Rais Kikwete anataka kuingizwa mkenge

Rais Kikwete anataka kuingizwa mkenge

Mkuu kweli huoni tatizo kwa hawa wageni kuja kufanya kazi ambazo watanzania wengi wapo mtaani wanaumia na njaa wakati wangeweza kuwa walinzi? tuna wastaafu wa Polisi, JWTZ, Magereza, JKT, Vijana waliokosa shule kuendelea na masomo kweli hawafai kufanya kazi ambazo ni unskilled ambazo wageni wengi wanazifanya hapa Tz? Kweli wewe unaona sawa tu wageni wanaletwa kufanya kazi ya kutupokea mahotelini wakati vijana wa kitanzania waliosomea mambo ya Hoteli wakiwa wamekosa kazi na kuishia kuuza bia kwenye viji Bar vya uchochoroni? ..Ndugu yangu kwenye suala la uzalendo hata kwenye biblia wameandika.."walio ndugu wapewe kwanza"
Katika mada yangu soma nukta namba 1 na namba 3 nimeshauri iangaliwe hapo tatizo liko wapi? Iwapo Idara zote mbili zinahusika kupitisha maombi ya ajira kwa wageni kisha wanapatikana wageni wasiyostahili kupewa ajira hiyo. Cha kuangalia hapa kuangalia mianya ilipo na siyo kukimbilia kubadili sheria.
 
Ni muhimu sana kwa sheria kubainisha nafasi zinazotakiwa kushikwa na wageni inakuwaje organization inakuwa na directors na deputy wote wanakuwa kutoka nje ya nchi, chief accountants na wengineo wanakuwa wageni, Hr anakuwa mgeni yaani watz wanakuwa katika position za chini tu hii si nzuri kwa usalama wa nchi na hata kwa mstakabali wa vihana tunaowasomesha.
Tatizo siyo sheria zilizopo ni nzuri sana zinatetea ajira kwa watanzania na hata utaratibu pia ni mzuri ukilinganisha ni nchi za EAC. Utaratibu unataka yafuatayo:-
- Nafasi za kazi zitangazwe ndiyo hata yanapopelekwa maombi inatakiwa unambatanishe na ‘press cutting’ ya gazeti ulilotangaza hiyo ajira.
- Mwombaji awe na sifa ambayo mtanzania wa kawaida hana
- Mgeni wakati yuko nchini ahakikishe kuna mtanzania anaandaliwa kushika nafasi yake
Hivyo cha kufanya ni kuziba mianya ili ajira kwa mtanzania ilindwe.




 
Ni muhimu sana kwa sheria kubainisha nafasi zinazotakiwa kushikwa na wageni inakuwaje organization inakuwa na directors na deputy wote wanakuwa kutoka nje ya nchi, chief accountants na wengineo wanakuwa wageni, Hr anakuwa mgeni yaani watz wanakuwa katika position za chini tu hii si nzuri kwa usalama wa nchi na hata kwa mstakabali wa vihana tunaowasomesha.
Tatizo tukipewa nafasi tunafikiria kupiga hela tu
 
Sifa ya kazi siyo kisomo peke yake au uwezo wa kufanya kazi kitu kikubwa kinachofanya wafanyabiashara kuajiri wafanyakazi toka nje ya nchi ni uaminifu, kitu tunatakiwa tujenge tabia ya kuwa waaminifu watanzania ili kujenga imani na wafanya biashara. Mwekezaji anafungua Hoteli mtu anaajiriwa anajisikia ni haki yake kumwibia tajiri na wageni wanaofikia hotelini kwa kisingiziyo ugumu wa maisha, kufanya starehe zake au mshahara hautoshi, hayo pia yanafanyika katika maduka sasa kuna mfanya biashara atakubali kufanya biashara huku akipata hasara. Mpaka pale tutapokua tunaheshimu kazi zetu na kujenga tabia ya kuwa waaminifu wafanya biashara wakilazimishwa kuajiri wananchi watafunga biashara zao.Mbele ya macho yetu tunaona mtu anaajiri dereva wa Prado yake akimwachia gari peke yake kosa atapakia abiria hata watu kumi na tano kuwapeleka tandika na anarudi haraka, kwa kweli tutakuja fikia hata madereva watatoka nje, kwasababu watu hawana pesa lakini tamaa na starehe wameweka mbele kwahiyo wanatafuta pesa kwa njia yeyote.
 
Haina haja ya kuondoa urasimu kwa wageni. Tutakapoondoa urasimu kwa waheni maana yake unataka kutoa mwanya zaidi kwa wageni. Inabidi tutambue kuwa Tanzania ndiyo kuna kiwango kikubwa cha usalama kilinganisha na majirani zetu na hii inatokana na urasimu huohuo. Tuwe wazalendo mie naona utaratibu ulipo sasa wa utoaji wa permit kwa wageni unafaa uendelee kwa vile unafaa katika udhibiti

Sijui kama ulielewa kauli ya rais ililenga nini? alisema kwa kuwa wageni wamekuwa holela anataka udhibiti uongezeke ili wazawa walindwe...sijajua kama unataka kusema rais analenga kuondoa urasimu ili wawe wageni holela, mh rais alilenga katika kukazia iwe ngumu kwa wageni kuchukua ajira kiholela...sorry kama hatujaelewana!
 
Rais Kikwete baada ya kupokea malalamiko juu ya ajira kwa wageni kutoka TUCTA Mheshimiwa Rais katika hotuba yake ya Mei mosi alitangaza nia yake ya kupeleka mswada bungeni ili kubadilisha sheria ili mamlaka ya utoaji vibali kwa wageni viwe vinatolewa na mamlaka moja badala ya ilivyo sasa. Kwa maana hii amedhamiria vibali vitolewe ama na Idara ya kazi au Idara ya Uhamiaji pekee.

Ikumbukwe hivi sasa maombi ya ajira kwa wageni yanatipishwa kwa kushirikiana na pande zote mbili, yaani maombi yanaanzia Ofisi ya Kazi kisha vibali vinamalizikia kutolewa na Ofisi ya Uhamiaji. Kwa maana nyingine Uhamiaji hawawezi kutoa kibali bila ya Ofisi ya Kazi kupitisha. Hivyo ni wazi moja yati ya Idara hizi kutokana ubinafsi na tamaa imejenga ushawishi ili itoe vibali peke yake. Mheshimiwa Rais akiingia kwenye mtego huu na akikubali vibali kutolewa na Idara moja atakuwa anafanya makosa makubwa sana.

Kwa vile kila Ofisi yati ya hizi ofisi mbili ina umuhimu wake, kwa upande wa Idara ya kazi ni wataalamu wa ajira na Uhamiaji ni chombo cha Ulinzi na Usalama katika masuala ya wageni wana mfumo wa kuwatambua wageni wakorofi nchini na duniani.

Mheshimiwa Rais kabla ya kufikia tamati ya uamuzi wa kufanya mabadiliko anapaswa kutafakari yafuatayo:-
1. Kama tatizo ni kupewa vibali wageni wasiyostahili je tatizo liko wapi wakati Ofisi zote mbili wanashughulikia kupitisha maombi ya hivyo vibali.
2. Je matatizo ya ajira kwa wageni malalamiko yanalingana na ukubwa wa tatizo au ni tabia tu ya watanzania kulalamika hata kwa tatizo dogo? Ikumbukwe nchi hii ina Raia wengi wenye asili ya kihindi hivyo isichukuliwe kuwa kila mhindi ni mgeni.
3. Je kuna wageni wangapi waliopewa vibali ambao wanakosa sifa ya kuajiriwa?
4. Je kama Tanzania kuna uholela wa kupewa vibali mbona nchi zingine za EAC wanatulalamikia kwa kubana utuaji wa vibali?
5. Ili tusiwe kituko. Je nchi nyingine dunia vibali vya kazi kwa wageni vinatolewa na mamlaka gani?
6. Kwa upande wa Usalama wa kudhibiti wageni hali ya Tanzania ikoje kulinganisha na nchi jirani?
7. Tusiingie kwenye mkoroganyo kama ulizikumba Sekta za Elimu, Kilimo na Serikali za Mitaa uliotokana na mabadiliko yaliyokuwa akifanywa bila kufanya utafiti wa kutosha na matokeo yake kuwa kero zaidi na kushindwa kupiga hatua.

Nimeona Mheshimiwa Rais nije na ushauri huu kwa vile nina uzoefu kwa kiasi fulani na suala la vibali vya ajira kwa wageni, tulishawahi kuzifanya shughuli hizi na Mheshimiwa William Ngereja tukiwa katika makampuni tofauti za ushauri consultancy wakati huo kabla hajawa Mbunge wala Waziri hivyo ni vyema pia ukamwita Mheshimiwa Ngereja anajua sana juu ya utendaji wa Ofisi hizi jinsi zinavyoshughulikia maombi ya ajira kwa wageni adhani atakupa ushauri mzuri. Namshauri Mheshimiwa Rais afanye subira akutane na watendaji na wataalamu kisha ili aweze kulitambua tatizo kwa undani zaidi kwa kuangalia pande zote mbili za shilingi.


Ndugu yangu appritiator kwa uandishi wako inadhihirisha wazi wewe ni mmoja wa watu wanaofaidika binafsi na mkanganyiko wa kisheria uliopo katika kusimamia vibali vya kazi vya wageni hapa nchi. Mfumo uliopo unaruhusu taasisi na Sheria zaidi ya moja kutoa vibali vya ajirakwa wageni hali ambayo ni hatari kwa mustakabali ya taifa letu hususan ajira kwa vijana. NI WAZI HUNGEPENDELEA YATOKEE MABORESHO KATIKA MKANGANYIKO HUO WA KISHERIA KWA KUWA UTAKUWEKA KANDO KATIKA UTOAJI WA VIBALI VYA AJIRA KWA WAGENI. Unavyojaribu kuelezea ni kana kwamba Rais Kikwete alikurupuka katika kalitolea ufafanuzi suala hili na kulitolea mwelekeo. Nikupe taarifa tuu ni kwamba suala hili limepitishwa katika vikao vingi vya maamuzi kabla ya kumfikia Mweshimiwa Rais.

Nikuulize swali moja, ni nchi gani katika dunia hii kuwa Resident permit ni sawa na Work permit. Ni wapi dunia, ni Tanzania pekeyake . Na wewe ndugu yangu inataka mfumo huu uendelee kwa kuwa unafaidika nao. Mfumo mbovu wa kisheria wa kumruhusu Kamishina na Uhamiaji aendelee kutoa vibali vya ajira badala ya yeye kutoa vibali vya ukaazi. Utoaji wa vibali vya ukaazi ndiyo kazi yake. Hii ndiyo kazi yake na ndiyo kazi iliyokasimiwa Wizara ya Mambo ya Ndani (Instrument ya Rais). Kamishina wa Uhamiaji kwa sasa inagawa vibali vya kazi tena vya muda (CTA) kwa wageni bila hata kuzingatia Sheria. Niambie CTA zinatolewa kwa Sheria ipi. Ni nyie kina Appritiator ndio mko nyuma ya uhaini huu kwa kugawa vibali vya ajira vya muda kama njugu baada ya kupokea hongo kutoka kwa wageni hao bila hata kujali ni vijana wangapi wa nchi hii mnawanyima ajira. Suala hili ni la kihaini na hatua za kisheria zitafuata mkondo wake.

Ndugu yangu Apritiator sheria hiyo mpya inalenga kuweka mipaka kati ya vibali vya ajira (Work Permit) na Vibali vya Ukaazi (Resident Permit) Kwa utaratibu huu kila Taasisi itawajibika ipasavyo kulingana na majukumu iliyokasimiwa na utaratibu huu utakuwa na manufaa kwa vijana wa kitanzania katika kupata ajira zinazotolewa kiholela kwa wageni katika mfumo ulipo sasa ambao kwa kiasi kikubwa nyie akina appriciator mnautumia kwa manufaa yenu. Kwa heri.
 
Ndugu yangu appritiator kwa uandishi wako inadhihirisha wazi wewe ni mmoja wa watu wanaofaidika binafsi na mkanganyiko wa kisheria uliopo katika kusimamia vibali vya kazi vya wageni hapa nchi. Mfumo uliopo unaruhusu taasisi na Sheria zaidi ya moja kutoa vibali vya ajirakwa wageni hali ambayo ni hatari kwa mustakabali ya taifa letu hususan ajira kwa vijana. NI WAZI HUNGEPENDELEA YATOKEE MABORESHO KATIKA MKANGANYIKO HUO WA KISHERIA KWA KUWA UTAKUWEKA KANDO KATIKA UTOAJI WA VIBALI VYA AJIRA KWA WAGENI. Unavyojaribu kuelezea ni kana kwamba Rais Kikwete alikurupuka katika kalitolea ufafanuzi suala hili na kulitolea mwelekeo. Nikupe taarifa tuu ni kwamba suala hili limepitishwa katika vikao vingi vya maamuzi kabla ya kumfikia Mweshimiwa Rais.

Nikuulize swali moja, ni nchi gani katika dunia hii kuwa Resident permit ni sawa na Work permit. Ni wapi dunia, ni Tanzania pekeyake . Na wewe ndugu yangu inataka mfumo huu uendelee kwa kuwa unafaidika nao. Mfumo mbovu wa kisheria wa kumruhusu Kamishina na Uhamiaji aendelee kutoa vibali vya ajira badala ya yeye kutoa vibali vya ukaazi. Utoaji wa vibali vya ukaazi ndiyo kazi yake. Hii ndiyo kazi yake na ndiyo kazi iliyokasimiwa Wizara ya Mambo ya Ndani (Instrument ya Rais). Kamishina wa Uhamiaji kwa sasa inagawa vibali vya kazi tena vya muda (CTA) kwa wageni bila hata kuzingatia Sheria. Niambie CTA zinatolewa kwa Sheria ipi. Ni nyie kina Appritiator ndio mko nyuma ya uhaini huu kwa kugawa vibali vya ajira vya muda kama njugu baada ya kupokea hongo kutoka kwa wageni hao bila hata kujali ni vijana wangapi wa nchi hii mnawanyima ajira. Suala hili ni la kihaini na hatua za kisheria zitafuata mkondo wake.

Ndugu yangu Apritiator sheria hiyo mpya inalenga kuweka mipaka kati ya vibali vya ajira (Work Permit) na Vibali vya Ukaazi (Resident Permit) Kwa utaratibu huu kila Taasisi itawajibika ipasavyo kulingana na majukumu iliyokasimiwa na utaratibu huu utakuwa na manufaa kwa vijana wa kitanzania katika kupata ajira zinazotolewa kiholela kwa wageni katika mfumo ulipo sasa ambao kwa kiasi kikubwa nyie akina appriciator mnautumia kwa manufaa yenu. Kwa heri.
Ndugu,
Umenena vilivyo,

ninaombi moja tu kwa mods yani post kama hizi hususan hii ni yakipumbavu inastaili mtu apewe kifungo kwa maslai ya taifa maanake hawa ndio wanaleta hisia za hasira mtu ukatamka la moyoni ukapigwa ban bure,asante
 
Samahani kwa kukukwaza sikuwa na nia mbaya lakini ndivyo watanzania tulivyo jakuwa siyo wote na ndiyo maana nikashauri Mheshimiwa Rais aangalie kwa mapana. Je hao wageni wengi wanaolalamikiwa tatizo ni kubwa kiasi gani? Je wanatanzania wanafahamu kuwa si kila mhindi ni mgeni? Maana kuna wahindi wengi wapo nchini lakini kisheria ni raia wa Tanzania

Tatizo sio centralization or distribution katika kuajiri wageni kwa maana ya MaTX, tatizo letu ni rushwa! Bila kudeal na kutokomeza rushwa hapa nchini ni vigumu kama kupenya katikati ya tundu la sindano kumaliza matatizo kama haya. Nchi hii imekubwa kwa kiasi kikubwa na mambo matatu makubwa kwa maoni yangu; (1) RUSHWA, (2) KUTOSEMA UKWELI DAIMA, (3) KUPOTEA KWA UZALENDO KWA KIWANGO KIKUBWA HASA KWA WATUMISHI WA UMMA.
 
Ushauri wa kuwa vibali vya wageni utolewe na mamlaka moja ni mzuri sana hasa kwa upande wa wageni au wawekezaji. Badala ya kutoa rushwa katika mamlaka mbili au zaidi sasa watatoa kwa mamlaka moja. Watakuwa wamepata "saving". Naunga mkono hoja. Hii inaweza kuwa moja ya vivutio vya wawekezaji katika kupunguza urasimu.
 
Ndugu yangu appritiator kwa uandishi wako inadhihirisha wazi wewe ni mmoja wa watu wanaofaidika binafsi na mkanganyiko wa kisheria uliopo katika kusimamia vibali vya kazi vya wageni hapa nchi. Mfumo uliopo unaruhusu taasisi na Sheria zaidi ya moja kutoa vibali vya ajirakwa wageni hali ambayo ni hatari kwa mustakabali ya taifa letu hususan ajira kwa vijana. NI WAZI HUNGEPENDELEA YATOKEE MABORESHO KATIKA MKANGANYIKO HUO WA KISHERIA KWA KUWA UTAKUWEKA KANDO KATIKA UTOAJI WA VIBALI VYA AJIRA KWA WAGENI. Unavyojaribu kuelezea ni kana kwamba Rais Kikwete alikurupuka katika kalitolea ufafanuzi suala hili na kulitolea mwelekeo. Nikupe taarifa tuu ni kwamba suala hili limepitishwa katika vikao vingi vya maamuzi kabla ya kumfikia Mweshimiwa Rais.

Nikuulize swali moja, ni nchi gani katika dunia hii kuwa Resident permit ni sawa na Work permit. Ni wapi dunia, ni Tanzania pekeyake . Na wewe ndugu yangu inataka mfumo huu uendelee kwa kuwa unafaidika nao. Mfumo mbovu wa kisheria wa kumruhusu Kamishina na Uhamiaji aendelee kutoa vibali vya ajira badala ya yeye kutoa vibali vya ukaazi. Utoaji wa vibali vya ukaazi ndiyo kazi yake. Hii ndiyo kazi yake na ndiyo kazi iliyokasimiwa Wizara ya Mambo ya Ndani (Instrument ya Rais). Kamishina wa Uhamiaji kwa sasa inagawa vibali vya kazi tena vya muda (CTA) kwa wageni bila hata kuzingatia Sheria. Niambie CTA zinatolewa kwa Sheria ipi. Ni nyie kina Appritiator ndio mko nyuma ya uhaini huu kwa kugawa vibali vya ajira vya muda kama njugu baada ya kupokea hongo kutoka kwa wageni hao bila hata kujali ni vijana wangapi wa nchi hii mnawanyima ajira. Suala hili ni la kihaini na hatua za kisheria zitafuata mkondo wake.

Ndugu yangu Apritiator sheria hiyo mpya inalenga kuweka mipaka kati ya vibali vya ajira (Work Permit) na Vibali vya Ukaazi (Resident Permit) Kwa utaratibu huu kila Taasisi itawajibika ipasavyo kulingana na majukumu iliyokasimiwa na utaratibu huu utakuwa na manufaa kwa vijana wa kitanzania katika kupata ajira zinazotolewa kiholela kwa wageni katika mfumo ulipo sasa ambao kwa kiasi kikubwa nyie akina appriciator mnautumia kwa manufaa yenu. Kwa heri.
Hapana hakuna ninachofaidika ndugu yangu soma isome vizuri mada yangu nimetoa angalizo tu kwa Mheshimiwa Rais na kwenye hilo angalizo nimemuelekeza kwenye zile nukta 7 nilizoonyesha lengo ikiwa ni kuonyesha kiasi cha udhibiti na usalama. Pia niliuliza iwapo Idara zote mbili hivi sasa zinashiriki mchakato, inakuwaje uthibiti ushindikane tatizo liko wapi? Nikasema hali ya udhibiti wa ajira kwa wageni hapa Tanzania iko juu ukilinganisha na majirani zetu wa EAC ndiyo maana kila leo wanatupigia kelele tupunguze vikwazo vya ajira kwa wageni.

Ulipotaja CTA naamini wewe pia ni mdau wa masuala haya na hasa ni kati ya wale vishoka wanaoishi hapa mjini kwa ujanjaujanja wa kuwapiga changa la macho wageni kwa kuwatendengenezea vibali vya kuishi na pia mlikuwa mnawatengenezea vibali ‘fake' na sasa mmebanwa baada ya Serikali kuvitoa hivyo vibali kwa njia ya kompyuta.

Kuhusu CTA siyo kibali cha kazi ila ni business visa kwa mgeni anayekuja kwenye shughuli maalumu kwa muda mfupi ambayo kwa kufanya shughuli hiyo itamuingizia kipato. Kwa mfano mgeni anakuja mara moja tu kwa siku mbili au mbili kuja kurekebisha mitambo iliyoharibika kiwandani au anafanya ‘promotion' ya bidhaa kwa wiki moja.

Kuhusu Work permit kuwa Residence permit huo ni utaratibu wa karibu nchi zote za EAC ukienda pale Nyayo house Nairobi wakitoa Work permit ndiyo hiyo hiyo Residence permit na nchi za Jumuiya ya madola utaratibu ndiyo huo pia nchi kubwa duniani kama vile USA, UK na Canada mambo yako hivyohivyo ila siye tusije tukajaribu kuvuruga mambo shauri ya tama ya watu wachache
 
Kuhusu Work permit kuwa Residence permit huo ni utaratibu wa karibu nchi zote za EAC ukienda pale Nyayo house Nairobi wakitoa Work permit ndiyo hiyo hiyo Residence permit na nchi za Jumuiya ya madola utaratibu ndiyo huo pia nchi kubwa duniani kama vile USA, UK na Canada mambo yako hivyohivyo ila siye tusije tukajaribu kuvuruga mambo shauri ya tama ya watu wachache
Hii naona ni vita ya kunyang'anyana tonge.
 
Sifa ya kazi siyo kisomo peke yake au uwezo wa kufanya kazi kitu kikubwa kinachofanya wafanyabiashara kuajiri wafanyakazi toka nje ya nchi ni uaminifu, kitu tunatakiwa tujenge tabia ya kuwa waaminifu watanzania ili kujenga imani na wafanya biashara. Mwekezaji anafungua Hoteli mtu anaajiriwa anajisikia ni haki yake kumwibia tajiri na wageni wanaofikia hotelini kwa kisingiziyo ugumu wa maisha, kufanya starehe zake au mshahara hautoshi, hayo pia yanafanyika katika maduka sasa kuna mfanya biashara atakubali kufanya biashara huku akipata hasara. Mpaka pale tutapokua tunaheshimu kazi zetu na kujenga tabia ya kuwa waaminifu wafanya biashara wakilazimishwa kuajiri wananchi watafunga biashara zao.Mbele ya macho yetu tunaona mtu anaajiri dereva wa Prado yake akimwachia gari peke yake kosa atapakia abiria hata watu kumi na tano kuwapeleka tandika na anarudi haraka, kwa kweli tutakuja fikia hata madereva watatoka nje, kwasababu watu hawana pesa lakini tamaa na starehe wameweka mbele kwahiyo wanatafuta pesa kwa njia yeyote.
Kama kazi ndogo kama ya reception na waiter kwenye hotel kubwa inatakiwa mtu uwe fluent in English. Je vijana wetu waliomaliza kidato cha 4 au 6 wana uwezo huo? Kama hawana uwezo huo kuna kosa gani mwekezaji akamuajiri darasa kijana wa darasa la 8 wa Kenya ambaye yuko sawasawa kwenye lugha ya kiingereza

 
Ndugu,
Umenena vilivyo,

ninaombi moja tu kwa mods yani post kama hizi hususan hii ni yakipumbavu inastaili mtu apewe kifungo kwa maslai ya taifa maanake hawa ndio wanaleta hisia za hasira mtu ukatamka la moyoni ukapigwa ban bure,asante
Huyu naye ni kati ya wale vishoka ‘agent' wanaoishi mjini kwa ujanjaujanja kuwatengenezea wageni vibali vya kuishi au vibali ‘fake' na sasa mmebanwa wanatafuta pakutokea.

 
Ushauri wa kuwa vibali vya wageni utolewe na mamlaka moja ni mzuri sana hasa kwa upande wa wageni au wawekezaji. Badala ya kutoa rushwa katika mamlaka mbili au zaidi sasa watatoa kwa mamlaka moja. Watakuwa wamepata "saving". Naunga mkono hoja. Hii inaweza kuwa moja ya vivutio vya wawekezaji katika kupunguza
urasimu.
Kishoka mwingine huyu

 
Back
Top Bottom