Rais kijana ni ghali sana hivyo hatufai

Rais kijana ni ghali sana hivyo hatufai

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
17,199
Reaction score
16,868
Nchi yetu ni maskini sana, hatuna pesa za kutosha kugharamia mahitaji ya msingi kama vile afya, elimu, maji, umeme, ulinzi, mahakama n.k.

Hivyo tungependa kuelekeza kila shilingi katika kusukuma mbele upatikanaji wa mahitaji haya ya msingi kwa wananchi badala ya kugharamia utunzaji wa marais wengi wastaafu kwa muda mrefu. Inajulikana kuwa mwisho wa urais ni miaka 10 tu baada ya hapo kiongozi huyo atastaafu na mtamtunza kama rais mstaafu hadi mwisho wa uhai wake.

Sasa hali itakuwaje kama mtamchagua rais mwenye umri mdogo?. Kwa mfano, mkichagua rais mwenye miaka 35 au 40 atamaliza vipindi 2 vya urais akiwa na miaka 45 au 50 tu, hivyo kodi zetu zitatumika kumtunza mtu huyo kwa kipindi kirefu sana cha kuazia miaka 20 - 40 hadi hapo atakapofariki dunia.

Hili sio jambo jema kwa nchi maskini kama sisi kuwa na msururu mrefu wa marais, makamu, mawaziri wakuu wengi kwa wakati mmoja watakahitaji kulipwa, kutunzwa, kulindwa na kusababisha foleni ndefu wanapopita barabarani.

Umri wa kuwa rais uwe angalau kuanzia miaka 45 ili tuokoe kodi zetu kwa kugharamia utitili wa VIJANA wastaafu wengi kwa gharama kubwa kwa muda mrefu.

Mimi binafsi siwezi kutoa consent yangu kuruhusu kodi yangu itumike kugharamia rais mstaafu mwenye miaka 45 au 50 labda ipelekwe huko bila ridhaa yangu.
 
kwani mtu wa miaka 50 ni lazima aishi miaka 40 mingine? na mtu wa miaka 60 ni lazima aishi muda mfupi? kufa ni automatic haitegemei hivyo usemavyo.
 
kama uzee ni sifa basi rais awe kingunge mwiru
 
kwani mtu wa miaka 50 ni lazima aishi miaka 40 mingine? na mtu wa miaka 60 ni lazima aishi muda mfupi? kufa ni automatic haitegemei hivyo usemavyo.

Unasema hivyo kwa kutumia uzoefu gani? tunao marais Moi, Chisano, Fidel Kasrol, Mwinyi, Mkapa, Mbeki, Kibaki, Mzee Kaunda n.k, hivi watu hawa wote wana umri gani? Kama Mugabe, Museveni na Kagame wangefanya urais wao kwa miaka 10 tu ya kwanza si wangekuwa wameshataafu pia? Rais Mandela kafa akiwa na umri gani?, alikuwa halipwi? acha hizo wewe. Labda tuweke ukomo wa kugharamia viongozi wastaafu.
 
JK alipoingia madarakani alijitahidi kuingiza vijana (akina Mathew, Ezekia, Angel na Marsha) ni kitu gani tofauti wameleta nchini. Huyo Ezekia ndo kabisaaaa wanyama wakaibiwa huku anaona.
 
kama uzee ni sifa basi rais awe kingunge mwiru
Kama wewe ni kijana lazima uwe na sifa za ziada sana na kutaka kuwa rais vinginevyo hutufai utatu cost kukutuza wewe na familia yako kwa miaka mingi huku ukiwa umeshatuibia ulipokuwa rais
 
Kama wewe ni kijana lazima uwe na sifa za ziada sana na kutaka kuwa rais vinginevyo hutufai utatu cost kukutuza wewe na familia yako kwa miaka mingi huku ukiwa umeshatuibia ulipokuwa rais

kwa hiyo unataka rais kikongwe.
 
kwa hiyo unataka rais kikongwe.

Naam, kwa kuwa tumeshashuhudia kuwa hakuna tofauti kati kiongozi kijana na mzee, maprofessor na wasiosoma, mwanaume na mwanamke wala mwislamu na mkristu, wazanaki wanasema wote manzanyange. Kilichobaki tuangalie tu namna ya kupunguza matumizi mabaya ya kodi zetu basi (to choose the least evil). The best solution is to choose the least evil, the least evil for us is to choose the oldest leader possible to avoid unnecessary expenditures in the future.
 
kama uzee ni sifa basi rais awe kingunge mwiru

Kama wewe ni kijana endelea kuwa rais wa familia yako kwanza hadi ufikie umri wa miaka 45 hivi. Kama huna mvi kichwani, we are sorry, we have no money to pay you for 20-40 years after your retirement
 
Naam, kwa kuwa tumeshashuhudia kuwa hakuna tofauti kati kiongozi kijana na mzee, maprofessor na wasiosoma, mwanaume na mwanamke wala mwislamu na mkristu, wazanaki wanasema wote manzanyange. Kilichobaki tuangalie tu namna ya kupunguza matumizi mabaya ya kodi zetu basi (to choose the least evil). The least evil for us is to choose the oldest leader possible to avoid unnecessary expenditures in the future

You're very genius my nigga,The oldest President might have a very short span of life.The shorter life he lives after retirement the better for everyone.The longer life he lives,the worse for everyone!
 
You're very genius my nigga,The oldest President might have a very short span of life.The shorter life he lives after retirement the better for everyone.The longer life he lives,the worse for everyone!

excellent!!!
 
kavulata
Umejadili jambo la mmsingi sana ila sasa umesimamia msingi dhaifu.

The delicacy of the issue inabebwa zaidi na instability na wala si pesa za kujikimu hao wastaafu vijana. Ikumbukwe kuwa nchi nyingi za africa si imara kitaasisi hivyo misingi/mifumo yake ni rahisi sana kuyumbishwa na influential individuals. Sote tunafahamu uzito wa nafasi ya rais wa nchi kimamlaka na kimadaraka. Haiwezekani kwa mtu aliyepata kufikia ngazi hiyo kupata fursa yenye madaraka makubwa ya jinsi hiyo baada ya kustaafu, madaraka matamu jamani, ataishije katika "ujana" wa muda mrefu thereafter pasipo hayo makuu?

Ndiyo haya sasa tunayaona ya kina Kagame, Kabila, Nkurunziza na "vijana" wote waliopata kuukwaa huo u-mungu mtu mapema kubaki waking'ang'ania madarakani kila kukicha. Naaam wakafanye kazi gani tena? Na bora tu waking'ang'ania hapo maana wakiwa pembeni ni hatari zaidi kwa stability ya serikali yoyote sababu yeyote aliyepata kuwa rais wa nchi anabaki kuwa an influential figure so ukiongeza na mentality ya "bado nimo" ni hatari kubwa.
 
Last edited by a moderator:
ndugu kweli huna akili,hujasoma kabisa,akili zako za kitoto ndugu yangu

Usitukane ndugu yangu toa hoja yako: So far hatujaona wonders zilizofanywa na madiwani, wabunge, mawaziri wala rais kijana katika kukwamua shida za wananchi wake zinazotushawishi tuamini kuwa kumpata rais kijana utakuwa muarobaini wa shida zetu kama taifa. Ila tunachokifahamu hadi sasa ni kuwa rais kijana atakuwa mzigo wa kudumu kwetu atakapostaafu urais. Hatushawishiki kuamini kuwa utendaji wa rais kijana utatofautiana saaana na wa rais mwenye umri wa wazee kama Salum A. Salum, Pinda, Sitta, Slaa, Lipumba, Shein, Lowassa, Membe, Maalim Sefu, Samia Hassan, Mongela, Makinda, Wasira, n.k. Tunachokifahamu kingine kuhusu marais vijana ni uwezekano wao wa kutaka kuendelea kubaki madarakani hata baada ya vipindi vyao kumalizika, na hapo tunayo mifano ya akina Kagame, Nkuruzinza, Museven, Kabila, Putin na Salmini Amour. Huu sio muda wa kujaribu ili tuone itafananaje. Pesa za kuwatunza wastaafu wetu tunazihitaji pia kuziwekeze kwenye elimu na afya za vijana wetu. Vijana wana haki pia ya kuchagua na kuchaguliwa lakini muda wetu wa kufanya hivyo bado haujafika.
 
Nchi yetu ni maskini sana, hatuna pesa za kutosha kugharamia mahitaji ya msingi kama vile afya, elimu, maji, umeme, ulinzi, mahakama n.k.

Hivyo tungependa kuelekeza kila shilingi katika kusukuma mbele upatikanaji wa mahitaji haya ya msingi kwa wananchi badala ya kugharamia utunzaji wa marais wengi wastaafu kwa muda mrefu. Inajulikana kuwa mwisho wa urais ni miaka 10 tu baada ya hapo kiongozi huyo atastaafu na mtamtunza kama rais mstaafu hadi mwisho wa uhai wake.

Sasa hali itakuwaje kama mtamchagua rais mwenye umri mdogo?. Kwa mfano, mkichagua rais mwenye miaka 35 au 40 atamaliza vipindi 2 vya urais akiwa na miaka 45 au 50 tu, hivyo kodi zetu zitatumika kumtunza mtu huyo kwa kipindi kirefu sana cha kuazia miaka 20 - 40 hadi hapo atakapofariki dunia.

Hili sio jambo jema kwa nchi maskini kama sisi kuwa na msururu mrefu wa marais, makamu, mawaziri wakuu wengi kwa wakati mmoja watakahitaji kulipwa, kutunzwa, kulindwa na kusababisha foleni ndefu wanapopita barabarani.

Umri wa kuwa rais uwe angalau kuanzia miaka 45 ili tuokoe kodi zetu kwa kugharamia utitili wa VIJANA wastaafu wengi kwa gharama kubwa kwa muda mrefu.

Mimi binafsi siwezi kutoa consent yangu kuruhusu kodi yangu itumike kugharamia rais mstaafu mwenye miaka 45 au 50 labda ipelekwe huko bila ridhaa yangu.

Mkuu Kavulata wewe ni GREAT THINKER siwezi nikasoma tu bila kukupongeza, Zitto ni Mchumi, lakini kwasababu ya tama ya madaraka amesahau na anashindwa kuelewa kwanini huo umri wa miaka 35 hatuutaki hasa sisi walala hoi. Just imagine jamaa anashinda urais akiwa 35 yrs old 35 + 10 = 45 anachia madaraka ataishi akila pension kwa miaka mingine 45 wakati huo kukiwa na maraisi WATANO wakiwa namna hiyo. Natamani hata ingekuwa mgombea awe na miaka 55.
 
Mkuu Kavulata wewe ni GREAT THINKER siwezi nikasoma tu bila kukupongeza, Zitto ni Mchumi, lakini kwasababu ya tama ya madaraka amesahau na anashindwa kuelewa kwanini huo umri wa miaka 35 hatuutaki hasa sisi walala hoi. Just imagine jamaa anashinda urais akiwa 35 yrs old 35 + 10 = 45 anachia madaraka ataishi akila pension kwa miaka mingine 45 wakati huo kukiwa na maraisi WATANO wakiwa namna hiyo. Natamani hata ingekuwa mgombea awe na miaka 55.
ahsante kaka, sina ugomvi na vijana, kwani hata mimi ni kijana pia ila tutangulize mbele maslahi ya jumla. Kama vijana tuna mawazo mapya ya namna ya kuijenga nchi yetu tuwape wazee wayatekeleze, japokuwa baadhi ya wazee hawashauriki (we used to.....kila wakati na mara zote)
 
Back
Top Bottom