Alibaba,Juhudi za Tanzania Association UK (TA UK) na zile za Zanzibar Walfare Association (ZAWA) Za kujaribu kumpata Rais wa Zanzibar ambae pia ni makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania ili aweze kukutana na watanzania waishio UK Ziliishia kupiga ukuta leo hii pale Ofisi ya Balozi wa Tanzania UK ilipovithibitishia Vyombo hivyo viwili kuwa Mheshimiwa huyo hataweza kuonana na Watanzania kutokana na Shughuli nyingi alizonazo.
Pamoja na wingi na umuhimu wa shughuli zake ningedhani kuwaona Watanzania ingekuwa moja ya yale yaliyomuhimu katika ratiba yake.
Binafsi nimefadhaishwa sana na Matokeo hayo na Rai yangu ni kuwataka viongozi wa TA UK na ZAWA kwa pamoja Kwenda Ubalozini na kujaribu kumshawishi Balozi aone umuhimu wa mkutano wa Mh. huyo na wananchi kwani sikumbuki tunapoendea miaka kumi ya uongozi wake kukutana na wananchi ajapo hapa Uingereza.
Juhudi za Tanzania Association UK (TA UK) na zile za Zanzibar Walfare Association (ZAWA) Za kujaribu kumpata Rais wa Zanzibar ambae pia ni makamu wa Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania ili aweze kukutana na watanzania waishio UK Ziliishia kupiga ukuta leo hii pale Ofisi ya Balozi wa Tanzania UK ilipovithibitishia Vyombo hivyo viwili kuwa Mheshimiwa huyo hataweza kuonana na Watanzania kutokana na Shughuli nyingi alizonazo.
Pamoja na wingi na umuhimu wa shughuli zake ningedhani kuwaona Watanzania ingekuwa moja ya yale yaliyomuhimu katika ratiba yake.
Binafsi nimefadhaishwa sana na Matokeo hayo na Rai yangu ni kuwataka viongozi wa TA UK na ZAWA kwa pamoja Kwenda Ubalozini na kujaribu kumshawishi Balozi aone umuhimu wa mkutano wa Mh. huyo na wananchi kwani sikumbuki tunapoendea miaka kumi ya uongozi wake kukutana na wananchi ajapo hapa Uingereza.