMarwa ME Nyang'wale
6 Bw.RodrickLazaroMpogolo ME Chato
7 Bw.ManzieOmarMangochie ME Geita
8 Bi.DarryIbrahimRwegasira KE Karagwe
9 Lt.Col.BenedictKulikilaKitenga ME Kyerwa
10 ConstantineJohnKanyasu ME Ngara
11 PazaTusamaleMwamulima ME Mpanda
12 PeterToimaKiroya ME Kakonko
13 HadijaRashidNyembo KE Uvinza
14 Dkt.CharlesO.Mlingwa ME Siha
15 ShaibuIssaNdemanga ME Mwanga
16 HermanClementKapufi ME Same
17 EphraimMfingiMbaga ME Liwale
18 AbdallahHamisUlega ME Kilwa
19 JoshuaChachaMirumbe ME Bunda
20 DeodatusLucasKinawiro ME Chunya
21 RosemaryStakiSenyamule KE Ileje
22 GulamhuseinKifuShaban ME Mbarali
23 ChristopherEdwardMagala ME Newala
24 BarakaMbikeKonisaga ME Nyamagana
25 SarahPhilipDumba KE Njombe
26 HanifaMahmoudKaramagi KE Gairo
27 HalimaMezaKihemba KE Kibaha
28 NurdinBabu ME Rufiji
29 MathewSarjaSedoyeka ME Sumbawanga
30 IddHassanKimanta ME Nkasi
31 ChandeBakariNalicho ME Tunduru
32 BibiSenyiSimonNgaga KE Mbinga
33 WilsonElishaNkambaku ME Kishapu
34 BensonMwailugulaMpesya ME Kahama
35 PaulChrisantMzindakaya ME Busega
36 GeorginaEliasBundala KE Itilima
37 FatumaHassanToufiq KE Manyoni
38 Lt.EdwardOleLenga ME Mkalama
39 HanifaMohamedSelengu KE Sikonge
40 SulemanOmarKumchaya ME Tabora
41 MboniMwanahamisMgaza KE Mkinga
42 SelemanSalumLiwowa ME Kilindi

Mabadiliko haya yameanza tarehe 18.02.2015 na ninawatakia wote utendaji kazi mahiri.


Mizengo K. P. Pinda
18.02.2015
WAZIRI MKUU
 
Kupitia ITV na Radio One hivi sasa wanasema Rais Jakaya Kikwete, amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya Wapya nchini na kuwaengua wengine katika nafasi zao.

Majina ya Wakuu hao wa Wilaya imetajwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Taarifa zaidi inakujia hivi punde.

Tatizo Mkuu una haraka sana ulishindwa nini kuyasubiri bhana haya sasa katatafute utuletee
 
W. Mkuu Mizengo Peter Pinda, kwa niaba ya J. K leo ametangaza majina ya wakuu wa wilaya wapya!

Katika mabadiliko hayo ya Dodoma leo, Paul Makonda ameteuliwa kuwa DC wa Kinondoni, Dsm!

Kuweka kumbu kumbu sawa, huyu ndiye yule Kijana aliehusika ktk purukushani iliomdhalilisha Mzee Warioba pale Ubungo Plaza, Dsm ktk mjadala wa Katiba pendekezwa!
 
Wapya wamo: Makonda, Mwakalebela na Kisu
Wengine wamehamishwa vituo na wengine wameondolewa kabisa!
 
Siasa za tanzania ni nyepesi sana Kumbe ka makonda na kelele zake zote na kumzalilisha mzee warioba ni ka ukuu wa wilaya alikuwa anapambania Sasa ngoja mamvi anakuja tuone kama hatokuwa mkimbizi!
 
Wapya wamo: Makonda, Mwakalebela na Kisu
Wengine wamehamishwa vituo na wengine wameondolewa kabisa!

Huu ndio muda wa kupeana vyeo,vyeo siku hizi watawala hawaangalii utendaji wa mtu wanaangalia urafiki
 
Leteni taarifa kutoka kwa SALVA hebu mfuateni hapo magogoni awape taarifa rasmi
 
Kuna mtangazaji mmoja ambaye amajadiliwa nadhani kuzidi wote hapa jf na inasemekana amekuwa akiunyemelea UDC.
Siwezi kuapa lakini jina lake likiwemo kati ya wazawadiwaji natafikiria kuhama nchi kwa muda!.
Mambo ya 'gheto'!
 
Back
Top Bottom