appriciator
JF-Expert Member
- Aug 28, 2013
- 276
- 46
Rais Kikwete baada ya kupokea malalamiko juu ya ajira kwa wageni kutoka TUCTA Mheshimiwa Rais katika hotuba yake ya Mei mosi alitangaza nia yake ya kupeleka mswada bungeni ili kubadilisha sheria ili mamlaka ya utoaji vibali kwa wageni viwe vinatolewa na mamlaka moja badala ya ilivyo sasa. Kwa maana hii amedhamiria vibali vitolewe ama na Idara ya kazi au Idara ya Uhamiaji pekee.
Ikumbukwe hivi sasa maombi ya ajira kwa wageni yanatipishwa kwa kushirikiana na pande zote mbili, yaani maombi yanaanzia Ofisi ya Kazi kisha vibali vinamalizikia kutolewa na Ofisi ya Uhamiaji. Kwa maana nyingine Uhamiaji hawawezi kutoa kibali bila ya Ofisi ya Kazi kupitisha. Hivyo ni wazi moja yati ya Idara hizi kutokana ubinafsi na tamaa imejenga ushawishi ili itoe vibali peke yake. Mheshimiwa Rais akiingia kwenye mtego huu na akikubali vibali kutolewa na Idara moja atakuwa anafanya makosa makubwa sana.
Kwa vile kila Ofisi yati ya hizi ofisi mbili ina umuhimu wake, kwa upande wa Idara ya kazi ni wataalamu wa ajira na Uhamiaji ni chombo cha Ulinzi na Usalama katika masuala ya wageni wana mfumo wa kuwatambua wageni wakorofi nchini na duniani.
Mheshimiwa Rais kabla ya kufikia tamati ya uamuzi wa kufanya mabadiliko anapaswa kutafakari yafuatayo:-
1. Kama tatizo ni kupewa vibali wageni wasiyostahili je tatizo liko wapi wakati Ofisi zote mbili wanashughulikia kupitisha maombi ya hivyo vibali.
2. Je matatizo ya ajira kwa wageni malalamiko yanalingana na ukubwa wa tatizo au ni tabia tu ya watanzania kulalamika hata kwa tatizo dogo? Ikumbukwe nchi hii ina Raia wengi wenye asili ya kihindi hivyo isichukuliwe kuwa kila mhindi ni mgeni.
3. Je kuna wageni wangapi waliopewa vibali ambao wanakosa sifa ya kuajiriwa?
4. Je kama Tanzania kuna uholela wa kupewa vibali mbona nchi zingine za EAC wanatulalamikia kwa kubana utuaji wa vibali?
5. Ili tusiwe kituko. Je nchi nyingine dunia vibali vya kazi kwa wageni vinatolewa na mamlaka gani?
6. Kwa upande wa Usalama wa kudhibiti wageni hali ya Tanzania ikoje kulinganisha na nchi jirani?
7. Tusiingie kwenye mkoroganyo kama ulizikumba Sekta za Elimu, Kilimo na Serikali za Mitaa uliotokana na mabadiliko yaliyokuwa akifanywa bila kufanya utafiti wa kutosha na matokeo yake kuwa kero zaidi na kushindwa kupiga hatua.
Nimeona Mheshimiwa Rais nije na ushauri huu kwa vile nina uzoefu kwa kiasi fulani na suala la vibali vya ajira kwa wageni, tulishawahi kuzifanya shughuli hizi na Mheshimiwa William Ngereja tukiwa katika makampuni tofauti za ushauri consultancy wakati huo kabla hajawa Mbunge wala Waziri hivyo ni vyema pia ukamwita Mheshimiwa Ngereja anajua sana juu ya utendaji wa Ofisi hizi jinsi zinavyoshughulikia maombi ya ajira kwa wageni adhani atakupa ushauri mzuri. Namshauri Mheshimiwa Rais afanye subira akutane na watendaji na wataalamu kisha ili aweze kulitambua tatizo kwa undani zaidi kwa kuangalia pande zote mbili za shilingi.
Ikumbukwe hivi sasa maombi ya ajira kwa wageni yanatipishwa kwa kushirikiana na pande zote mbili, yaani maombi yanaanzia Ofisi ya Kazi kisha vibali vinamalizikia kutolewa na Ofisi ya Uhamiaji. Kwa maana nyingine Uhamiaji hawawezi kutoa kibali bila ya Ofisi ya Kazi kupitisha. Hivyo ni wazi moja yati ya Idara hizi kutokana ubinafsi na tamaa imejenga ushawishi ili itoe vibali peke yake. Mheshimiwa Rais akiingia kwenye mtego huu na akikubali vibali kutolewa na Idara moja atakuwa anafanya makosa makubwa sana.
Kwa vile kila Ofisi yati ya hizi ofisi mbili ina umuhimu wake, kwa upande wa Idara ya kazi ni wataalamu wa ajira na Uhamiaji ni chombo cha Ulinzi na Usalama katika masuala ya wageni wana mfumo wa kuwatambua wageni wakorofi nchini na duniani.
Mheshimiwa Rais kabla ya kufikia tamati ya uamuzi wa kufanya mabadiliko anapaswa kutafakari yafuatayo:-
1. Kama tatizo ni kupewa vibali wageni wasiyostahili je tatizo liko wapi wakati Ofisi zote mbili wanashughulikia kupitisha maombi ya hivyo vibali.
2. Je matatizo ya ajira kwa wageni malalamiko yanalingana na ukubwa wa tatizo au ni tabia tu ya watanzania kulalamika hata kwa tatizo dogo? Ikumbukwe nchi hii ina Raia wengi wenye asili ya kihindi hivyo isichukuliwe kuwa kila mhindi ni mgeni.
3. Je kuna wageni wangapi waliopewa vibali ambao wanakosa sifa ya kuajiriwa?
4. Je kama Tanzania kuna uholela wa kupewa vibali mbona nchi zingine za EAC wanatulalamikia kwa kubana utuaji wa vibali?
5. Ili tusiwe kituko. Je nchi nyingine dunia vibali vya kazi kwa wageni vinatolewa na mamlaka gani?
6. Kwa upande wa Usalama wa kudhibiti wageni hali ya Tanzania ikoje kulinganisha na nchi jirani?
7. Tusiingie kwenye mkoroganyo kama ulizikumba Sekta za Elimu, Kilimo na Serikali za Mitaa uliotokana na mabadiliko yaliyokuwa akifanywa bila kufanya utafiti wa kutosha na matokeo yake kuwa kero zaidi na kushindwa kupiga hatua.
Nimeona Mheshimiwa Rais nije na ushauri huu kwa vile nina uzoefu kwa kiasi fulani na suala la vibali vya ajira kwa wageni, tulishawahi kuzifanya shughuli hizi na Mheshimiwa William Ngereja tukiwa katika makampuni tofauti za ushauri consultancy wakati huo kabla hajawa Mbunge wala Waziri hivyo ni vyema pia ukamwita Mheshimiwa Ngereja anajua sana juu ya utendaji wa Ofisi hizi jinsi zinavyoshughulikia maombi ya ajira kwa wageni adhani atakupa ushauri mzuri. Namshauri Mheshimiwa Rais afanye subira akutane na watendaji na wataalamu kisha ili aweze kulitambua tatizo kwa undani zaidi kwa kuangalia pande zote mbili za shilingi.